Tundu Lissu: Wamilili wa Online Tv walipwe fidia, waliozifungia wachukuliwe hatua, maana Rais amesema zilifungia kimakosa

Tundu Lissu: Wamilili wa Online Tv walipwe fidia, waliozifungia wachukuliwe hatua, maana Rais amesema zilifungia kimakosa

Hujaelewa mtego wa Lissu.Wamesema magazeti yaliyofungiwa ilikuwa ni kwa mujibu wa sheria.Inamaana huko ni kukiri kuwa kwa Hizi online tv ambazo zimefunguliwa sheria haikufuatwa!Au kama sheria ilifuatwa kwa vyote,na ni msamaha kama unavyosema, kwa nini wasivifungulie vyote?Huu ndo ujumbe wa Lissu kwa undani wake kidogo....
Nilielewa sana na msamaha ukitolewa sio lazima kwa wote
 
Huyu nae hata kama tunamsapoti kuna mambo anapaswa atumie akili kiutawala, sitaki kuamini Lissu haelewi kilichofanyika. Hii sasa ataanza kupoteza watu tunaomuelewa.

In short, mama alichofanya ni kwamba angeweza kuamua kukaza kwani mngemfanya nini? Sababu waliofungiwa walitumia utaratibu wa Sheria iliyopo/zilizopo. Yawezekana Sheria hizo ndio kandamizi, Rais hawezi kuziongelea pale ndio maana ametoa kwanza waliofungiwa wafunguliwe halafu ndio tuanze upya.

Kwenye kuanza upya ndipo ataambiwa kwamba tatizo ni sheria iliwekwa ya kikandamizi sana hapo ndipo ataweza kuchukua steps zaidi.

Kimsingi hiyo ni amnesty/msamaha, sababu haimhusu yeye, yeye anataka uhuru wa habari uwepo ndio maana amegusia kwani ai angeweza kukaa kimya tu nani angemsumbua?

Sasa basi, kwa msamaha huo maana yaje ndio yale maneno kwamba tusameheane tuanze upya sasa Lissu anataka ligi ya nini?
Haki hupewi kwa hisani ya mtu, ni ya kuidai tena sheria, kanuni na taratibu zipo.
 
Huu ni ukweli mtupu, mwanasheria nguli na mgombea urais wa JMT kupitia Chadema anasema kweli tupu. Kama hawakuwa na makosa walipwe fidia na walioshiriki kuzifungia bila makosa wachukuliwe hatua.

CAG nae anasema kuna 14+ Billion zinadaiwa huko kama Riba,
Sababu bila shaka ni ujuaji wa kuanzisha mamiradi ya kukurupuka pasi kufuata taratibu na Ushauri wa wataalam.
CCM Oye!
 
Back
Top Bottom