LGE2024 Tundu Lissu yuko sahihi, mfano Kilosa Kuna Vijiji 138 CHADEMA ina Wagombea 70, Kuna Vitongoji zaidi ya 800 CHADEMA ina Wagombea 200!

LGE2024 Tundu Lissu yuko sahihi, mfano Kilosa Kuna Vijiji 138 CHADEMA ina Wagombea 70, Kuna Vitongoji zaidi ya 800 CHADEMA ina Wagombea 200!

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
09 November 2024
Berege, Mpwapwa
Dodoma
Tanzania

WAKILI MSOMI AENGULIWA KUGOMBEA NAFASI YA UENYEKITI WA KIJIJI DODOMA

View: https://m.youtube.com/watch?v=Py6xouFmbys

Wakili wa mahakama kuu mwanasheria msomi Deogratias Cosmas Mahinyila ampa somo msimamizi wa uchaguzi msaidizi awasilisha mapingamizi / mtendaji ajikanyaga

Hekaheka hiyo inafuatia mgombea wa CHADEMA kwa nafasi ya uenyekiti wa kijiji cha Berege wilaya ya Mpwapwa ambapo mgombea uenyekiti wa kijiji cha Berege kupitia CHADEMA Wakili wa mahakama kuu mwanasheria msomi Deogratias Cosmas Mahinyila alienguliwa ...
 
Moja ya Sifa kuu ya Tundu Lissu ni Mkweli

Alisema CHADEMA bado haijawa na Wagombea wa kutosha kuikabili CCM

Hiyo imejionesha kwenye wilaya karibu zote

Mfano mzuri ni Kilosa Vijiji 138 Chadema ina wagombea 70 tu

Vitongoji zaidi ya 800 lakini Chadema ina wagombea 200 na ushee tu

Safari bado ni ndefu 🐼
....Na hapo bado hawajaenguliwa kwenye uteuzi!
 
TAHARUKI KIJIJI CHA KIBANGA, POLISI WAWAOKOA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI. WANANCHI WADAI MAJINA YA WAGOMBEA


View: https://m.youtube.com/watch?v=fxIZ2CFCmX0
Wananchi wadai majina ya wagombea wa CHADEMA kutoka kwa watendaji. Wananchi wajilaza barabarani kuzuia watendaji wasiondike na karandinga la Polisi..
 
09 November 2024

Mtaa wa Medeli
Dodoma Tanzanoa

CHADEMA YAMJIA JUU MSIMAMIZI MSAIDIZI BAADA YA KUKATA JINA LA MGOMBEA WA MTAA WA MEDELI DODOMA


View: https://m.youtube.com/watch?v=RfFvzbn7b8k

Mtaa wa Medeli mjini Dodoma vituko vya wasimamizi wasaidizi kukata jina la mgombea wa CHADEMA Amosi Sylvester Lyaki yawekwa wazi ...

Mgombea huyo wa Amosi Sylvester Lyaki mkazi wa mtaa Kisasa Medeli Dodoma amekuwa kwa miaka 5 mjumbe wa serikali ya mtaa wa Kisasa Medeli toka mwaka 2019 hadi 19 October 2024.

Cha kushangaza nyumba yangu ipo Medeli, nina familia na ninejiandikisha katika daftari la mkazi wa mtaa wa Medeli, kitambulisho cha mpiga kura ni mkazi wa Medeli .... lakini naambiwa mimi siyo mkaazi wa Medeli wakidai mimi ni mkazi wa Bwawani

Kwanini wagombea wa CHADEMA tu ndiyo tunaenguliwa, tunaonelewa sana sisi wapinzani ... mimi nimemuongoza msimamizi msaidizi kama mjumbe wa serikali ya mtaa ...

Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma atoa maelekezo ya uchaguzi wa serikali za mitaa​

thumb_4867_800x420_0_0_auto.jpg
Imewekwa tarehe: September 28th, 2024
Na. Dennis Gondwe, DODOMA

WANANCHI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameshauriwa kujitokeza kwa wingi siku ya uchaguzi wa serikali za mitaa tarehe 27 Novemba, 2024 ili kuchagua viongozi bora.

Kauli hiyo ilitolewa na Msimamizi wa Uchaguzi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akitoa Maelekezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 kwa waandishi wa habari ofisini kwake leo tarehe 26 Septemba, 2024.

Dkt. Sagamiko alisema “niwahamasishe wananchi wa halmashauri ya jiji la Dodoma kujitoleza kwa wingi siku ya uchaguzi ambayo ni jumatano ya tarehe 27 Novemba, 2024 ili kuchagua viongozi bora watakaoongoza”.

Msimamizi huyo wa uchaguzi alisema kuwa wananchi wenye sifa za kushiriki wanatakiwa kushiriki. “Ninatoa wito kwa wananchi wote wenye sifa kushiriki kikamilifu katika mchakato huu wa uchaguzi, kuanzia hatua ya kujiandikisha kwenye orodha ya mpiga kura. Kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura ni hatua inayompa kila mwananchi mwenye sifa haki ya kisheria kushiriki uchaguzi kama mpiga kura au mgombea nafasi ya uongozi” alisema Dkt. Sagamiko.

Akiongelea nafasi zitakazogombewa alizitaja kuwa ni mwenyekiti wa mtaa, wajumbe wa kamati ya mtaa mchanganyiko na kundi la wanawake. “hivyo, wananchi wenye sifa wanahimizwa kuchukua na kurudisha fomu za kugombea nafasi hizo kwa tarehe zilizoainishwa katika maelekezo haya. Ushiriki wa wananchi wengi katika kugombea nafasi hizi ni muhimu katika kukuza demokrasia na kuhakikisha upatikanaji wa viongozi bora kwa maendeleo ya taifa letu” alisisitiza Dkt. Sagamiko.

Msimamizi wa Uchaguzi Halmashauri ya Jiji la Dodoma alitoa maelekezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 mbele ya waandishi wa habari, viongozi wa vyama vya siasa na makundi maalum pamoja na wadau wengine.

MWISHO
 
amekuwa kwa miaka 5 mjumbe wa serikali ya mtaa wa Kisasa Medeli toka mwaka 2019 hadi 19 October 2024.

Mkuu wa mkoa wa Dodoma akitangaza ukomo wa uongozi

TOKA MAKTABA:
19 October 2024
Ukomo wa madaraka kwa viongozi wa Serikali za mitaa leo Oktoba 19, 2024

View: https://m.youtube.com/watch?v=GJWbkiCLsK8
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary S. Senyamule, ametangaza ukomo wa madaraka kwa viongozi wa Serikali za mitaa leo Oktoba 19, 2024 kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye ukumbi wa ofisi yaje jengo la MKapa Jijini Dodoma.

Ukomo huo wa madaraka ni kwa viongozi ngazi za wenyeviti wa vijiji, vitongoji, mitaa pamoja na wajumbe wa Halmashauri za vijiji na Kamati za mitaa.

Tangazo la mkuu wa mkoa wa Dodoma limefuatia tamko la waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI ndugu Mohamed Mchengerwa kuwataka viongozi wote ngazi za za wenyeviti wa vijiji, vitongoji, mitaa pamoja na wajumbe wa Halmashauri za vijiji na Kamati za mitaa ya kukoma kufanya kazi na kuachia ofisi na vifaa vya ofisi:


View: https://m.youtube.com/watch?v=OVfs3NFplLM
 
..Ccm jaribuni kujiendesha kwa ruzuku kiduchu, au sifuri, kama wanayopata vyama vya upinzani tuone mtafika wapi.


..au waachiene wapinzani wamiliki Tume ya Uchaguzi, Polisi, na mahakama, tuone kama Ccm wote hamtaacha siasa.
Miradi ya CCM inaingiza tsh 40 billion kila mwaka 😀
 
10 November 2024
Bukoba, Kagera
Tanzania

Mwenyekiti wa BAVICHA mkoa Kagera aelezea uchafuzi wa mchakato wa uchaguzi wa TAMISEMI unaoendelea mkoani Kagera


View: https://m.youtube.com/watch?v=uj-85WqIErk

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana CHADEMA - BAVICHA mkoani Kagera kamanda Felius Festo Kinimi azungumzia mchakato mzima ulivyohujumia kuanzia hatua za mwanzo za uandikishajji katika daftari la mkazi na hujuma hizo hazikupewa majibu na TAMISEMI na hatua ya kuchukua fomu mkurugenzi wa halmashauri Kyerwa, mkuu wa wilaya ya Karagwe naye anaingilia mchakato wa uchaguzi wa serikali za vijiji, mitaa na vitongoji

Tarehe 8 November 2024 uteuzi wa wagombea hadi tarehe 9 November ndiyo majina yanabandikwa katika kuta za matangazo masaa machache kabla ya muda ya wagombea kujibu mapingamizi kata Kanoni, Nyaishozi, Kyerwa, Ngara, Muleba Kusini pia Kaskazini n.k wagombea wa CHADEMA wameenguliwa kwa kanuni za kufikirika zisizokuwepo kisheria ....

1731255487019.jpeg

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ŵilaya ya Kyerwa SACF. James John
 
10 November 2024
Ukumbi wa Shabaan Mloo
Makao makuu ya CUF
Buguruni
Dar es Salaam

CUF NAO WATOA TAMKO LAO SAKATA LA WAGOMBEA KUENGULIWA / MAGDALENA SAKAYA AMVAA MCHENGERWA, RIS SAMIA HASSAN


View: https://m.youtube.com/watch?v=gNGHgKNad9U

kigogo cha chama Bi. Magdalena Sakaya, Naibu Katibu mkuu wa CUF - ( Civic United Front), kwa niaba ya chama aongea na waandishi wa habari pia umma mpana wa waTanzania kuelezea kinachoendelea katika mchakato mzima wa uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji .....

Orodha ya wapiga kura katika daftari la mkaazi lilichezewa lakini mamlaka zinazohusika haikulifanyia kazi ... hivyo orodha hiyo ni batili...

katika zoezi zima la kuchukua fomu na kurejesha fomu, limegubikwa na ubabaishwaji mkubwa na hujuma mfano wasimamizi wasaidizi wameshindwa kuelewa siku, kanuni na maamuzi mfano huko Misungwi na Ubungo waliandika barua batili...vitisho Liwale kwa wagombea wetu ...



Huko Mtwara vijijini wagombea karibia wote wa CUF wameenguliwa ... huko Magu wagombea 80% wa CUF wameenguliwa ... wasimamizi wasaidizi watumia sababu za kufikirika zisizo katika kanuni wala sheria ya ....

Huko Kondoa wagombea wa CUF wameenguliwa kwa madai hawajarejesha fomu ... wilaya ya Ubungo wagombea waenguliwa ... Geita, Tunduru, Kaliua, Tabora Kinondoni, Mwananyamala DSM n.k ni uchafuzi mtupu wa uchaguzi.

HABARI ZA HIVI PUNDE:

10 November 2024

Mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala azungumzia zoezi la uchaguzi za serikali za mitaa


View: https://m.youtube.com/watch?v=e9tCjhWhXhk

amewapongeza wananchi wote waliojitokeza kushiriki Katika zoezi zima la kujiandikisha kwenye daftari la mpiga kura pamoja na wagombea wenye sifa walio jitokeza kuchukua form za kungombea Katika vyama mbalimbali kupitia vyama vyao vya siasa.

Aidha amewaomba wangombea wote ambao hawajaridhishwa na uteuzi wafate taratibu zilizopo ili kuweza kuwasilisha pingamizi lao katika eneo husika ili shughuri hizo za uchanguzi ziendelee kwa amani na utulivu Katika mkoa huo wa Mtwara.

Vilevile amewaomba wananchi wote walio jiandikisha kwenye daftari la mpiga kura wajitokeze kupiga kura Novemba 27,2024 kwaajili ya kuchagua viongozi wao.

Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo Novemba 10,2024 ofsini kwake amesema mtu yeyote au kikundi chochote kitakacho panga kufanya kitendo cha uvunjifu wa amani katika kipindi hiki cha uchaguzi na wakati mwingine wowote serikali haitosita kuchukua hatua sitahiki za kisheria.
 
..hiyo miradi chanzo chake si mabilioni ya fedha za kodi ya wananchi?

..Je, Tlp, Tadea, wangekuwa wanapewa mabilioni kama Ccm wasingekuwa mbali?
Chadema baada ya maridhiano wamepewa billion 3, mmewekeza wapi?
 
Ukubwa wa ACT Wazalendo Kigoma wadhihiri

View: https://m.youtube.com/watch?v=X39XiI7SRDA
tumezunguka kata zote 139 za mkoani Kigoma na tunashiriki kindakindaki uchaguzi wa serikali za vijiji, vitongoji na mitaa hayo amesema kiongozi wa ngome ya vijana ACT Wazalendo Abdul Nondo, na kiongozi mstaafu Zitto Kabwe walipotembelea maeneo Kagunga n.k mkoani Kigoma kuonesha utayari wa kushinda uchaguzi wa serikali za mitaa 27 November 2024

BREAKING NEWS 9 November 2024
View attachment 3147961

KIGOMA KUMEWAKA, WAGOMBEA ACT-WAZALENDO NA CHADEMA WAKATWA MSIMAMIZI WA UCHAGUZI ATOLEA UFAFANUZI


View: https://m.youtube.com/watch?v=JQB90s3FjXg

mkurugenzi wa Halmashauri DED Kigoma mjini ambaye ni msimamizi wa uchaguzi ndugu Kisena Magena Mabuba asema kuna nafasi ya kukata rufaa kupinga kuenguliwa ...
1731253257783.jpeg

Picha maktaba : ndugu Kisena Magena Mabuba akitoa hotuba akiwa katika shughuli za majukumu yake mengi
 
Mheshimiwa Emmanuel Godfrey Masonga Katibu Kanda ya Kati CHADEMA - Warejesheni mara moja wagombea wetu mliowaengua


View: https://m.youtube.com/watch?v=4xSEWM_IpxM

Katibu wa kanda ya kati atoa takwimu za wagombea wa CHADEMA kanda ya kati katika majimbo ya mikoa ya Singida, Dodoma, Morogoro walioenguliwa ...

Katibu wa Kanda CHADEMA anarejea kanunI namba 9 (1).... na ..... zinazohusika mgombea kukosa sifa ...

Katika halmashauri ya Chemba mkoa wa Dodoma wagombea wa CHADEMA ... wagombea 61 wa CHADEMA walifanikiwa kurejesha fomu kisha wasimamizi wasaidizi wameengua wagombea 38 wa CHADEMA na tukienda maeneo ya Kondoa ....

1731254533130.png

Picha maktaba : Bi. Siwema Hamoud Jumaa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Chemba katika vikao / shughuli kazi za kawaida za halmashauri
1731254768896.jpeg
 
10 November 2024
Arusha Tanzania

VILIO KILA KONA : WAGOMBEA WA CHADEMA WAWEKEWA MAPINGAMIZI KISIRI, HAWAKUPEWA NAFASI YA KUPINGA MAPINGAMIZI , WAENGULIWA


View: https://m.youtube.com/watch?v=pxsTvo_xmLs

Wasimamizi wasaidizi waandikia barua wagombea wa CHADEMA na kuwakabidhi barua kwa dispatch muda umekwisha jumapili saa 10 jioni muda ukiwa umekwisha kujibu pingamizi ...

Mkurugenzi mpya wa Jiji la Arusha Bwana John Lipesi Kayombo afikiwa kwa simu ashindwa kupatikana.. kama msimamizi mkuu ngazi ya wilaya atasikiliza rufani hizo za CHADEMA baada ya wasimamizi wasaidizi kufanya madudu
1731272828214.jpeg

Mkurugenzi mpya wa Jiji la Arusha, ndugu John Lipesi Kayombo (kulia) tarehe 21 Agosti 2024 akipokea nyaraka ikiwa ni ishara ya kukabidhiwa ofisi hiyo kutoka kwa Juma Hamsini (kushoto). Awali Kayombo alikuwa Jiji la Dodoma huku Hamsini akihamishiwa kwenda Jiji la Tanga.
 
11 November 2024
Shinyanga, Tanzania

WAGOMBEA WA CHADEMA WAENGULIWA

CHADEMA WANAZUNGUMZA MUDA HUU SHINYANGA, SIMIYU NA MARA WADAI WAGOMBEA WAO KUENGULIWA ASILIMIA 90


View: https://m.youtube.com/watch?v=3B56EkLUeYk

Msimamizi wa uchaguzi Halmashauri ya Shinyanga Mkurugenzi Mtendaji DED Dkt. Kalekwa Kasanga, sasa rufaa zinategemewa wilayani kwa DED
1731350002135.jpeg

Picha maktaba : Mkurugenzi DED Dkt. Kalekwa Kasanga akiwa ktk shughuli za kawaida
 
11 November 2024
Tunduma, Tanzania

Boniface William Mwakabaje mwenyekiti wa CHADEMA jimbo la Tunduma, tumejipanga

View: https://m.youtube.com/watch?v=2fZO4UFKz7Y
Uchaguzi ni mchakato, na mchakato umetekwa nyara na chama dola kongwe CCM

Hatuwezi kukaa kimya wakati tunakabiliana na changamoto kubwa kama nchi nzima kwa wagombea wetu wa CHADEMA kuenguliwa kwa wingi uchaguzi wa serikali za mitaa, vitongoji na vijiji 2024..

Mitaa 71 wagomea 41 wa chadema hapa Tunduma ili kuipa ushindi haramu CCM . Na upande wa mìtaa ...

Viongozi wagombea wa CHADEMA nyumba zao zimevamiwa zimevunjwa milango na wanaCCM ili kuwatisha, makada wa CHADEMA wamecharangwa mapanga ofisini na fomu za wagombea wetu kuporwa wakijitayarisha kukata rufaa.... na jeshi la polisi taarifa imetolewa lakini hatua,...

Viongozi wa wizara ya TAMISEMI na serikali kuu imekuwa kimya kwa hali hii mbaya ya kisiasa, kiuchaguzi na usalama ... bila kutoa tamko wakati kuna tishio la uwezekano wa machafuko kutokea nchini maana ...

Sasa rufani za wagombea zinaelekezwa ngazi ya wilaya kwa mkurugenzi DED ambaye ni msimamizi mkuu wa uchaguzi Tunduma wilaya ili wagombea wa CHADEMA na wananchi wapate haki

Picha maktaba : Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Tunduma, Mariam Chaurembo akisisitiza jambo ktk majukumu yake ya kawaida kama DED
1731360908038.jpeg
 
Back
Top Bottom