LGE2024 Tundu Lissu yuko sahihi, mfano Kilosa Kuna Vijiji 138 CHADEMA ina Wagombea 70, Kuna Vitongoji zaidi ya 800 CHADEMA ina Wagombea 200!

LGE2024 Tundu Lissu yuko sahihi, mfano Kilosa Kuna Vijiji 138 CHADEMA ina Wagombea 70, Kuna Vitongoji zaidi ya 800 CHADEMA ina Wagombea 200!

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
11 November 2024
Tarime Vijijiji, Mara
Tanzania

CHADEMA TARIME WACHARUKA WAGOMBEA WAO KUENGULIWA "CCM NDIO WANAWEKA MAPINGAMIZI BADALA YA WAGOMBEA"


View: https://m.youtube.com/watch?v=ljUZoM61U9I
Viongozi wa chama kikuu cha upinzani Tanzania kamanda Mwita Isasi mwenyekiti CHADEMA wilaya ya Tarime na kamanda Mrimi Zabroni katibu wa CHADEMA jimbo la Tarime vijijini, wakiongea na wanachadema mbele ya waandishi wa habari, CHADEMA imeweza kusimamisha wagombea zaidi ya 900

Mrimi Zabroni katibu wa CHADEMA jimbo la Tarime vijijini abainisha madudu ya ajabu uchafuzi wa uchaguzi wa serikali za mitaa 2024 ... mfano kijiji kimoja msimamizi uchaguzi msaidizi amewaengua wagombea wote ...

Kamanda Nyangoko Paul Thomas mgombea wa CHADEMA katika kijiji kata ya Sirari amewekewa pingamizi ana uraia pacha wa Tanzania na Kenya hivyo kuenguliwa ..


Mrimi Zabroni katibu wa CHADEMA jimbo la Tarime vijijini asomea wana Tarime Vijijini sababu zote moja baada nyingine za kufikirika kutokana na shindikizo la ....

Naye Bi. Fatuma Migela mwanachama mwandamizi wa CHADEMA Sirari Tarime anasema nchi hii sasa inaburuzwa, fujo na vurugu za CCM zitaopeleka nchi pabaya..

Bi Fatuma Migela amuomba rais Samia Hassan aingilie katika wananchi wasibaguliwe, waachiwe wachague viongozi wanaoona wanafaa badala ya kuenguliwa kisa ni wagombea wa CHADEMA chama halali kilichosajiliwa na msajili wa vyama vya siasa

Mrimi Zabroni katibu wa CHADEMA jimbo la Tarime vijijini amesema rufani dhidi ya mapingamizi yaliyowekwa na CCM wanayapeleka wilayani kusikilizwa ..

1731376355248.jpeg

1731376722288.jpeg

Picha maktaba : Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime (Vijijini), Simion Kiles.


1731376395263.jpeg
 
12 November 2024
Serengeti, Tanzania


CHADEMA KANDA YA SERENGETI WAIBUKA NA TUHUMA KWA MSIMAMIZI WA UCHAGUZI - WADAI KENGULIWA KWENYE UCHAGUZI 2024....

View: https://m.youtube.com/watch?v=d0pTLlzF_NE
Wasimamizi wasaidizi wakimbia ofisi kiasi wagombea wa CHADEMA walioenguliwa wanahaha kutafuta wapi wawasilishe rufaa za mapingamizi... katibu wa CHADEMA kanda ya Serengeti kamanda Jackson Mnyawami akiongea ....

CHADEMA KANDA YA SERENGETI YADAI WAGOMBEA WAKE KUENGULIWA BILA SABABU (MAJIMBO 24) SHINYANGA, SIMIYU NA MARA​

MisalabaNovember 11, 2024

Na Mapuli Kitina Misalaba
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kanda ya Serengeti leo kimeibua malalamiko baada ya kudai kuwa wagombea wake kwa asilimia 90 walioomba nafasi katika uchaguzi wa serikali za mitaa wameenguliwa katika mikoa ya Shinyanga, Simiyu, na Mara.
1731405207092.jpeg

Akizungumza na waandishi wa habari leo Novemba 11, 2024, katika ofisi za kanda hiyo, Katibu wa CHADEMA kanda ya Serengeti Jackson Mnyawami, amesema kuwa wagombea wa CHADEMA wamekuwa wakikumbana na changamoto mbalimbali katika mchakato wa uchaguzi, akieleza kuwa zaidi ya asilimia 90 ya wagombea chama hicho katika kila mtaa wameenguliwa.
Mnyawami ameeleza kuwa chama kimekuwa kikitekeleza majukumu yake kwa kufuata kanuni za uchaguzi wa serikali za mitaa za mwaka huu, lakini licha ya jitihada hizo, wagombea wake wengi wameondolewa, huku baadhi ya wagombea waliopitishwa wakikumbana na pingamizi.
“Watanzania kama ambavyo mnafahamu tulianza uteuzi wa wagombea ikiwemo jimbo la Shinyanga mjini na majimbo mengine ya kanda ya Serengeti ambayo inamajimbo 24 na Mikoa 3 na baadhi ya wagombea wetu waliteuliwa na kuna mamia ya mamia kama siyo maelfu ya wagombea wetu wajateuliwa katika mchakato huu, na kama mnavyofahamu uchaguzi unaendeshwa kwa kanuni za uchaguzi wa serikali za mitaa za 2024, mpaka sasa asilimia 90 ya wagombea wetu mpaka 95 walioenguliwa hawajaenguliwa kwa sababu za kikanuni lakini kama haitoshi hata wale ambao waliteuliwa wamewekewa pingamizi kinyume na kanuni za uchaguzi wa serikali za mitaa”amesema Mnyawami


CHADEMA imechukua hatua za kukata rufaa juu ya uamuzi huo na kueleza kuwa timu za kanda zimepelekwa maeneo ya Maswa, Bariadi, Itilima, na Serengeti kusaidia wagombea wake kuandaa rufaa.
Mnyawami amesisitiza kuwa licha ya changamoto zinazowakumba, chama hicho kimejizatiti kufuata taratibu zote za kikanuni ili kuhakikisha haki inatendeka.

Mnyawami pia ametoa wito kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), kuwarudisha wagombea wa CHADEMA na vyama vingine waliotimuliwa na kuwaruhusu kushiriki kikamilifu katika uchaguzi ujao ili wananchi waweze kuwachagua viongozi wanaowataka.

HABARI ZA KINA :
“Leo tuna timu imeenda Maswa, kuna timu Imeenda Bariadi, Kuna timu imeenda Itilima, kuna timu imeenda jimbo la Serengeti kusaidia na tupo hapa kwenye awamu ya kuandika rufaa pamoja na mizengwe yote ambayo inafanyika hatutakata tama kufuata taratibu zote za kikanuni kuhakikisha wagombea wetu wote wanaandika rufaa na wanaziwasilisha kwa mwenyekiti wa kamati ya rufaa”

1731405708998.jpeg

Picha maktaba : Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Bariadi Ndugu Adrian Jungu


“Pamoja na kufuata hatua zote tunamtaka waziri wa TAMISEMI Nchengelwa kuwarejesha wagombea wa CHADEMA na vyama vingine wote warudi twende kwa wananchi tukaombe kura na wananchi wapate fursa ya kuchangua viongozi wanaowataka”. Amesema Mnyawami

Kwa upande wake, Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Shinyanga, Agatha Mamunya, pamoja na Katibu wa CHADEMA jimbo la Shinyanga mjini, Sebastian Polepole, wameunga mkono hoja hiyo, wakisisitiza umuhimu wa wagombea walioenguliwa kurejeshwa.

CHADEMA wamedai kuwa utaratibu unaotumika kuwaengua wagombea hao si wa haki, ambapo wameisisitiza serikali kuheshimu misingi ya kidemokrasia kwa kutoa nafasi kwa wagombea wote kuwania nafasi walizoomba.

Misalaba Media, imezungumza na baadhi ya wagombea wa CHADEMA walioenguliwa wameeleza kusikitishwa na uamuzi wa kuwaondoa katika kinyang’anyiro hicho.

Wamesema kuwa uamuzi huo unaenda kinyume na kanuni za uchaguzi na kuiomba serikali kuwaangalia kwa haki na kurudisha majina yao ili waweze kushiriki katika uchaguzi wa Novemba 27, 2024.

Misalaba Media inaendelea kuwasiliana na wahusika ili kupata ufafanuzi zaidi kuhusu madai ya kuenguliwa kwa wagombea hao
Source : Misalaba Media
 
12 November 2024
Singida, Tanzania

MAPINGAMIZI YA WAGOMBEA WA CHADEMA YAMEWEKWA NA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI NA SI WAGOMBEA WA CCM?


View: https://m.youtube.com/watch?v=B-LZcKOzQAM
mwenyekiti wa CHADEMA Singida mjini tumeambiwa na wasimamizi wa uchaguzi ambao ni watendai wa serikali kuwa tunapoteza mafuta na muda kukata rufaa
 
Moja ya Sifa kuu ya Tundu Lissu ni Mkweli

Alisema CHADEMA bado haijawa na Wagombea wa kutosha kuikabili CCM

Hiyo imejionesha kwenye wilaya karibu zote

Mfano mzuri ni Kilosa Vijiji 138 Chadema ina wagombea 70 tu

Vitongoji zaidi ya 800 lakini Chadema ina wagombea 200 na ushee tu

Safari bado ni ndefu 🐼
Na hao Wachache tunawakata ili tupite bila kupingwa sio!!!badala ya kuulea upinzani utusaidie kumulika maovu ndani ya chama chetu au sio!!?
 
12 November 2024
Dodoma, Tanzania

Mwenyekiti wa CHADEMA Dodoma kamanda Aisha Madoga aiva CCM uchaguzi uchafuzi 2024


View: https://m.youtube.com/watch?v=_XZijzUd0oA

Mwenyekiti mpya wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoa wa Dodoma, kamanda Aisha Madoga, ameahidi kupambana kuhakikisha wagombea wa CHADEMA walioenguliwa uchaguzi wa serikali za mitaa 2024 wanarejeshwa kwenye mbio kukabiliana na CCM tarehe 27 November 2024..
 
Picha maktaba : Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Tunduma, Mariam Chaurembo akisisitiza jambo ktk majukumu yake ya kawaida kama DED
1731360908038.jpeg
12 November 2024

DED MARIAM CHAUREMBO MSIMAMIZI WA UCHAGUZI AWAJIBU CHADEMA TUNDUMA

Msimamizi wa uchaguzi ambaye pia ni mkurugenzi wa halmashauri DED Tunduma ajitokeza na kujibu uenguliwaji na uteuzi wa wagombea wa CHADEMA Tunduma

View: https://m.youtube.com/watch?v=wEZh1ma4TUo
 
Moja ya Sifa kuu ya Tundu Lissu ni Mkweli

Alisema CHADEMA bado haijawa na Wagombea wa kutosha kuikabili CCM

Hiyo imejionesha kwenye wilaya karibu zote

Mfano mzuri ni Kilosa Vijiji 138 Chadema ina wagombea 70 tu

Vitongoji zaidi ya 800 lakini Chadema ina wagombea 200 na ushee tu

Safari bado ni ndefu 🐼
yes noted
 
13 November 2024

TUNDU LISSU ATOA UFAFANUZI YA KAULI YA KATIBU MKUU WA CCM DR. NCHIMBI NA MWONGOZO MPYA ALIOTOA WAZIRI MOHAMED MCHENGERWA


View: https://m.youtube.com/watch?v=T4AIOZK3yfA

Makamu mwenyekiti wa CHADEMA bara mheshimiwa Tundu Lissu anakazia kuwa kauli za vigogo wawili wa CCM mmoja katibu mkuu wa CCM mwingine waziri wa serikali ya CCM ni ushahidi tosha kuwa hakuna sheria au taratibu zinazofutwa bali matamko ya viongozi wa CCM kama rais Samia Hassan mwenyekiti wa CCM na katibu
 
09 November 2024
Berege, Mpwapwa
Dodoma
Tanzania

WAKILI MSOMI AENGULIWA KUGOMBEA NAFASI YA UENYEKITI WA KIJIJI DODOMA

View: https://m.youtube.com/watch?v=Py6xouFmbys

Wakili wa mahakama kuu mwanasheria msomi Deogratias Cosmas Mahinyila ampa somo msimamizi wa uchaguzi msaidizi awasilisha mapingamizi / mtendaji ajikanyaga

Hekaheka hiyo inafuatia mgombea wa CHADEMA kwa nafasi ya uenyekiti wa kijiji cha Berege wilaya ya Mpwapwa ambapo mgombea uenyekiti wa kijiji cha Berege kupitia CHADEMA Wakili wa mahakama kuu mwanasheria msomi Deogratias Cosmas Mahinyila alienguliwa ...



Baada ya Hukumu leo 15 November 2024
View: https://m.youtube.com/watch?v=g5wiXSnNZd8
 
Moja ya Sifa kuu ya Tundu Lissu ni Mkweli

Alisema CHADEMA bado haijawa na Wagombea wa kutosha kuikabili CCM

Hiyo imejionesha kwenye wilaya karibu zote

Mfano mzuri ni Kilosa Vijiji 138 Chadema ina wagombea 70 tu

Vitongoji zaidi ya 800 lakini Chadema ina wagombea 200 na ushee tu

Safari bado ni ndefu 🐼

Tatizo hili ni la pili hata wangeweka 100% na wakaenguliwa 100% tatizo liko palepale. Hao waliowekwa karibu wote wameenguliwa sasa hili ni tatizo la idadi ya wagombea na hujuma za demokrasia
 
Moja ya Sifa kuu ya Tundu Lissu ni Mkweli

Alisema CHADEMA bado haijawa na Wagombea wa kutosha kuikabili CCM

Hiyo imejionesha kwenye wilaya karibu zote

Mfano mzuri ni Kilosa Vijiji 138 Chadema ina wagombea 70 tu

Vitongoji zaidi ya 800 lakini Chadema ina wagombea 200 na ushee tu

Safari bado ni ndefu 🐼
Hoja si idadi ya wagombea, hoja iliyopo mezani ni hii engua engua ya wagombea wa Upinzani Je imekidhi Sheria na Kanuni za uchaguzi serikali za mitaa 2024?

Je wagombea wa upinzani hawana uwezo wa kujaza hizo form kwa usahihi na kufanya 90% kuwa ni makosa?
 


Yanayotokea Tanzania uchaguzi wa TAMISEMI yanafanana kabisa na yaliyotokea chini ya utawala wa chama dola kongwe katika uchaguzi mkuu wa Mozambique uliofanyika tarehe 9 Oktoba 2024 : RC DC DAS DED na Kamati za Halmashauri za wilaya za CCM ndiyo wanapokea maelekezo kwenda kwa wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi. Je hizi mbinu za CCM na FRELIMO ya Msumbiji kufanya uchafuzi wa mchakato wa uchaguzi ni zipi:

Kigogo wa Tume ya Uchaguzi Mozambique ktk mahojiano exclusive - Mchakato na Uchaguzi uligubikwa na uchafuzi


View: https://m.youtube.com/watch?v=2B_xQtuZLW8

Naibu mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Bw. Fernando Mazanga asema uchafuzi wa uchaguzi na uchafuzi wa chakato wa uchaguzi, Tume haiwezi kusema nani alishinda..

Kwanza kiukweli kulikuwa na Tume mbili zinazosimamia mchakato, moja ni Tume ya Uchaguzi halisi isiyo na meno, na nyingine ni Tume Kificho ya Watu Wachache wa Frelimo waliokuwa na meno, rasilimali fedha na maamuzi ya kupika matokeo asema Fernando Mazanga

Alipoulizwa kuhusu Tume Kificho ya Watu wachache wa Frelimo ikifanyaje kufanya uchachuzi wa mchakato wa mzima wa matayarisho ya uchaguzi, uandikishaji na upigaji kura siku ya uchaguzi tarehe 9 Oktoba 2024 kigogo Fernado Mazanga alifunguka ...

Tume ya Ukweli ya uchaguzi ilinyimwa fedha na wizara ya fedha ya Mozambique na hata pesa zikipotolewa kidogo zote zikitumika makao makuu ya tume huku mikoani, wilayani na mitaani wasimamizi na wasimamizi uchaguzi walikuwa hoi si kifedha bali hata kimafunzo ya kuwapa uwezo wa kuandikisha wapiga kura, uteuzi na rufaa za mapingamizi.

Wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi walikuwa hawaelewi kanuni, sheria na miongozo ya kufanikisha uchaguzi ulio wa kiwango cha kukubalika ni huru, usiopendelea upande wowote na wakuweza kutoa matokeo sahihi ya kura zilizopigwa na mgombea yupi kazoa kura halali.

Fernando Mazanga anaongeza kuwa kutokana na Tume halisi kunyimwa uwezo wa kila aina, Tume kificho ya FRELIMO iliingia kazi kutangaza idadi ya watu waliojiandikisha ambayo haiwiani na takwimu za sensa ya taifa ya Mozambique ikiyofanyika 2023.

Wasimamizi wakuu na wasimamizi wasaidizi katika majimbo na wilaya walikosa kuwa na idadi za kulinganisha idadi ya watu katika maeneo yao ya majimbo, wilaya, kata na mitaa hivyo kura za ziada ya kuongezwa na FRELIMO ziliweza kutangazwa.

Huku wananchi hawafahamu idadi ya watu rasmo ktk maeneo yao kama sensa ya taifa ilivyokuwa ikionesha eneo kwa eneo, kijiji kwa kijiji, mtaa na kata.

Ingawa vyama makini vya upinzani zilipiga kelele kuwa idadi ya kuandikishwa watu katika sensa hailingani idadi ya wapiga kura watarajiwa na kura za matokeo yaliyotangazwa zimezidi kwa mbali idadi ya watu katika ripoti za sensa za taifa .

Wananchi baada ya kustuliwa kuhusu wafanye rejea za idadi ya watu na idadi ya wapiga kura wakabaini uchafuzi uliofanyika na kupelekea maandamano nchini Msumbiji kupinga matokeo yaliyotangazwa.

Mahakama ya Kikatiba iliyopewa mamlaka kusikiliza mapingamizi ya matokeo, imeomba tume ya uchaguzi ya taifa iwasilishe nyaraka ili ukaguzi ufanyike. Tume ilipewa siku 8 iwe imewasilisha nyaraka zote za uchaguzi uliofanyika 9 Oktoba 2024 zipitiwe na kufanyiwa ukaguzi wa kina.

Bw. Fernando Mazanga Naibu mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi nchini Mozambique anasema siku 8 zimepita na zinayosha kuwasilisha nyaraka zote zilizohifadhiwa katika Ofisi za Majimbo na Wilaya.

Lakini pamoja na nyarala hizo kukufanywa sehemu, Mahakama ya Kikatiba hawajapewa makaratasi hayo ya kura na rejister za wapiga kura leo.

Inasemekana serikali inalaumu kutofika makaratasi hayo kutokana na vurugu za maandamano, lakini kigogo huyo Fernando Maganza anatillia shaka sababu hiyo kuwa vurugu zimezuia katatasi hizo kufika mji mkuu wa Mozambique Maputo.

Pengine Tume fiche ya Uchaguzi ya FRELIMO imeshikilia makaratasi hayo katika kituo salama (safe house) ikiyapitia matokeo hayo ya uchafuzi wa uchaguzi na kujiuliza wayawasilishe au la. Pia wanatafuta njia nyingine ya kuingilia mchakato wa Mahakama ya Kikatiba n.k n.k kujiokoa kutoka skandali hilo zito.

Fernando Mazanga alipoulizwa kama matokeo yanaweza kufutwa kutokana na uchafuzi wa wazi wa mchakato na uchaguzi sawia, kigogo huyo mzalendo wa Tume Halisi ya Uchaguzi anasema hawezi kutoa mawazo yake sasa kwa kuwa yeye ni mtu wa ndani kabisa katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi Mozambique.

Hivyo anaiachie Mahakama ya Kikatiba ibebe majukumu yake kuhakiki na kutoa hukumu sahihi baada ya kujiridhisha na ushahidi wote anahitimisha naibu mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Taifa nchi Mozambique Bw. Fernado Mazanga.

Muito Abrigado kwa kutusikiliza
Source : DW Português para África : DW Kireno Africa

More info :
Maputo, Mozambique
Mahakama ya Katiba Mozambique yataka wasimamizi wa uchafuzi wa uchaguzi kujitetea madudu ya wazi yaliyojitokeza katika uchaguzi wa 9 Oktoba 2024 nchini Mozambique

1731692635573.jpeg

Picha : Waheshimiwa majaji wa Mahakama ya Kikatiba Mozambique
 

Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma atoa maelekezo ya uchaguzi wa serikali za mitaa​

thumb_4867_800x420_0_0_auto.jpg
Imewekwa tarehe: September 28th, 2024
Na. Dennis Gondwe, DODOMA

16 November 2024
Dodoma, Tanzania

PATASHIKA; CHADEMA DODOMA WALIOENGULIWA WAKWAMA KWENYE RUFAA, POLISI WAZUNGUKIA, VILIO VYATANDA



View: https://m.youtube.com/watch?v=xzEix_7kRU0
Mfano Mgombea huyo wa Amosi Sylvester Lyaki mkazi wa mtaa Kisasa Medeli Dodoma amekuwa kwa miaka 5 mjumbe wa serikali ya mtaa wa Kisasa Medeli toka mwaka 2019 hadi 19 October 2024... lakini yeye na wagombea wa Chadema rufani zao...
 
Moja ya Sifa kuu ya Tundu Lissu ni Mkweli

Alisema CHADEMA bado haijawa na Wagombea wa kutosha kuikabili CCM

Hiyo imejionesha kwenye wilaya karibu zote

Mfano mzuri ni Kilosa Vijiji 138 Chadema ina wagombea 70 tu

Vitongoji zaidi ya 800 lakini Chadema ina wagombea 200 na ushee tu

Safari bado ni ndefu 🐼

Mnafiki wewe
 
Back
Top Bottom