Tungekufa ajali mbaya sana kitaifa daraja walipokufa Wajapan pale Moshi kwa ajili ya trafiki kupafanya mradi wa taifa wa kutolea faini!

Tungekufa ajali mbaya sana kitaifa daraja walipokufa Wajapan pale Moshi kwa ajili ya trafiki kupafanya mradi wa taifa wa kutolea faini!

Ni sehemu iko katika barabara ya Moshi kwenda Arusha. Kuna bonde kubwa na daraja na huko nyuma Wajapan walikufa kwa ajali mbaya na hata pamejengwa mnara wa kumbukumbu kwa ajili yao. Kutokana na uwepo wa daraja hili na bonde pamefanywa kuwa sehemu ambayo huruhusiwi ku-overtake na sasa trafiki wamepafanya mradi wa kutoza watu faini.

Trafiki wanakaaa upande wa kuelekea Moshi, wengine wanajificha katikati, na wengine wanakaaa upande wa kuelekea Arusha wa daraja. Ni sehemu ndefu sana katika sehemu hii ambayo huruhusiwi ku-overtake, japo upande wa kuelekea Moshi kuna sehemu ambayo barabara imenyooka sana na unaweza kuona mbali na ku-overtake bila hatari, bado huruhusiwi ku-overtake.

Uki-overtake sehemu hii basi utakuta trafiki wanakusubiri mbele upigwe faini kwa kuwa wapo waliojificha na kazi yao ni kuangalia gari inayo overtake na kuwaambia wenzao. Matokeo ni kwamba mara kadhaa sehemu hii inakuwa na misururu mirefu sana ya magari pande zote mbili, hasa kukiwa na lori linaloenda taratibu.

Sasa wiki iliyopita tulikuwa na msururu mrefu sana wa magari kuelekea upande wa Arusha. Mbele yetu kulikuwa na lori la mafuta. Tukawa tunalifuata nyuma taratibu. Tulivuka daraja na kuanza kupanda mlima kuelelekea Arusha. Ghafla lile lori lilionekana kuanza kuishiwa nguvu, likitoa moshi mwingi. Likaanza kurudi nyuma na kukawa na honi nyingi sana za kupanick toka magari yaliyokuwa nyuma. Upande wa pili kulikuwa na magari mengi tu na hivyo wote tuliokuwa nyuma ya hili lori hatukuwa na sehemu ya kukimbilia zaidi ya kupiga honi! Mbele ya uso wangu nikaona ajali mbaya sana inakuja!

Dereva wa lori kwa namna fulani alifanikiwa kulisimamisha lori lake, na baada ya kupiga less (revs) nyingi lilianza kwenda mbele tena.

Ilinifanya niwaze sana, kwa kuwa kama dereva wa lile lori asingefaniiwa kulidhidhibiti, lingerudi nyuma na kufagia magari mengi sana kuelekea mtoni! Na katika watu kujaribu kulikwepa kungekuwa na kugongana kwingi sana! Na hata nikawaza vipi lile lori lingeanguka na kumwaga mafuta na moto kuwaka? Basi kwa kuwa ile sehemu hakuna sehemu ya kukimbili, magari yote yaliyokuwa nyuma ya lile lori yangewaka moto!

Hapo ndipo nikafikiria, je uwepo wa polisi hizi sehemu tatu za barabara kweli unalenga kusaidia au kupata fedha? Serikali ya Tanzania imeona suluhisho ya uhatari wa sehemu hii ni kuweka askari ili kupiga faini watu wanao overtake hata kama mbele yako ni lori la mafuta linaloenda spidi ya 20km/hr?

Kama serikali imeliona eneo hili kuwa la hatari sana, kwa nini haijaweka climbing lanes pande zote mbili za daraja? Au serikali itaua mradi wa kupiga watu faini? Nafasi ya climbing lanes ipo ya kutosha, kwa nini hawajaweka? Je serikali inaona kuweka miundo mbinu ya kuzuia janga baya sehemu kama hii si jambo la haraka kuliko kujenga fly-over Dar es Salaam? Gharama ya kuweka climbing lanes pande zote mbili za hili daraja ni kubwa kiasi gani kiasi kwamba serikali isifanye hivyo kwa haraka? Je serikali inasubiri hadi ajali mbaya itokeee ndipo iamshwe kujenga climbing lanes?

Eneo hili kwa wakati wote linakuwa na askari wa trafiki karibu 20, ambao kama climbing lanes zingewekwa wangepelekwa sehemu nyingine kuangalia usalama badala ya kukaa hapa kutwa nzima wakisubiri watu wa kupiga faini kwa ku-overtake au kwenda zaidi ya 50km/hr!

Kuna maeneo hatarishi sana katika barabara zetu ambayo yameua sana na suluhisho lake ni kuweka climbing lanes. Hili lilifanywa katika barabara ya Dar- es-Salaam - Morogoro ambayo ilikuwa inaua kila siku na ajali zikakoma baada ya kuweka climbing lanes. Sehemu hii ya Moshi, na ile ya pale mlima wa Mbalizi Mbeya na nyinginezo ni maeneo hatarishi sana na suluhisho lake ni rahisi sana kuweka climbing lanes, lakini naona kama Tanroads wako busy kujenga flyover Dar es Salaam kwa kuwa zitaitwa kwa majina yao, bila kujali usalama wa raia katika maeneo hatarishi sana!
wanasubiri rambirambi
 
Jaman tuache uchawi, yaan pale kwa Sadala wasiwepo askar ili tuumizane?
Mleta Mada ww ni mwepes Sanaa. Sasa ulitaka TRAFFIC aende akaizuie gar isirud nyuma?TRAFFIC piga mikeka hawa watu wazembe
 
Jaman tuache uchawi, yaan pale kwa Sadala wasiwepo askar ili tuumizane?
Mleta Mada ww ni mwepes Sanaa. Sasa ulitaka TRAFFIC aende akaizuie gar isirud nyuma?TRAFFIC piga mikeka hawa watu wazembe

Nimesema kuna watu humu ndani mnachangia lakini sio madereva. Ninachosema ni kwamba, kuweka trafiki pale na kusababisha magari yawe yanapanda kwa msururu ni hatari sana, kama ambavyo ilivyotaka kututokea. Pili nimesema upande wa huku moshi ile solid line imerefushwa sana pasipo sababu za msingi. Tatu nikasema, kama serikali inaona lile ni eneo hatari sana panapaswa kuwa na zaidi ya trafiki 20 kila siku, basi waweke climbing lanes. Kumbuka sababu za kuweka trafiki pale ni kuzuia ku-overtake na hiyo 50km/hr. Ukiweka climbing lanes unaondoa vyote viwili na kufanya eneo liwe salama sana kwa magari.

Na ukiniuliza nitakuambia bora kuchelewesha SGR kwa mwezi mmoja ili tuweke climbing lanes pale.
 
wanasubiri rambirambi
Na kutangaza kuwa serikali itanunua majeneza, kutembelea majeruhi hospiali na kusema nakupa laki tano. Yaani kuna watu wamefanya ajali kuwa fursa ya kiki za kisiasa. Ni kama sehemu wanazojua ni hatari wanaacha makusudi kushughulikia!
 
Hali kama hiyo iliwahi kunikuta maeneo ya Vigwaza mizani. Ukiwa unaelekea Morogoro baada ya mizani kuna mlima mkali na hairuhusiwi kuovertake. Mara nyingi magari yenye uzito mkubwa hupanda kwa shida sana.
Sasa siku moja nimeongozana na lori na nimempa nafasi ya kutosha. Nikaanza kuona lori linatoa moshi mwingi na baadaye akaanza kurudi nyuma. Kuona hatari ile nikaingia kulia kumwepa na bahati nzuri hakukuwa na gari linashuka. Dereva alifanikiwa kusimamisha lori na baadaye akapiga race chuma ikakubali. Wakati haya yanatendeka maaskari wanaokaa pale mlimani wameshanipiga mkono kwa kuovertake na wanataka nilipe fain. Nikawauliza kama wameona kilichokuwa kinafanyika pale wakadai wao hawaelewi nilipe fine. Yule mwenye lori akatupita (nilimwelewa maana angejifanya kunitetea angeng'ang'aniwa kwa kuendesha gari bovu). Kuna mshikaji alikuwa nyuma akaja akawaeleza jamaa wakagoma. Ikabidi nichukue cheti nitembee maana niliona naendelea kupoteza muda pale.
Huna hobby ya kubishana wewe.

Hapo hadi wanasheria wangepigiwa simu.

Kwanza nisingesimama.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sheria inasemaje to keep distance,endapo wewe nidereva umepita chuo!!!kwasababu stori yako hujazungumzia ulikua umbali UPI...siungani na polisi ,maranyingisana unaweza kuta magari yanapandisha mlima nafasi yameachiana sentmita 30.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hata kama umeacha mita 100. Gari linalorudi nyuma halina guarantee ya kusimamia wapi. Linaweza likakukuta na kukupita vilevile.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama unanijibu mimi inaonekana eidha wewe sio dereva au hujui kutumia akili yako. Wewe tunakuambia lori ilishindwa kupanda unaleta mambo ya kujua eti ulikuwa distance gani? Sasa kama tungekuwa karibu si ningeweka thread ya kugongwa hapa? Kwani hiyo distance kati ya gari kwa gari ni kwa ajili ya nafasi ya gari kurudi nyuma ikishindwa kupanda au nafasi ya gari ya nyuma kuweza kusimama bila kuigonga gari ya mbele ikiwa kuna emergency. Mnajifanya wajuaji wakati hamna kitu. Ovyo kabisa.
Ulikua unanijibu Mimi ,kama ndiyo nakupa pole ,naona unajibu kama bado umeshika usukani nalori linarudi vile

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huna hobby ya kubishana wewe.

Hapo hadi wanasheria wangepigiwa simu.Kwanza nisingesimama.Sent using Jamii Forums mobile app

Mimi ninachoona ni kwamba kwa akili ya uongozi wa Tanzania na Trafiki, suluhisho la kupunguza ajali nchini ni kuweka askari wa trafiki kila baada ya mita mia katika barabara zote kuu za Tanzania! Huko ndiko kufikiri kwao.
 
Ulikua unanijibu Mimi ,kama ndiyo nakupa pole ,naona unajibu kama bado umeshika usukani nalori linarudi vile

Sent using Jamii Forums mobile app
Ningetamani siku moja wewe ndio ikutokee ukiwa na familia yako na lori linarudi nyuma na huna kwa kukimbilia kwa kuwa kuna msururu wa magari nyuma yako unaosababishwa na uwepo wa trafiki kukamata overtaking, lakini ukiwa hiyo distance ya sheria unayoisema, tuone kama itakuokoa! Labda itasaidia kukuhekimisha, kama hatutakutoa kwenye gari yako ukiwa mifupa myeusi iliyoungua inayotoa tabasamu la kutisha.
 
Ni sehemu iko katika barabara ya Moshi kwenda Arusha. Kuna bonde kubwa na daraja na huko nyuma Wajapan walikufa kwa ajali mbaya na hata pamejengwa mnara wa kumbukumbu kwa ajili yao. Kutokana na uwepo wa daraja hili na bonde pamefanywa kuwa sehemu ambayo huruhusiwi ku-overtake na sasa trafiki wamepafanya mradi wa kutoza watu faini.

Trafiki wanakaaa upande wa kuelekea Moshi, wengine wanajificha katikati, na wengine wanakaaa upande wa kuelekea Arusha wa daraja. Ni sehemu ndefu sana katika sehemu hii ambayo huruhusiwi ku-overtake, japo upande wa kuelekea Moshi kuna sehemu ambayo barabara imenyooka sana na unaweza kuona mbali na ku-overtake bila hatari, bado huruhusiwi ku-overtake.

Uki-overtake sehemu hii basi utakuta trafiki wanakusubiri mbele upigwe faini kwa kuwa wapo waliojificha na kazi yao ni kuangalia gari inayo overtake na kuwaambia wenzao. Matokeo ni kwamba mara kadhaa sehemu hii inakuwa na misururu mirefu sana ya magari pande zote mbili, hasa kukiwa na lori linaloenda taratibu.

Sasa wiki iliyopita tulikuwa na msururu mrefu sana wa magari kuelekea upande wa Arusha. Mbele yetu kulikuwa na lori la mafuta. Tukawa tunalifuata nyuma taratibu. Tulivuka daraja na kuanza kupanda mlima kuelelekea Arusha. Ghafla lile lori lilionekana kuanza kuishiwa nguvu, likitoa moshi mwingi. Likaanza kurudi nyuma na kukawa na honi nyingi sana za kupanick toka magari yaliyokuwa nyuma. Upande wa pili kulikuwa na magari mengi tu na hivyo wote tuliokuwa nyuma ya hili lori hatukuwa na sehemu ya kukimbilia zaidi ya kupiga honi! Mbele ya uso wangu nikaona ajali mbaya sana inakuja!

Dereva wa lori kwa namna fulani alifanikiwa kulisimamisha lori lake, na baada ya kupiga less (revs) nyingi lilianza kwenda mbele tena.

Ilinifanya niwaze sana, kwa kuwa kama dereva wa lile lori asingefaniiwa kulidhidhibiti, lingerudi nyuma na kufagia magari mengi sana kuelekea mtoni! Na katika watu kujaribu kulikwepa kungekuwa na kugongana kwingi sana! Na hata nikawaza vipi lile lori lingeanguka na kumwaga mafuta na moto kuwaka? Basi kwa kuwa ile sehemu hakuna sehemu ya kukimbili, magari yote yaliyokuwa nyuma ya lile lori yangewaka moto!

Hapo ndipo nikafikiria, je uwepo wa polisi hizi sehemu tatu za barabara kweli unalenga kusaidia au kupata fedha? Serikali ya Tanzania imeona suluhisho ya uhatari wa sehemu hii ni kuweka askari ili kupiga faini watu wanao overtake hata kama mbele yako ni lori la mafuta linaloenda spidi ya 20km/hr?

Kama serikali imeliona eneo hili kuwa la hatari sana, kwa nini haijaweka climbing lanes pande zote mbili za daraja? Au serikali itaua mradi wa kupiga watu faini? Nafasi ya climbing lanes ipo ya kutosha, kwa nini hawajaweka? Je serikali inaona kuweka miundo mbinu ya kuzuia janga baya sehemu kama hii si jambo la haraka kuliko kujenga fly-over Dar es Salaam? Gharama ya kuweka climbing lanes pande zote mbili za hili daraja ni kubwa kiasi gani kiasi kwamba serikali isifanye hivyo kwa haraka? Je serikali inasubiri hadi ajali mbaya itokeee ndipo iamshwe kujenga climbing lanes?

Eneo hili kwa wakati wote linakuwa na askari wa trafiki karibu 20, ambao kama climbing lanes zingewekwa wangepelekwa sehemu nyingine kuangalia usalama badala ya kukaa hapa kutwa nzima wakisubiri watu wa kupiga faini kwa ku-overtake au kwenda zaidi ya 50km/hr!

Kuna maeneo hatarishi sana katika barabara zetu ambayo yameua sana na suluhisho lake ni kuweka climbing lanes. Hili lilifanywa katika barabara ya Dar- es-Salaam - Morogoro ambayo ilikuwa inaua kila siku na ajali zikakoma baada ya kuweka climbing lanes. Sehemu hii ya Moshi, na ile ya pale mlima wa Mbalizi Mbeya na nyinginezo ni maeneo hatarishi sana na suluhisho lake ni rahisi sana kuweka climbing lanes, lakini naona kama Tanroads wako busy kujenga flyover Dar es Salaam kwa kuwa zitaitwa kwa majina yao, bila kujali usalama wa raia katika maeneo hatarishi sana!
kwa sadala au ganda la ndizi
 
Back
Top Bottom