Tungekuwa tunatumia akili, tungeisapoti timu ya Biashara

Tungekuwa tunatumia akili, tungeisapoti timu ya Biashara

Pumbavu zao hiyo ni timu ya ccm wacha ife kabisa sasa bado namungo
 
Kwa bahati mbaya sana akili zetu tunazitumia kukimbizana na CHADEMA kila kukicha.

Kwa MTU mwenye akili angetumia fursa ya Biashara United kuitanganza Tanzania! Tungeweza kuitangaza nchi hii kwa bei chee sana.

Hivi unawezaje kununua ndege kwa pesa Cash kisha ushindwe kuipa support Biashara United ambao ni Ambassadors wazuri sana kuitangaza nchi kimataifa??

Nani anajua kuwa huenda Vijana wa biashara wangeweza kuonwa huko Na timu nyingine? Tungeitangaza Tanzania, tungeingizia nchi fedha, tungezalisha akina Samantha wengine wengi.

Tunasubiri washinde kisha tuwapokee kwa Kamera za TBC huku tukisema ni juhudi za serikali....jinga kabisa!

Hivi tuna Wizara? Ni kweli Tanzania imeshindwa kuwasaidia hawa Wawakilishi? Wakitoka Nje ya nchi wawe ni Simba, Azam, Yanga au Biashara etc hawatambuliki kwa majina yao Bali kwa jina la nchi! Tanzania.

Hivi TFF kazi yao ni nini? Nimeumia sana Biashara kukosa mchezo wao kwa uzembe wa hali ya juu.

Serikali ya CCM inazidi kuua ndoto za vijana aiseeee
Kuna mifano hai tangia FAT mpaka imekuwa TFF hawajawahi kuwaacha Simba au Yanga wakwame kwe kuwakilisha nchi. Uyanga na Usimba umetufikisha hapo
 
Biashara Ni wapumbavu kwenda tu Ethiopia walijivutamwsho wa siku wakafika saa 5 asubuhi alaf saa 10 mechi hawajapata hata muda wa mazoezi.
Upumbavu huohuo wameendelea nao na wakat wanajua wanaenda safar ndefu mwsho wa siku wamekwama njian uwanjan hawajatokea na wametolewa kwenye mashindano huo ni upuuzi wao wenyewe
 
Biashara nayo haina malengo waache tu soka huenda wanapenda kucheza gem za ndan tu sijui walianzisha tim ya nn wanapata nafas kucheza kimataifa wanaleta uzembe
Serikal yetu nayo hasa wizara ya michezo tumlaumu wazir ameshindwa kuwafanyia connection biashara na atcl sas wazir wa michezo kaz yake sijui nin amebumbwa tu hana mchango wowote
 
CAF wameipiga fani timu ya Biashara $20,000 na kutoshiliki mashindano miaka 2.
 
Kwa bahati mbaya sana akili zetu tunazitumia kukimbizana na CHADEMA kila kukicha.

Kwa MTU mwenye akili angetumia fursa ya Biashara United kuitanganza Tanzania! Tungeweza kuitangaza nchi hii kwa bei chee sana.

Hivi unawezaje kununua ndege kwa pesa Cash kisha ushindwe kuipa support Biashara United ambao ni Ambassadors wazuri sana kuitangaza nchi kimataifa??

Nani anajua kuwa huenda Vijana wa biashara wangeweza kuonwa huko Na timu nyingine? Tungeitangaza Tanzania, tungeingizia nchi fedha, tungezalisha akina Samantha wengine wengi.

Tunasubiri washinde kisha tuwapokee kwa Kamera za TBC huku tukisema ni juhudi za serikali....jinga kabisa!

Hivi tuna Wizara? Ni kweli Tanzania imeshindwa kuwasaidia hawa Wawakilishi? Wakitoka Nje ya nchi wawe ni Simba, Azam, Yanga au Biashara etc hawatambuliki kwa majina yao Bali kwa jina la nchi! Tanzania.

Hivi TFF kazi yao ni nini? Nimeumia sana Biashara kukosa mchezo wao kwa uzembe wa hali ya juu.

Serikali ya CCM inazidi kuua ndoto za vijana aiseeee
Mtunwa kwanza anae stahili adhabu ni viongozi wa biashara wenyewe , kwann wao hawakujipangankisaka mdhamini walau wa kuwapa 200M, tangu msimu ulipo isha walikuwa wana fahamu ya kuwa wana paswa kushiriki mashindano ya kimataifa ...

nafikiri baada ya tukio hili sasa ndipo wa Tz tuataanza kuelewa tukimsikia MO akisema anatoa B2 kama gharama za kuendesha club ya simba,
Biashara wale hawaakustahili kushiriki CAF CC.C kwa sababu hawana shekeli na mdhamini pia wa kuwapa shekeli hawana, serikali ilishaku ali kutoa ndege A220 lkn Sudan, sudan kusini na Libya wenyewe hawaku ruhusu anga lao litumike sasa ndege inge pita ardhini ?
 
Hakuna cha maana tunachokiweza zaidi ya porojo na kutishiana ujinga tu.Sekta zote zipo zipo tu.Miaka 10 iliyopita nchi ya libya ilikua kwenye vita vilivyomwondoa Gadaffi madarakani na sehemu kubwa ya nchi iliharibika vibaya,hali ya kiuchumi,usalama,kisiasa vikawa tete hadi kuna wabongo wasio na mbele wala nyuma wakawa wanalaani sana nchi ya libya kuharibiwa ila miaka michache mbele timu ya libya inaweza kuja na ndege Tanzania ikasubiri hadi mwisho wa mechi wakaondoka ila Tanzania ambayo haijawai kua na mgogoro ata wa kijiji toka mwaka 79 baada ya vita vya kagera timu ya nchi yake haiwezi kwenda libya sababu ya ufukara.Hii inaonyesha hatuko serious vyakutosha kwenye mambo yetu.Hii sio hali ya kawaida.
 
Mimi nasema Tff ya Karia Ni hovyoo tu. Kazi yao kubwa Ni kujipendekexa kwa watawala na kuipendelea timu Makolo fulstop.
 
Nasikitishwa sana na hizi taarifa kwanza figisu ilianza pale timu ilipotoka kwenda kwenye mechi yao ya kwanza nje vijana waliondoka siku mmoja kabla ya mechi yaan walifika hata hawakupumzika wakifikia kwenye mazoezi na kuingia uwanjan ila vijana wakapambana na kushinda pia leo wanashindwa kuondoka kabisa na matokeo yake wanapigwa faini na kufungiwa miaka2 na TFF ipo tu na sijui kazi yake ninin ombi langu viongozi wote wa TFF wajiuzuru basi
 
Back
Top Bottom