Tuondokane na kununua Matrekta used kwa bei kubwa yanayokaribiana na bei ya trekta jipya

mimi pia naamini ipo siku nitakuwa mkulima. Tatizo kubwa la nchi yetu tumekuwa nchi ya watumiaji na si wazalishaji, ndiyo maana hata farm machinery zinakuwa so damn expensive. Kila kitu tunategemea toka nje ya nchi hata kama kitu kidogo.
Mkuu kwa kilimo chetu cha Tanzania nakushauri ufanye utafiti kwanza hata kabla hujamua kulima or kununuwa trector nenda physical hilo eneo unalotaka kulima kaangalia changamoto zake zipojee kwani kilimo kina changamoto nyingi unaweza nunua trector na bado usipate chochote utakumbana na matatizi utapelekwa kwenye ardhi isio na rutuba.
 

Asante sana kwa ushauri, nitazingatia hayo mkuu.
 

Mkuu Kirongwe na wanandugu wengineo, ahsanteni kwa mchango wenu. Nami nataka kujiunga na hii team kilimo. Kwa wiki kadhaa nimekua nafanya research ndogo kuhusu tractors tofauti..

Swala moja ambalo nimekosa majibu ya uhakika ni .... Je tractor ya Hoursepower ngapi ni njema zaidi? Je iwe 4WD au 2WD, weka kwenye consideration yako nahitaji ambalo nitalimia watu, nitajilimia na pia kubeba mizigo ikibidi

Natanguliza shukrani
 
New Holland ni uhakika vipi zinaanzia ngapi sasa
 
Naomba muongozo wa trekta ipi nzuri yenye kuweza kulima heka 30 kwa siku
 
Kwa udongo wa aina gani? Yeyote anayekwambia kiasi cha ekari kwa masaa bila kutaja aina ya udongo, hawezi kuwa sahihi. Mi nina uzoefu wa udongo wa mfinyanzi mweusi na kichanga.

Kwa udongo wa mfinyanzi mweusi unaopasuka kiangazi, hakuna trekta ya kulima ekari 30 hata kwa masaa 24 kwa shamba jipya na trekta isiwe chini ya hp 75. Tena mtu asikudanganye trekta za farmtrack wala swalaji.
Kwa udongo wa kichanga peleka hizo farm track na swalaji hata hp. 45 inalima.

Hivyo, jiridhishe kwanza na aina ya udongo.

Kwa wanaolinganisha massey used na farm track, mmmmmhhh!!!!

Car junction pale ubungo plaza, massey used huwezi pata chini ya 45ml. Mpya unazikuta hapo hapo na waweza pata hata chini ya 40, nilishafika pale nina uhakika na nisemayo.

All in all huwezi linganisha massey Used za Uk na new holland, labda kama ni massey za pakistan.

Nimeona mwingine amelinganisha ford 6610 na farm track hp.75 mmmmmmhhh. Hakuna kitu kama hiyo, huyo hiyo ford huwa anaisikia tu, hiyo ford hata kama aliingiza nchini used akaitumia kwa miaka 10, akitaka kuiuza hata muda huu kwa wanaozifahamu bei yake hata haiwezi lingana na farm track iliyokuja mpya na imetumika miaka 3.

Kwa fuel consumption nakubali tractor mpya zinatumia kidogo sana, lakini sio kwa uimara na work load. Bahati nzuri ninalima na wenye hizo tractor mpya, swaraji, farm track na tafe,

Uliza popote massey 375 used za uk yard zote uone jinsi ambavyo bei yake Iko juu sawa na kununua farm track mpya na accessories zake zote, kwa akili yako unadhani wauzaji na wanunuzi hawana akili?
 
Hii biashara ninaipenda mnoo ila ninatamani kupata mkopo wa Massey Ferguson 275 au 290 used.
 
Totally fact siongezi wala sipunguzi
 
Mkuu mie nimekaa na MF 185 pia nina uzoefu na trekta mbali mbali ikiwa ni MF. koboto, john deer, ford sina utaalamu nalo sana ila mie napenda kukushauri ka unauwezo wa kumiliki massey ni nzuri hasa kwa maisha yetu ya kitanzania maana vipuri ni vingi ni ka vile tunapozungumzia toyota kwa upande wa magari,
ila ukiwa na MF375 ni trekta nzuri sana shamba lina uwezo wa kukimbia ka lipo njiani hasa kwa udongo wa kawaida na ule wa kichanga, kingine inategemea we unalima mashamba gani ka ni ya mpunga kuwa na 4WD ni muhimu sana ila ka ni mashamba ya kawaida waweza kuwa na 2WD ambayo ni 75HP ambayo inatosha kabisa kwa matumizi ya kilimo na kubeba mizigo na shughuli nyingine nyingi za kawaida, japo saivi watu wanashauri sana kina newholand na farmtrack ila kwaupande wangu na uzoefu mie siyakubali sana.

Ukitaka trekta zuri unaweza nunua jipya ambalo utakuta lipo complete nikimaanisha ni kwanzia jembe, tela, na baadhi ya vifaa vingine ila ka hela ni ya kawaida unaweza agiza hapo afrika kusini ambayo ni used ila yamefanyiwa marekebisho kabla ya kuuzwa,pia nchi nyingine za ulaya.
 
Totally fact siongezi wala cpunguzi
Mkuu sikupitia post yako vizuri, nakubali mzee unajua mashine, massey 375 ni mashine hatari sana tena sana shamba inakimbia ka hailimi tena inanguvu ya ajabu, mie nilishawahi fuatilia wale jamaa wa Ubungo sema nao wajanja janja wakati mwingine wanakuwa na trekta za kuokota ndani.

MF za ukweli ni hapo Uk ka ulivyowahi sema mie ninajamaa yupo Finland alishawahi taka niuzia chombo ila mifuko
 
Habari kaka, hivi usalama wa hela upoje pindi unapotuma huko nje kununua trekta coz hakuna mtandao maalum kama beforward au SBT. Kuna mtandao unaitwa dumelow wanauza trekta nzuri sana ila naogopa kutuma hela wakapotelea huko huko.
 
Habar mkuu. Unaagiza mtandao gani?
 
Habari kaka,hivi usalama wa hela upoje pindi unapotuma huko nje kununua trekta coz hakuna mtandao maalum kama beforward au sbt. Kuna mtandao unaitwa dumelow wanauza trekta nzuri sana ila naogopa kutuma hela wakapotelea huko huko.
Jamaa wa Dumelow ni mtu wa uhakika na ameshafanya kazi na tafiti Tanzania akiwa Chuo cha Kilimo cha Sokoine Arusha. Ana experience na mazingira ya kilimo ya Tanzania ingawa bei za tractor bei ni ghali kwa £ za UK na yuko na ujuzi wa MF.

John Dumelow
Director
Dumelow International Limited
Email: john@dumelow.co.uk
Tel: +44 118 9487000
Mobile: +44 7957 864043
 
Nafikiri mpaka sasa kuna haja ya kurudisha asante kwa mleta uzi huu, unajua hizi swalaji kwa bonde kama la kilombero sio nzuli Sana'a kwa maaana udongo wa kule ni mgumu sanaa mpaka mmvua inyeshee ndio linaweza Lima japo linatumia mafuta machache, kule kilombero trekta ni jon dear ,Massey ,New holand hizi ndio zinazotamba na kufaulu kwa udongo WA kule, udongo wa kubaigwa ni kama changalawe hivi kwa hiyo ukipeleka newholand kule inakuwa hasar kwa maana ulaji afuta wa swalaji ni mdogo sanaaa,
 
Asante kiongozi nmewasiliana nao last week shida hawana trekta hapa Tanzania lazima nitume hela ndio watume trekta, risk ya kutuma kwa transfer hela kudhulumiwa ni kubwa bora ingekuwa pay pal una uhakika wa refund
 
Asante kiongozi nmewasiliana nao last week shida hawana trekta hapa Tanzania lazima nitume hela ndio watumetrekta risk ya kutuma kwa transfer hela kuzulumiwa ni kubwa bora ingekuwa pay pal unauhakika wa refund
Nakubali kama hujawahi kufanya transfer au kufanya transfer ya kiwango kikubwa hata PayPal kwa kiasi kama pounds 10,000 ni kikubwa. Hii ni kampuni reliable cha msingi ili uwe na amani kitu cha kwanza ni kumuomba reference za watu walionunua kwao hapa Tanzania uongee nao ikiwezekana kuona hizo tractor na ushauri zaidi. Unaweza pia kumwambia kuwa unataka akupe guarantor aliyeko Tanzania atakayemdhamini kuwa tractor yako itafika bila shida. Mara nyingine pia unaweza kulipa advance na makubaliano tractor itakapopakiwa kwenye meli ukatumia documents utalipa kiasi kilichobaki. Kwa nchi za wenzetu unalindwa na sheria kama kampuni iko registered umepewa invoice fanya malipo kupitia bank kama Barclays au Standard Chartered wana jinsi ya kutuma hela na kuweka maelezo muhimu ya mali unayotaka kununua. Option ya pili, kuna agents wa Kitanzania wanatoza fee huko UK kwa mkataba wataweza kununua hiyo tractor na kuituma mara tu ikiwa kwenye meli unawalipa process za kutoa bandarini na ushuru ni zako na hawahusiki na condition ya tractor.
 
Habari kaka,hivi usalama wa hela upoje pindi unapotuma huko nje kununua trekta coz hakuna mtandao maalum kama beforward au sbt. Kuna mtandao unaitwa dumelow wanauza trekta nzuri sana ila naogopa kutuma hela wakapotelea huko huko.
Sina uzoefu wa manunuz kupitia kwao ila hapo ukitaka nunua mpaka utafute wazoefu hasa agent ndo wanaweza kukupa taarifa kamili
 
[emoji101]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…