Tupe stori za msanii uliesoma au kujuana nae kabla ya umaarufu

Tupe stori za msanii uliesoma au kujuana nae kabla ya umaarufu

Singida ndio home

JF-Expert Member
Joined
Feb 23, 2012
Posts
3,188
Reaction score
3,370
Kijiwe niaje!

Ni wengi ambao tunawajua watu wakiwa maarufu ila ni wachache zaidi tunaowajua kabla ya kuwa maarufu aidha kwa kusoma nao, kujuana nao, kucheza nao utotoni, n.k

Binafsi kwa huku Mbeya namkumbuka Izzo Business alikuwa ni mtu moja mchangamfu ila muziki wake alionekana na watu lazima wengi kama muhuni, huku sisi vijana wadogo tukiwa tunatamani angalau kuwa na urafiki nae au kuchana mistari kama yeye, miaka ya 2005 nakumbuka alifanyiwa interview na Mbeya Tv basi ile interview niliirekodi kwenye mkanda wa deki, huo mkanda ulizunguka sana mitaani watu wamcheki Izzo B anavyohojiwa.

Nakumbuka pia alifahamika shule kibao za sekondari kama Sangu tukitoka alikuwa na washkaji zake na vile alivyo staa wa Mbeya tulipenda sana kampani yake.

Wasanii wengine nliowajua kwa juu juu kuna msamiati huyu alieimba yeye na Rapcha "Moto Unaweka" nae wa mbeya alisomaga mbalizi nahisi, ila alikuwa mtoro na mzee wa wida.

Karibuni, muwe mnatia nyama basi, sio unasema tu umesoma au kufahamiana na fulani, jaribu kuelezea kwa undani.
 
2009 naingia Tandika Sec, namkuta Hamisa mobetto yupo form 2 asee yule demu alikua hatulii anapiga misele shule nzima na viswaswadu wenzie.

Siku za dini utamkuta kwa walokole anaimbisha kwaya hadi nilijuaga mlokole kumbe wapi.
 
nil
2010 naingia Tandika sec, namkuta Hamisa mobetto yupo form 2 asee yule demu alikua hatulii anapiga misele shule nzima na viswaswadu wenzie.
Siku za dini utamkuta kwa walokole anaimbisha kwaya hadi nilijuaga mlokole kumbe wapi.
Nilikua apo tandika sec nikaambiwa kasoma hapo nikadhani ni fix tu
 
Mi nimesoma na wengi ila ngoja nianze na hawa wawili.

1. Baghdad
Niko form one pale Azania yeye yuko form 3 jamaa alikua bonge kishenzi halafu peace na alikua anakubali sana na wahuni wakina pengo, mjerumani, max nk...event za shule alikua anapewa maiki anaimba wimbo wake mkubwa ninaokumbuka mpaka kesho ulikuaunaitwa "MAPODA" Msemo aliouchukua kwa masanja mkandamizaji kipindi hiko Ze Comedy imeshika hatamu.

2. Hemedi Chande
Huyu alikua mwanangu kabisa japo si sana, mchizi nakumbuka wakati tunasoma pale form 2 H muda mwingi alikua ana solve Logarithm afu zinamtandika [emoji16][emoji16][emoji16] hakuwa anaringa sana maana kipindi hiko alikuwa njaa kali pale school waarabu waliotamba walikua wanajiita Swaga boi.

Nitaendelea ngoja niload mafaili kwanza .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza kabisa Diamond alinichoma na spoke ya baiskeli akilitaka barafu la sh 20 nililokuwa nikilinyonya Kijitonyama Kisiwani pale uwanja wa mpira miaka ya 1997-99 (sikumbuki the exact year). Tulikuwa tuna kawaida ya kucheza mpira tukitoka mazoezi ya uministrant kigangoni kabla ya kujengwa kanisa lililopo sasa. Mashindano ni kati ya watoto tunaotokea upande wa Knyama kuu na wale wanaoishi kuanzia kijitonyama kisiwani mpaka Tandale huko. Padre alikuwa akitokea parokia ya mwananyamala kuja kusalisha kigangoni.

Haha nikaja kukutana nae kwenye event yake 2014-15 pale Mlimani City keshakuwa maarufu, isingekuwa Ruge na mdogo wangu ambaye yuko THT clue yakina Linah, Rachel, Barnabas, Ditto na wengine asingenikumbuka. Tulikumbushana, tukacheka na tumeshayasahau hayo

Pili Nimeisoma na Feruzi wa Daz Nundas Kizuka TPDF Sec. School Moro hiyo, kama atasoma hii post alikuwa anapenda sana kuniita toto tundu maana nilikuwa napenda sana kuimba nyimbo zao. Tatu mtaani kwetu akahamia Mangwear akiwa chini ya jamaa mmoja anaitwa Evans na mdogo wake Nancy Kijitonyama wakiwa wanapigisha simu (ile ya waya TTCL unatoa hela kwa dakika kama sijasahau ilikuwa 250). Hapo ndipo lilipozaliwa kundi la East Zoo

Prof J usimsahau dogo lako uliyekuwa ukimshauri maliza kwanza shule ndio uingie kwenye sanaa maana wewe ndio ulikuwa rol modal wangu mpaka kwenda kwa MI Kamwamba Upanga kurekodi. Nilifuata ushauri wako na namshukuru Mungu now ni mhasibu na ni muajiriwa, mambo ya bongo flavor nilishatupa kule
Kwa leo tuishie hapo...
 
Kweli wewe umesoma Azaboi, ongeza kwenye list hapo watu wakorofi kama man tapa, Pengo, Zinde hukumkuta wewe, Muddy Kipande nae hukumkuta pia.

Sema pale watu maarufu ni Mohamed yupo Azam pale, Iman Nsamila mpiga picha maarufu wa January Makamba na Samatta, Ben Paul tulisoma nae pale Advance ila yeye hakusoma PCM na kipindi hicho hakua maarufu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nimesoma na huyu dogo anajiita S2kiz . Jina lake halisi ni Salmini Kasim dah aisee tangu dalasa la kwanza mpaka form 4 alikuwa mshkaji wangu kinom uyo fara ninaangalia nae mweleka enzi izo wakina Undertaker, Shawn Michael, Randy Orton. Dah aisee kipindi icho anampenda sana One The Incredible nyimbo zake akina Nikki Mbishi, yaani in short yeye na Lunduno walikuwa damdam na baada ya kumaliza form 4 nimekaa nae sana Mbeya, Uyole geto moja tunalala kwenye kagodolo enzi izo tunauza nae software nilikuwa hata sizifaham ila yeye anazifaham sijui flstudio, antivirus na nyingine mpaka akapata kastationaly flan ivi akaistall iyo flstudio ndio akaendelea kutengeneza izo bit dah aisee maisha haya matam sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom