Tupeane mawazo wapendwa

Tupeane mawazo wapendwa

Nyie watu acheni kuchakachua changieni, tusikie na kutokwa kwenu bana
Maty kuna vitu ambavyo obviously unaweza kuvumilia lakini ndio wife anakung'utwa nje na limjamaa hapo ngumu sana banaa.
 
ni kweli watoto ndo wanapata matatizo na matatizo yapo mengi na wakati mwingine sio lazima mtu awe malaya

Mpendwa uma.....a sio lazima!Baada ya kuchoshana sana huko ndani viburudisho vinaweza kutafutwa..magonjwa yanaweza kupatikana...bahati yako nzuri msipohusiana utaishia kua muuguzi tu!
 
kama mnazungumza kila siku hayaishi je?????? Huoni unahatarisha maisha yako kimsingi!!!
Pia inategemea ni mambo gani,yaani nyie kila siku mnazungumza tu na hamfikii muafaka hapo kuna mmoja atakuwa na tatizo au mmoja anajifanya anajua kuliko mwenzake
 
Huwa najiuliza mara nyingi lakini nakosa jibu zuri, naomba nipate mawazo tofauti tofauti, inaweza kutusaidia wengi wetu.

Wanandoa wengi hasa wa miaka ya sasa, wakikorofishana korofishana baada ya muda wanachoamua ni tuachane bwana kila mtu ataanza nataka niishi kwa amani, nahitaji furaha mimi maisha yenyewe mafupi haya. Ukute hiyo ndoa baba msomi ana kazi nzuri na mama vile vile ndio balaa, kila mtu anasema usinibabaishe ninaweza kumudu maisha.

Hapo kuna watoto mmezaa, lakini kila mtu utamsikia napenda kuishi kwa amani, ni vipi kuhusu watoto? Je hao hawatakiwi kuishi kwa furaha na amani wakiwa na baba na mama? Hivi hamuwezi kukaa mkazungumza na kuelewana ili mlee watoto pamoja badala yake mnafikiria kuachana?

Hivi kuachana ni suluhisho la matatizo yako? Na je ukiachana na mwenzio ndio kusema hutaki kuoa/kuolewa tena? Na je ukioa/olewa halafu huyo mwingine akawa na matatizo pia pengine kuliko uliyoyakimbia mwanzo utaachana nae pia? Au utavumilia?

Tushirikiane kupeana mawazo wandugu

Maty,

Maisha ya ndoa ni mkanganyiko mtupu (confusion). Ukibahatika kuwa na amani basi mshukuru Mungu. Ila kwa uzoefu wangu ni watu wachache sana wanayo hiyo amani.

Kuhusu watoto..Inabidi wahusika wawafikirie sana ila isiwe kikwazo cha kuachana. Ikionekana kwamba hiyo ndoa haiwezekani kwa hali yoyote ile, basi ni vizuri sana watu wakaachana ili waanze upya. There is life after the first or second marriage ingawa huwezi kujua ipi itakuwa nzuri zaidi. Hata hivyo ni bora kumaliza tatizo la leo bila kujali kama kesho utakutana na kubwa zaidi au la. Kung'ang'ania kwenye ndoa ni hatari sana. Aunt yangu aliuawa na mume wake aliyempiga sana ikiwa ni kama siku 3 toka ajifungue. Inauma sana. Kama angewasikiliza wazee waliomwambia kuwa ile ndoa yake ilikuwa haiwezekani kabisa, labda hadi leo angekuwa hai.

Kuhusu maisha baada ya kutengena huwezi kujua kwa sasa. Ila kama biashara hailipi basi funga duka na kufanya kazi nyingine.

Mzee DC
 
Maty,

Hii mvua lazima niwahi kuondoka (kuacha) ofisini kuwahi Kanisa La Mtakatifu Kolbe - Mwenge...

Baadaye aka Later
 
Katika hili naomba tuwe wakweli na wawazi kabisa, mwanamke analaumiwa kwa vile ni mwanamke lakini si ndoa zote zenye matatizo wanawake ndio tatizo, no no no no and big no!!!!!!!!! Nina mfano mzuri kabisa wa mwanaume mwenye gubu lisiloelezeka! Angalia kwanza
Mwanaume form iv
Mwanamke Masters
Mwanaume baba wa nyumbani
Mwanamke anafanya kazi yenye akili
Mwanamke ndo anaendesha familia including yeye mwanaume hadi gari mwanaume kamnunulia na mambo mengine meeeeengi
Lakini cha ajabu na kushangaza mwanaume hajatulia na ana gubu acha tu hadi watu wanamuonea huruma mwanamke. Sasa hapo utasema wanawake wana matatizo jamani? Mwanaume na mwanamke woooooote wanapaswa kuheshimiana kama mke na mume si jukumu la mwanamke pekee!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Aine naona unataka kuigeuza hii ni vita ya kijinsia. Sijasema kuwa ndoa zote matatizo ni wanawake no. Bali ndoa nyingi ambazo wanawake wanaonekana kuwa juu kielimu/kiuchumi zaidi ya wanaume, matatizo huwa yanaanzia upande wa kikeni (believe me or not, na tusigombane hapo). Na mifano ipo mingi mingi na nina uhakika hata wewe unaifahamu mingine (sitaki kutaja watu majina).

Huo mfano ulioutoa kuwa mwanamme anapewa kila kitu na mkewe lakini ana gubu, umejaribu kuangalia ni kwa nini huyo mwanaume anakuwa hivyo? Mimi siwafahamu hao watu lakini inaweza kunirudisha kulekule ambako wewe unanikatalia, ya kuwa kuna uwezekano mwanaume anapata manyanyaso ya aina fulani kutoka kwa huyo mkewe kwa sababu tu ya huo udhaifu wake. Na yeye kwa kujijua kuwa ni mwanaume hapendi kuiona hali hiyo so ana-react. Kama si hivyo basi kutakuwa na tatizo la kisaikolojia kwa huyo mwanaume (Inferiority complex).
 
Ni dhambi kubwa sana mwanamke kumwacha mwanaume.

Mwanamke anaachwa kama anavyo fuatwa kipindi cha kutongozana.

Mwanamke hapaswi kumwacha mwanaume kamwe bali anaachwa.

mmh!!?????????????????????????????????????????????

majibu ya FIDEL180 na
Baba _Enock yanazidi kuniongezea siku za kuishi....lol
 
maty,

maisha ya ndoa ni mkanganyiko mtupu (confusion). Ukibahatika kuwa na amani basi mshukuru mungu. Ila kwa uzoefu wangu ni watu wachache sana wanayo hiyo amani.

Kuhusu watoto..inabidi wahusika wawafikirie sana ila isiwe kikwazo cha kuachana. Ikionekana kwamba hiyo ndoa haiwezekani kwa hali yoyote ile, basi ni vizuri sana watu wakaachana ili waanze upya. There is life after the first or second marriage ingawa huwezi kujua ipi itakuwa nzuri zaidi. Hata hivyo ni bora kumaliza tatizo la leo bila kujali kama kesho utakutana na kubwa zaidi au la. Kung'ang'ania kwenye ndoa ni hatari sana. Aunt yangu aliuawa na mume wake aliyempiga sana ikiwa ni kama siku 3 toka ajifungue. Inauma sana. Kama angewasikiliza wazee waliomwambia kuwa ile ndoa yake ilikuwa haiwezekani kabisa, labda hadi leo angekuwa hai.

Kuhusu maisha baada ya kutengena huwezi kujua kwa sasa. Ila kama biashara hailipi basi funga duka na kufanya kazi nyingine.

Mzee dc


r i p roho ya marehemu aunt yako.

imezidi kudhihirisha kuwa siyo kila jambo linavumilika.
Tuwe na kipimo kwa kila jambo.
 
ni kweli watoto ndo wanapata matatizo na matatizo yapo mengi na wakati mwingine sio lazima mtu awe malaya

Ni kweli ndugu,

Hata hivyo ukumbuke kuwa hakuna nafsi hata moja iliyo tayari kufia nyingine isipokuwa ya Yesu peke yake. Kwa hiyo suala la watoto inabidi lipewe nafasi lakini lisimfikishe mtu mahali pa kupoteza uhai kama nilivyosema kuhusu aunt yangu! Bahati mbaya hata mitoto mingine aliyoifia iliishia kuwa michokoraa!
 
r i p roho ya marehemu aunt yako.

imezidi kudhihirisha kuwa siyo kila jambo linavumilika.
Tuwe na kipimo kwa kila jambo.

Sioni sababu kabisa ya kukuta mtu yuko ICU kwa pressure eti anaogopa kuachana na mume/mke wake kwa sababu ya watoto au sababu nyingine yoyote. Maji yakizidi unga unayamwaga na kuendelea kujaribu kuokoa huo unga kidogo usipotee.


Mzee DC
 
Ukifikiria mara mbili mbili naona kama ni bora kubaki single hivi, nimenufaishwa na mawazo yenu wote, naona bora nibaki single tu
 
degree ya uvumilivu kwenye ndoa ni ndogo sana kwa maisha ya sasa
ukizingatia wana ndoa wengi wana'jua' haki zao na hakuna anayetaka kujiweka chini
haya yote nadhani yameletwa na utandawazi..na hii kitu equality wanawake tunaililia pia i think inachangia kwa namna moja au nyingine
hakuna mwanamke wa siku hizi anataka kunyenyekea, wote wana/tuna penda kujilinganisha na wanaume..
mbaya zaidi ukikuta mdada kasoma ndo kabisaa hapo ni maswala ya 'nini nini usinichoshe nisikuchoshe nataka amani'..
tofauti na mama zetu walikuwa ni wanyenyekevu wazuri sana na wao pia walikuwa wanaangalia consequences za kuachana kwa watoto
lifestyle imebadilika generation hii ni selfish haiangalii watoto

in a nutshell, anayeweza kuifanya ndoa iendelee kuwepo ni mwanamke, na mwanamke wa sasa si mvumilivu.

Ni mtazamo tu.

Nunga mkono hoja kwa kuongezea usemi wa wahenga:- MAFAHALI WAWILI HAWAKAI ZIZI MOJA

Halafu napendekeza kwamba wapenzi wachaguane kwa vigezo vya tofauti za kipato, yaani wahakikishe mmoja awe nacho na mwingine awe mlalahoi ili kujenga heshima, kwa hiyo mama akiwa nacho achague baba hohehahe, na baba akiwa nacho achague mama hohehahe na wahakikishe hali hii haibadiliki. si inasemekana eti ukiona watu wawili wanapatana basi mmoja ni mjinga, lazima kuwe na Mr. au Mrs. yes ndio mambo yaende sawa, mnaonaje hiyo?
 
Ukifikiria mara mbili mbili naona kama ni bora kubaki single hivi, nimenufaishwa na mawazo yenu wote, naona bora nibaki single tu

Usije ukajutia uamuzi wako baadaye..
kumbuka wengi wa waliochangia humu hawajaingia kwenye maisha ya ndoa.
Kama ukifuatilia michango ya wale walioko kwenye ndoa kama Paka Jimmy, DC, utagundua kwamba misingi ya ndoa inajengwa kwa UPENDO, UVUMILIVU na HESHIMA.
Kama hautakuwa tayari kuyatekeleza hayo ni vyema mtu ukapata nafasi ya kujifunza.
Hakuna shule wala mazoezi ya ndoa, kwa sababu watu hawafanani na mazingira hayafanani.

Kubwa ninaloliona mimi, kadiri wanawake/wasichana uchumi wao unavyozidi kuimarika ndivyo matatizo yanaweza kuongezeka. Hii ni kwa sababu kiasilia wanawake wameumbwa kuhudumiwa. Na mara nyingi anayetakiwa kuhudumiwa ni mwanamume. Hivyo basi mwanamke anapokuwa na uchumi mzuri, automatically anakuwa anahudumiwa na mshahara wake, kwa hiyo nafasi ya mwanamume inapungua maishani mwake.

Mifano iko mingi, especially mikoani na vijijini ambako uchumi wa wanawake sio mzuri sana na hivyo wengi na wavumilivu kwenye ndoa zao.
Dhumuni la kuyasema haya ni kwa sababu kudumu kwa ndoa yoyote kunategemea MWANAMKE, kwa wakristo wanajua kabisa sifa za mwanamke kwenye MITHALI 31.. na pia inasema Mwanamke mpumbavu huingamiza nyumba yake.

Kingine ni kuwa watu hatumshirikishi sana Mungu linapokuja swala la mtu wa kuishi naye. tunaendeshwa na HISIA zaidi. na mara zote hisia zinakufa nguvu, na ndipo hupelekea matatizo kwenye ndoa. Nafikiri kama kweli mtu unamshirikisha Mungu katika kila kitu, atakupa tu mtu wa kufanana na wewe.
 
Niliwahi kuandika humu kuwa "I think I love my wife" watu wakaniona mwehu fulani.

Kupendana, Kuvumiliana, Kusameheana, kuheshimiana, kuaminiana ni nguzo kuu za kudimisha amani katika ndoa zinazozungumzika kirahisi, lakini ngumu sana kutekeleza kwa vitendo.

Hatutakiwi tu kuimba "I love U", tunatakiwa kufikiria kwa makini kama ninachosema nakitekeleza, ndo maana mimi nilisema 'I think I love my wife'

Hili suala la kusema mkikosana 'myaweke mezani myaongee' ndilo hatari zaidi kuliko kila kitu kinachoweza kusababisha ndoa na mahusiano kuvunjika.

I say it, zaidi ya 80% ya wanandoa hawajui sanaa ya 'kuyaweka mezani na kuyaongea' na wanapofanya hivyo, hapo hapo ndipo ndoa inapovunjikia. Watu wanajidanganya kuwa ukiwa na mgogoro na mwenzio, kaeni chini muongee yataisha, weee! nani kakudanganya? Sitaki niandke mengi but kwa taarifa yako, 'kukaa chini na kuongea' ni hatari mara mia zaidi ya kwa ndoa yako kuliko kukaa kimya, unless taken very technically. Nitaanzisha thread nyingine (ili nisitoke nje ya mada), ya namna salama ya kumuweka chini na kumuongelesha mwenzako katika ndoa.
 
Back
Top Bottom