Tupeane mbinu: Ni uwekezaji gani wa zao la kudumu ambalo nikilima linaweza kunipa kipato toshelezi?

Nauza miche ya matunda mbalimbali karibu mkuu..
 
Kabisa kwa upande wa ajira pamekuwa pagumu sana pia biashara nazo azieleweki.
 
Lima kahawa Mbeya au Mbinga Songea. Kahawa ya kisasa miaka mitatu unaanza kuvuna.

Pia korosho ya mda mfupi nadhani miaka miwili au mitatu unaanza kuvuna.


Kahawa nifuate nikupe update zake me nimelima naanza kuvuna mwaka huu.
Kahawa hata huko huko Buhigwe alipo zinastawi vizuri sana na huenda ikamtoa kama atazingatia mbinu bora za kilimo.

Hana sababu ya kukimbilia Mbeya, Mbinga wala Songea kama ulivyomshauri.
 
Nenda maeneo ya manyovu ( Munanila, mwayaya, nyakimue na muhinda) tafuta shamba si chini ya hekari 3 - 5 Lima ndizi na kahawa baada ya Miaka 3/2 utakuja kunishukuru
manyovu ni moro mkuu?
 
Kama hali ya hewa inaruhusu. Lima zao la mchikichi. Uzalishe mafuta ya mawese na mafuta ya mise. Tafuta mbegu ya kisasa
 
Korosho kwa sasa ni pasua kichwa! sisi tuliopo kwenye korosho tumekimbilia kwenye ufuta! na wengine wamefyeka mikorosho yote wamepanda miembe.
Hapo ndipo tunapo feli wakulima,na ufuta ukidondoka bei na korosho bei ukawa nzuri utaanza tena kupanda mikorosho uliyoikata?ukiambiwa zao la kudumu ni uwekezaji,kabla ya kuanza inatakiwa ukae chini ufikiri kwa mapana yake,changamoto ambazo ikitokea ukakutana nazo utafanya Nini?kama hiyo ya kuporomoka kwa bei,pia lazima ujue Kila penye changamoto fursa ipo nyuma yake imejificha,Mimi pia imenigusa KWENYE korosho kwa mwaka huu,ila sijakata tamaa au kukata mikorosho au kukimbilia zao lingine, bali nimepata nguvu mpya ya kuwekeza zaidi KWENYE zao la korosho, sababu nimepata njia mbadala ya kuliendea zao Hilo kwa mwaka huu MWENYEEZI MUNGU akipenda

Sent from my TECNO CC7 using JamiiForums mobile app
 
noted chief
 

Bless,sijawahi acha iamini korosho,plan ni kupanda shamba la minazi ukanda wa pwani ya mkoa wa lindi.
 
Bless,sijawahi acha iamini korosho,plan ni kupanda shamba la minazi ukanda wa pwani ya mkoa wa lindi.
Kiongozi shukran sana,kama umeingia kichwani kwangu, Nina heka zinakaribia 40 zimebaki ukitoa nilizopanda korosho nataka nianze mchakato wa kupanda minazi, unajua kiongozi uwekezaji ni vita,ufe au upone ila watu wengi wanachukulia simple sana, angalizo kama mtu una roho nyepesi ya kutaka matokeo mapema usijiingize kuwekeza kwenye mazao ya kudumu ya muda mrefu, ni Bora ukajihusisha na mazao ya muda mfupi,kama vile,nyanya,ufuta,mpunga,maharage,n,k

Sent from my TECNO CC7 using JamiiForums mobile app
 
noted chief
 

Ni kweli kabisa mazai ya muda mrefu yanahitaji uvumilivu sana ila yakianza kutoa ni faida.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…