Tupeni mrejesho mliowekeza kwenye mashamba ya miti

Safi na hongera kwa juhudi, muhimu umejua tatizo na umejipanga kwa asiyejua tatizo bado ni changamoto kubwa kwake.
Changamoto hazifanani, chamsingi ni kuwa na subira. Kila biashara/uwekezaji una changamoto zake. Hivi walionunua hisa za TOL wamewahi pata gawio?
 
Naam,
Fedha inatokana na shughuli yenyewe. Huwa naanda vitalu vya miche, nauza miche mingi, faida nanunulia mashamba na kuendeleza, kwa hiyo ni uwekezaji unaojiendesha wenyewe. mwanzo nilikuwa nanunua vimisitu vidogo nafuga, akija mteja napiga bei, kwa hiyo vikaniinua sana. Huku nina miche na kule kamsitu kamepata mteja, basi siku zinasonga.

Niko njombe pia napiga parachichi. Nimeangukia pua mara mbili kwenye parachichi, yaaani miche ilikufa sana. Nikagundua miche ya bei rahisi ni hasara. Sasa hivi natumia miche ya bei mbaya, haifi.

Kule Lutukira niliangukia pua kwenye Tangawizi, ile namalizia camping, bei ikashuka vibaya nikaondoka fasta.
 
Pole sana mdau moto ulitokana na nini?
Jirani yangu alikuwa na madeni sugu, vijana wakalipa kisasi kwa kuchoma moto bila kuzingatia kuwa tutakaopata hasara ni wengi. Zaidi ya eka 5000 ziliteketea kule Mgala njombe.
 
Nilipoamua kuingia kwenye hii game nilianza na eka moja na nusu kule Kilolo, Mheshimiwa Mbunge Mwamoto alinipa msaada mpaka kufika kile kijiji na nikapata shamba eka moja na nusu kwa Tsh 22,000/.

Nikaagiza hela jamaa wanioteshee, hawakuotesha lote, msimu uliofuata nikakaza buti mwenyewe, nikamalizia kipande, yaani miaka miwili nikaotesha eka moja na nusu.

Wakati wote nilikuwa nasoma game kwa madogo na wenyeji. Nilipolijua game, nikawatimulia vumbi kwa speed ya 120km/h. Imebaki historia pale kijijini. Huwa nawapitia siku nikienda kukagua misitu, basi kukiwepo maji tunakunywa.
 
Hapo nimekusoma vema.
Tupo pamoja pande hizi.. nafanya organic farming soko ni nje nje na wanunuzi wa nje wanazidi kuongezeka na bei inapanda vizuri, lengo ni kuwauzia wanaoexport Europe.

Avocado nadeal na rungwe avocado kwasababu wao ni global gap certified na seedlings nachukua kwao sababu pia ni global gap certified, nami pia wamenicertify, export market ya Europe inaangalia kuanzia historia ya mche, ukuzaji mpaka uvunaji pia ni lazima ufanye organic farming japo ni gharama sana.

Miche ya mtaani ni ya kuepuka wengi wanaangamia na wanazidi kupotea, huku wanachojua wao avocado ni deal basi mradi mche uwe grafted wanajibebea tu na kupanda mwisho wa siku kwenye kuuza wanabaki kushangaa mzungu amekuja kuvuna na semi shambani kwangu huku mimi nakunywa kahawa chini ya mti nasubiri amalize tupime kilo nipate milioni zangu
 
Jirani yangu alikuwa na madeni sugu, vijana wakalipa kisasi kwa kuchoma moto bila kuzingatia kuwa tutakaopata hasara ni wengi. Zaidi ya eka 5000 ziliteketea kule Mgala njombe.
Mgala, ihanga ni wahuni sana wale halafu matapeli sana, ardhi hawana walishawauzia wageni sasa hivi ni migogoro tupu huko wamebaki kuuza mashamba waliyouza miaka mingi iliyopita. Shamba moja linauzwa mara 5.
 
Jirani yangu alikuwa na madeni sugu, vijana wakalipa kisasi kwa kuchoma moto bila kuzingatia kuwa tutakaopata hasara ni wengi. Zaidi ya eka 5000 ziliteketea kule Mgala njombe.
Aisee[emoji22][emoji22][emoji22][emoji22][emoji24]
 
Kweli changamoto hazifanani kama ni project tofauti,ila kama unapanda miti nyanda za juu kusini aina za matatizo zinawiana kwa wapandaji wote wa eneo husika, ndio maana research inahusu zone nzima.
Changamoto hazifanani, chamsingi ni kuwa na subira. Kila biashara/uwekezaji una changamoto zake. Hivi walionunua hisa za TOL wamewahi pata gawio?
 
Hii inategemeana na unapoishi. Hiyo bei ni miti ya Iringa

Kuna sehemu, kuna miti inaitwa mburumatare (sijui hili jina ni common maeneo yote au laa), hii miti baada ya miaka 5 unavuna na mti mmoja unauza kati ya Tsh 50-70 elfu. Hapo bado unabaki na mabanzi na kuni ambazo pia unaweza kuziuza. Hivyo hiyo biashara si kichaa kama wengine wanavyodhani

Uzuri wa hiyo miti, ukikata, unachipuka mwingine ambao Baada ya miaka 5 mwingine unaweza kuuza tena kwa kati ya Tsh 50-70

Wazo la kupanda miti ya matunda pia ni wazo zuri, kwani ukipanda miti ya matunda ya asili kama miparachichi unaweza kuvuna hata kwa miaka 10 (mazao yakiwa mengi katika peak yake)

Uzuri wa biashara ya miti, ukipanda ikikaa ndani ya miaka 2 bila kusumbuliwa, unaendelea na mambo mengine huku shamba lako likiendelea kukutengenezea utajiri
 
Binafsi ni mpenzi pia wa kilimo cha miti, mitiki, nina ekari zangu 10 za mitiki na mwakani nategemea kupanda nyingine nyingi.

Changamoto kubwa ninayokutana nayo ni pesa, kilimo cha miti hasa ikiwa na umri mdogo chini ya miaka 2 unahitaji palizi kama nne kwa mwaka vinginevyo miche mingi itakufa, pesa ikikata katikati kichwa kinawaka moto.

Solution ya changamoto hii hakikisha ukipanda miti panda na zao jingine rafiki kwa hiyo miti kama Mahindi hivi kupunguza gharama za palizi, tunajifunza kwa njia ngumu. MITI INAKATA NYORORO YA UMASKINI KWENYE FAMILIA.
 
Ku prone, kuna watu wengi wanataka kuni mkuu, kwanini kwako iwe gharama

Kwanini utoe hela mfukoni, wakati unacho prone chenyewe ni mali
 
hapo kwenye global gap hapo,
I am sorry, wakulima wengi watapata shock siku wanaambiwa kuwa matunda yako yote ni reject. Tuna miche fake mingi sana mitaani kule njombe.
 

Ni sehemu Gani hiyo ambako hii miti inapandwa?
 

Mkuu Malila karibu sana, Hizi nondo zako hasa kwenye ujasiria mali ni rotuba tosha kichwani mwangu Sijui ndugu yako kanyagio alipoteaga wapi?
 
Ni sehemu Gani hiyo ambako hii miti inapandwa?
Hiyo miti nadhani inaweza kuota sehemu yoyote ambayo miti ya miarubaini inaota (kwa mtazamo wangu) maana kila kitu ni kama miarabaini

Ukiangalia mbegu zake, majani yake, uchungu wake (japo sio michungu kwa kiwango cha miarabuaini) ni kama maiarubaini

Ukiiprone inaenda juu tu. Na ukiacha ikae miaka mingi, inaharibika, ndani inakuwa kama mabunzi yanavyokuwa katikati
 
Kila biashara ina changamoto zake. Ila binafsi niseme yafuatayo.
1. Kuwekeza kwenye Kilimo cha miti kinafaa sana kwa mtu mwenye malengo ya mda mrefu.
2. Kwa wale wanaotokea mikoa yenye ardhi hasa za urithi haihitaji mtaji bali nguvu yako tu inatosha. Miche unawatika mwenyewe, mashimo unachimba mwenyewe na kupanda, kuzuia moto utafanya mwenyewe na prooning fanya mwenyewe.
3. Faida ya kuwekeza kwenye miti ni kubwa kuliko hasara na vijana wengi kutoka iringa, njombe, nk waliojielewa mapema mambo yako njema.
4. Kwa ambao hawana mashamba ya urithi bei ya eka moja ni 150000-200000 hivyo ukiamua kufanya hiyo biashara fanya kila mwaka panda eka ya miti kwa mtaji mdogo

Ushuhuda wa kweli mimi nikiwa a,level mwaka 2009 nilianza kupanda miti na nilifanya hivyo miaka yote iliyofuata hadi namaliza chuo kikuu mwaka 2014 nilikuwa na miti zaidi ya eka 15 na hadi sasa naendelea kupanda miti kwa kwa juhudi kubwa sana. Na miti yangu hadi sasa inatosha kupasuliwa na ni mikubwa sana tu. Ninavyoongea hadi sasa naweza kuuza zaidi ya 60+mlns ya pesa.

Nishauri tu vijana wenzangu kuna haja ya kuamua unataka baadae uwe na uchumi wa aina gani na uitwe nani. Amka sasa na ufikirie ardhi ya kijijini kwenu au ya familia bado ipo iddle kabisa nenda ikakupe matunda ya maisha ili baadae uitwe majina tofauti ya udon
 
Kila biashara ina changamoto zake.sasa kama unataka biashara yenye cashflow za karibu karibu kalime mboga mboga.ni kama kuku wa mayai vile.unalisha miezi mitano bila kukuingizia hata mia .baada ya hapo unaanzakuingiza hela
 
Jirani yangu alikuwa na madeni sugu, vijana wakalipa kisasi kwa kuchoma moto bila kuzingatia kuwa tutakaopata hasara ni wengi. Zaidi ya eka 5000 ziliteketea kule Mgala njombe.

Kuna kitu wanaita fireline, yaani unaacha kama hatua kumi au ishirini kutoka kwa shamba la jirani
 
Hongera mkuu.. ukiwa na kipato cha uhakika ni uwekezaji mzuri sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…