Tupia jina la mwalimu aliyekuwa mnoko shuleni/chuoni kwenu

Tupia jina la mwalimu aliyekuwa mnoko shuleni/chuoni kwenu

tpaul

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
24,225
Reaction score
22,632
Katika shule/chuo hakosekani mwalimu msumbufu na ambaye huwafuatilia sana wanafunzi hata ktk mambo madogo madogo na kuwapa adhabu za ajabu ajabu.

Leo nataka tuwakumbuke walimu hawa pamoja na kujikumbusha vituko walivyowahi kuvifanya.

Mimi shuleni kwetu Mara Sekondari kulikuwa na mwalimu mmoja aliyeitwa Jigge. Basi siku moja kuna wanafunzi walitoroka kwenda mjini bila ruhusa. Na kibaya zaidi, walipokuwa huko mjini wakafanya fujo na kuharibu mali za wananchi.

Taarifa zao zikafika shuleni. Ilikuwa jioni na kiza kilikuwa kimeanza kukolea. Mwalimu Jigge akapiga kengere. Wanafunzi wote tuliokuwepo shuleni tukakusanyika bwaloni na akaanza kuchuka roll call.

Ili kumkomesha mwalimu huyu, pamoja na kuwanusuru wale wanafunzi 'wahalifu' waliokuwa wamefanya tukio mjini, wanafunzi wakapanga kuzima umeme main switch na kumpopoa kwa mawe. Ghafla tu, umeme ulipozimika, mwalimu alichomoka kama mshale na kutokomea kizani. Wanafunzi walimtupia mawe lakini, kwa ile speed aliyochomoka, hakuna jiwe lililompata. Ana bahati sana.
 
yani nakumbuka Ashira kulikuwa na mwalimu wa kike anaitwa mwalimu Mbele anasura ngumuje sasa alikuwa hapendi watu kuvumisha chakula dom na wadada weng wanapenda kwenda kulia dom akikukamata yani hafu alikuwa ana roho ngumu

kuna siku marafki zangu walivusha uji kila mtu ana chupa mbili aliwaambia wanywe wote na haukuwa na sukari yani chuoni sasa kulikuwa kuna Dr anaitwa Saanane alikuwa anafundisha proposal ni mkali unaenda kupresent unatetemeka mpaka basi Dr yule alinipa pressure hadi semister inaisha ckuamini aise kila mtu alikuwa ana mwogape
 
Basi unaambiwa kwamba kuna mwalimu anaitwa Bachubila. Jina la utani tulikuwa tunamuita Ruba. Huyu ticha alikuwa hacheki na mtu yeyote yule. Tangu nianze fomu wani mpaka namaliza fomu foo sikuwahi kumuona akicheka. Usiombe ukutane na Ruba hujachomekea shati, hujahudhuria assembly au ukiwa umetoroka shule--utajuta kuzaliwa!

Kuna siku alinitaka niokote makombo ya chakula nimpelekee alishie kuku wake, nikamdis. Siku 1 alinivizia nikiwa natoka DH akanizaba konzi kidogo nizimie! Kisha alinipa adhabu ambayo niliifanya wiki nzima bila ku-attend class. Nilikomaje!

Sasa huyu bwana kiingereza chake kilikuwa na matege. Siku 1 kuna mwanafunzi wa fomu tuu alimpiga mwanafunzi wa fomu wani mbele yake, Ruba akadakia: 'WHY YOU BEAT FORM ONE IN MY FRONT?'. Hapa alikuwa na maana kwamba: 'KWANINI UNAMPIGA FOMU WANI MBELE YANGU?'. Bora hata alipokuwa hajui kiingereza, angekijua angekuwa mnoko zaidi. Kwa kweli mwalimu huyu alikuwa mtata sana, hakuna mwanafunzi shuleni kwetu Mara Sekondari asiyemfahamu huyu ticha mnoko.
 
Basi unaambiwa kwamba kuna mwalimu anaitwa Bachubila. Jina la utani tulikuwa tunamuita Ruba. Huyu ticha alikuwa hacheki na mtu yeyote yule. Tangu nianze fomu wani mpaka namaliza fomu foo sikuwahi kumuona akicheka. Usiombe ukutane na Ruba hujachomekea shati, hujahudhuria assembly au ukiwa umetoroka shule--utajuta kuzaliwa!

Kuna siku alinitaka niokote makombo ya chakula nimpelekee alishie kuku wake, nikamdis. Siku 1 alinivizia nikiwa natoka DH akanizaba konzi kidogo nizimie! Kisha alinipa adhabu ambayo niliifanya wiki nzima bila ku-attend class. Nilikomaje!

Sasa huyu bwana kiingereza chake kilikuwa na matege. Siku 1 kuna mwanafunzi wa fomu tuu alimpiga mwanafunzi wa fomu wani mbele yake, Ruba akadakia: 'WHY YOU BEAT FORM ONE IN MY FRONT?'. Hapa alikuwa na maana kwamba: 'KWANINI UNAMPIGA FOMU WANI MBELE YANGU?'. Bora hata alipokuwa hajui kiingereza, angekijua angekuwa mnoko zaidi. Kwa kweli mwalimu huyu alikuwa mtata sana, hakuna mwanafunzi shuleni kwetu Mara Sekondari asiyemfahamu huyu ticha mnoko.

Hiki kilikua kipindi cha utawala wa Daniel Goyayi au alikua alishahama? Nakumbuka hii ilikua kati ya 1998 hadi 2000
 
daaah aisee kuna mwalimu alikua anaitwa mnelamwana(mtwara tech)uyu jamaa ni balaa,,alikuaanaogopeka na wanafunzi na walimu wote ispokua mama mkulemba tu,,aliamishwa wakt tuko form3 na kupelekwa shule fulan ambapo alimpiga mwanafunz mateke ya tumbo na kumsababishia kulazwa hosp.ya mkoa ligula na kisha muhimbili,,,kwa tukio hilo alikua antembea na ulinzi maana wanakijiji walikua wanamwandama
 
Hiki kilikua kipindi cha utawala wa Daniel Goyayi au alikua alishahama? Nakumbuka hii ilikua kati ya 1998 hadi 2000

Ilikuwa kipindi cha Salvatory Magesa (Dingi) na hata kipindi cha Daniel Goyayi, huyu mwalimu Ruba alikuwepo. Nadhani hata Goyayi alipohamishwa kutoka Mara Sec alimuacha Ruba akiendelea kutesa. Hii ilikuwa miaka 90's.
Mkuu, naona hata wewe unamkumbuka Ruba, eeh? Ruba alikuwa tishio.
 
daaah aisee kuna mwalimu alikua anaitwa mnelamwana(mtwara tech)uyu jamaa ni balaa,,alikuaanaogopeka na wanafunzi na walimu wote ispokua mama mkulemba tu,,aliamishwa wakt tuko form3 na kupelekwa shule fulan ambapo alimpiga mwanafunz mateke ya tumbo na kumsababishia kulazwa hosp.ya mkoa ligula na kisha muhimbili,,,kwa tukio hilo alikua antembea na ulinzi maana wanakijiji walikua wanamwandama

hahahaha! ilibidi atafute body guard eti? maticha wa zamani walikuwa noma sana.
 
Mr. Kiddu Emmanuel...daah au Mr. Mkandawire..hatariiii
 
Back
Top Bottom