Tupia jina la mwalimu aliyekuwa mnoko shuleni/chuoni kwenu

Tupia jina la mwalimu aliyekuwa mnoko shuleni/chuoni kwenu

Jamani naona huyu Okwonko wa Kibasila amepata kura nyingi. Alikuwa noumer sana ati? ... Au sio?
kutokana na mwonekano wake(urefu&ukomavu) akapewa jna la okonkwo na hakuwa na maskhara na wanafunz. but alshafark
 
musoma tech(alliance) kulikuwa na mwl.mikomangwa alikuwa ni noma.. lakini alikomeshwa baada kupigwa mimba mabinti zake wawili

Namkumbuka sana huyo jina lake aliitwa Pastory Mikomangwa aka mikoma-G, alikua msukuma na mabinti zake walikua weupe pee. Alikua akikutana nawe kule mjini au baruti anakukariri sura na akija shule kesho yake lazima akukamate paredi.

"musoma shule ya sekondari, ufundi Tanzania ..." wimbo wa shule nimeukumbuka mwanzo wake
 
duuuu kulikua na jamaa mmoja anaitwa mdigo aisee alikua anapenda kunionea atari yaani akisimama tu assembly lzm nikutwe na kosa yaani,na mbabe mmoja anaitwa shavunza akicheka ndo amekacrika na adhabu yake utakoma,na jamaa mmoja alikua mshamba atari anachomekea mayenu mpk gnz anaitwa kisayo nilikua cmpendi mwanaume anakimbelembele kama cha kwanza
 
Mwalimu Mgimwa--Mkwawa High School. Huyu mwalimu alikuwa discipline master. Ni kimwalimu fulani kimbilikimo hivi--kifupifupi. Lakini hiyo shughuli yake ilikuwa baraaaa!
Basi siku moja, kiMgimwa na na Mwalimu mmoja wa Maths anaitwa Mwaipaja, akaamua kuzama eneo moja linaitwa Makanyagio--hapa ndipo wanafunzi watoro walipokuwa wakienda kujificha wakinywa pombe moja ya Kihehe inaitwa ULANZI.

Basi siku hiyo Mgimwa na swahiba wake Mwaipaja (huyu naye alikuwa mnoko sana) wakaamua kuzama huko Mkanyagio na kuwaibua hao 'wahalifu' wakinywa ulanzi. Wakakamatwa wazima wazima, na kuswagwa kama kondoo hadi assembly ground. Walichapwaje!!!!!!!!!!!!!! Walichapwa mpaka wakajuta kusoma shule. Chezea Mgimwa wewe!

nafikiri mwl Makwaya na mama masawe wa mkwawa pia walikuwa na huu unoko
 
mikoroti wa mapinduzi primary, unakunja saba unakula bakora. mayo - udsm.
 
kutokana na mwonekano wake(urefu&ukomavu) akapewa jna la okonkwo na hakuwa na maskhara na wanafunz. but alshafark

hahaha! halafu hawo walimu wanoko huwa hawakosi kupewa majina na wanafunzi wao.
 
Ngui aka baba kadoda

Hahaha! Nakumbuka jinsi Ngui (RIP) alivyokuwa akituzuia tusiende Makanyagio lakini tukawa hatumuelewi. Maandazi ya makanyagio yalivyokuwa matamu vile nani angemuelewa? Thubutu!

Basi siku moja baada ya kutubania sana tusitoke bwenini (Shaaban Robert East), tukaamua tuchume mahindi shambani mwake tukaenda kuyachomea DH. Chezea Mkwawa Complex wewe!
 
Mwalimu Mgimwa--Mkwawa High School. Huyu mwalimu alikuwa discipline master. Ni kimwalimu fulani kimbilikimo hivi--kifupifupi. Lakini hiyo shughuli yake ilikuwa baraaaa!
Basi siku moja, kiMgimwa na na Mwalimu mmoja wa Maths anaitwa Mwaipaja, akaamua kuzama eneo moja linaitwa Makanyagio--hapa ndipo wanafunzi watoro walipokuwa wakienda kujificha wakinywa pombe moja ya Kihehe inaitwa ULANZI.

Basi siku hiyo Mgimwa na swahiba wake Mwaipaja (huyu naye alikuwa mnoko sana) wakaamua kuzama huko Mkanyagio na kuwaibua hao 'wahalifu' wakinywa ulanzi. Wakakamatwa wazima wazima, na kuswagwa kama kondoo hadi assembly ground. Walichapwaje!!!!!!!!!!!!!! Walichapwa mpaka wakajuta kusoma shule. Chezea Mgimwa wewe!

mwaipaja ndiye yule alikuwa mwanariadha wa makongoro west?
 
Hahaha! Nakumbuka jinsi Ngui (RIP) alivyokuwa akituzuia tusiende Makanyagio lakini tukawa hatumuelewi. Maandazi ya makanyagio yalivyokuwa matamu vile nani angemuelewa? Thubutu!

Basi siku moja baada ya kutubania sana tusitoke bwenini (Shaaban Robert East), tukaamua tuchume mahindi shambani mwake tukaenda kuyachomea DH. Chezea Mkwawa Complex wewe!

nyie ndiyo mliyofeka mahindi ya Mgimwa?
 
Sisi tulikuta kila sehemu pale Mazengo pameandikwa "Dudu **#&# (tusi)" Yaani huyu nashukuru Mungu sikumkuta.

Sisi tulimkuta Dungu na Msasa. Msasa akikuta na kosa lolote, una hali mbaya. Ila darasani unaweza kumchezea sharubu kabisa, mhh, mkivuka tu mlango wa darasa, anawewe. Darasani alikuwa Mpole sana.
Dungu akikuta na kosa dogo, umelia. Akikukuta na kosa la kufukuzwa shule, anakusema mbaya tena mbele za Waalimu, ila hakutaji jina na haendi kushtaki ufukuzwe.

Pia Mlokole mmoja anaitwa Mwakyembe, kichaa wa Mahesabu sana ila Mkorofi mno.
Mazengo kuna ticha alikuwa anaitwa Unyamaunyama dah huyu mnyakyusa alikuwa na mkwara sana
 
Lusifeli enzi zake Peponi, alikuwa Mkali kweli. Heri Mungu aliamua kumfukuza Mwalimu huyu.

Inasemekana ndiye alianza kula Tunda la Katikati na mwisho Adamu na yeye ndiyo akaonjeshwa.

Matokeo yake Binadamu wote tunasota hadi leo. Huyu ndiye Mwalimu mnoko kuliko wote waliowahi kutokea Ulimwenguni.
 
Ihungo sekondari kulikuwa na mwl anaitwa D. HUNTER ni balaa walio soma miaka ya 2000 wana mdaka vyema. HUYU JAMAA alikuwa hatumii akili katika kutekeleza majukumu yake. Mwingine ni Byamungu ambae tuliamua kumuita Pilato kwa roho chafu. Alikuwa mkuda kupindukia.
 
Back
Top Bottom