Tupia jina la mwalimu aliyekuwa mnoko shuleni/chuoni kwenu

Tupia jina la mwalimu aliyekuwa mnoko shuleni/chuoni kwenu

yani nakumbuka Ashira kulikuwa na mwalimu wa kike anaitwa mwalimu Mbele anasura ngumuje sasa alikuwa hapendi watu kuvumisha chakula dom na wadada weng wanapenda kwenda kulia dom akikukamata yani hafu alikuwa ana roho ngumu

kuna siku marafki zangu walivusha uji kila mtu ana chupa mbili aliwaambia wanywe wote na haukuwa na sukari yani chuoni sasa kulikuwa kuna Dr anaitwa Saanane alikuwa anafundisha proposal ni mkali unaenda kupresent unatetemeka mpaka basi Dr yule alinipa pressure hadi semister inaisha ckuamini aise kila mtu alikuwa ana mwogape
Dr saannane yupi? Kuna mmoja aliwahi kunifundisha Archaeology lakini ilikuwa part time SAUT Mwanza. Yeye alikuwa anapenda kuvaa shati jeupe na sigara saan very complicator
 
Mazengo kuna ticha alikuwa anaitwa Unyamaunyama dah huyu mnyakyusa alikuwa na mkwara sana
Mwaka gani mkuu.
Mie nilikuwa hapo Enzi za Msasa, Lungu, piuaz, Sichone, mkwizu, Suri na mkewe wale singasinga , Nyanda, Shabaan nk
Headmaster akiwa Silvester Mkoba[emoji2]
 
Inanikumbusha Shule ya Msingi Jangwani SUMBAWANGA alikuwa anaitwa Mwasumbi na Mwalimu mkuu alikuwa anaitwa KIBONA ukikutwa na hao watu utapulwa Kama Nyoka huku miguu ikiwa imening'inizwa ukutani kichwa chini.
SUMBAWANGA SECONDARY
Kuna mkuu wa shule alikuwa anaitwa SALEHE NJANGA na mtaaluma alikuwa anaitwa KIMITI ilikuwa usiombe kukutwa nao Utang'oa visiki vya zaidi ya umri wako na mvua ya viboko
WALIMU WAANDAMIZI WACHAPAJI VIBOKO
Mwalimu Amosi Mmewa
Mwalimu Moshi
Mwalimu Tamba na ukuda wa kutosha
Mwalimu Sangu
Yaani wewe achaaa
 
Iwalanje sekondari miaka fulani nilipata binti anaitwa Happy Emanuel basi night nikabonga na dogo vizuri tu safi kumbe huyo mwalimu umeme uliokatwa usiku akawa anapiga patrol akaona watu kwa mbaali. Binti akadakwa kuwa ulisimama na nani dogo kwa uoga akawa analia tu. Kesho yake binti na mwalimu huyo wakatimba darasani kwetu binti mbele mwalimu nyuma, akanyoosha hadi kwangu kuwa ni huyu tulikuwa nae. Nikapelekwa staff room nikagongwa stick na mwalimu ikumbukwe nilikuwa form six, toka siku hizo nikamchukia sana mwalimu JOSHUA MHOTELWA sijui yupo wapi siku hizi.

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Mazengo sekondari enzi za headmaster Silvester Mkoba palikuwa na second headmaster mnoko kweli kwa jina la Msasa akisaidiwa na mnoko mwingine alijulikana kwa jina la Mkwizu.
Ila S. Mkoba alikuwa mtu poa sana na humble person.
Wahenga mliopita Mazengo kule Dodoma mnawakumbuka hawa watu?
Baadae Mkwizu alikuja kufanyiwa fujo moja ya hatari sana. Miaka ya 1990s
 
Omary mtaka enzi hizo mbemba sec masasi mtwara,kitu kidogo utaskia wee mbuzi njoo apo ushakula makofi Kama yote na kutembezwa kwenye korido na magoti, kali kuliko nilienda kuchukua cheti miaka miwili baada ya kumaliza shule sasa kosa nilienda bila kuchana nywele nikaambiwa nikalete ndoo 20 za mchanga mtoni ndipo nipewe cheti daaaa!! Nilienda tu kishingo upande
 
Mara Sec kulikuwa na mwalimu mmoja anaitwa RUBA (Sostheness Bachubira); hii mbegu ya kihaya achana nayo aisee. Hasa ukifanya kosa la kijinga mbele yake, utaomba ufukuzwe shule tu kuliko kukabiliana na hiki kiumbe. Ila alikuwa anaongea kingereza kibovu balaa. Utasikia anakuuliza: "Why you beat Form I in my front?" eti hapo anamaanisha "Kwanini unampiga fomu wani mbele yangu"? 😀 😀 😀 😀
 
Omary mtaka enzi hizo mbemba sec masasi mtwara,kitu kidogo utaskia wee mbuzi njoo apo ushakula makofi Kama yote na kutembezwa kwenye korido na magoti, kali kuliko nilienda kuchukua cheti miaka miwili baada ya kumaliza shule sasa kosa nilienda bila kuchana nywele nikaambiwa nikalete ndoo 20 za mchanga mtoni ndipo nipewe cheti daaaa!! Nilienda tu kishingo upande
Eee bwana eehh!!!! Huyu mwalimu apewe Tuzo ya Nobel si kwa unoko huu. Yaani umeenda kuchukua cheti bado unapewa adhabu? Huyu kiumbe sio mtu aisee!! 😳 😳 😳 😳 😳 😳 😳 😳 😳
 
Baadae Mkwizu alikuja kufanyiwa fujo moja ya hatari sana. Miaka ya 1990s
Fujo gani mkuu? Wanafunzi walilipiza?

Nakumbuka Mara Sec kulikuwa na mwalimu mmoja mtata sana. Sasa kabla ya kuingia darasani wanafunzi wakamtega kwa kutumia kiti kilichovunjika.......wakakiungaunga na kukiweka mbele ya meza ya mwalimu. Basi teacher alipokuja kukalia kile kiti kikampiga mweleka nyeti zote zikakaa uchi. Mara moja aligundua kwamba ametegwa na kuwaomba wanafunzi wamtaje aliyefanya mtego ule lakini darasa lilionyesha solidarity ya kufa mtu.....no kutaja mtu.

Kuona vile, teacher akawarepoti wanafunzi kwa mwalimu wa nidhamu; wakala mboko kama zote na kuchimbishwa shimo la maji taka kwa wiki nzima bila kuingia darasani. Ilikuwa balaa unaambiwa, usipime!!!
 
Fujo gani mkuu? Wanafunzi walilipiza?

Nakumbuka Mara Sec kulikuwa na mwalimu mmoja mtata sana. Sasa kabla ya kuingia darasani wanafunzi wakamtega kwa kutumia kiti kilichovunjika.......wakakiungaunga na kukiweka mbele ya meza ya mwalimu. Basi teacher alipokuja kukalia kile kiti kikampiga mweleka nyeti zote zikakaa uchi. Mara moja aligundua kwamba ametegwa na kuwaomba wanafunzi wamtaje aliyefanya mtego ule lakini darasa lilionyesha solidarity ya kufa mtu.....no kutaja mtu.

Kuona vile, teacher akawarepoti wanafunzi kwa mwalimu wa nidhamu; wakala mboko kama zote na kuchimbishwa shimo la maji taka kwa wiki nzima bila kuingia darasani. Ilikuwa balaa unaambiwa, usipime!!!
Vijana walivamia nyumbani kwa Mwl Mkwizu usiku usiku hivi, choma moto vibanda vya mifugo, katakata miwa ilopandwa pale kwake, piga mawe madirisha na fujo zingine za namna hiyo.
 
Omary mtaka enzi hizo mbemba sec masasi mtwara,kitu kidogo utaskia wee mbuzi njoo apo ushakula makofi Kama yote na kutembezwa kwenye korido na magoti, kali kuliko nilienda kuchukua cheti miaka miwili baada ya kumaliza shule sasa kosa nilienda bila kuchana nywele nikaambiwa nikalete ndoo 20 za mchanga mtoni ndipo nipewe cheti daaaa!! Nilienda tu kishingo upande
Kabisaaa ulienda kubeba mchanga?
 
Back
Top Bottom