Anyway, kufanya mapenzi kipindi chote cha ujauzito ni salama kabisa endapo mama haoneshi dalili zozote za hatari au kuwa na historia isiyo njema hapo kabla.
Kinachopaswa kufanyika kwa usahihi ni aina ya style. Aina ya style zote ambazo huenda zikamuumiza mtoto, kama baba kuwa juu ya mama zinahitaji kusimama kwa muda mpaka pale mama atakapojifungua. Badala yake mama ndiye awe juu na style zingine ambazo hazitambugudhi mtoto.
Kufanya mapenzi kipindi cha ujauzito kuna faida lukuki, zikiwemo za kiafya na kisaikolojia.