Tuseme ukweli tu, Mike Tyson hatembei kwa Evander!

duuuuuuuuh aisee wew unafatilia boxing kwel???
 
Floyd kaanza ngumi tokea miaka ya 90 enzi hizo bado kijana mdogo , kaanza ngumi akiwa na miaka 19 kama sikosei , sasa hivi anayo 35+ ,

Sasa wewe unabisha floyd hakuwepo miaka ya 90 inashangaza kiukweli,
Na ndio maana nikasema wengi Floyd mmemjulia kwenye Pambano lake na Pacquiao
Huyo tyson hata kama ni heavy weight atapigwa kirahisi sana
 
Mechi za hawa jamaa nimezitizama sana tu. Mechi ya kwanza kweli Tyson alizidiwa ufundi. Mechi ya pili Evander aliamua kutumia 'MBINU MBADALA'. Aliamua kutumia kichwa zaidi ya mikono. kila Tyson akisogea jamaa anapiga 'HEAD'. Angalia vizuri hilo pambano utaona, hata watangazaji (commentantors) waliliona hili na wakasema laivu-mubashara. Baada ya pambano Tyson pia akasema kuwa hakuwa na namna sababu mpinzani wake alikuwa anpiga head. Hata lile jeraha alilipata Tyson lilitokana na kupigwa kichwa, siyo ngumi.
Kacheki vizuri
 
Alaf kingine nikwambie huyo floyd hakuanza kucheza ngumi za kulipwa alianza kucheza ngumi za ridhaa ,sawa bwana mdogo siku nyingine usipende kubisha bisha vitu usivyovijua utaonekana fala
 
Tyson bana aliondoka na masumbwi yake...nakumbuka siku anapigana na Evander home tulikuwa hatujui kuoimia tofauti za masaa huku kwetu na kwao basi tulikesha kwa tv kusubiria. Chaaa na ndo ilikuwa siku yanguvya mwisho kuangalia ngumi baada ya pambano lile.
 
Wanaosema Mike Tyson ndiyo bondia bora ni mashabiki juu juu tu wa boxing
I can write more than ten pages kukanusha hilo..
Ktk list ya mabondia kumi bora kuwahi kutokea duniani tena kwenye Heavyweight category Tyson wala hayumo...
Vile vipigo alivyopokea toka kwa Evander na Lenox Lewis vilikuwa vya aibu sana kwa bondia yeyote duniani kuvipata...
Na kile kitendo cha kubite mara mbili kwa Evander ndiyo kikamtoa kabisa kwani ule ni uhuni uliopitiliza..
 
Kweli kabisa ki Tyson akina lolote hivi hawa wangeangalia mabondia kama Timothy Bladley, Maidana, au Amir Khan watasemaje
 
Mechi za hawa jamaa nimezitizama sana tu. Mechi ya kwanza kweli Tyson alizidiwa ufundi. Mechi ya pili Evander aliamua kutumia 'MBINU MBADALA'. Aliamua kutumia kichwa zaidi ya mikono. kila Tyson akisogea jamaa anapiga 'HEAD'. Angalia vizuri hilo pambano utaona, hata watangazaji (commentantors) waliliona hili na wakasema laivu-mubashara. Baada ya pambano Tyson pia akasema kuwa hakuwa na namna sababu mpinzani wake alikuwa anpiga head. Hata lile jeraha alilipata Tyson lilitokana na kupigwa kichwa, siyo ngumi.
Kacheki vizuri
 

Mkuu; kwa mujibu wa Telegraph la June, 5, Mike Tyson ktk Heavyweight category, ni bondia wa 6 kwa ubora, nyuma ya Ali, Schmeling, Gene, Sony, Jack na Na. 7 akiwa Klitschko.

Kwa mujibu wa boxingnewsonline leo, Tyson ni Na 10 ktk ubora wa Heavyweight category. Nakushauri pitia link mbali mbali, ktk tafiti zako angalia Heavyweight category All time.
 
Ushabiki huo...na ya lewis je?
 
floyd yupo vizuri sana , Tyson hagusi kabisa hapa hata kama yeye ni heavy weight,


Floyd yupo vizuri kwanza ana shabaha alaf anajua sana kukwepa, ila ukitaka kumfaidi zaidi floyd angalia mapambano yake ya miaka ya 90
Mkuu hebu mtake radhi Tyson
Na huo ni uchochezi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…