Tushauriane: Hawa Panya Road tunawatokomeza kwa namna gani?

Tushauriane: Hawa Panya Road tunawatokomeza kwa namna gani?

Lihove2

JF-Expert Member
Joined
Mar 23, 2018
Posts
3,545
Reaction score
6,512
Hili la panya road lilkuwepo miaka fulani ya hapo nyuma ila likapotea miaka ya 2015 na kuendelea. Na maeneo ya wahanga wa hili zaidi ni mkoa wa Dar es salaam

Hawa ni watoto wetu wa mitaani mwetu kabisa. Walikuwa watukutu hawataki kwenda shule, hata kule shuleni hakuna mwalimu yeyote atahangaika na mwanafunzi ambaye hafiki shule kwa sababu madarasa yenyewe ni machache. Unakuta darasa la watoto 40, lina watoto 120. Wazazi pia wakawaacha kwa kuwakatia tamaa baada ya kushindikana kuwarekebisha.

Hawa wengi wao walishia darasa la 5 mpaka kidato cha 2. Ni wachache sana waliofikia form 4, wengi wa watoto wanatoka ktk familia duni sana au familia zinazolelewa na mama wa kufikia.

Huwa wanapanga muda na maeneo ya kukutania ili kupata ulevi, ni humu humu kwenye mitaa yetu. Kwa sababu ya umri wao kuwa mdogo, kifikra huwaga wakishapanga jambo lao la kufanya uharifu huwa wanaendeshwa na mihemuko ya bange au madawa mengine ya kulevya.

Katika kila mtaa familia wanakotoka panya road zinajulikana kabisa. Mara nyingine ni za wajumbe wa nyumba 10 au ndugu wa wajumbe (wazawa). Narudia tena panya road huwezi wakuta huko Masaki, Posta au Osterbay. Ni huko huko uswahilini kwenye maisha ya hovyo hovyo hivi.

Panya Road huwa hawanaga eneo maalumu la kufanyia uharifu, popote pale na muda wowote ule wao wanafanya. Nyumba yoyote ile wanaingia, maana target yao ni kupata chochote ili kukidhi mahitaji yao ya wakati huo.

Sasa nini kifanyike:
  1. Kwanza ule ulinzi shirikishi upewe kipaumbele maana hawa ni watoto wa Mitaani kwetu, tunawafahamu katika ulinzi shirikishi vijana wapewe motisha kwa kushiriki ktk kufanya ulinzi
  2. Kila mtaa utengeneze register ya vijana walio jobless, hasa wale walioacha shule, kujua wanafanya nini. Hili si gumu ni kupitia wajumbe wa nyumba kumi
  3. Serikali iwe na mipango shirikishi ya muda mrefu ya kunusuru haya makundi ya vijana waliokosa fursa. Kutengeneza vikundi na kupewa shughuli za kufanya kama kuzoa taka mtaani n.k
  4. Ikitokea panya roads wakafanya tukio, basi kipaumbele kiwekwe kuwapata viongozi wa panyaroad maana hao mara nyingi ni vijana wenye ushawishi mkubwa katika makundi haya. Wakipatikana wadhibitiwe kabisa.
  5. Serikali iweke mkakati wa kudumu wa kudhibiti panyaroads kabla tatizo halijawa kubwa sababu hawa panyaroad wakikomaa ndiyo wanakuwa wale majambazi wakubwa kabisa yaani wanaweza kuwa recruited kwenye makundi makubwa ya uhalifu sababu tayari wana basics za uhalifu. Pia, ni best candidates kwenye vikundi vya kigaidi
  6. Inatakiwa "tone from the Top" Yaani Mkuu wa nchi aoneshe kwa vitendo kutokulipenda jambo hili. Ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua kali kwa Wizara husika. Maana mara nyingi Jeshi la Polisi ni "reactive" na siyo "proactive". Yaani kukiwa shwari nao wanalala usingizi. Hakuna muendelezo wa kujifunza mbinu mpya za kukabiliana na uhalifu mpya kabla ya kutokea.Mara nyingi wanajifunza mbinu mara baada ya uharifu kutokea
  7. Jambo la mwisho ni kuhusu wakuu wa vyombo vya usalama, yaani kuanzia IGP (akae madarakani based on performance), RPC na wakuu wa vituo vidogo pamoja na wapelelezi hawa wanakaa muda mrefu kituo kimoja bila kuhamishwa.Kiasi kwamba wanakuwa wamefahamiana na waharifu wote na baadaye wanakuwa kama ndugu.
Mwisho; Matukio yq uharifu wa aina hii hutokea zaidi wiki ya kuelekea sikuuu
 
Hili la panyaroad lilkuwepo miaka flani ya hapo nyuma,ila likapotea miaka ya 2015 na kuendelea .Na maeneo wahanga wa hili zaidi ni mkoa wa Dar es salaam

Hawa ni watoto wetu wa mitaani mwetu kabisa.Walikuwa watukutu hawataki kwenda shule.hata kule shuleni hakuna mwalimu yoyote atahangaika na mwanafunzi ambaye hafiki shule.sababu madarasa yenyewe ni machache ,unakuta darasa la watoto 40,lina watoto 120.Wazazi pia wakawaacha kwa kuwakatia tamaa baada ya kushindikana kuwarekebisha.

Hawa wengi wao walishia darasa la 5 mpaka fomu 2.Ni wachache sana waliofikia form 4.wengi wa watoto wanatoka ktk familia duni sana au familia zinazolelewa na mama wa kufikia.

Huwa wanapanga muda na maeneo ya kukutania ili kupata ulevi,ni humu humu kwenye mitaa yetu.kwa sababu ya umri wao kuwa mdogo, ki-fikra huwaga wakishapanga jambo lao la kufanya uharifu huwa wanaendeshwa na mihemuko ya bange au madawa mengine ya kulevya.

Katika kila mtaa familia wanakotoka panya road zinajulikana kabisa.mara nyingine ni za wajumbe wa nyumba 10 au ndugu wa wajumbe (wazawa).Narudia tena panya road huwezi wakuta huko masaki ,posta au osterbay.Ni huko huko uswahilini kwenye maisha ya hovyo hovyo hivi.

Panyaroad huwa hawanaga eneo maalumu la kufanyia uharifu.popote pale na muda wowote ule wao wanafanya.Nyumba yoyote ile wanaingia, maana target yao ni kupata chochote ili kukidhi mahitaji yao ya wakati huo.

Sasa nini kifanyike:
1)Kwanza ule ulinzi shirikishi upewe kipaumbele maana hawa ni watoto wa Mitaani kwetu,tunawafahamu.katika ulinzi shirikishi vijana wapewe motisha kwa kushiriki ktk kufanya ulinzi

2)Kila mtaa utengeneze register ya vijana walio jobless,hasa wale walioacha shule,kujua wanafanya nini.Hili si gumu,ni kupitia wajumbe wa nyumba kumi

3)Serikali iwe na mipango shirikishi ya muda mrefu ya kunusuru haya makundi ya vijana waliokosa fursa.kutengeneza vikundi na kupewa shughuli za kufanya,kama kuzoa taka mtaani n.k

4.Ikitokea panya roads wakafanya tukio,basi kipaumbele kiwekwe kuwapata viongozi wa panyaroad.maana hao mara nyingi ni vijana wenye ushawishi mkubwa katika makundi haya.wakipatikana wadhibitiwe kabisa.

5.Serikali iweke mkakati wa kudumu wa kudhibiti panyaroads kabla tatizo halijawa kubwa.sababu hawa panyaroad wakikomaa ndiyo wanakuwa wale majambazi wakubwa kabisa.yaani wanaweza kuwa recruited kwenye makundi makubwa ya uhalifu. sababu tayari wana basics za uhalifu.Pia ni best candidates kwenye vikundi vya kigaidi

6.Inatakiwa "tone from the Top" Yaani.mkuu wa nchi aonyeshe kwa vitendo kutokulipenda jambo hili.Ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua kali kwa wizara husika.Maana mara nyingi jeshi la polisi ni "reactive" na siyo "proactive".Yaani kukiwa shwari nao wanalala usingizi.Hakuna muendelezo wa kujifunza mbinu mpya za kukabiliana na uhalifu mpya kabla ya kutokea.Mara nyingi wanajifunza mbinu mara baada ya uharifu kutokea

7.Jambo la mwisho,ni kuhusu wakuu wa vyombo vya usalama,yaani kuanzia IGP(akae madarakani based on performance), RPC na wakuu wa vituo vidogo pamoja na wapelelezi hawa wanakaa muda mrefu kituo kimoja bila kuhamishwa.Kiasi kwamba wanakuwa wamefahamiana na waharifu wote na baadaye wanakuwa kama ndugu.

Mwisho;matukio yq uharifu wa aina hii hutokea zaidi wiki ya kuelekea sikuuu
Hapa wapo waliolala,kama Kwa makusudi au bahati mbaya Hilo sita wasemea,ila mamlaka ya uteuzi wa wakuu wanaohusika kukabiliana na Hali hizi pia waone kwanini wenye jukumu la kukabiliana na matendo haya ovu wamelala.
 
Jeshi la polisi ni pambo tu siku hizi, hili swala lilikuwa sio lakufanywa na ulinzi shirikishi.

Ulinzi shirikishi walipaswa waungane na polisi na kuanza kufanya msako mkali wa kukamata mmoja baada ya mwingine kisha wapigike hadharani sio kuwapeleka polisi afu baada ya siku mbili wanarudi kuanza tena uhalifu.

Serikali kama inataka kutuaminisha kuwa jeshi la polisi limeshindwa kuwadhibiti basi at least watupe silaha katika ngazi za serikali za mitaa afu hiyo kazi tuifanye wenyewe.
 
Jeshi la polisi ni pambo tu siku hizi, hili swala lilikuwa sio lakufanywa na ulinzi shirikishi.

Ulinzi shirikishi walipaswa waungane na polisi na kuanza kufanya msako mkali wa kukamata mmoja baada ya mwingine kisha wapigike hadharani sio kuwapeleka polisi afu baada ya siku mbili wanarudi kuanza tena uhalifu.

Serikali kama inataka kutuaminisha kuwa jeshi la polisi limeshindwa kuwadhibiti basi at least watupe silaha katika ngazi za serikali za mitaa afu hiyo kazi tuifanye wenyewe.
Huenda wapo waliomsusia ntu,SII Bure hawatekelezi majukumu yao,ndio maana naweza sema hayuko wamoja kiihivyo kama taifa na hili lafaa liangaziwe vyema
 
Miaka ya mwanzo ya 90 kulikuwa na vikundi vinaitwa komando yoso na kiboko msheli.Vilisumbua sana na kulikuwa hakuna communication ya kuspread message kama leo lakini vilikomeshwa kwa mapigo makali ya wananchi na polisi..
Hivi visharobaro vya tandika na temeke mikoroshini vinasumbuaje kiasi hiki?
 
Hapa ndio eneo ambapo namsifu sana mwendazake, hakupenda kusikia ujinga huu ktk masikio yake na maaskari walifanya kazi zao kwa weledi na ukomavu!
Sasa maaskari wetu wame-relax sana, hadi watu 24 wanajeruhiwa ktk mkoa wako wewe upo tu na umekalia kiti bado! Hawa Ma - RPC na RCO walikuwa wanatakiwa wawe wameondolewa kazini kwa uzembe na kushindwa kufanya kazi walizoajiriwa nazo!
 
.Ikitokea panya roads wakafanya tukio,basi kipaumbele kiwekwe kuwapata viongozi wa panyaroad.maana hao mara nyingi ni vijana wenye ushawishi mkubwa katika makundi haya.wakipatikana wadhibitiwe kabisa.
Bila kupepesa macho wanatakiwa kupelekwa 'msitu wa pande' na wakabaki huko milele wasionekane tena ktk ulimwengu wa kistaarabu!
 
Kuwadhibiti panya road first kiongozi wa nchi unatakiwa uwe na roho mbaya kama Maghufuli, Kim Jong , Ghadafi , Kagame au Putin ... Bila attitude ya high command hakuna kitu mtawafanya hao panya road , huo uongozi wenu wa watu laini wa Pwani na Zanzibar wa kuoneana huruma na kuchekeana , hao panya road watawanyonya mavi Sana .....!! Hao panya road wapelekeni kanda ya ziwa , wote wanageuzwa mishikaki. Hakuna Mura atacheka na hvyo vitoto
 
Hili la panyaroad lilkuwepo miaka flani ya hapo nyuma,ila likapotea miaka ya 2015 na kuendelea .Na maeneo wahanga wa hili zaidi ni mkoa wa Dar es salaam

Hawa ni watoto wetu wa mitaani mwetu kabisa.Walikuwa watukutu hawataki kwenda shule.hata kule shuleni hakuna mwalimu yoyote atahangaika na mwanafunzi ambaye hafiki shule.sababu madarasa yenyewe ni machache ,unakuta darasa la watoto 40,lina watoto 120.Wazazi pia wakawaacha kwa kuwakatia tamaa baada ya kushindikana kuwarekebisha.

Hawa wengi wao walishia darasa la 5 mpaka fomu 2.Ni wachache sana waliofikia form 4.wengi wa watoto wanatoka ktk familia duni sana au familia zinazolelewa na mama wa kufikia.

Huwa wanapanga muda na maeneo ya kukutania ili kupata ulevi,ni humu humu kwenye mitaa yetu.kwa sababu ya umri wao kuwa mdogo, ki-fikra huwaga wakishapanga jambo lao la kufanya uharifu huwa wanaendeshwa na mihemuko ya bange au madawa mengine ya kulevya.

Katika kila mtaa familia wanakotoka panya road zinajulikana kabisa.mara nyingine ni za wajumbe wa nyumba 10 au ndugu wa wajumbe (wazawa).Narudia tena panya road huwezi wakuta huko masaki ,posta au osterbay.Ni huko huko uswahilini kwenye maisha ya hovyo hovyo hivi.

Panyaroad huwa hawanaga eneo maalumu la kufanyia uharifu.popote pale na muda wowote ule wao wanafanya.Nyumba yoyote ile wanaingia, maana target yao ni kupata chochote ili kukidhi mahitaji yao ya wakati huo.

Sasa nini kifanyike:
1)Kwanza ule ulinzi shirikishi upewe kipaumbele maana hawa ni watoto wa Mitaani kwetu,tunawafahamu.katika ulinzi shirikishi vijana wapewe motisha kwa kushiriki ktk kufanya ulinzi

2)Kila mtaa utengeneze register ya vijana walio jobless,hasa wale walioacha shule,kujua wanafanya nini.Hili si gumu,ni kupitia wajumbe wa nyumba kumi

3)Serikali iwe na mipango shirikishi ya muda mrefu ya kunusuru haya makundi ya vijana waliokosa fursa.kutengeneza vikundi na kupewa shughuli za kufanya,kama kuzoa taka mtaani n.k

4.Ikitokea panya roads wakafanya tukio,basi kipaumbele kiwekwe kuwapata viongozi wa panyaroad.maana hao mara nyingi ni vijana wenye ushawishi mkubwa katika makundi haya.wakipatikana wadhibitiwe kabisa.

5.Serikali iweke mkakati wa kudumu wa kudhibiti panyaroads kabla tatizo halijawa kubwa.sababu hawa panyaroad wakikomaa ndiyo wanakuwa wale majambazi wakubwa kabisa.yaani wanaweza kuwa recruited kwenye makundi makubwa ya uhalifu. sababu tayari wana basics za uhalifu.Pia ni best candidates kwenye vikundi vya kigaidi

6.Inatakiwa "tone from the Top" Yaani.mkuu wa nchi aonyeshe kwa vitendo kutokulipenda jambo hili.Ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua kali kwa wizara husika.Maana mara nyingi jeshi la polisi ni "reactive" na siyo "proactive".Yaani kukiwa shwari nao wanalala usingizi.Hakuna muendelezo wa kujifunza mbinu mpya za kukabiliana na uhalifu mpya kabla ya kutokea.Mara nyingi wanajifunza mbinu mara baada ya uharifu kutokea

7.Jambo la mwisho,ni kuhusu wakuu wa vyombo vya usalama,yaani kuanzia IGP(akae madarakani based on performance), RPC na wakuu wa vituo vidogo pamoja na wapelelezi hawa wanakaa muda mrefu kituo kimoja bila kuhamishwa.Kiasi kwamba wanakuwa wamefahamiana na waharifu wote na baadaye wanakuwa kama ndugu.

Mwisho;matukio yq uharifu wa aina hii hutokea zaidi wiki ya kuelekea sikuuu
Nakubaliana na wewe mkuu. jana hali ilikuwa mbaya sana. cha kushangaza polisi wanafanya doria kwenye barabara kubwa tu hawaingii vichochoroni kabisaa. maskani zote wanazoshinda hawa vijana zinajulikana vituoni shida ipo wapi
 
Tuwachemshe supu kama watatu hivi 😂😂


Suluhisho ni ulinzi shirikishi katika kaya zetu. Na kupeana taarifa
 
Makonda alivitokomeza kirahisi sana, kipanya kikikamatwa na wazazi wake pia wanaungana nae jelA bila dhamana!! Mbona walipotea wiki tu jiji shwariiii....!

Huyu mkuu wa mkoa wa sasa sijui kazi yake nini yaan?? Yaan tunaona gaps za akili za kina Makonda sometimes kuamrisha kibabe na kufuatilia utekelezaji!!
 
Mimi nawaunga mkono panya road waendelee kuwatandika mapanga mpaka akili ziwakae sawa.

Haiwezekani wanaume wazima mnalialia kisa hivi vitoto vilivyozaliwa mwaka 2000.

Kwani nyinyi mapanga hamna, na kama hamna mapanga si yanauzwa madukani?

Mimi hawa watoto mtaani wananijuwa vizuri mimi mwenyewe mafuta ya taa.
 
Makonda alivitokomeza kirahisi sana, kipanya kikikamatwa na wazazi wake pia wanaungana nae jelA bila dhamana!! Mbona walipotea wiki tu jiji shwariiii....!

Huyu mkuu wa mkoa wa sasa sijui kazi yake nini yaan?? Yaan tunaona gaps za akili za kina Makonda sometimes kuamrisha kibabe na kufuatilia utekelezaji!!
Unamuongelea huyu?
 

Attachments

  • VID-20220502-WA0010.mp4
    577.6 KB
Hapa ndio eneo ambapo namsifu sana mwendazake, hakupenda kusikia ujinga huu ktk masikio yake na maaskari walifanya kazi zao kwa weledi na ukomavu!
Sasa maaskari wetu wame-relax sana, hadi watu 24 wanajeruhiwa ktk mkoa wako wewe upo tu na umekalia kiti bado! Hawa Ma - RPC na RCO walikuwa wanatakiwa wawe wameondolewa kazini kwa uzembe na kushindwa kufanya kazi walizoajiriwa nazo!
Semaga na ukweli kama walitakiwa kutofuata Sheria hata haki
 
Hili kundi likikua litatusumbua sana. Wathibitiwe haraka sana.
Zonal Kamanda(ZPC) ashughulike. Tuone shughuli yake.
 
Back
Top Bottom