Tushauriane: Hawa Panya Road tunawatokomeza kwa namna gani?

Tushauriane: Hawa Panya Road tunawatokomeza kwa namna gani?

Wanaume wa Dar nao ni wanaume
 
Hili la Panya road nami nitie neno.Kwa maoni yangu Kuna udhaifu mkubwa kwa jeshi la polisi.Inawezekanaje watu wajeruhi watu takribani 20 na hakuna aliyeshikwa hata mmoja??.Intelligensia ya Polisi Iko wapi? .
Ushauri Polisi waongeze Intelligensia na doria ili kuhakikisha wahusika wanatiwa mbaroni.
Police hawezi Linda KILA mtu
 
Panya ujua mitaa ya kuvamia mingine wanajua awatoki
 
Unapopiga na panya piga kama unapigana na shetani maana wamejitoa kufa so tumia silaha yeyeto.
 
Kwenye panya road bwanA makonda aliupiga mwingi sana
giphy.gif
 
Hakuna siri ya watu 50+ ni swala la kuomba jamii kuwataja ukiona majina yanajirudia kamata top five kwenye list kwa nyakati tofauti kimya kimya, wape kichapo kidogo, ingia nao plea bargain wakishirikiana na jeshi la polisi adhabu yao itapungua.

Kazi yao iwe kukupa taarifa tukio linalofuata na onyo lao likitokea tukio awajatoa habari mziki wake kwao autakuwa mdogo. So una five potential informants ambao awajuani chances are utapata habari tu tukio linalofuata, set a sting operation na askari wa kutosha.

Yaani vitoto vidogo vitusumbue, Dar Es Salaam ya Makonda wasingethubutu.
 
Polisi nawaomba radhi jamani hapo kabla nilikuwa sitambui umuhimu wenu katika hii nchi ila baada ya hawa wasengerema wanaojiita "Panya Road" kutikisa hapa mtaani kwetu nimetambua kuwa ninyi ndio mnaofanya tutambe huku mjini kwa jitihada zenu za kuimarisha usalama.Natangaza rasmi nawakubali kuanzia leo.!
 
Polisi nawaomba radhi jamani hapo kabla nilikuwa sitambui umuhimu wenu katika hii nchi ila baada ya hawa wasengerema wanaojiita "Panya Road" kutikisa hapa mtaani kwetu nimetambua kuwa ninyi ndio mnaofanya tutambe huku mjini kwa jitihada zenu za kuimarisha usalama.
Wameenda wapi siku hizi hao polisi?
 
Ni jukumu la Jamii husika kuwamaliza panyaroad na sio kutegemea sijui raisi , rpc , IGP sijui nani elewa hawa si waathirika wa vitendo vya panya labda tu endapo mabinti zao wakiporwa au kubakwa ndipo wanaweza chukua hatua. Nature ya jiwe alikuwa anapenda mbilinge mbilinge zile na mambo yafananayo na ubabe thus panyaroad, Vibaka, wezi awakumchezea.
 
Sijui kama sheria inaruhusu kuziingiza but kwa njia ya panya unaweza.
Check Amazon. Kwa panya zinafanya Kazi nzuri Sana hata waje elf moja

View attachment 2208499

View attachment 2208500
Kuna vitu vinazuiliwa kwa maslahi ya umma, kuna mikasi fulani mikubwa inakata kufuli, inakata nondo hata geti la grill, sasa wakipata wahalifu huwa nishida.

Hata mitungi midogo ya gesi huwa inatumika kwenye uhalifu kwenda kukatia vitu, au kuna zike vifaa ukimgusa mtu anapigwa short anazimika.

South Africa vinapatikana, mijizi inayotokeaga huko ndio inaingizaga hivi vitu.
 
Polisi nawaomba radhi jamani hapo kabla nilikuwa sitambui umuhimu wenu katika hii nchi ila baada ya hawa wasengerema wanaojiita "Panya Road" kutikisa hapa mtaani kwetu nimetambua kuwa ninyi ndio mnaofanya tutambe huku mjini kwa jitihada zenu za kuimarisha usalama.Natangaza rasmi nawakubali kuanzia leo.!
Huoni aibu kusema haya? Yani unategemea wanaume wenzio ndio wakulinde?
 
Hao watoto wanafanya matukio jioni wanaenda kula wali wa kengere majumbani mwao,Hainingii Akilini kabisa hawa kushindikana!
 
Dawa ya hawa ni kuwaua kama polisi watakuwa serious
Mnajaribu ku-solve complex problems kwa simple solutions. Nisikilize: Unawajua bodaboda? Unawajua wamachinga? Basi hawa ni hatari kuliko panya road mara kumi. Trust me! Ni suala la muda tu na matokeo yake yataonekana.
 
Makonda alivitokomeza kirahisi sana, kipanya kikikamatwa na wazazi wake pia wanaungana nae jelA bila dhamana!! Mbona walipotea wiki tu jiji shwariiii....!

Huyu mkuu wa mkoa wa sasa sijui kazi yake nini yaan?? Yaan tunaona gaps za akili za kina Makonda sometimes kuamrisha kibabe na kufuatilia utekelezaji!!
Unajiliwaza tu na wala hujui unachosema. Panya road walikuwepo hata kipindi cha Magufuli, wakati huyu mjinga Makonda akiwa kwenye kilele chake cha unyama.
 
Ushauri wa bure, tupeni leseni ya kuwamaliza hawa madogo, ndani ya wiki moja woote watakuwa mochwari, kama mpo serious lakini.
 
Hili la panya road lilkuwepo miaka fulani ya hapo nyuma ila likapotea miaka ya 2015 na kuendelea. Na maeneo ya wahanga wa hili zaidi ni mkoa wa Dar es salaam

Hawa ni watoto wetu wa mitaani mwetu kabisa. Walikuwa watukutu hawataki kwenda shule, hata kule shuleni hakuna mwalimu yeyote atahangaika na mwanafunzi ambaye hafiki shule kwa sababu madarasa yenyewe ni machache. Unakuta darasa la watoto 40, lina watoto 120. Wazazi pia wakawaacha kwa kuwakatia tamaa baada ya kushindikana kuwarekebisha.

Hawa wengi wao walishia darasa la 5 mpaka kidato cha 2. Ni wachache sana waliofikia form 4, wengi wa watoto wanatoka ktk familia duni sana au familia zinazolelewa na mama wa kufikia.

Huwa wanapanga muda na maeneo ya kukutania ili kupata ulevi, ni humu humu kwenye mitaa yetu. Kwa sababu ya umri wao kuwa mdogo, kifikra huwaga wakishapanga jambo lao la kufanya uharifu huwa wanaendeshwa na mihemuko ya bange au madawa mengine ya kulevya.

Katika kila mtaa familia wanakotoka panya road zinajulikana kabisa. Mara nyingine ni za wajumbe wa nyumba 10 au ndugu wa wajumbe (wazawa). Narudia tena panya road huwezi wakuta huko Masaki, Posta au Osterbay. Ni huko huko uswahilini kwenye maisha ya hovyo hovyo hivi.

Panya Road huwa hawanaga eneo maalumu la kufanyia uharifu, popote pale na muda wowote ule wao wanafanya. Nyumba yoyote ile wanaingia, maana target yao ni kupata chochote ili kukidhi mahitaji yao ya wakati huo.

Sasa nini kifanyike:
  1. Kwanza ule ulinzi shirikishi upewe kipaumbele maana hawa ni watoto wa Mitaani kwetu, tunawafahamu katika ulinzi shirikishi vijana wapewe motisha kwa kushiriki ktk kufanya ulinzi
  2. Kila mtaa utengeneze register ya vijana walio jobless, hasa wale walioacha shule, kujua wanafanya nini. Hili si gumu ni kupitia wajumbe wa nyumba kumi
  3. Serikali iwe na mipango shirikishi ya muda mrefu ya kunusuru haya makundi ya vijana waliokosa fursa. Kutengeneza vikundi na kupewa shughuli za kufanya kama kuzoa taka mtaani n.k
  4. Ikitokea panya roads wakafanya tukio, basi kipaumbele kiwekwe kuwapata viongozi wa panyaroad maana hao mara nyingi ni vijana wenye ushawishi mkubwa katika makundi haya. Wakipatikana wadhibitiwe kabisa.
  5. Serikali iweke mkakati wa kudumu wa kudhibiti panyaroads kabla tatizo halijawa kubwa sababu hawa panyaroad wakikomaa ndiyo wanakuwa wale majambazi wakubwa kabisa yaani wanaweza kuwa recruited kwenye makundi makubwa ya uhalifu sababu tayari wana basics za uhalifu. Pia, ni best candidates kwenye vikundi vya kigaidi
  6. Inatakiwa "tone from the Top" Yaani Mkuu wa nchi aoneshe kwa vitendo kutokulipenda jambo hili. Ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua kali kwa Wizara husika. Maana mara nyingi Jeshi la Polisi ni "reactive" na siyo "proactive". Yaani kukiwa shwari nao wanalala usingizi. Hakuna muendelezo wa kujifunza mbinu mpya za kukabiliana na uhalifu mpya kabla ya kutokea.Mara nyingi wanajifunza mbinu mara baada ya uharifu kutokea
  7. Jambo la mwisho ni kuhusu wakuu wa vyombo vya usalama, yaani kuanzia IGP (akae madarakani based on performance), RPC na wakuu wa vituo vidogo pamoja na wapelelezi hawa wanakaa muda mrefu kituo kimoja bila kuhamishwa.Kiasi kwamba wanakuwa wamefahamiana na waharifu wote na baadaye wanakuwa kama ndugu.
Mwisho; Matukio yq uharifu wa aina hii hutokea zaidi wiki ya kuelekea sikuuu
Hao hawaishi mbinguni wanajulikana,subiria oparesheni mtaani siku wakibanwa mbupu na kuletwa kwenye magereza ya kulima wataisha wenyewe..

Endeleeni tuu kuwalea kwa kisingizio cha damu ni nzito kuliko maji..

Kamata wote,kuna mashamba kibao tuu huku mikoani hayalimwi.
 
Unajiliwaza tu na wala hujui unachosema. Panya road walikuwepo hata kipindi cha Magufuli, wakati huyu mjinga Makonda akiwa kwenye kilele chake cha unyama.

Najiliwaza na nini sasa katika hili?? Mi sijasema hawakuwepo, kwani Makonda alipata ukuu wa mkoa kipindi cha Nyerere??

Ukweli ni kwamba, yeye ndiye alitoa order kuwa akikamatwa kipanya na mzazi wake wote wawekwe ndani!! Wakati huo Kigogo imechafuka na tuliona wazazi waliokamatwa na makundi kupungua kwa kiwango kikubwa!!

Hata kama Makonda ana mabaya yake, hili ni jambo jema sana alilofanya!! Namsifia kwa hilo maana huyu Mkuu wa mkoa wa sasa keshafeli!
 
Back
Top Bottom