Wasalaam wanaJF !
Tukiamua kuhukumu tunatakiwa kukusanya ushahidi na kuhukumu kwa haki.
Mada hii inawaendea wote kwa maana ya Chadema asilia,wanaccm,Team lowassa na wananchi kwa ujumla.
Natangulia kusema kuwa tunachagua mtu wa kuibadilisha system iliyooza ndani na nje ya serikali!!
Tunachagua mtu muhimu wa kwenda kubeba zege la kuijenga upya Tanzania.
Tunachagua mtu jeuri kiasi cha wanaomzunguka wajue hivyo.
Nachelea kusema kuwa makosa ya Boyz 2 men kamwe hayawezi kutumiwa kumuhukumu mwana mchapakazi na askari kamili wa mwamvuli ndugu John Pombe Magufuli.
Magufuli anaibuka kivyake vyake kama mzuka ama kwa uweza wa mola ama kwa weledi wa kitengo!
Kura za watanzania zitajikita kwa kuangalia Magufuli,lowassa,Anna na wengine ni kina nani hasa katika siasa na maendeleo au ustawi wa Taifa.
Wapo wengi wanaoulaumu mfumo bila tafakari ya kina kuwa tatizo sio mfumo bali wanaopewa dhamana ya kuusimamia mfumo.
Mfumo upo tu na hata wanaolilia mabadiliko ni sehemu ya mfumo huo huo unaoitwa mchafu
utamsikia Mkurugenzi au mkuu wa taasisi akiulaumu mfumo ilihali kwenye halmashauri yake kuna uchafu unatendeka!
TATIZO NI MTANDAO
Hili ni tatizo la muda mrefu ndani ya ccm hata kabla mwalimu Nyerere hajatutoka na aligundua hili na kulikemea na kujaribu kulifuta bila mafanikio na pengine ni chanzo cha yeye kututoka!
Mtandao huu ulimea na kuota mizizi ndani ya ccm na ndani ya serikali kiasi cha kufikia dharau kubwa dhidi ya wengi na wenye mamlaka ya nchi hii.
Mzee butiku alitugusia kiasi juu ya huu mtandao na muenendo wake kwa miongo kadhaa ya ccm.
MAKOSA YA BOYZ TWO MEN
Hili ni kundi la vijana wawili walioshibana ingawa mmoja inawezekana alikuwa mjanja na kumtumia mwingine.
Ni kundi lililotuletea mtandao wa kihuni ndani ya chama na hatimaye ndani ya nchi.
Ni kundi lililokuja na style ya propaganda kupitia media hasa hasa magazeti na hatimaye likashinda na kupewa 'kiwembe' wacheze nacho ...kilichotokea sitaki kukisema.
leo hii tunapolilia mabadiliko tunalia kutokana na ukosefu mkubwa wa weledi na uwezo wa kikundi hiki cha boyz 2 men.
Tunalilia mabadiliko kutokana na kushindwa kwa mabwana hawa wawili iwe kabla ya kuhaidiana na kugeukana au kabla ya kutuzingua.
They failed us as they failed themselves!!
Ni kundi hili hili linalotuweka kwenye state ya kutojitambua sasa na kutuondoa kwenye ajenda zetu za msingi.
Ni kundi hili hili linalotufanya tujichanganye na kutojielewa ni nini hasa tunachohitaji kama taifa!
MAKOSA YA WAWILI HAWA HAYAWEZI KUTUPOFUSHA KUCHAGUA KILICHO SAHIHI
Ni maono yangu kuwa nyuma ya wananchi kuna kundi la wazalendo na wazoefu ambao walikubali kukaa chini na kutafakari na kukubali kukataa kuliona Taifa likizamishwa na wanamtandao.wazee wakaamua kuignore propaganda za media na ushawishi wa kifedha.
wazee wakaamua iwe mbaya au nzuri lakini mwisho wa vurugu za boyz two men umeshafika.
Wazee wakaamua kutuletea JOHN P MAGUFULI just from nowhere but amongst us!!
Hukumu ya Magufuli haiwezi kuchanganywa na ushahidi wa vurugu ya boyz two men.
Hukumu ya Magufuli itatokana na ushahidi wa utendaji wake na haiba yake au makosa yake yeye kama yeye.
Ni uhuni kutaka kumchanganya Magufuli na uozo uliofanywa na boyz two men.
Kwa ufupi ni kwamba tumhukumu Magufuli kama Magufuli na sio kiujumlajumla.
Hapo tutakuwa tumetenda haki.
CIAO!!
JF NAOMBA MSIUFUTE UZI HUU ILI TUELIMISHANE TUACHE MABAYA TUFANYE MEMA!!!!
CCM IMEKUWA IKITUMIA MBINU HIZI KTK KAMPENI MIAKA YOTE 55. NAWASHAURI WAACHANE NA MBINU HIZI ZA DIVIDE & RULE KWANI ZITALETA MAUAJI
JANA KTK MKUTANO WA KUFULI KAHAMA AJENDA KUU ILIKUWA UDINI,UKABILA,UKANDA,UONGO,VITISHO,SLOGANI
*****CCM KUWENI MAKINI MBINU HIZI WATANZANIA WALIKWISHA WASHITUKIA SASA MNAPOKUWA MIAKA YOTE NINYI MNATUMIA NJIA HIYO TU BILA KUJISITUKIA MNAONEKANA MABOYA!!*****
***TUNAWANYWA MWAKA HUU***NA NINYI MUANZE KUPANGA FOLENI MAHOSPITALI HUKU MKIKOSA DAWA****
****MKAKUMBANE NA ADHA YA RUSHWA HOSPTALI****MKAFIE HOSPTALI KWA KUKOSA DAWA****
@@BAADA YA KUWASITUKIA JANA KADI YENU NIMEICHOMA MOTO NA NIMEJIVUA RASMI SINA CHAMA****ILA KURA YANGU NAIPELEKA KWA LOWASA WA MABADILIKO******
NI MTU GANI ASIJALI AMANI YA TAIFA KISA ANAUROHO WA KWENDA IKULU???NIMEWAPIGA CHINI NYOOOOOOOO! NIMESITUKA DUH!
***************************************************************************************
kwanza naomba kudeclare interest; mimi ni mwanaccm kindakinda na nasema haya kwa lengo moja wagombea tuheshimu haki za binadamu na tusiwachukulie kama nyumbu ,ng'ombe,mizigo au mifugo.
Nilikuwa siamini kama haya mambo yanafanywa na chama changu lkn jana kwa macho yangu mwenyewe nimejionea pale kahama mkutano wa kufuli, mimi sikubahatika huhudhuria kwa sababu ya shughuli za biashara zangu ndogondogo kunitinga, sasa wakati mkutano unaisha nikiwa maeneo ya fantom niliona malori ya kubebea mkaa na pamba yameja watu wengi sana huku yakiwa mwendo kasi kuelekea isaka,kagongwa, watu wamejazana kikwelikweli ndani ya malori hayo kitu ambacho sio salama
sasa najiuliza hivi mabilioni yaliyo andaliwa na chama changu kwa ajiri ya kupambana na ukawa kwa nini yasitumike kukodi mabasi ili kuonesha kuwaheshimu wapiga kura?
Kwanini watu wa usalama barabarani wapo kimya au wanasubiri ajari itokee ndio waje kuzungumza?
Nasikitishwa sana na wanaccm wenzangu ukiweleza kuwa hili sio salama wanakimbilia majibu mepesi eti hawakulazimishwa? Hapana hii sio sawa kama watu wale wangeng'amua kuwa wanavunja sheria ya usalama wasinge panda malori hayo kwahiyo basi, elimu itolewe kwao ili waepuke kujidhalilisha kama mizigo/mifugo
utafikiri ni malori ya ng'ombe yanapeleka mnadani? Hii sifurahishwi nayo. Ndio maana wakati mwingine chama hiki kinadharau maoni yetu ktk katiba ya warioba kwa kututafsiri kama nyumbu/mifugo
duniani kote mikutano haina maana ya kuwasafilisha watu kama ng'ombe mgombea huwafuata waliko na kunadi sera za chama chake. Au watu wenyewe bila kupewa 1000,2000,3000,5000,10000 kwa mapenzi yao wajigaramie kupanda magari/usafiri wa abiria na sio malori waje mkutanoni. Utakuta malori yanasomba kutoa watu km90 du! Sijapenda kabisa. KAMA NDIO HIVI SIIONI DHAMIRA YA CHAMA CHANGU KUITOA TANZANIA MAHALI ILIPOKWAMA. PENGINE NASHAWISHIKA KUMPA KURA YANGU LOWASA WA MABADILIKO!
watanzania umefika wakati wa kuheshimiwa na watawala; kuna kijiji kimoja niliona wananchi wamebomolewa nyumba zao chini ya dola na watu hao waliishi kwenye mahema kwa takriban miaka3. Sasa hii sio heshima kama tungekuwa tunaheshimiwa mambo haya yangefanyiwa utafiti kabla ya kuhamisha watu kwa nguvu
tuombe kila siku watoa haki wafanye haki ktk mchakato huu ili nchi iwe na amani ya kikatiba na sio amani ya uoga/utulivu.
Huwezi kutafisiri amani kabla hujatafisiri haki!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Nb: Ni ktk kufundishana na kuelimishana tuache mabaya tuchukue mazuri. Sitasita kushauri chama chochote kitakacho kosea na nikaona kwa macho yangu wala sio propaganda
wenu prof. Muhindo
*******mungu ibariki tanzania ,mungu ibariki africa,mungu ibariki dunia********tusifanye utani na amani****vyombo vitende haki kuboresha amani yetu****naipenda tanzania******mama tanzania kwanza!