Tusio na magari tukutane hapa

Tusio na magari tukutane hapa

Huu ndio ukweli mchungu sana ambao watu wengi wenye magari hawapendi kuusema na hawatausema mbele ya watu wasiokuwa na magari.

1/Kununua gari kumewapelekea kwenye madeni kutoka kwenye taasisi za kipesa. Walikuwa hawajawahi kukopa benki lakini kupitia gari walikopa. Na mikopo hiyo ni ya muda mrefu na yenye riba.

2/Gari limepelekea utumwa wa matumizi ya Pesa ili kulihudumia hilo gari au kwenda sambamba na maisha ya kumiliki gari. Gharama za maisha kwao zimekuwa juu wakati huo huo kipato chao ni kile kile au kimepungua.

3/Furaha na Amani ya kumiliki gari ni kidogo sana tofauti kabisa na mategemeo na matazamio yao kabla ya kumiliki hilo gari au mapema wakati ndio wameanza kulimiliki. Kiufupi gari limeleta karaha pia katika maisha yao.

4/Wengi wanajuta kimoyomoyo kuhusu maamuzi ya kununua gari wakati walipaswa kufanya baadhi ya mambo mengine kwanza au aina ya gari walioamua kuimiliki haikuwa sahihi kwao.

5/Kumiliki kwao gari hakukuwafanya kujisikia kupata utoshelevu bali kumeongeza uhitaji wa kutaka kumiliki gari tofauti na hilo au kumeleta unyonge fulani mbele ya watu wengine wenye magari mazuri na bora zaidi yao.
Dahh!! Umeuchana ukweli wenyewe, gari si lolote linapokuja suala la usafiri wa ndani ya mji au mkoa ni sawa tu na kumiliki pikipiki, gharama zake ni kubwa sana halafu unakuta mmiliki ni ticha wa shule ya msingi lazima akili zimkae vzr, kabla ya kununua gari jenga kwanza nyumba ya kuishi na uwe na biashara iliyonyooka.
 
Dahh!! Umeuchana ukweli wenyewe, gari si lolote linapokuja suala la usafiri wa ndani ya mji au mkoa ni sawa tu na kumiliki pikipiki, gharama zake ni kubwa sana halafu unakuta mmiliki ni ticha wa shule ya msingi lazima akili zimkae vzr, kabla ya kununua gari jenga kwanza nyumba ya kuishi na uwe na biashara iliyonyooka.
Kila mtu na kipaumbele chake!
 
IMG_20170801_221844.jpg
 
Raha na karaha ya ngoma ni kuingia kucheza, Raha na karaha ya ndoa ni kuingia kwenye ndoa...
Ukitaka kujua karaha za kumiliki gari basi miliki gari kwanza. Wenye magari hawawezi kukwambia ukweli wa hizo karaha kwa sababu umiliki wao wa gari ndio umetengeneza status zao kwenye jamii, hivyo watajitahidi kuonyesha kuwa ni watu wenye furaha ili kulinda status. Ni sawa sawa na ndoa. Wanandoa nao wana hiyo tabia.

Ulishawahi kuwaza haya...
1/Motor vehicle insurance.
2/Kodi ya mapato.
3/Bei za Diseal na Petrol.
4/Car Parking fee.
5/Bei za kuoshewa gari.
6/Mafundi Garage.
7/Faini za barabarani.
8/Bei za oil, Filter, Plug.
9/Kuziba pancha.
10/Kusukuma gari.

Miliki gari yako ndio utayajua hayo na utajua gharama zake zikoje na kwa vipi zinaathiri maisha ya mtu ya kila siku.
 
Huu ndio ukweli mchungu sana ambao watu wengi wenye magari hawapendi kuusema na hawatausema mbele ya watu wasiokuwa na magari.

1/Kununua gari kumewapelekea kwenye madeni kutoka kwenye taasisi za kipesa. Walikuwa hawajawahi kukopa benki lakini kupitia gari walikopa. Na mikopo hiyo ni ya muda mrefu na yenye riba.

2/Gari limepelekea utumwa wa matumizi ya Pesa ili kulihudumia hilo gari au kwenda sambamba na maisha ya kumiliki gari. Gharama za maisha kwao zimekuwa juu wakati huo huo kipato chao ni kile kile au kimepungua.

3/Furaha na Amani ya kumiliki gari ni kidogo sana tofauti kabisa na mategemeo na matazamio yao kabla ya kumiliki hilo gari au mapema wakati ndio wameanza kulimiliki. Kiufupi gari limeleta karaha pia katika maisha yao.

4/Wengi wanajuta kimoyomoyo kuhusu maamuzi ya kununua gari wakati walipaswa kufanya baadhi ya mambo mengine kwanza au aina ya gari walioamua kuimiliki haikuwa sahihi kwao.

5/Kumiliki kwao gari hakukuwafanya kujisikia kupata utoshelevu bali kumeongeza uhitaji wa kutaka kumiliki gari tofauti na hilo au kumeleta unyonge fulani mbele ya watu wengine wenye magari mazuri na bora zaidi yao.
Am impressed with the way you think and approached this thread!!
Most awesome comment I have read today !!! Ever...
Bitter truth.. But truth must be said!!
 
Back
Top Bottom