Tusipofanya sasa, Tutajuta Milele, ni lazima Wamasai waondoke Ngorongoro

Tusipofanya sasa, Tutajuta Milele, ni lazima Wamasai waondoke Ngorongoro

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Amani iwe nanyi

Kama kichwa cha uzi kinavyosema, Kama Mtanzania ninayeipenda nchi yangu, ninayejali maendeleo ya Watanzania wote vizazi na vizazi, leo nasema kwa Sauti moja, Kama tunajali maendeleo ya Tanzania yetu, Ni lazima wamasai waondoke Ngorongoro ili lile eneo liendelee kuwa na wanyama wengi na kuvutia watalii ambao ni moja ya vyanzo vikuu vya mapato kwa Taifa letu

Kwa nini nasema haya?

1. Ngorongoro ni moja ya sehemu chache hapa Tanzania ambazo mtalii ana uhakika wa kuona wanyama walio kwenye hatari ya kupotea Duniani yaani Tembo, Faru, Simba, Nyati na Chui.

Nimefika ngorongoro kusema ukweli hadi Tour guides wanakwambia hivi karibuni imekuwa ngumu sana kuwaona baadhi ya hawa wanyama na sio tu hawa bali hata wanyama wengine ambao huko mwanzoni walikuwa ni wengi na wanaonekana kirahisi na kuvutia watalii wengi na kuongeza mapato mf pundamilia, pofu na wengineo. Hii ni kwa sababu wanadamu wameongezeka sana Ngorongoro na asili ya wanyama pori ni kuwa hawapendi kuchangamana na binadamu na shughuli za kibinadamu zikizidi huwa wanahama.

2. Kuna taarifa za uhakika kuwa Wanyama wanaohama Tanzania wanahamia upande wa pili yaani Kenya hivyo Kenya anafaidika kwa kuongezeka kwa shughuli za kibinadamu Ngorongoro ambazo zinahamishia wanyama wetu Kenya. Hii ni hatari sana kwa uchumi wa Tanzania kwa sababu siku si nyingi, Watalii hawataona umuhimu wa kuja Ngorongoro na hivyo kwenda Kenya na kufanya nchi yetu kukosa Mapato.

3. Kuna taarifa za uhakika pia kuwa Wamasai waishio Ngorongoro hawana hata makabuli. Hivyo ikitokea mmasai amefariki anaachwa aliwe na fisi na mbweha. kibinadamu hii si sawa.

Napenda kumaliza kwa kusema imefika wakati sasa kwa maslahi mapana ya Tanzania, Wamasai wahamishwe Ngorongoro. Eneo hili ni nyeti na Tanzania nzima tunalitegemea kimapato. Likiangamia, Tanzania imeangamia. Ni wakati sasa Fedha zinazotengwa kuwalisha wamasai takribani bilioni 3-4 kwa mwaka zielekezwe sasa kuwajengea makazi ya kudumu wamasai hawa eneo jingine na kuwapatia teknolojia ya kufuga wanyama wachache tena kibiashara na kuachana na Maisha yale ya kijima

Naomba kuwasilisha!
 
Usiwapangie watu jinsi ya kuzika, wengine wanafukia chini kwenye ardhi, wengine wanachoma moto, wengine wananing'iniza juu kama mizinga, wengine wanakuwa cadavers. Wamasai waachwe katika hili.
 
Kabla ya kuandika huu upupu ungejiuliza wamasai wameishi na hao wanyama Kwa miaka mingapi? Hivi huko Kenya wanakohamia hakuna "wamasai"?

Wakiwapa fisi mizoga Yao shida nini Kwako? Mbona wapo wanaochoma Wapendwa wao kwa moto? Ni life style Yao.

Tukiwatoa wamasai tunaweka waarabu, CCM ni mashetani aiseeee
 
Usiwapangie watu jinsi ya kuzika, wengine wanafukia chini kwenye ardhi, wengine wanachoma moto, wengine wananing'iniza juu kama mizinga, wengine wanakuwa cadavers. Wamasai waachwe katika hili.
AMEN, halafu wanakuja na hoja mfu kweli! CCM Kuna siku watatuwekea sumu tufe wote
 
Wewe binafsi Wamasai wakiondolewa unafaidika nini?

Tusifuate tu mkumbo!
Umesoma uzi na kuelewa au umekurupuka tu ku comment kama kawaida yako

Shughuli za kibinadamu zinakimbiza wanyama Ngorongoro na wanaenda Kenya. Siku zijazo hakutakuwa na wanyama Tanzania na wote watahamia Kenya. Hakutakuwa na haja ya Watalii kuja Tanzania hivyo nchi yetu itakosa mapato ya kukuhudumia wewe na ukoo wako
 
Ukiona jambo limeingiliwa na Wanasiasa kwa nguvu sana ujue kuwa na maslahi yao ya Moja Kwa Moja...!
Ni kweli kina haki za Binadamu na Wanyama pia...hapa Busara Iko wako ni muhimu kubalansisha'
Ngorongoro tunaihitaji na Utalii (wanyama na uoto was asili) tunauhitaji!
 
Ukiona jambo limeingiliwa na Wanasiasa kwa nguvu sana ujue kuwa na maslahi yao ya Moja Kwa Moja...!
Ni kweli kina haki za Binadamu na Wanyama pia...hapa Busara Iko wako ni muhimu kubalansisha'
Ngorongoro tunaihitaji na Utalii (wanyama na uoto was asili) tunauhitaji!
Humo ndani kuna rushwa kubwa sn
 
Kwa nini wanaharakati wanafurahia binadamu wenzetu kuishi kama wanyama? Mwanadamu amepita stage nyingi za maendeleo kuanzia
Dryopithecus,
Ramapithecus,
Australopithecus,
Homo Erectus,
Homo Sapiens na hatimaye
Civilization

Kwa nini tunapenda watanzania wenzetu wabakie kama Sanaa ya kutazamwa na watalii? Wamasai watoke tu Ngorongoro
 
Wamasai kuongezeka Hifadhi ya Ngorongoro inaweza kuwa tatizo kubwa ila baadhi ya sababu mnazotoa watu kama nyie na kina Kitenge inaonyesha kuna hila kubwa.
kwa iyo unaona sawa Shughuli za kibinadamu kuzidi Ngorongoro na wanyama kuhamia Kenya kuondoka Tanzania?
 
Sababu gani zinaonesha kuwepo kwa hila?
Wamasai kuongezeka Hifadhi ya Ngorongoro inaweza kuwa tatizo kubwa ila baadhi ya sababu mnazotoa watu kama nyie na kina Kitenge inaonyesha kuna hila kubwa.
 
Kwa nini wanaharakati wanafurahia binadamu wenzetu kuishi kama wanyama? Mwanadamu amepita stage nyingi za maendeleo kuanzia
Dryopithecus,
Ramapithecus,
Australopithecus,
Homo Erectus,
Homo Sapiens na hatimaye
Civilization

Kwa nini tunapenda watanzania wenzetu wabakie kama Sanaa ya kutazamwa na watalii? Wamasai watoke tu Ngorongoro
Ndivyo ulivyofundishwa kwenye dini yako?
Hao wanaotaka kuwaondoa wamasai ndivyo wanavyoamini kwenye dini zao?
 
Back
Top Bottom