Tusipowakemea hawa wabunge wanaobeza elimu yetu na wasomi wetu, tutazalisha Taifa la hovyo kabisa

Tusipowakemea hawa wabunge wanaobeza elimu yetu na wasomi wetu, tutazalisha Taifa la hovyo kabisa

Habari wanaBodi...

Nimekua mfatiliaji kidogo wa mijadala ya Bungeni hasa michango inayotolewa na wabunge mashuhuri wawili watatu hivi kuhusu Taifa na maendeleo yake Kiuchumi kisiasa na kiteknolojia.

Lengo la kuandika huu uzi sio kuwataja hao wabunge au kuwadhalilisha Bali ni kuwakosoa ili kujenga Taifa Bora Zaidi.

Mara zote katika michango yao, wabunge Hawa wawili wamekua wakipinga Sana ajenda ya usomi na wasomi wenyewe. Kwa haraka haraka wanaamini kabisa wasomi wetu ambao wapo katika sekta mbalimbali hakuna wanalolifanya kwa Kutumia elimu yao. Yaani kimsingi wanaamini mambo yataenda tu kienyeji bila elimu. Kifupi hawaamini kama elimu Ina msaada wowote katika kukuza chumi za nchi na ustawi wa Wananchi wake.

Hawa watu ukiwafatilia kiundani ni watu waliofanikiwa Kiuchumi kwa njia ambazo wao wanaamini hazikuhitaji elimu, sababu wao wameishia la Saba. Hivyo wanaamini mtu yoyote sio lazima asome ili afanikiwe, kisa tu wao hawajasoma na wametoboa.

Tusipowadhibiti au kupinga hizi kauli zao za kibaguzi dhidi ya wasomi wetu, yamkini watoto au wajukuu zetu huko mbeleni wakipata hizi Hansard hawataona umuhimu wa kusoma, wataamini kama huyu "Joshua" alitoboa(ga) bila kusoma basi kumbe Kuna short cut ya Maisha inawezekana.

TUWAKEMEE MARA MOJA.

Nawasilisha.
Yale majinga ya kisukuma yalishindwa shule sasa yanaumwa ugonjwa unaitwa "inferiority complex". Shida waliowachagua, pili kuruhusu std VII kugombea. Wanatukana elimu wakati watoto wao wanasoma shule za gharama kubwa, ila nna wasiwasi km hao watoto wenyewe watakuwa na akili
 
So kifupi Mkuu unaona ni Bora bunge lijaze Darasa la Saba wote ambao ndio washiriki kwenye utunzi wa Sheria na kuendesha nchi? Nauliza sababu nawe waona wasomi hawana maana
Tujaribu tuone, maana hao wachache waneonekana wana nafuu kuliko wasomi wengi. Au unaonaje mwanetu 😂
 
Habari wanaBodi...

Nimekua mfatiliaji kidogo wa mijadala ya Bungeni hasa michango inayotolewa na wabunge mashuhuri wawili watatu hivi kuhusu Taifa na maendeleo yake Kiuchumi kisiasa na kiteknolojia.

Lengo la kuandika huu uzi sio kuwataja hao wabunge au kuwadhalilisha Bali ni kuwakosoa ili kujenga Taifa Bora Zaidi.

Mara zote katika michango yao, wabunge Hawa wawili wamekua wakipinga Sana ajenda ya usomi na wasomi wenyewe. Kwa haraka haraka wanaamini kabisa wasomi wetu ambao wapo katika sekta mbalimbali hakuna wanalolifanya kwa Kutumia elimu yao. Yaani kimsingi wanaamini mambo yataenda tu kienyeji bila elimu. Kifupi hawaamini kama elimu Ina msaada wowote katika kukuza chumi za nchi na ustawi wa Wananchi wake.

Hawa watu ukiwafatilia kiundani ni watu waliofanikiwa Kiuchumi kwa njia ambazo wao wanaamini hazikuhitaji elimu, sababu wao wameishia la Saba. Hivyo wanaamini mtu yoyote sio lazima asome ili afanikiwe, kisa tu wao hawajasoma na wametoboa.

Tusipowadhibiti au kupinga hizi kauli zao za kibaguzi dhidi ya wasomi wetu, yamkini watoto au wajukuu zetu huko mbeleni wakipata hizi Hansard hawataona umuhimu wa kusoma, wataamini kama huyu "Joshua" alitoboa(ga) bila kusoma basi kumbe Kuna short cut ya Maisha inawezekana.

TUWAKEMEE MARA MOJA.

Nawasilisha.
UKWELI LAZIMA USEMWE.
Kwa wele tuliokuwa wafuatiliaji wa shindano la kujibu maswali la vyuo vikuu vya Afrika Mashariki lililokuwa likidhaminiwa na kampuni ya TOYOTA, tulishuhudia Udsm ilivyokuwa ikishika mkia kila mara.
Je, umesahau alichokisema Jenerali Ulimwengu kuhusu chuo kikuu cha Dar es Salaam, kwa kifupi ni SEKONDARI ILIYO JIONGEZA.
Ninakushauri mwezi wa saba katembelee banda la chuo kikuu cha Dar es Salaam kwenye uwanja wa maonesho wa Dar es Salaam barabara ya Kilwa, utapata jibu sahihi.
 
Nguvu ya Elimu ina Umuhimu Pale Elimu inapotumika,kama Una degree na unafanya mambo kama layman,nani ataona Umuhimu wa Elimu??Una masters ya SUA huna ajira unalalamika njaa??

Professor PhD holder unakua Ass kisser kwa Wana Ccm ku chase Teuzi,hiyo Ina sound vipi??

Hawa tunao waita "wasomi" ndio ilitakiwa wafanye mapinduzi katika nyanja zote,Kiuchumi,siasa,jamii,

Sasa hivi Kuna hoja ya muundo wa Muungano,mfate doctor Udsm akupe maoni yake na ushauri Nini kifanyike,Lazima amshukuru Mama.. pathetic,

NB: Wote hawakutaki Jalalani
 
Hao akina Msukuma ni wa kupuuzwa,wanaongea Ujinga na kudharau Wasomi wakati huohuo watoto wao wanasoma shule za kimataifa!!!
Sasa shida ndio ipo hapo hawapuuzwi.... Kila watakaloongea ndio linakua headline katika media zetu.... Yaani nchi yetu imekua ya kupenda kusambaza taarifu za hovyo zaidi kuliko Bora za kujenga. Wenye mawazo jengefu hawapati airtime Ila mawazo hovyo ndio airtime zaidi.
 
Nadhani wewe ni mmoja wapo wawasomi wasikuwa na faida . kwanza tuanze na wewe uliye soma umeisadia nn jamii yako kupitia elimu yako ya juu?

sisi wafugaji na wakulima hawa wasomi wametutia hasara sana kwenye miradi yetu ya kilimo na mfugo
mtu katoka sua degree yake mlete shambani sasa hata kwenye kuku muulize kuku wangu anaumwa anaumwa nini
ni lazima azeme kwenye simu tena bila woga ana google kule mashambani ndo usiseme hakuna cha maana wanachofanya

imefikia hatua sasa ni heri uende kwa mkulima mzoefu akakupe abc kuliko hawa wasomi wasiokuwa na msaada wowote kwenye jamii.

mimi naungana na kishimba kwa 100% wasomi ndo mmetifika hapa tulipo sana sana mnasoma ili mjue namna nzuri ya kutuibia tu.

pale SUA kuna wasomi kibao lkn kinachofanyika hata hakieleweki lkn ni chuo kikubwa hasa
mbegu zote nzuri iwe breed ya ng,ombe wa maziwa tunatoa kenya mbuzi kenya ama uganda. ukija mbegu zinzo fanya vyema hasa za matunda kenya imetuacha mbali mno sio kwamba wasomi wanao semwa hatuna la hasha tuna maprofesa kibao yamkini hata ukijitolea umchimbie bwawa la samaki na kila kitu ukaleta kama hata ajiri mfugaji asiye soma basi tegemea maajabu makuu
Mkuu wewe ukiumwa hua unahudhuria hospitali kupata matibabu au unajitibu mwenyewe?

Kuhusu Kuagiza Baadhi ya bidhaa/vitu nje Ambavyo ndani vipi sio ishu ya wasomi ni ishu ya mfumo na mfumo huo inaanzia Bungeni kwenye kutengeneza sera... Huwezi Kuta mtu kama Tundu Lissu (sio siasa) akawa Bungeni akasapoti "Sheria" ya (let say) SAMAKI anatoka ziwa Victoria anapelekwa Kenya wanamtoa ngozi au mifupa then arudishwe kuja kuuzwa Tena hapa... Noway.... Hayo yanafanywa na hao tunaowalalamikia kutuharibia mfumo wa nchi kwa kuiponda elimu...
 
kwamba wafungwe mdomo wakose uhuru wa kutoa maoni na mtazamo wao, right?

kwamba hicho ndicho wanachostahili kufanyiwa, baada ya kuwasema ukweli kwamba wasomi kulalamika hawana ajira na wana madigrii mbalimbali ni aibu, na wale wa darasa la saba kule vijijini ndio wameshikilia chumi za vijijini na kata, kwamba wasiseme ukweli huo right?
No yote uliyosema sio lengo. Lengo ni kwamba wapunguze kudharau au kuishusha elimu yetu. Na kuaminika kwamba kwa kua wasomi Wachache hawafikii Matarajio yao/yetu basi elimu ionekane Haina maana.
 
Kwanza kabisa, ili tuwe pamoja, elimu ni nini?
Elimu Ina tafsiri Pana kutokana na Mahala wataka tumia.

Darasani: Elimu ni maarifa anayopata mtu au Maelekezo rasmi ambayo hakua nayo au Kuzaliwa nayo ili kumsaidia kubadili mfumo wa fikra zake katika kuchochea ubunifu. Na hupatikana darasani.

Mtaani: Elimu ni utambuzi wa Fursa mbalimbali ambazo hukua nazo ili kuzitumia kupambana na maisha. Na hupatikana Mtaani.

Dini: Elimu ni kumjua Mungu na mambo yake. Na hupatikana dinini au kidogo darasani.

NB: Hizi ni tafsiri zangu binafsi hazina uhusiano na tafsiri rasmi. Lakini pili mjadala huu ujikite kwenye elimu ya kwanza (darasani) ambayo inaenda kwa hatua.
 
Faza, unaisema hii elimu ya kuambiwa binadamu wa kwanza alitokana na sokwe akaenda akibadilika kutokana na mazingira ili hali mpaka leo kuna masokwe kibao yako porini?

Elimu hii isofata uhalisia miaka nenda rudi? Hivi unamfundisha mtoto kuhusu vita ya pili na kwanza ya dunia, inamsaidia nini?
 
Nakunaliana na hoja yako, haiwezekani wasomi wote wakadeliver sawa.... Watakaofeli, basi ni kuwaadress hao hawa particularly.... Lakini Hawa jamaa wanaponda wasomi kiujumla.... Hiyo ndio hoja yangu... Na angalia nilivyomalizia mwishoni
Wasomi wengi wamekuwa machawa hawana msaada ni wasaka vyeo wacha wapondwe
 
No yote uliyosema sio lengo. Lengo ni kwamba wapunguze kudharau au kuishusha elimu yetu. Na kuaminika kwamba kwa kua wasomi Wachache hawafikii Matarajio yao/yetu basi elimu ionekane Haina maana.
hakuna dharau kwenye Ukweli gentleman 🐒

unatakiwa uwaprove wrong kwa kwa vitendo na kwa kuibua alternatives plans kwakutumia maarifa ulopata kutokana na hayo madigrii yako kutatatua changamoto mbalimbali binafsi na kwenye jamii, ambazo hawa darasa la saba wanaziibua na kuwabeza waliosoma kwamba they have failed 🐒

lakini pia msomi kubishana na asie msomi ni changamoto, au msomi kumlalamikia asie msomi ni changamoto zaidi.

ni dhahiri kuna kutokujiamini na hofu tena ni ile fear of unknown, miongoni mwa wasomi dhidi ya wasio wasomi 🐒
 
Sema wasomi wengi mlio kwenye utumishi wa umma ni wazembe, wezi na wavivu.

Matarajio ya wananchi juu yenu yalikuwa makubwa, lakini mnachokifanya haki akisi usomi wenu. Kwakweli ninyi ndio mnaofanya, wasomi tuonekane hatuna tija katika taifa hili.

Hamtimizi majukumu yenu, ndio maana mnadharauriwa na darasa la saba.
Vipi na wasomi tulio nje ya ajira ndugu mlalamikaji Mtanzania 🤔
 
Rais Ruto wa Kenya sio tu kasoma Sana Tena nchi za ulaya na america Bali nchini mwake kiingereza ni lugha ya kawaida, lakini bado juzi alikiri mbele ya umati kwamba kinamsumbua kuelewa anapokutana ma mfasaha wa lugha hiyo... Take note!!
Yuko sahihi,lakini huwezi mfananisha na Jiwe ambaye hakuweza kunyoosha hata sentensi moja ya kiingereza. Wewe pia waweza sema kuwa kiswahili hukijui vizuri lakini siyo huwezi kuwa sawa na mtu kutoka Burundi
 
Habari wanabodi...

Nimekua mfatiliaji kidogo wa mijadala ya Bungeni hasa michango inayotolewa na wabunge mashuhuri wawili watatu hivi kuhusu Taifa na maendeleo yake Kiuchumi kisiasa na kiteknolojia.

Lengo la kuandika huu uzi sio kuwataja hao wabunge au kuwadhalilisha bali ni kuwakosoa ili kujenga Taifa bora Zaidi.

Mara zote katika michango yao, wabunge hawa wawili wamekua wakipinga sana ajenda ya usomi na wasomi wenyewe. Kwa haraka haraka wanaamini kabisa wasomi wetu ambao wapo katika sekta mbalimbali hakuna wanalolifanya kwa Kutumia elimu yao. Yaani kimsingi wanaamini mambo yataenda tu kienyeji bila elimu. Kifupi hawaamini kama elimu Ina msaada wowote katika kukuza chumi za nchi na ustawi wa wananchi wake.

Hawa watu ukiwafatilia kiundani ni watu waliofanikiwa kiuchumi kwa njia ambazo wao wanaamini hazikuhitaji elimu, sababu wao wameishia la saba. Hivyo wanaamini mtu yoyote sio lazima asome ili afanikiwe, kisa tu wao hawajasoma na wametoboa.

Tusipowadhibiti au kupinga hizi kauli zao za kibaguzi dhidi ya wasomi wetu, yamkini watoto au wajukuu zetu huko mbeleni wakipata hizi Hansard hawataona umuhimu wa kusoma, wataamini kama huyu "Joshua" alitoboa(ga) bila kusoma basi kumbe kuna short cut ya Maisha inawezekana.

TUWAKEMEE MARA MOJA.

Nawasilisha.
WEWE UTAKUWA NI MMOJA WAO WA WASOMI WAPUMBAVU .....NI UKWELI USIO PINGIKA KUWA TZ INAWASOMI FEKI TUPU KUANZIA WALIMU MPAKA WANAFUNZI ...KUANZIA PRIMARY MPAKA VYUONI ...TENA WASOMI WENYEWE SIYO FEKI TU HATA AKILI HAWANA
 
Acha ukweli usemwe wasomi wabovu ni zao la mfumo wa elimu mbovu, turekebishe mfumo wetu wa elimu kwanza.Leo hii tunaowaita wasomi ndio majizi makubwa, ndio wavivu hata kufikiria tu hawawezi matokeo yake hufanya maamuzi ya ovyo kabisa hata wasioenda shule hawawezi kufanya huo ujinga.Usomi ndio kufanya huo upuuzi?
 
NKNS...

#Mambo imechemka!

Usomi mashudu ni shida kweli--si uongo wala utani.

Mambo ya kumezeshwa, kumeza na kujimezesha mashudu ya maarifa yaliyochenjuliwa na 'wahuni'.

Hmmm



HAPANA,

Si fikra/maoni/mtungo/mjengeko wa uono na 'tafsiri na mapelekeo yake' ulio na 'uzima' hasa.

Tuende mbali kupiliza mawaidha ama/na maarifa ya Elimu ya Kupeana darasani na 'Kustaarabishwa' na visomo mashudu.

Kufanya hivi, udumishaji wa usahihi wa kisiasa juu ya mambo, daima itakuwa ni sawa na kuimbiana ngojera na ukasuku wa fikra/maoni/maoni mushkeli.

Tuwe waangalifu na ukuhani wa visomo 1.0 na janja zake za ulimwengu wa kileo 2024--Elimu 1.0.

Ukiweza kutambua misingi ya UHURU, UDUGU, HAKI na AMANI--utashangazwa na kiasi ambacho Elimu iliyotamalaki ni mashudu matupu kwa kiasi kikubwa--bado hatujafikia kubaini 'Uwele' ama 'Pumba'--ndiyo maana tuna mabaraza, mazungumzo na majadiliano yasiyo na tija halisi ya maendeleo ya UTU.
 
Vipi na wasomi tulio nje ya ajira ndugu mlalamikaji Mtanzania 🤔
Tafuta kazi ndugu msomaji.. si unaona mwenzio hapo juu katoka povu unadhani mi ndo babaake niliyemzaa 😂😂
 
Yuko sahihi,lakini huwezi mfananisha na Jiwe ambaye hakuweza kunyoosha hata sentensi moja ya kiingereza. Wewe pia waweza sema kuwa kiswahili hukijui vizuri lakini siyo huwezi kuwa sawa na mtu kutoka Burundi
Jiwe alikua mkemia si mlugha
 
WEWE UTAKUWA NI MMOJA WAO WA WASOMI WAPUMBAVU .....NI UKWELI USIO PINGIKA KUWA TZ INAWASOMI FEKI TUPU KUANZIA WALIMU MPAKA WANAFUNZI ...KUANZIA PRIMARY MPAKA VYUONI ...TENA WASOMI WENYEWE SIYO FEKI TU HATA AKILI HAWANA
Mkuu Kuna mawili, either tafuta hela au tafuta ajira, maana hizi hasira hakika ni za stress!!
 
Back
Top Bottom