Tusipowakemea hawa wabunge wanaobeza elimu yetu na wasomi wetu, tutazalisha Taifa la hovyo kabisa

WEWE UTAKUWA NI MMOJA WAO WA WASOMI WAPUMBAVU .....NI UKWELI USIO PINGIKA KUWA TZ INAWASOMI FEKI TUPU KUANZIA WALIMU MPAKA WANAFUNZI ...KUANZIA PRIMARY MPAKA VYUONI ...TENA WASOMI WENYEWE SIYO FEKI TU HATA AKILI HAWANA
Tatizo sio elimu tatizo ni common sense na logic Kwa Mtanzania , inajulikana watz wengi hawatumii akili wala logic kufikiri na kutenda .
Hao mbumbumbu ambao unasema hawana elimu ndio worse kabisa.
Utakuwa ni mtu wa ajabu kudhani hao la saba ndio better .
 
Tanzania watu wamesoma ila hawajaelimika inasikitisha kuona watu wanaojiita great thinkers wanapinga elimu

Ninachoona mimi sio kuwa walio na phd na elimu zingine kuwa wanashindwa kuleta ubunifu wao katika sector mbalimbali bali mfumo wetu wa utawala na hali ya nchi mwenye pesa na mamlaka ndio mjuzi wa kila kitu hata uwe na elimu yako huna ubavu wa kupinga

Kingine elimu na pesa vinaendana wavumbuzi wengi wa ulaya mfano wa ocean gate na makampuni mengine ni watu matajiri na wasomi pia yaani mtu kasoma kabobea na ana pesa kwaiyo anatumia pesa zake kugundua kitu au kuendeleza ugunduzi ulioishia njiani

Nchi yetu unatakiwa ukiwa msomi uwe kama Mungu yaani ugundue vitu kwa miujiza bila incentives zozote huku mamlaka zikikupuuza na wanajamii kukubeza

Kiukweli kuna watu wamesoma na wamebobea kwenye walivyovisomea ila mazingira hayawapi wao kutekeleza walichosomea mfano mtu anamlaumu Mh mwigulu kisa ni waziri wa uchumi kwaiyo hamna mwitikio chanya kwenye sector aliyopewa hizi mimi naona ni siasa tu ila kiukweli tanzania njaa nyingi wewe ukijifanya msomi mfia taifa wenzio wanapiga wanasepa hapo ndipo kwenye tatizo

Mimi naongoza familia yangu changamoto hizi naziona sana yaani watu ni wapigaji na njaa nyingi wewe usomi wako atauelewa nani?
 
Unachanganya siasa na elimu, kinachoturudisha nyuma ni siasa za tz sio elimu

Elimu ikiheshimiwa na tukaweka siasa uchwara na njaa pembeni maendeleo ni dk 0
 
Bora nimeona comment hii. Bravo!!!
 
Kweli Dr. Biteko, dk mwigulu
Hizi PhD zonamsaada Gani?

Profesa kabudi katiba mpya haitaki teana
Mkuu hao uliowataja shida sio elimu shida ni njaa na siasa za tz ukiondoa ivyo vitu viwili hao ni madocta na maprofesa wa uhakika
 
Watu ni wajinga sana nchi hii ,kuna wasomi nchi hii ni smart kichwani , mtu kama Tundu Lisu , Peter Kibatala nk
Hata kujenga hoja unaona kabisa huyu mtu ana akili na elimu .
Kama nilivyotangulia kusema
Tatizo ni mfumo mibovu ya nchi hii ambao haitoi incentives na kuwaforce watu kutumia akili na elimu zao katika jamii .
Mbumbumbu wamejazana humo bungeni akina msukuma , akina Lusinde na mazwazwa wengine .
Ni kwasababu tuna katiba mbovu ya kishenzi inayotoa mwanya kwa mbumbumbu asiye na elimu kugombea na kuwa mbunge ,na tunajua uchaguzi nchi hii ni upuuzi tu .
As long as upo chama tawala unapita ,hata kama ni bogus kiasi gani .
Hii inasababisha hata hawa ambao wana elimu kuona hamna haja ya kutumia elimu zao nao ni bora waunge tela Tu ili kubehave kama hawa mahayawani wasio na elimu as long as kushibisha tumbo , ndio unakuta kundi la machawa , walamba viatu watu wasio na misimamo wala visions wameingia kwenye mifumo ya nchi hii na kuleta contaminations Kwa jamii nzima
Nchi imetengeneza culture ya mediocrity mfano mzuri ni ccm yenyewe , chama kilichoongoza nchi kwa miaka zaidi ya 60 sasa , angalia aina ya watu walioko huko na mambo wanayoyafanya , ni aibu na upuuzi mtupu .
Kiufupi Tanzania ni mediocracy state , hii imeenda mpaka kwenye majeshi ,angalia recruitment ya kwenye vyombo vya dola mfano polisi ,jwtz ,magereza ,TISS nk
Kigezo ni kuwa failure ndio uingie huko , yaani elimu inakuwa disincentivized kwa uwazi kabisa na tuna ona kawaida kabisa , angalia mwisho wa siku ,yanayofanyika huko , ni aibu na upuuzi .
Na products ndio hizo ,full mediocity au ukilaza sugu , mwisho wa siku mnalaumu upuuzi unaoendeshwa na vyombo vya dola nchi hii , ni mifumo na misingi mibovu ndio imeleta hizo results .
Ukiona baadhi ya wasomi kubehave kama mahayawani ujue hiyo ni result tu na ina mzizi wake ,na mzizi ndio huo nilitangulia kusema , mifumo na misingi mibovu isiyotoa mwanya kwa matumizi ya akili ,utashi na taaluma katika nchi hii .

Leo hii unasimama kwa ujasiri na kusema wasomi wa nchi hii ni shida ,
Hapo unakuwa hujaangalia mzizi wa tatizo ni nini pia .
 
Mtu kama Mwigulu miguu ya Chemba ni product ya mediocrity iliyolelewa na serikali ya CM miaka zaidi ya 60 nchi hii
 
Kwenye uringo wa siasa hamna msomi mkuu hata hao akina lisu siku wakipata madaraka utarudia kuandika hapa, mfano muangalie polepole wa bunge la katiba na polepole wa magufuli utaniambia shida iko wapi

Si sahihi kupima kiwango cha elimu kwa nyanja za kisiasa hizi sector ziwe tofauti maswala ya kisiasa yaendeshwe kisiasa na maswala ya kielimu yaendeshwe kielimu hapo ndio utaona umuhimu wa elimu

Nchi yetu mwanasiasa yupo juu kuliko mwenye elimu sasa hapo unategemea nini? Ndio matokea una degree lakini unakuwa chawa wa mtoto wa jk aliokimbia shule akapewa uongozi(ni mfano tu)
 
Wasomi inabidi muelewe kwamba Elimu sio chanzo za utajiri ila elimu ni ufunguo tu wa maisha kukufanya ujue kitu kizuri ni kipi na unakipataje. Shida inayofanya tuone elimu haina umuhimu kwa sasa ni sababu wengi baada ya kugundua kwamba elimu haiwapi ajira katika sekta rasmi, hatuoni mkitumia usomi wenu kutimiza malengo yenu.
 
Kwa baadhi ya vitivo wanafanya ivo mkuu japo kwa uchache mfano waliosomea kilimo na ufugaji, lakini kwa elimu ya tz kuna vitivo vimewekwa kwa ajili ya kuendesha sector za nchi mfano udaktari, ualimu, na masomo ya uraia(human resources)

Sasa wataka profesa wa kitivo cha elimu asie na mamlaka wala pesa agundue nini wakati yeye kasomea elimu ili apate nafasi serikalini aweze kuwafundisha wanafunzi maswala mbalimbali ya kielimu au anatakiwa nae agundue chaki zenye wino
 
Tanzania njaa nyingi sana yaani mtu akiwa na pesa wengine wote ni wapumbavu na hii inaletwa na kuwepo kwa gap kubwa lililopo baina ya wenye nacho na wasio nacho

Lakini level ikiwa sawa na watu wakaacha kulingishiana vigari vya afu 3 ushamba utatutoka wa kuiba rasilimali za nchi na kudharau taaluma
 

Wapi nimesema la saba ndiyo better ?🙄 ila hata hivyo kwenye hoja yako kuna logic hii nibora ..darasa la saba mpumbavu kuliko professor mpumbavu ...mfano ni bora machinga mpumbavu kuliko Rais mpumbavu ni bora masikini mpumbavu kuliko tajiri mpumbavu ...unajua kwanini ? Tumia akili ....hivyo darada la 7 mpumbavu madhara yake ni madogo kuliko professor mpumbavu.
 
Mkuu Elimu Gani unayozungumzia hii hii ya makaratasi ya bongo????
 
Kwa watu walioelimika wangeweza kujua hii ni Socratic Method.

Hujaelimika wewe.

Hujaweza hata kusema utamjuaje mtu aliyeelimika, hivyo hujafikia kiwango cha kusema nani kaelimika.
Kwa namna hii, huyu mpigania hadhi za wasomi ni kilaza?
 
Kwa namna hii, huyu mpigania hadhi za wasomi ni kilaza?
Kwa Tanzania, unaweza kabisa kukuta huyo mbunge anayewasema wasomi, hao wasomi, na huyu member wa JF anayewatetea wasomi wote ni vilaza.

We si unaona mjadala mdogo tu nampeleka mdogomdogo kwa Socratic Method tujue mzizi wa fitna kakimbia tayari?

Sasa msomi ni mtu wa kukimbia maswali ya Socratic Method kwenye mazungumzo basic kama haya?
 
Bado yupo pangoni huyo. Hakuna msomi hapa. instagramer unakwepa mjadala sheikh? [emoji3]
 
Hili sasa ni tatizo la mfumo sio la wasomi mmoja mmoja. Badala ya kuwafanyia bullying wasomi kama anavyofanya Msukuma bungeni tupige kelele mfumo ufanyiwe mageuzi otherwise mfumo utatuzalishia wasomi hawa hawa tu tulionao.
Uko sahihi. Mfumo uboreshwe na usimamiwe
 
Umenena mkubwa, hoja nzito sana hii.
 
Tufunge shule zote mtoto akifikia miaka 7 aende kupambana mtaani
Unaona sasa!!! Ndio maana wasomi wetu mnadharaulika, sababu yapoor reasoning!
Next time Nikikwambia siendi Kusi haimaanishi kuwa naenda Kaskazi.!!
Ngumbaro ku dharau wasomi wetu inatokana na wasomi wetu ku under perform, haimaanishi kwa amba elimu haina umuhimu.
Nimetoka mfano hapo wa mtoto wa collage aliyezindua world's first peer to peer music sharing program( napster) akiwa dormitory, Msomi wetu anamaliza chuonna degree halafu wala hajui ataifanya nini kutokana na elimu yake zaidi ya utumwa wa ajira.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…