Tusirudie tena Makosa Kwenye mchakato wa Katiba Mpya

Tusirudie tena Makosa Kwenye mchakato wa Katiba Mpya

Waziri wa katiba na sheria ameshatangaza rasmi kwamba mchakato wa katiba mpya utaanza mwezi wa Saba mwanzoni. Nilikuwa na ushauri kwamba makosa yaliyopelekea mchakato wa katiba mpya mwaka 2014 kukwama yasijirudie.

Nimeanisha makosa Kama yafuatayo:

1. Tume ya katiba ndio ipewe mamlaka ya kisheria ya kuandika rasimu ya katiba itakayojadiliwa na kupitishwa na Bunge la Katiba. Tusirudie kosa la kuliachia bunge la Katiba kuandika rasimu yake na kuitupa kapuni ile ya Tume ya Katiba.

2. Kabla ya kuanza mchakato wa katiba mpya, ningeshauri tuanze na kura ya maoni ili wananchi waamue ni mfumo gani wa muungano wanaoutaka. Je wanataka mfumo wa Unitary, Federal au confederation. Wananchi wengi wakikubali mfumo mmojawapo, basi rasimu ya Tume ya Katiba itengenezwe kwa kufuata muundo ulioamuriwa Kwenye kura ya maoni.

3. Rais asioneshe upande wake Kwenye rasimu ya katiba. Ili kosa alilifanya Mh Rais Mstaafu Kikwete. Aliposimama Kwenye bunge la Katiba na kuonesha kwamba yeye anataka katiba ya aina gani, hivyo kupelekea wajumbe wa chama chake kufuata maelekezo yake. Mwisho wa siku katiba mpya haikupatikana. Rais ajitenge kuwapelekesha wanachama wa chama chake wafuate maoni yake baadala yake awaachie Uhuru wa kujadili.

4. Tuangalie mahitaji ya Sasa na sio misismamo ya chama. Tunapoenda kuandika katiba mpya tushughulike zaidi ya matatizo yanayotukumba Leo na namna ya kuyaondoa na sio kuangalia vyama vinataka Nini. Ufisadi, maadili, Uhuru katika uchaguzi, mfumo wa kiuchumi, mamlaka ya bunge, haki jinai, sera ya kimataifa, vyombo vya ulinzi, Uhuru wa mahakama, mamlaka ya Rais, ajira, mfuko wa mapato ya gesi na mafuta, mikopo ya wanafunzi iwe Ruzuku sio mkopo, vyama vya siasa, Tume huru, shirika la Taifa la habari etc.

5. Spika au Mwenyekiti wa bunge la Katiba asitokane na chama Cha siasa. Ateuliwe jaji wa mahakama ya Rufaa ambaye atasimamia bila upendeleo bunge la katiba. Tukiweka watu wa vyama sampuli ya Tulia Akson tutapata bunge la hovyo na litakalo toa rasimu ya hovyo na ya kichama.

NB:Tukirudia makosa hatutapata katiba mpya kamwe, na Kama hatupo tayari kuandika katiba mpya ni Bora kuacha kuliko kufanya maigizo.
Asante mkuu.
 
Hapana mkuu. Ndio maana nikashauri kama hawana nia ya kuleta katiba mpya, waache kuliko kufanya maigizo.
Hapo ndipo mnakosea. Unadhani ni nani mwenye NIA hapa Tanzania ya kukuletea wewe katika sahani katiba mpya ambayo inapunguza madaraka ya Rais, inamnyanyua mwananchi na kupunguza mamlaka ya viongozi. Katiba itakayoweka usawa wa kimapato kati ya wakubwa na wadogo. Katiba itakayofanya kiongozi wa sasa ambaye alipata uongozi kwa hila; apatikani kwa matakwa ya wapiga kura. ETC

Kwa upande wangu, nitakubaliana na uundwaji wa katiba mpya IWAPO kutakuwa na katazo katika sheria kuwa mtu yeyote atakayehusika na uandaaji, utungaji na upitishwaji wa katiba mpya asigombee nafasi yoyote kwa muda wa miaka 20 including RAIS. Au asiajiriwe serikalini kwa muda wa miaka 20. Hapo tutapata katiba mpya. Zaidi ya hapo, watu watakuwa wanajitafutia ULAJI tu. Umenipata
 
Hapo ndipo mnakosea. Unadhani ni nani mwenye NIA hapa Tanzania ya kukuletea wewe katika sahani katiba mpya ambayo inapunguza madaraka ya Rais, inamnyanyua mwananchi na kupunguza mamlaka ya viongozi. Katiba itakayoweka usawa wa kimapato kati ya wakubwa na wadogo. Katiba itakayofanya kiongozi wa sasa ambaye alipata uongozi kwa hila; apatikani kwa matakwa ya wapiga kura. ETC

Kwa upande wangu, nitakubaliana na uundwaji wa katiba mpya IWAPO kutakuwa na katazo katika sheria kuwa mtu yeyote atakayehusika na uandaaji, utungaji na upitishwaji wa katiba mpya asigombee nafasi yoyote kwa muda wa miaka 20 including RAIS. Au asiajiriwe serikalini kwa muda wa miaka 20. Hapo tutapata katiba mpya. Zaidi ya hapo, watu watakuwa wanajitafutia ULAJI tu. Umenipata
Umeleta jambo zuri lakini utekelezaji wake ni mgumu. Ukisema kila aliyeshiriki kutengeneza katiba mpya asiajiriwe Wala kuteuliwa serikalini kwa miaka ishirini hiyo sheria itakuwa batili, maana itabagua baadhi ya watu. Hivyo, itapingwa mahakamani na hata bungeni haitapitishwa.

Ingawa unanipinga, ila msimamo wangu upo palepale kwamba Kama tunataka kutengeneza katiba mpya tutulie tutengeneze katiba mpya, Kama tunabahatisha tuache huo mchakato , tuendelee na ripoti za CAG na kujenga SGR.
 
Umeleta jambo zuri lakini utekelezaji wake ni mgumu. Ukisema kila aliyeshiriki kutengeneza katiba mpya asiajiriwe Wala kuteuliwa serikalini kwa miaka ishirini hiyo sheria itakuwa batili, maana itabagua baadhi ya watu. Hivyo, itapingwa mahakamani na hata bungeni haitapitishwa.

Ingawa unanipinga, ila msimamo wangu upo palepale kwamba Kama tunataka kutengeneza katiba mpya tutulie tutengeneze katiba mpya, Kama tunabahatisha tuache huo mchakato , tuendelee na ripoti za CAG na kujenga SGR.
Hakuna kitu kiliniboa wakati ule pale JK aliuliza Wabunge, nyie hamtaki kuwa mawaziri? Wote wakasema tunataka. Unajua rasimu ya Wariyoba ilitaka Wabunge wasiwe Mawaziri (kitu ambacho ni cha maana katika nchi). Siamini tulivyo tunaweza kutoa katiba mpya ya maana. Ngoja nifunge domo langu
 
Hakuna kitu kiliniboa wakati ule pale JK aliuliza Wabunge, nyie hamtaki kuwa mawaziri? Wote wakasema tunataka. Unajua rasimu ya Wariyoba ilitaka Wabunge wasiwe Mawaziri (kitu ambacho ni cha maana katika nchi). Siamini tulivyo tunaweza kutoa katiba mpya ya maana. Ngoja nifunge domo langu

Kweli mkuu, JK alikosea kuwauliza wabunge lile swali. Nakubaliana na wewe kwa jinsi mambo yanavyoenda nadhani Viongozi wetu hawawezi kutuletea katiba mpya iliyo Bora. Ndio maana nikashauri kama wanataka kuendeleza ujinga wao ni Bora waache Mara moja tufanye mengine, kuliko kuzungushwa kwa Jambo ambalo halina uhalisia.

Kenya walipata shida Kama hiyo ikabidi Mwenyekiti wa Tume ya Katiba wamtoe Hong Kong alikuwa anaitwa profesa Yash Pal Ghai. Nadhani waliona asimamie yeye aliyeko nje mchakato kuliko wenyeji wa Kenya.
 
Kweli mkuu, JK alikosea kuwauliza wabunge lile swali. Nakubaliana na wewe kwa jinsi mambo yanavyoenda nadhani Viongozi wetu hawawezi kutuletea katiba mpya iliyo Bora. Ndio maana nikashauri kama wanataka kuendeleza ujinga wao ni Bora waache Mara moja tufanye mengine, kuliko kuzungushwa kwa Jambo ambalo halina uhalisia.

Kenya walipata shida Kama hiyo ikabidi Mwenyekiti wa Tume ya Katiba wamtoe Hong Kong alikuwa anaitwa profesa Yash Pal Ghai. Nadhani waliona asimamie yeye aliyeko nje mchakato kuliko wenyeji wa Kenya.
Hapo unaanza kujielewa! Kwetu hatuwezi maana tunataka kushibisha matumbo yetu. Unajua kwanini ile ya Wariyoba ilikuwa nzuri, kwa vile Wariyoba hakuwa na vest interest. Alitenda kihaki lakini uliona alivyonyanyaswa.
 
Mzee wetu WARIOBA arudishwe ktk Tume Ili amalizie KAZI aliyoianza.

Rasimu alosimamia Judge WARIOBA kabla haijaitwa KATIBA pendekezwa irudi mezani,

Wananchi tupewe fursa ya kuongeza na kuiboresha Rasimu hiyo.

Baada ya hapo, tujadiliane mfumo upi mzuri wa kuwapata wajumbe wa kuingia Bunge la Katiba ambao watatoka Kila kundi bila mashinikizo Kutoka vyama vya siasa.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo, TANZANIA.

Amen
 
Waziri wa katiba na sheria ameshatangaza rasmi kwamba mchakato wa katiba mpya utaanza mwezi wa Saba mwanzoni. Nilikuwa na ushauri kwamba makosa yaliyopelekea mchakato wa katiba mpya mwaka 2014 kukwama yasijirudie.

Nimeanisha makosa Kama yafuatayo:

1. Tume ya katiba ndio ipewe mamlaka ya kisheria ya kuandika rasimu ya katiba itakayojadiliwa na kupitishwa na Bunge la Katiba. Tusirudie kosa la kuliachia bunge la Katiba kuandika rasimu yake na kuitupa kapuni ile ya Tume ya Katiba.

2. Kabla ya kuanza mchakato wa katiba mpya, ningeshauri tuanze na kura ya maoni ili wananchi waamue ni mfumo gani wa muungano wanaoutaka. Je wanataka mfumo wa Unitary, Federal au confederation. Wananchi wengi wakikubali mfumo mmojawapo, basi rasimu ya Tume ya Katiba itengenezwe kwa kufuata muundo ulioamuriwa Kwenye kura ya maoni.

3. Rais asioneshe upande wake Kwenye rasimu ya katiba. Ili kosa alilifanya Mh Rais Mstaafu Kikwete. Aliposimama Kwenye bunge la Katiba na kuonesha kwamba yeye anataka katiba ya aina gani, hivyo kupelekea wajumbe wa chama chake kufuata maelekezo yake. Mwisho wa siku katiba mpya haikupatikana. Rais ajitenge kuwapelekesha wanachama wa chama chake wafuate maoni yake baadala yake awaachie Uhuru wa kujadili.

4. Tuangalie mahitaji ya Sasa na sio misismamo ya chama. Tunapoenda kuandika katiba mpya tushughulike zaidi ya matatizo yanayotukumba Leo na namna ya kuyaondoa na sio kuangalia vyama vinataka Nini. Ufisadi, maadili, Uhuru katika uchaguzi, mfumo wa kiuchumi, mamlaka ya bunge, haki jinai, sera ya kimataifa, vyombo vya ulinzi, Uhuru wa mahakama, mamlaka ya Rais, ajira, mfuko wa mapato ya gesi na mafuta, mikopo ya wanafunzi iwe Ruzuku sio mkopo, vyama vya siasa, Tume huru, shirika la Taifa la habari etc.

5. Spika au Mwenyekiti wa bunge la Katiba asitokane na chama Cha siasa. Ateuliwe jaji wa mahakama ya Rufaa ambaye atasimamia bila upendeleo bunge la katiba. Tukiweka watu wa vyama sampuli ya Tulia Akson tutapata bunge la hovyo na litakalo toa rasimu ya hovyo na ya kichama.

NB:Tukirudia makosa hatutapata katiba mpya kamwe, na Kama hatupo tayari kuandika katiba mpya ni Bora kuacha kuliko kufanya maigizo.
ushindi mkubwa sana sana kwa CHADEMA hongera sana sana
 
Hapo unaanza kujielewa! Kwetu hatuwezi maana tunataka kushibisha matumbo yetu. Unajua kwanini ile ya Wariyoba ilikuwa nzuri, kwa vile Wariyoba hakuwa na vest interest. Alitenda kihaki lakini uliona alivyonyanyaswa.

Tatizo tunaendekeza uchama Sana baadala ya utaifa. Nadhani itakuwa ngumu kupata katiba mpya.
 
Mzee wetu WARIOBA arudishwe ktk Tume Ili amalizie KAZI aliyoianza.

Rasimu alosimamia Judge WARIOBA kabla haijaitwa KATIBA pendekezwa irudi mezani,

Wananchi tupewe fursa ya kuongeza na kuiboresha Rasimu hiyo.

Baada ya hapo, tujadiliane mfumo upi mzuri wa kuwapata wajumbe wa kuingia Bunge la Katiba ambao watatoka Kila kundi bila mashinikizo Kutoka vyama vya siasa.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo, TANZANIA.

Amen

Kweli kabisa. Lazima tupate njia Bora ya kuwateua wajumbe wa Bunge la Katiba mpya. Mimi ningependekeza kila kundi litoe wajumbe wenye idadi sawa.
 
Waziri wa katiba na sheria ameshatangaza rasmi kwamba mchakato wa katiba mpya utaanza mwezi wa Saba mwanzoni. Nilikuwa na ushauri kwamba makosa yaliyopelekea mchakato wa katiba mpya mwaka 2014 kukwama yasijirudie.

Nimeanisha makosa Kama yafuatayo:

1. Tume ya katiba ndio ipewe mamlaka ya kisheria ya kuandika rasimu ya katiba itakayojadiliwa na kupitishwa na Bunge la Katiba. Tusirudie kosa la kuliachia bunge la Katiba kuandika rasimu yake na kuitupa kapuni ile ya Tume ya Katiba.

2. Kabla ya kuanza mchakato wa katiba mpya, ningeshauri tuanze na kura ya maoni ili wananchi waamue ni mfumo gani wa muungano wanaoutaka. Je wanataka mfumo wa Unitary, Federal au confederation. Wananchi wengi wakikubali mfumo mmojawapo, basi rasimu ya Tume ya Katiba itengenezwe kwa kufuata muundo ulioamuriwa Kwenye kura ya maoni.

3. Rais asioneshe upande wake Kwenye rasimu ya katiba. Ili kosa alilifanya Mh Rais Mstaafu Kikwete. Aliposimama Kwenye bunge la Katiba na kuonesha kwamba yeye anataka katiba ya aina gani, hivyo kupelekea wajumbe wa chama chake kufuata maelekezo yake. Mwisho wa siku katiba mpya haikupatikana. Rais ajitenge kuwapelekesha wanachama wa chama chake wafuate maoni yake baadala yake awaachie Uhuru wa kujadili.

4. Tuangalie mahitaji ya Sasa na sio misismamo ya chama. Tunapoenda kuandika katiba mpya tushughulike zaidi ya matatizo yanayotukumba Leo na namna ya kuyaondoa na sio kuangalia vyama vinataka Nini. Ufisadi, maadili, Uhuru katika uchaguzi, mfumo wa kiuchumi, mamlaka ya bunge, haki jinai, sera ya kimataifa, vyombo vya ulinzi, Uhuru wa mahakama, mamlaka ya Rais, ajira, mfuko wa mapato ya gesi na mafuta, mikopo ya wanafunzi iwe Ruzuku sio mkopo, vyama vya siasa, Tume huru, shirika la Taifa la habari etc.

5. Spika au Mwenyekiti wa bunge la Katiba asitokane na chama Cha siasa. Ateuliwe jaji wa mahakama ya Rufaa ambaye atasimamia bila upendeleo bunge la katiba. Tukiweka watu wa vyama sampuli ya Tulia Akson tutapata bunge la hovyo na litakalo toa rasimu ya hovyo na ya kichama.

NB:Tukirudia makosa hatutapata katiba mpya kamwe, na Kama hatupo tayari kuandika katiba mpya ni Bora kuacha kuliko kufanya maigizo.
Ile rasimu ya Warioba ndio itajadiliwa upya na bunge la katiba au ile ya kina Sitta (Rip) itajadiliwa upya na kupigiwa kura ?

JokaKuu zitto junior Bams
 
Kweli kabisa. Lazima tupate njia Bora ya kuwateua wajumbe wa Bunge la Katiba mpya. Mimi ningependekeza kila kundi litoe wajumbe wenye idadi sawa.
Iwepo pia kamati au watu makini watakaopita wateuliwa wa makundi hayo wasijekuwa wameteuliwa kisiasa.

Kwa mfano, mfumo uliopo, ukienda kutafuta wawakilishi wa walimu Tz, utakuta mkono wa CCM,

Ukienda Kwa MACHINGA, CCM wamepenyeza viongozi wao huko, sekta ya usafirishaji CCM wameweka viongozi Kwa maslah Yao, ktk michezo ndo usiseme, ukienda Majeshi utawakuta, ukija ktk viongozi wa dini, wengi wamo kwenye payrol, waandishi wa habari ndo usiseme,nk nk nk.

In short, ukienda ktk makundi hayo na kupeak viongozi, utajikuta unakokota mapandikizi ya KIJANI bila kujua.

Ingeundwa Tume hiyo ambayo ingeenda ktk kundi moja moja na kuendesha uchaguzi na kuchambua Kwa weledi kupata watakaosimamia maslah ya nchi bila kuingiliwa na mashinikizo ya vyama vya siasa.
 
Mzee wetu WARIOBA arudishwe ktk Tume Ili amalizie KAZI aliyoianza.

Rasimu alosimamia Judge WARIOBA kabla haijaitwa KATIBA pendekezwa irudi mezani,

Wananchi tupewe fursa ya kuongeza na kuiboresha Rasimu hiyo.

Baada ya hapo, tujadiliane mfumo upi mzuri wa kuwapata wajumbe wa kuingia Bunge la Katiba ambao watatoka Kila kundi bila mashinikizo Kutoka vyama vya siasa.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo, TANZANIA.

Amen
Rasimu ya Katiba ya Warioba na Ya Sitta zijadiliwe kwa pamoja na kuongeza au kupunguza mambo muhimu na bila kuathiri uwepo wa muungano hapo mtafaulu. Mengine ni mepesi ukiondoa suala la muungano tu,ukarabati wake usilenge kuleta mabadliko ya kimuundo,bora ucheze na mifumo yake.
 
Mzee wetu WARIOBA arudishwe ktk Tume Ili amalizie KAZI aliyoianza.

Rasimu alosimamia Judge WARIOBA kabla haijaitwa KATIBA pendekezwa irudi mezani,

Wananchi tupewe fursa ya kuongeza na kuiboresha Rasimu hiyo.

Baada ya hapo, tujadiliane mfumo upi mzuri wa kuwapata wajumbe wa kuingia Bunge la Katiba ambao watatoka Kila kundi bila mashinikizo Kutoka vyama vya siasa.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo, TANZANIA.

Amen
Rasimu ya Katiba ya Warioba na Ya Sitta zijadiliwe kwa pamoja na kuongeza au kupunguza mambo muhimu na bila kuathiri uwepo wa muungano hapo mtafaulu. Mengine ni mepesi ukiondoa suala la muundo wa muungano tu,ukarabati wake usilenge kuleta mabadliko ya kimuundo,bora ucheze na mfumo na sera zinazoendana na uimarishaji wake. Mbinu nyingine ni kukubaliana na machache yasiyo radical baadaye makubwa yatakuja kulingana na mabadiliko ya kijamii kuliko kungangania radicalism ukakosa vyote km wakati ule.
 
Rasimu ya Katiba ya Warioba na Ya Sitta zijadiliwe kwa pamoja na kuongeza au kupunguza mambo muhimu na bila kuathiri uwepo wa muungano hapo mtafaulu. Mengine ni mepesi ukiondos suala la muungano tu,ukarabati wake usilenge kuleta mabadliko ya kimuundo,bora ucheze na mifumo.
Rasimu ya Warioba ilipendekeza ziwe 3 na ilionyesha njia Bora sana ya kupunguza gharama za uendeshaji wa Serikali.

Anyway tukijadiliana Kwa kina tutaelewana tu, idadi ya sirikali Si issue, tunataka Kodi za raia ziwarudie,

Kodi zirudi kusaidia kuwalipa posho wasio na ajira angalau waweze kujikimu, wasirudi kutegemea wazazi kama watoto.

Kodi zetu zisaidie wazee wote walipwe pension bila kujali waliajiriwa au hawakuajiriwa sirikalini maana wote walilitumikia Taifa sekta rasmi na isiyo rasmi.

Kodi zetu zisaidie matibabu yawe Bure Kwa wananchi wote. Bima Kwa wote iwezekane sababu tunalipa Kodi.
 
Back
Top Bottom