Tusiwasimange wanawake kwa kuchelewa kuolewa

Tusiwasimange wanawake kwa kuchelewa kuolewa

Joel360

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2013
Posts
986
Reaction score
657
Habari za mchana huu.

Naomba nizungumzie jambo moja lisilo zuri leo.

Kumekuwa na tabia ya kusimanga wanawake ambao hawajaolewa na kuwafanya wajione hawafai. Watanzania wenzangu hii tabia sio nzuri. Naomba tusiwasimange wanawake ambao hawajaolewa kwa maneno ya kejeli au dharau.

Kufanya hivyo kutawafanya wajione wana hatia kwa wao kuchelewa kuolewa na kunaweza kuwapelekea kufanya maamuzi yasiyo sahihi yaani kuolewa na mtu asiye sahihi kisa tu kupunguza masimango.

Tusiwasukume dada zetu, wadogo zetu au mabinti zetu kufanya maamuzi mabaya na ya haraka haraka eti kisa tu wanapaswa kuolewa. Hili suala sio tu linawaathiri mabinti zetu kisaikolojia lakini pia linaweza kuwasababishia kuharibu maisha yao kwa kufunga ndoa na watu wasio sahihi (violent person au asiejali familia) kwa sababu ya kuharakisha ndoa.

Wewe mwanamke ambao bado hujaolewa. Ndoa ni maamuzi ya maisha na ni maamuzi BINAFSI kuyafanya. Hakuna umri ambao si sahihi kuolewa. Huna haja ya kufanya maamuzi haya kwa sababu tu ya maneno wanayozungumza majirani zako.

Nimalize kwa kushauri kuwa, kutokuolewa kusikufanye ukataka kumkosea Mungu kwa kufanya ngono kabla ya ndoa. Mwanamke JITUNZE. Njia sahihi ya kutosheleza mahitaji ya kimwili kati ya mwanamke na mwanaume ni kupitia ndoa tu katika njia inayofaa na inayoendana na asili ya mwanadamu.
 
Single Mother wengi vichomi japo sio wote,nakumbuka mjomba wangu ameoa akiwa kama na miaka 40,alimuoa single mother aliyepewa mimba shule ila kajiendeleza mpaka chuo.

Yule shangazi alikuwa anampenda mjomba na alimbadilisha mjomba sisi wenyewe hatukuamini,mjomba alikuwa mtu wa fegi, bange na mitungi,halafu maisha yake ya ujana yalikuwa fujo sana.Ila tokea aoe bangi na sigara kaacha ila pombe kapunguza, mwili umerudi na akajenga nyumba mbili na gari faster mpaka kanisani akawa anaenda.

Ila kumpata kama aliye mpata mjomba wangu shughuli.
 
Single Mother wengi vichomi japo sio wote,nakumbuka mjomba wangu ameoa akiwa kama na miaka 40,alimuoa single mother aliyepewa mimba shule ila kajiendeleza mpaka chuo.

Yule shangazi alikuwa anampenda mjomba na alimbadilisha mjomba sisi wenyewe hatukuamini,mjomba alikuwa mtu wa fegi, bange na mitungi,halafu maisha yake ya jana yalikuwa fujo sana.Ila tokea aoe bangi na sigara kaacha ila pombe kapunguza, mwili umerudi na akajenga nyumba mbili na gari faster mpaka kanisani akawa anaenda.

Ila kumpata kama aliye mpata mjomba wangu shughuli.
Siyo shughuli mkuu ni mbinde...
 
Umenitisha kidogo,ila mi nadhani tunaongoza kwa stress kiukweli
Stress gani unayo mamy??
IMG_20210715_154727_9.jpg
 
Mi nimeolewa,hatuongoz kwa kufa ila tunaongoza kwa stress na ndoa zetu.Sitoacha kutetea single mothers wala wasichana age 30s ambao bado hawajaolewa coz ndiko nilikotoka na sijaona umuhimu wa ndoa kiukweli.Nimemiss usingle wangu
Kuolewa Ni mipango tu.kuolewa uolewe na perfect match
Kama uliolewa ili uonekane utakoma
Maisha Ni mipango tu furaha yako utaiset mwenyewe
 
Kweli mtoa mada umenena kama vile pastor upo madhabahuni.
Kuna dada 2 nawafahamu wanahangaika sana kuolewa mpaka mwingine kaniambia akipata mwanamume anatamani aolewe na apart watoto mapacha maana kachelew kuzaa.

Anawaza hivyo akati hata mume mwenyw hajampata.!
 
Mi nimeolewa,hatuongoz kwa kufa ila tunaongoza kwa stress na ndoa zetu.Sitoacha kutetea single mothers wala wasichana age 30s ambao bado hawajaolewa coz ndiko nilikotoka na sijaona umuhimu wa ndoa kiukweli.Nimemiss usingle wangu
Kuna mdada pia aliwahi kuniambia ni bora angekua single kuliko ndoa aliyonayo.

Huwa mnapitia nini huko ndoani mpaka muwe na hali kama hiyo kina dada??
 
Single Mother wengi vichomi japo sio wote,nakumbuka mjomba wangu ameoa akiwa kama na miaka 40,alimuoa single mother aliyepewa mimba shule ila kajiendeleza mpaka chuo.

Yule shangazi alikuwa anampenda mjomba na alimbadilisha mjomba sisi wenyewe hatukuamini,mjomba alikuwa mtu wa fegi, bange na mitungi,halafu maisha yake ya ujana yalikuwa fujo sana.Ila tokea aoe bangi na sigara kaacha ila pombe kapunguza, mwili umerudi na akajenga nyumba mbili na gari faster mpaka kanisani akawa anaenda.

Ila kumpata kama aliye mpata mjomba wangu shughuli.
Tupo wengi tu masingle mother ,tukiamua kuolewa huwa tunafanya kila liwezekanalo kuifanya ndoa iwe na maana kwakila nyanja
 
Back
Top Bottom