Tuulize chochote kuhusu mbao na changamoto zake

Tuulize chochote kuhusu mbao na changamoto zake

Huu mnakasha una majibu ya maswali mengi. Pitia neno kwa neno.
 
Mbao ya mwembe ni nafuu na nzuri kwa kutengenezea samani,lkn zinaliwa sana na wadudu,nifanyeje ili zisiliwe?
 
Nina wasiwasi lkn ukizitreat halafu ukaziranda si ile dawa itapotea?
Kuna namna nyingi za kufanya treatment mojawapo ni kuziloweka mbao kwenye dawa. Ubao unanyonya dawa mpaka ndani, hata ukiziranda dawa inabaki.
 
Heri ya mwezi mpya,

Sisi ni wataalamu wa mbao za aina mbalimbali zinazozalishwa nchini Tanzania. Tupo Dar es Salaam. Tunao ujuzi na uzoefu wa miaka mingi.

Kama inavyofahamika, shughuli za ujenzi wa majengo na baadhi ya miundombinu hapa kwetu kwa kiasi kikubwa bado hutegemea mbao kama mojawapo ya nyenzo muhimu.

Je, unawezaje kutambua mbao nzuri, imara na zinazofaa kwa mradi anuai?

Tumekuja JamiiForums kujuzana na kuepusha hasara ambayo wadau wa ujenzi hukumbana nazo, yakiwemo makampuni na watu binafsi kutokana na kutokuwa na uelewa wa kutosha.

Tutajibu maswali yote tutakayoyamudu kwa wakati.

Karibuni sana.
Natafuta machine ya kuchana mbao
 
Wewe lazima utakuwa multi-millionea, kuezeka nyumba kwa kutumia mbao za mninga? Unajua bei ya mninga?
Kwanza kupatikana ni shughuli, hata hizi furniture wanazotuuzia mpaka million kadhaa kwa kitanda huwa sio Mninga hasa, ni wanatuchota tu
 
Back
Top Bottom