Tuungane kukemea ajali hizi, nyingi zina uzembe ndani yake

Tuungane kukemea ajali hizi, nyingi zina uzembe ndani yake

Determinantor

Platinum Member
Joined
Mar 17, 2008
Posts
59,045
Reaction score
94,974
Ni takribani mwezi na Kidogo tangu gari ya serikali ipate ajali mbaya sana na kuwamaliza abiria wote. Ilikua STL iliyoaminika kuwa ilikua ya Ofisi ya Waziri Mkuu.

Leo Tena gari ya serikali imeondoka na roho 14 za Watanzania ambao ni nyuma Yao wanategemewa na familia zao na ndugu zao.

Kuna tukio lingine (sikumbuki vyema) la gari la Jeshi kusababisha ajali.

Hii ni mifano michache tu inayoumiza saana maana tunavyoandika muda huu Kuna watoto tayari wameshakua yatima... inaumiza sana!

Chanzo Cha ajali nyingi za magari ya serikali ni mwendokasi na kutokujali alama za barabarani huku Askari waliokabidhiwa ada ya kusimamia Sheria na kanuni wakiishia kuwabana Maderava wa magari binafsi.

Magari ya Polisi, Serikali, Jeshi, Mahakama na wengine wa dizaini Yao ndio wanaongoza kwa kuvunja Sheria na kanuni za matumizi ya Barabara bila kuchukuliwa hatua.

Mfano, Leo ni gari ngapi za Polisi ambazo hazina usajili kamili? Zinatumia namba za Malaysia na nchi nyingine as if ni sahihi, mambo kama haya ndio wahalifu kama Akina Sabaya walitumia namba bandia kuvamia makazi ya Mbowe.

STL, STK, STJ, SU, JW na wengine hakuna anayeona kibao Cha 50km/hr Wala Zebra crossing 🚸. Wakitaka kupita Wala hawaangalii Wala kuchukua tahadhari yoyote matokeo yake ajali ikitokea Polisi wanakubebesha wewe, rejea ajali ya Tanga ambapo RTO Tanga aliandika maelezo ya uongo.

Wakuu, tumezika sana inatosha, tumelia sana inatosha! Polisi waache kuwaogopa, wasimamie haki.

Pia sio lazima misafara ya Viongozi iendeshwe kwa speed Hali Barabara zetu na magari yetu havina ubora huo. Rejea ajali ya DC wa Moro na yule Mkurugenzi Binti wa Morogoro sikumbuki wilaya.

Nyingi ni uzembe, TUANZE KUWARIPOTI POLISI AMBAO HAWAWACHUKULII HATUA MADEREVA WA SERIKALI wanaovunja Sheria ikiwa ni pamoja na abiria wao kutokufunga mikanda wawapo safarini.

Tujifunze kwa International NGOs Tena hapa bongo ambapo kama Boss au Abiria hajafunga belt dereva anaruhusiwa kutokuondosha gari Hadi ufunge.
 
Kuna ile ajali ya TRA, yaani wanaona wao ndo wana haki ya kuwahi,wanatanua wanawasha mataa ole wako usipishe?

Unategemea hawa ndi madereva kutoka NIT wanaujuzi wote lakini ndo majanga zaidi.

Kunakipindi kampuni zinazohusika na kujaza mafuta kwenye minara ya simu ziliweka namba za simu na maneno yameandikwa "Ninaendeshaje?" . Baada ya muda mfupi madereva wote walikuwa wanaendesha kwa nidhamu.

Naona hata hili litumike pawe na namba tureport pia polisi wafanye kazi yao.
 
Wakati zinatakiwa gari za ccm ndio zipate kashikashi kama hizo.

Matokeo ya mwendo wao ni kupoteza maisha ya watanzania wasiopenda mwendo
December nilikua Mkoa Fulani nikakutana na msafara wa CCM eti wanakagua miradi, basi msafara mrefuuuu wakawa wanakagua ujenzi wa Barabara ya lami.....nikacheka sana. Bonge la msafara na wale vijana wamekula vumbi utadhani wanakimbiza mwenge
 
kiujumla mamlaka hazichukulii serious ajira za madereva kuanzia serikali mpaka huku uraiani.

Utoaji wa driving licence Tanzania ni wakiholela sana kwa madereva wote tu.

Askari wa usalama barabarani hawako serious kwenye usimamizi wa sheria barabarani.

Tanroad na Tarura hawako serious kwenye ujenzi na usimamizi wa barabara.

Matatizo ni mengi sana
 
Mkuu wa police hatoshi kwenye nafasi hiyo ajiuzulu
Kama anashindwa kutoa amri na kuwawajibisha wa chini basi aondoke

Nchi zilizoendelea angejiuzulu mwenyewe
Ingawa hakuna ajali za kizembe hivyo

Watu wa serikali ndio wanaongoza kuuwa kwa ajali Tz
Hawana nidhamu na Mkuu wa Police anawaogopa
 
Hizi gali za serikali nchi nzima ndio vinara wa kusababisha ajali, kwanza hawajali kabisa sehemu yapaswa kutembea mwendo mdogo wao spidi zote wanamaliza alafu hakuna hatua yoyote inayochukuliwa na polisi wamekaa tu, iyo ajali ya jana ni uzembe matokeo yake watu wamepoteza wapendwa wao bila sababu za msingi eti wanaenda kukagua miradi maspidi makubwa ambayo ayana tija yoyote matokeo yake miajali
 
Back
Top Bottom