Tuungane mkono dhidi ya Kunyamazishwa

Tuungane mkono dhidi ya Kunyamazishwa

Wakipatikana Kina, Ben 9.Azor,Lijenje thread yako itakuwa na uharali mioyoni mwa wengi ndugu.
Tunashukuru Mungu kutuondolea Dubwasha Fran Hivi.

Kunya anye kuku,akinya Bata.....
 
Tumia falsafa ya hali ya juu! Namna ya kumpinga mtu aliyeshikilia mpini wa kisu nawe umeshika makali. Hakika asipoachia mpini wewe wa makali utaumia. Ni muungano wa hali ya juu kumfanya aachie mpini.
 
Tumia falsafa ya hali ya juu! Namna ya kumpinga mtu aliyeshikilia mpini wa kisu nawe umeshika makali. Hakika asipoachia mpini wewe wa makali utaumia. Ni muungano wa hali ya juu kumfanya aachie mpini.

Kwani huu mpini anaushika kwa niaba ya nani?
 
Mpini anaushika kwa niaba ya wanachi! Mkimpa mpini asiyeeleweka ni juu yenu, SI mliamua wenyewe? Mbunge akiwahonga na mkampa idhini ya ubunge ni juu yenu!!
 
Haki ya maoni ni haki ya kikatiba.

Anayedai katiba kuheshimiwa anastahili kuungwa mkono kikamilifu kwa mukthadha huo.

Polepole kupinga kunyamazishwa ni dai halali kwa mujibu wa katiba.

Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.

Pamoja na mapungufu yake kwa kutoa maoni yake, hili la watu wasiojulikana kumwandama ni la kupigiwa kelele hata kama yeye alidhani halimhusu:

View attachment 2042530

Leo ni TV na watu wasiojulikana kesho ya akina Ben, Lijenje na kina Mhina yatamhusu.

Ikumbukwe juzi ilikuwa kina Lijenje kesho nani aijuaye?

Tuupinge udhwalimu bila kujali mtendwa nani.

Acha Polepole ashughulikiwe, wakati wenzake wanapigwa risasi hakuona sababu ya kuzungumza wala kutoa shule ya uongozi kwa sababu alikuwa kivulini.

Naomba sana wamshughulikie na wamnyamazishe alaf ndo turudi kuomba hilo unaloleta hapa leo
 
Back
Top Bottom