Tuwafahamu Watu Maarufu waliokuwa wanatajwa sana na Wanamuziki wa Band nchini Tanzania

[emoji23][emoji23][emoji23]Fikiri madinda kanichekesha sana
 
Kuna pedeshee mmoja alimtwanga mtu risasi mitaa ya Magomeni usalama kwa anaekumbuka alikua ni pedeshee yupi?
 
Nshawah kumilik kiofis mitaa hio ikawa nikiwapa adress ya ofis clients wangu wanajua mimi ninja sometimes wananilitea michongo yao tata niwasaidie nikawa nashangaa inamaana ninamuonekano wa kininja? Ndio baadae nikaja kujua niko kwa empire ya maninja na mengine yashakua majamaa yangu since then huniambii kitu kuhusu huu mji
 
Umemsahau Andrew Sekedia
 
sijui kwanini huwa napenda sana stori za kitambo.za wajanja wa zamani na vituko vyao.
majamaa zamani walifaidi sana maisha.
Wakati huo mambo yalikuwa ni moto, pale Salender club pink coconut kuanzia ijumaa ni bolingo la kufa mtu, huku Radio one unakuta DJ Rankim Ramadhani Nyamka yuko hewani anaachia Bolingo za hatari.

Ukiwa na peugeot 504 umeifunga mziki mkubwa dunia yote ilikuwa ni yako na tiketi ya kuingia hadi kwa watoto wa kishuwa unawakula tu.

Ukumbuke kipindi hicho ukitaka kwenda Uingereza ni kama unaenda Kenya tu, unakata ticket unaruka tu unaenda kugongewa entry Heathrow London.
 
ila diamond amefanya mambo ya kutajana majina(shout out)kwenye nyimbo kuwa jambo rahisi sana. imagine siku hizi hata akina juma lokole majina yao yanasikika kutajwa kwenye nyimbo za bongofleva.

miaka ile haikuwa jambo rahisi, ilitakiwa lazima uwe financially stable ili uweze ku facilitate mahitaji muhimu ya wanamuziki.

mathalani,kuwalipia pesa studio wakati wa kurecord album, kuwalipia kodi pale wanapokwama, kuwajazia mafuta kwenye gari zao, kuwapa pesa ya matumizi yao binafsi, kutumia connection zako kurescue situation pale mwanamziki anapokuwa ameingia ktk matatizo na vyombo vya dola nk. hayo ndio maeneo mapeshee walikuwa wanachukua point tatu.

nje ya hapo, ili jina lako liwe linatajwa sana, ilitakiwa uwe shabiki kindakindaki(loyal fan)wa
mziki wa dansi na usiwe unakosa kwenye show za band kila zinapotumbuiza.
 
Nasikiliza Maria nyimbo ya Fali Ipupa sasa hivi mwisho naskia anamtaja Erick Mandala.
uyu Erick Mandala ni mwanasia,mfanya biashara ama nani kule Congo?
Hao Wanamuziki wa Congo wote break yao kuna Don wa Ki Ivory coast anaishi Paris anaitwa Hemed Bakayoko, huyu ndio funga kazi, hii treasure.

Huyu ndio hakauki mdomoni mwa Boss ya Mboka Koffi Ollomide then ndio anakula shavu Samuel Etoo, hizi ni international level.
 
Kweli huyu bakayoko kwnye twanga fotoo nimesikia jina lake
 
kuna siku nilishuhudia tukio la kusikitisha na kuchekesha pia.

tukio lenyewe lilitokea mtaa wa india street mkabala na jengo la haidary plaza jirani na bureau change moja maarufu wakati huo.

mission town walikuwa wamempiga mkenya vidollar vyake. walimuwahi nje akiwa anaelekea kuingia ndani ya ile bureau ku exchange dollar zake.

wakamwambia ndani ya bureau atapata pesa kidogo, ila wao watamfanyia exchange rate na atapata pesa nyingi za ktz.

mkenya akakubali. masikini hakujua kama zile fedha za ktz alizopewa na wale mission town zilikuwa fake.

baadae akarudi pale hakukuta mtu, akabaki anatukana tu hovyo hovyo. kajaa hasira huku jasho likimtoka, kalowa chapachapa.

watu wanamtazama tu, wengine wanamcheka.
 
Huo ni uzembe wa mtu binafsi, angalau enzi za Nyerere na Mwinyi pale Empress Cinema wazungu walipigwa sana kwenye kuchange Dollar maana zamani maduka ya kubadili pesa za kigeni yalikuwa yamebaniwa.

Mimi mwaka 1996 mara yangu ya kwanza kufika Jiji la Johannesburg nilikutana na changamoto hiyo hakukuwa na Bereau de change nilielekezwa dukani kwa muhindi Carton Center karibu na holiday inn hotel nikachenjiwa hapo, dollar moja kwa Rand 4.

Kuna vitu hata kama siyo rasmi ni lazima uangalie unafanya katika mazingira gani.
 
hamed bakayoko is no more, alifariki last year kwa Covid . koffi olomide aliomboleza sana msiba wake. yeye na koffi walikuwa ni marafiki wa karibu sana.

bakayoko alikuwa ni raia wa ivory coast. a politician, rich businessman, music promoter, influencer and prominent figure in francophone countries.

nilikuwa nafatilia sana habari zake wakati angali hai.

 
Mkuu Mboni alitisha nashindwa kuamini kama ndio huyu Mboni wa sasa kwenye runinga au yule wa fally Ipupa ni Mboni mwingine, sidhani kama siku ile alienda kulala kwao au kwake..
 
Nteze wa Nteze jee!!??
Mimi sijaona jina langu,nikaangalia kumbe ni list ya miaka ya 90 na 2000.
Sisi wa enzi za Watunjatanjata, Ngoma za maghorofani, tunacomment wapi!!?
Nimekumbuka Marques Du Zaire, MK Beats, Juwata, Vijana, Tancut Almas.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…