Tuwafahamu Watu Maarufu waliokuwa wanatajwa sana na Wanamuziki wa Band nchini Tanzania

pedeshee kifaranga toto ya kuku, pedeshee diamond totoo ya bisandra pedeshee konde baby ya kajala, haya ongezeeni....
Hahah hakuna petdeshee za hivyo mkuu kipindi hiko wenye petdeshee yao mkiwa live band akitajwa jina kule mbele toka anatoka alikokaa mpaka anafika stejin katikati hapo anaowajua wote washalamba ten ten wewe kazi yako mtaje jina tu anajua huyu mwana unakoga hela.

Jamaa walikuwa na maisha flani classic sana amtake demu wako amkatae?umempa nini wewe huyo mwanamke?
 
ahsante ndugu mwandishi kiufupi mie sio mhenga kiivo lakini nafurahishwa na nyimbo hizo na ndo mara nyingi husikiliza,kiufupi umeukonga moyo wangu
[emoji1431][emoji1431][emoji1431]
 
Kuna pedeshee mmoja alimtwanga mtu risasi mitaa ya Magomeni usalama kwa anaekumbuka alikua ni pedeshee yupi?
Ni Papaa Msofe na marehemu alikuwa muuza madini!

Ila Msofe yeye alikuwa hana mambo ya bunduki alijichanganya kwa Mchagha Masawe Alex akanunua nyumba iliyokuwa dhamana ya mkopo kati ya marehemu na Masawe so Mchagha alivyopokea hela akavunja uwa akaenda South huku nyuma Msofe akamtaka mmiliki wa awali ahame achukue nyumba yake jamaa akagoma akataka kupeleka kesi mahakamani Masawe kusikia hivyo na kuogopa kuambiwa arudishe hela akarudi akatuma kikosi kazi kikammaliza jamaa ilikuwa mapema tu saa 19:50 usiku.

Msofe aliunganishwa kwenye kesi kutokana na simu ya marehemu kukutwa na chatting kutoka # yake zilizoonyesha kutofautiana na jamaa muda mfupi kabla ya kifo chake.
 
Aisee..
Umenikumbusha zamani sana, ilikuwa wazee wote wa mishen town wako Salamander na Empress cinema....mara Mzee Michuzi anapita na kamera yake
 
Duuh..
Yaani kama najikumbuka nimemaliza O level miaka ile, naeda kuegesha kwa mshikaji mitaa ya Samora, karibu na R.I.P Mzee wa Pazi basketball alikuwa na Clearing/Forward kawapa wachezaji wote dili za mishemishe za bandarini , nilikuwa nikipita sana mitaa ya Salamander.
 
Sio Mchezo..
Halafu miaka hiyo, sio muda mrefu kurudi nyuma ilikuwa kwenda UK na nchi kadhaa ni "viza free"
Nimewapeleka sana wasomali kwa wazeewa bandika bandua na vifo na vizazi halafu hao wanakwea pipa na dili linasawazishwa mpaka airport wanakuwa wameshatonywa wanapitishwa hapo ni mpaka UK.
 
[emoji91][emoji91][emoji91][emoji91]
 
Hawa ndio wamesababisha bond mahakamani wanataka mtumishi wa serikali.
 
Ndama mtoto ya ng'ombe maisha haya yana leo na kesho
Huyu Ndama mtoto wa ng'ombe nae kaanzia hapo hapo kwenye kijiwe cha Azam kwa shoe shiner, alikua mshamba tu tunamtia makwenzi enzi zetu. kakulia kule magomeni mapipa ukitoka mjini kushotojuu kule kama unaenda kigogo. Alitoka huko kwao kigoma mdogo kaja sijui kwa ankali wake basi tukicheza mpira tunamtia mikwenzi tu. Na mtu aliemleta mjini kwenye kile kijiwe ni jamaa mmoja nimemsahau jina lake(alikua na anaweka Culkit) yeye kijiwe chake Empress pale na kina Masudi-marehemu. eti Ndama baadae akawa pedeshee daah maisha haya acha tu. Ila deals iliomuinua nasikia walimzika myahudi kumuuzia dhahabu fake. Pedeshee ndama!!!πŸ˜‚πŸ˜‚ Ila nasikia ndama baadae alivopata pesa akamuoa mnenguaji wa kikongo wa FM academia akiitwa Mirayesa na ndio wako nae mpaka sasa.
 
Ha hah ila Wakongo na njaa zao wakiamua kukupamba utapewa kila aina ya cheo,wewe warushie buku 10 tu na usikose kwenye dansi lao.ila shida wakikuzoiea wanahamishia shida zao kwako.
Siku moja nilikwenda Ngwasuma Heineken house, nilikuwa na katibu wa Wacongoman Tanzania, basi tulikula senene wa kutosha na mimi siku hiyo nilikuwa PDG, yule jamaa akawapa jina langu, basi nilivyokwenda kuwatunza nikashangaa wanalitaja jina langu halafu Nyoshi anasema baada ya Mungu ni wewe, kwakweli nilichoka aisee, hawa jamaa funga kazi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…