Tuwakumbuke waandishi wetu wa Riwaya


LOL! Kufa na Kupona = Live and Let Die ?
 
XP hivyo vyote uli visoma? You must be very rich! Riwaya zina utamu wake ingawa sidhani kama ukienda pale TPH Samora Avenue utavikuta hivyo vitabu

vinapatikana, unamkumbuka lakini BWANA MSA?
 
Mpenzi, Kitanda cha mauti - KAJUBI MUKAJANGA
Makuadi wa Soko huria - SEITHY CHACHAGE
Gamba la Nyoka - Euphrase Kezilahabi
Nyota ya Rehema - Mohamed S. Mohamed
Doa Jeupe - Comrade Companero
Miradi Bubu ya Wazalendo - Gabriel Ruhumbuka
Mukwava wa Uhehe - Mugyabuso Mulokozi
Kumbatio la Mwenye Makosa - Mzee Mwanakijiji
 
Aisee ni kweli kuwakumbuka lakini cha kusikitisha ni kwa nini baadhi ya vitabu vilifungiwa au kuondolewa kwenye mtaala? kimtindo naona kama sio sawa... naomba mnisaidie wakati tunawakumbuka tutafakari na hilo jamani AU?
 
Wapi hivi vitabu vinapatikana kwa sasa?
 

mkubwa tuazime jamani!ntakupm
 
Shangwe na Juma mtoto yatima "tonge nyama" vilikuwa vitabu vya ukweli...
 
Hapa ningependa kumtambua Mtunzi na mfanya biashara maarufu sana kule kanda ya Ziwa.
Elistablus Elvis Musiba. yeye alitunga vitabu hivi
1. Kikosi cha kisasi
2. Njama
3. Kikomo
4. Hujuma.
 
Mzimu wa Watu wa Kale, Kisiwa cha Giningi, Duniani Kuna Watu, Siri ya Sifuri, Mke Mmoja Watume Watatu, Mwana wa Yungi Hulewa, By Muhammed Said Abdulla

Umenikumbusha mbaaali sana kuhusu mtunzi huyu Ammi Moh'd.

Hakika asiyesoma vitabu vake basi amekosa mengi sana. Siku zote nilikuwa namfananisha na Marhum Shaaban Roberts.
 
Umenikumbusha mbaaali sana kuhusu mtunzi huyu Ammi Moh'd.

Hakika asiyesoma vitabu vake basi amekosa mengi sana. Siku zote nilikuwa namfananisha na Marhum Shaaban Roberts.

His books are splendid and heartwarming...!
 

Kumbe ndiyo maana ile shule ina upungufu wa Vitabu !!Unaonaje ukivirudisha Mkuu? aha aha aha. utani tu
 
Wakati titi la Nyati, hukamuliwa kwa shaka.
Wakati mwana Banati, waendao wana shaka.

Wakuu wenye kukumbuka ,tafadhali naomba mniwekee beti mbili tatu za Shairi hili
 
Shaaban Robert
1. Adili na nduguze
2. Kusadikika
3. Kufikirika
4. Maisha yangu na baada ya miaka 50

JOMSSI(John Msimbe Simon Simbamwene)
vitabu vingi tu vya kamanda shupavu Inspecta Fog

TV zimeua kabisa utamaduni wa kupenda kusoma, zama hizo tukishindana idadi ya novel ulizosoma mfano nakumbuka nikiwa form three, Tanga School back in 1993, nilisoma novel kubwa about 600 pages in less that 4 days, novel yenyewe ikiitwa Kane and Abel.

Siku hizi wenetu wanashindana kwa idadi ya movie walizoona katika TV na video plus kama unaweza kuchezea playstation na other video games, badili ya kucheza soka uwanjani siku hizi inachezewa kwenye video!!!

kweli wakati umebadilika!!!!
 
Wimbi la kitintale, (Ibra radi washokera kama sijasahau)
 
Ongeza Hofu na Hujuma
Hapa ningependa kumtambua Mtunzi na mfanya biashara maarufu sana kule kanda ya Ziwa.
Elistablus Elvis Musiba. yeye alitunga vitabu hivi
1. Kikosi cha kisasi
2. Njama
3. Kikomo
4. Hujuma.
 
.... KIJASHO CHEMBAMBA ! ................... Eddi Ganzel
Kabla sijaanza kusoma 'novel' za kiingereza k.m. James Hadley Chase na Nick Carter, huyu mwandishi mzalendo alikuwa ananivutia sana na hadithi zake hasa zile zilizokuwa zikitoka gazetini (sikumbuki ni gazeti gani). Kuna hadithi yake ilikuwa inasimulia kachero mmoja aliyekuwa anapambana na kundi la majambazi yaliyokuwa yanaitwa 'Vinyamkela'. Nilikuwa najificha chumbani ili nisome hizo hadithi bila bughdha, na mara nyingi tu nilikuwa natafutwa sionekani, hasa wakati wa chakula, kumbe nasoma hadithi za kusisimua za 'Vinyamkela'. R.I.P. Eddie Ganzel, you really made my days!
 
Dadi Athumani katunga vitabu vitamu kama 1. MAPUTO 2. OPERESHENI VIPUSA. Msisahau vitabu kama: Mirathi ya Hatari, Njozi Iliyopotea,Pandu, Akuanzae Mmalize, Mbigili Tupu,Bwana na Bibi Myombekere, Kamlete,Akibisha Mlipue, Mashimo ya Mfalme Suleiman, Najisikia kuua tena, Mashetani, Nchi ya Wazuvendi, Miradi Bubu ya Wazalendo, Janga sugu la Wazawa, Harusi, Asali Chungu,Sitaki Sijavunja ungo, Kuli, Kasri la Mwinyi Fuadi, n.k.
 
Kwa kweli leo nimejisikia furaha sana, kukumbuka na mimi enzi ninakua maana nami ni mpenzi wa vitabu. Nyumbani tulikuwa wa vitabu vingi vya hadithi na vilivyonigusa ni mfano Nyota ya Rehema, Kasri ya Mwinyi Fuad na pia hadithi za Ben Mtobwa. Pamoja na gazeti la sani enzi hizo.....

Nakumbuka pia hadithi za alfu lela ulela, niliona mara ya mwisho Walter Bgoya ametoa machapisho mapya ya hizi hadithi nadhani waliokuwa wanaulizia wanaweza kupata ila sijui ikiwa wana duka maalumu wanakouzia vitabu vyao.

Katika moja ya interview zake pia anaongelea ugumu wa uchapishaji wa vitabu Tanzania na kukosa kwa wanunuzi. Wakati ninakua maktaba pale nilikuwa ninaishi walikuwa na vitabu vingi pia mara moja kwa wiki walikuwa na ukumbi ambako mmoja wa wafanyakazi alikuwa anasoma hadithi kwa watoto wa chekechea na shule za msingi.

Huu utaratibu sijui kama bado unaendelea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…