Tuwatambue Wanaopotosha Ajenda kuhusu Katiba Mpya

Tuwatambue Wanaopotosha Ajenda kuhusu Katiba Mpya

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Kuna upotoshaji mkubwa dhidi ya hoja za wanaoitisha kurejelewa kwa mchakato wa kupatikana kwa katiba mpya.

Mama wamemfanya kuamini kuwa hizo ni chokochoko.

Katiba ni haki ya raia. Kudai katiba mpya dhidi ya iliyopo yenye mapungufu hakuwezi kuwa ni chokochoko.

Hoja hupingwa kwa hoja.

Katiba bora haiwezi kupatikana kama hisani toka kwa watawala ambao ni wanufaika wa iliyopo na wenye vingi vya kupoteza kwa kuja kwa mpya.

Tuzifahamu tabia za wapotoshaji hawa, kwa maslahi ya mwendelezo wa kudai katiba mpya iliyoboreshwa kama jambo la haki:

1. Wengi wao ni wakereketwa wa awamu ile
2. Wengi wao ni wale wale waliokuwa wakimzunguka JPM na kutaka apewe mitano tena kinyume cha katiba
3. Wengi wao ndiyo hao hao wanaomzunguka mama leo
4. Ajenda yao kuu ni kuendeleza ya JPM bila kuwapo JPM
5. Ndiyo walio waasisi wa ile salamu yetu pendwa "kwa jina la JMT"
6. Ndiyo walio waasisi wa kuwa Samia = JPM
7. Misingi ya hoja zao ni ile ile ya JPM, rejea misimamo kuhusu Corona, Chanjo, na hata mahusiano ya kisiasa ndani ya nchi
8. Wote ni CCM
9. Nk

Hawa ndiyo waliotufikisha hapa kwenye chokochoko:

IMG_20210704_051559_619.jpg


Kuwafahamu wanyoa viduku hawa kunatuweka katika hatua bora zaidi za kuyasimamia mahitajio yetu ya kupata katiba mpya sasa.
 
Katiba mpya Ni lazima!
Huu upotoshwaji unaofanywa na kina lumumba utashindwa na nguvu ya umma, ama watake au wasitake katiba tutaidai na itapatikana kwa namna yoyote
 
Kuna upotoshaji mkubwa dhidi ya hoja za wanaoitisha kurejelewa kwa mchakato wa kupatikana kwa katiba mpya.

Mama wamemfanya kuamini kuwa hizo ni chokochoko:

Katiba ni haki ya raia. Kudai katiba mpya dhidi ya iliyopo yenye mapungufu hakuwezi kuwa ni chokochoko.

Hoja hupingwa kwa hoja.

Katiba bora haiwezi kupatikana kama hisani toka kwa watawala ambao ni wanufaika wa iliyopo na wenye vingi vya kupoteza kwa kuja kwa mpya.

Tuzifahamu tabia za wapotoshaji hawa, kwa maslahi ya mwendelezo wa kudai katiba mpya iliyoboreshwa kama jambo la haki:

1. Wengi wao ni wakereketwa wa awamu ile
2. Wengi wao ni wale wale waliokuwa wakimzunguka JPM na kutaka apewe mitano tena kinyume cha katiba
3. Wengi wao ndiyo hao hao wanaomzunguka mama leo
4. Ajenda yao kuu ni kuendeleza ya JPM bila kuwapo JPM
5. Ndiyo walio waasisi wa ile salamu yetu pendwa "kwa jina la JMT"
6. Ndiyo walio waasisi wa kuwa Samia = JPM
7. Misingi ya hoja zao ni ile ile ya JPM, rejea misimamo kuhusu Corona, Chanjo, na hata mahusiano ya kisiasa ndani ya nchi
8. Wote ni CCM
9. Nk

Hawa ndiyo waliotufikisha hapa kwenye chokochoko:

View attachment 1845508

Kuwafahamu wanyoa viduku hawa kunatuweka katika hatua bora zaidi za kuyasimamia mahitajio yetu ya kupata katiba mpya sasa.
Katiba inhekuwa hoja ya ushawishi CHADEMELA wasongetanguliza shinikizo wakati wanajua kabisa huo uwezo wa kushinikiza chochote hawana.
 
Katiba iliyopo ina mazuri mengi tu.....

Wanasiasa wanajaribu kuupotosha umma kwa maslahi yao ya uchu wa madaraka.....

Wako wale wanaoitaka TANGANYIKA......
Wako wale wasioutaka huu MUUNGANO......
Wako wanaozitaka Serikali 3 kwa udi na uvumba.....

Ni uroho tu wa MADARAKA.....

Katiba iliyopo IMEUNDWA VYEMA SANA ,inaakisi DEMOKRASIA TUITAKAYO....Tanzania si nchi ya KILIBERALI ,ukitaka uige demokrasia ya nchi nyinginezo basi ni sawa na kutaka KUIFUTA HISTORIA YA TAIFA HILI.....

#KatibaMpyaSiHitajiLaWatanzaniaWote
#KaziIendelee
 
Katiba inhekuwa hoja ya ushawishi CHADEMELA wasongetanguliza shinikizo wakati wanajua kabisa huo uwezo wa kushinikiza chochote hawana.

Shinikizo linakuja kutokana na kuwa:

IMG_20210708_103605_811.jpg


Jambo la haki lisilotegemea hisani ya wenye kukinzana na Maslahi ya wenye nalo hupatikana kwa shinikizo. Ndivyo tulivyopata uhuru, ndivyo apartheid ilovyoondoshwa nk.

Hata hivyo kumbuka, kuna tofauti kati ya wanaopinga kuanza kwa mchakato wa katiba mpya na Wanaopotosha.

1. Kwenye wanaopinga kuna wenye matatizo ya elimu na wanufaika wa katiba iliyopo walio na ubinafsi uliopitiliza.

2. Wanaompotosha ni wanufaika wa katiba iliyopo walio na ubinafsi uliopitiliza pekee.
 
Katiba iliyopo ina mazuri mengi tu.....

Wanasiasa wanajaribu kuupotosha umma kwa maslahi yao ya uchu wa madaraka.....

Wako wale wanaoitaka TANGANYIKA......
Wako wale wasioutaka huu MUUNGANO......
Wako wanaozitaka Serikali 3 kwa udi na uvumba.....

Ni uroho tu wa MADARAKA.....

Katiba iliyopo IMEUNDWA VYEMA SANA ,inaakisi DEMOKRASIA TUITAKAYO....Tanzania si nchi ya KILIBERALI ,ukitaka uige demokrasia ya nchi nyinginezo basi ni sawa na kutaka KUIFUTA HISTORIA YA TAIFA HILI.....

#KatibaMpyaSiHitajiLaWatanzaniaWote
#KaziIendelee

Panapo sintofahamu kuhusiana na tafsiri yoyote katika katiba walioiandika ndiyo lililo tegemeo la mwisho kutoa tafsiri sahihi ya sehemu husika:

IMG_20210707_085335_184.jpg


Mzee Kingunge alikuwa mmoja wa waliotayarisha na kuiandika katiba iliyopo na wengine 7.

Pamoja naye walikuwamo mzee Msekwa, Nicodemus Banduka na wenzao.

Bado una hoja nyingine?
 
Shinikizo linakuja kutokana na kuwa:

View attachment 1845541

Jambo la haki lisilotegemea hisani ya wenye kukinzana na Maslahi ya wenye nalo hupatikana kwa shinikizo. Ndivyo tulivyopata uhuru, ndivyo apartheid ilovyoondoshwa nk.

Hata hivyo kumbuka, kuna tofauti kati ya wanaopinga kuanza kwa mchakato wa katiba mpya na Wanaopotosha.

1. Kwenye wanaopinga kuna wenye matatizo ya elimu na wanufaika wa katiba iliyopo walio na ubinafsi uliopitiliza.

2. Wanaompotosha ni wanufaika wa katiba iliyopo walio na ubinafsi uliopitiliza pekee.
CHADEMA hamjui historia ya nchi hii, ndio maana mkishavuta bangi mnapuyanga tu.

Tanganyika tulipata uhuru kwa shinikizo ?
 
CHADEMA hamjui historia ya nchi hii, ndio maana mkishavuta bangi mnapuyanga tu.

Tanganyika tulipata uhuru kwa shinikizo ?

Sina hakika uchadema mnausomaga wapi au hao Chadema huwa mnakutana nao wapi. Nisiache kuwaitisha kuweka kumbukumbu sawa sawa. Palikuwa na uzi hapa pia:

Watambue Wanachama wa Vyama Mitandaoni

Hakuna uhuru ambao haukupatikana bila shinikizo (za ndani au nje ya nchi au zote kwa pamoja).

Shinikizo za kupata uhuru wa Tanganyika zilikuwapo tangia kwenye biashara za utumwa, kwa akina Mkwawa, Milambo, Kimweri na wengi wengine.

Au kwako shinikizo maana yake ni mitutu ya bunduki?
 
Kuna upotoshaji mkubwa dhidi ya hoja za wanaoitisha kurejelewa kwa mchakato wa kupatikana kwa katiba mpya.

Mama wamemfanya kuamini kuwa hizo ni chokochoko:

Katiba ni haki ya raia. Kudai katiba mpya dhidi ya iliyopo yenye mapungufu hakuwezi kuwa ni chokochoko.

Hoja hupingwa kwa hoja.

Katiba bora haiwezi kupatikana kama hisani toka kwa watawala ambao ni wanufaika wa iliyopo na wenye vingi vya kupoteza kwa kuja kwa mpya.

Tuzifahamu tabia za wapotoshaji hawa, kwa maslahi ya mwendelezo wa kudai katiba mpya iliyoboreshwa kama jambo la haki:

1. Wengi wao ni wakereketwa wa awamu ile
2. Wengi wao ni wale wale waliokuwa wakimzunguka JPM na kutaka apewe mitano tena kinyume cha katiba
3. Wengi wao ndiyo hao hao wanaomzunguka mama leo
4. Ajenda yao kuu ni kuendeleza ya JPM bila kuwapo JPM
5. Ndiyo walio waasisi wa ile salamu yetu pendwa "kwa jina la JMT"
6. Ndiyo walio waasisi wa kuwa Samia = JPM
7. Misingi ya hoja zao ni ile ile ya JPM, rejea misimamo kuhusu Corona, Chanjo, na hata mahusiano ya kisiasa ndani ya nchi
8. Wote ni CCM
9. Nk

Hawa ndiyo waliotufikisha hapa kwenye chokochoko:

View attachment 1845508

Kuwafahamu wanyoa viduku hawa kunatuweka katika hatua bora zaidi za kuyasimamia mahitajio yetu ya kupata katiba mpya sasa.
A Rubbish thread ever,even though I didn't accomplish the whole thread.
 
Sina hakika uchadema mnausomaga wapi au hao Chadema huwa mnakutana nao wapi. Nisiache kuwaitisha kuweka kumbukumbu sawa sawa. Palikuwa na uzi hapa pia:

Hakuna uhuru ambao haukupatikana bila shinikizo za ndani au nje ya nchi au zote kwa pamoja.

Shinikizo za kupata uhuru wa Tanganyika zilikuwapo tangia kwenye biashara za utumwa, kwa akina Mkwawa, Milambo, Kimweri na wengi wengine.

Au kwako shinikizo maana yake ni mitutu ya bunduki?
Anyway, hivi unajua wakati wa kupambania uhuru Nyerere alishawishi makundi yote ya kijamii kuunga mkono harakati za uhuru, kama:
  • Vyama vya wafanyakazi
  • Viongozi wa dini
  • Wasomi vyuoni
  • Wanafunzi
  • Jumuiya za kimataifa
  • Wakulima
  • Tawala za machief
  • Wafanyakazi

Tena Nyerere mwenyewe alikuwa na mahusiano mazuri mpaka na aliyekuwa Gavana wa mwisho wa Uingereza, Richard Turnbull.

Leo CHADEMA wanajifanya wao ndio wao, wapigania haki, wengind wote hawafai, ni wasaliti. Wao ndio chama cha upinzani, wengine wote mamluki.
Hawataki kushirikiana na yeyote, wewe ndio unatakiwa kuwaunga mkono na siyo vinginevyo.

Leo wanashinikiza katiba ya kwa kushirikiana na kundi gani la kijamii ?
 
Anyway, hivi unajua wakati wa kupambania uhuru Nyerere alishawishi makundi yote ya kijamii kuunga mkono harakati za uhuru, kama:
  • Vyama vya wafanyakazi
  • Viongozi wa dini
  • Wasomi vyuoni
  • Wanafunzi
  • Jumuiya za kimataifa
  • Wakulima
  • Tawala za machief
  • Wafanyakazi

Tena Nyerere mwenyewe alikuwa na mahusiano mazuri mpaka na aliyekuwa Gavana wa mwisho wa Uingereza, Richard Turnbull.

Leo CHADEMA wanajifanya wao ndio wao, wapigania haki, wengind wote hawafai, ni wasaliti. Wao ndio chama cha upinzani, wengine wote mamluki.
Hawataki kushirikiana na yeyote, wewe ndio unatakiwa kuwaunga mkono na siyo vinginevyo.

Leo wanashinikiza katiba ya kwa kushirikiana na kundi gani la kijamii ?

Kwanza ni vyema kuwa tunakubaliana hakuna uhuru wala haki isiyopatikana kwa shinikizo kutokea kwa anayeihodhi kinyume cha utaratibu.

Si kila anayehodhi kinachodaiwa kurejeshwa huwa yuko tayari kwa maridhiano ya amani kiasi cha kuwa na mahusiano mazuri na mdai wake.

Wapo ambao hujifanya jiwe au hata mawe; hao hata kwetu wapo. Wapo ambao huwaita wadai kuwa ni waleta chokochoko; hao hata kwetu wapo. Nk, nk.

Kwa kujifanya mawe Nyerere aliunganisha nguvu kushinikiza kijeshi kupatikana kwa uhuru sehemu nyingi Afrika. Si kweli kuwa Nyerere hakuwa akitumia mashinikizo kudai haki. Labda kama nia ni kuleta upotoshaji mwingine.

Hata kwa mwingireza mashinikizo ya Nyerere na TANU hayakuwa chamtoto!

Wapi unaposoma kuwa Chadema wanajifanya wao ndiyo wao?

IMG_20210704_051559_619.jpg


Unawasikiliza hawa viduku au wewe ni mmoja wao?
 
Panapo sintofahamu kuhusiana na tafsiri yoyote katika katiba walioiandika ndiyo lililo tegemeo la mwisho kutoa tafsiri sahihi ya sehemu husika:

View attachment 1845545

Mzee Kingunge alikuwa mmoja wa waliotayarisha na kuiandika katiba iliyopo na wengine 7.

Pamoja naye walikuwamo mzee Msekwa, Nicodemus Banduka na wenzao.

Bado una hoja nyingine?
Madaraka hayapatikani kwa "maneno tu"....

Ujinga uliojaa vichwani mwenu utawaisha lini?!!!
 
Back
Top Bottom