Tuwe makini, nahisi hii mitandao ya simu haina ulinzi wa uhakika

Tuwe makini, nahisi hii mitandao ya simu haina ulinzi wa uhakika

Satirical Yet Awesome

JF-Expert Member
Joined
Oct 11, 2023
Posts
629
Reaction score
1,688
Iko hivi, siku za nyuma kama wiki tatu zilizopita nilikuwa naongea na mama kweny simu, tulikuwa tunaongea kuhusu maswala ya kutumiana pesa, nikwambia ntamtumia muda si mrefu tukimaliza kuongea, cha kushangaza baada ya kukata tuu simu, kuna message ikaingia ya namba nyingine ngeni inasema "mwanangu tuma kweny hii namba 07xx xxx xxx. Nikashtuka kidogo ila kwa kuwa najua mambo ya utapeli wa mitandao nikakausha.

Ila kilichonishangaza, kwanini ile message mtu aliyetuma imeandika "mwanangu" just momentarily baada ya kuongea na mama, muda uliotumwa hio message pamoja na context za hio message zilinishtua.

Nilimpigia simu mama akasema sio yeye, nikapotezea nikawaza maybe it's just a coincidence.

Second scenario, imetokea wiki iliyopita, nilikuwa naongea na binti flani hivi kwenye simu, nayeye hivohivo tulikuwa tunaongea maswala ya kutumiana pesa. Cha kushangaza baada ya kuongea nae nilivokata simu tuu baada ya kama dakika moja ikaingia message "Tuma kwenye namba 07xx xxxx xxx".

Nilivompigia akasema sio yeye na hajawahi miliki hio namba. Nikawaza kuhusu precession ya ile message, mbona imetumwa muda muafaka kabisa, ila nikapotezea pia.

Leo imetokea tena, huyuhuyu dada amenicheki sema this time hatujaongea, tumetumiana tuu message nikamwambia sawa nakutumia. From tulivoongea saa 12 jioni, saa 12 unusu message mbili zikaingia namba ngeni, ya kwanza "Ntumie basi hio hela" ya pili "tuma humu 07xx xxx xxx", kumuuliza anasema sio yeye.

Hii ya leo imenifikirisha sana na ndio imenifanya nikumbuke scenario za nyuma, kwanini hizi message zinaingia just after kuongea na watu kuhusu kutumiana pesa, wanajuaje? Or is it just a coincidence??

Mi nadhani hii mitandao haina ulinzi, haina privacy kabisa, na nahisi kuna watu huwa wanatusikiliza na kusoma message zetu, this can't be a simple coincidence.

Soma Pia: Utapeli wa ‘hiyo pesa tuma kwenye namba hii’ umeshika kasi, nimegundua mbinu ya kuwazuia, napendekeza haya yafanyike kuwakomesha

Sitautaja mtandao ninao tumia ila nina mpango wa kuuhama.

Nyie wenzangu vipi hamjawahi kutana na haya mambo??
 
kuna siku nilipiga simu kulalamika. kwanini nikipokea hela kwenye line haipiti siku 3 lazima nipate sms au call za matapeli. mwisho wa siku watasema report kwenye ile namba ya utapeli. ila ile timing kuna muda inatia mashaka sana
 
Hata Mimi imenitokea hii kitu, tena Mimi tulipanga bei na muuzaji, likabaki zoezi la kutuma hela nitumiwe mzigo. Baada ya muda naona SMS ikisema Lita tano 150,000 na tuma muda huu. Ikabidi nimpandie tena muuzaji nimuulize mbona umebadilisha bei kulikoni? Akaniambia hajabadilisha bei na wala hajatuma ujumbe wowote Kwangu. Hivyo kupitia matukio yako pamoja na langu nadiliki kusema Kuna kitu hakipo Sawa kwenye mitandao hii ya simu.
 
Back
Top Bottom