Tuzo aliyopewa Rais Samia na shukrani zake kwa mtangulizi Hayati John Magufuli

Tuzo aliyopewa Rais Samia na shukrani zake kwa mtangulizi Hayati John Magufuli

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2015
Posts
18,487
Reaction score
13,611
Unaweza ukamkejeli kadri unavyojisikia kwamba alikuwa mtesaji, alikuwa mkabila alikuwa mkatili. Unaweza ukamsimanga kadri ya uwezo wa akili yako utakavyokuwezesha, hataweza kukujibu amelala usingizi wa milele na hataweza kuamka.

Amepumzika nyumbani kwake Chato, na siku alipokuwa njiani kuelekea huko, kina Mama walimtandikia kanga njiani na wakalia machozi halisi ya kutoka moyoni na sio yale ya usoni ya kutimiza wajibu. Ameacha ushahidi mwingi wa kazi yake, ambazo kwa kweli zilikuwa ni kazi zenye ugumu wake katika kuzianzisha.

Unaweza ukasema alijfufua shirika la ndege kwa kodi zetu, lakini kuweza kufanya hivyo mpaka shirika likasimama kulihitaji ujasiri mkubwa, siku zote kuwa na mtaji wa kuanzisha shirika la ndege katikati ya majukumu mengine mengi ya kitaifa kunautaka uwezo wa ziada wa kuiongozi ambao hayati JPM alikuwa nao.

Kuweza kusimama mpaka viwanja vya ndege vikaweza kujengwa karibu nchi nzima huku majukumu hayo akiwapa TANROAD badala ya mamlaka ya viwanja vya ndege Tanzania, ni sehemu ya maamuzi magumu yasiyoweza kueleweka miongoni mwa wengi wetu wenye mawazo ya kirasimu ya jumla jumla. Alikuwa na uthubutu na ukampatia umaarufu dunia nzima.

Kuweza kuanzisha ujenzi wa SGR kutoka hapa Dar mpaka mikoa ya kanda ya ziwa, ni zaidi ya maamuzi ya kishujaa, watangulizi wake wengi walipita wakishindwa kufanya maamuzi ambayo ni lazima yaumize sehemu ya uchumi wetu lakini katika kipindi cha muda mredu unaokuja yanakuwa na faida kwa Taifa zima. Mtaji wa kufanya hivyo kuupata haikuwa ni suala jepesi tu.

Kuwakoromea watu wa madini mpaka bosi wa BARRICK akafunga safari kutoka Canada mpaka Ikulu pale Magogoni, yalikuwa ni maamuzi ya kijasiri yaliyompaisha kimataifa, kwamba Tanzania imepata mtetezi wa kweli wa rasilimali zake, watangulizi wake walishindwa au hawakupenda kuonyesha msimamo unaojisimamia katika maswali yanayogusa hatima za mamilioni ya wanaowaongoza na ni hapa ndio JPM anapojitofautisha na kizazi cha viongozi wengi wa kiafrika.

Nimemuelewa Rais Samia kuuheshimu hadharani mchango mpana sana wa mtangulizi wake hayati JPM. Hakukuwa na sababu ya kujikweza na ameonyesha uungwana wa kiuongozi wa kuheshimu kazi nzito iliyofanywa na hayati japokuwa akiwa ni msaidizi wake mkuu walifanya mengi kwa pamoja.

Madaraja anayoyamalizia kuyajenga Rais SSH yalianzwa kujengwa na hayati, miradi inayoisha kwa sasa ni jasho la JPM pamoja na marais waliomtangulia. Ni suala la haki kabisa kwamba jema linalofanyika siku zote huwa na malipo mema hata kama anayelitenda anakuwa keshatangulia mbele za haki. Na hii ni maana ya uongozi kwa mapana yake.

Haufanyi haya yote kwa malengo binafsi, kiongozi mwenye maono na mwenye uthubutu huyafanya mengi yanayokuja kumtetea hata akiwa ndani ya kaburi kwa miaka na miaka. Kiongozi wa kweli hajali sana dhihaka za wanaompinga na maneno mengi ya kebehi na yenye kumkatisha tamaa, husimamia katika utimizaji wa maono yake.

Na siku zote watu huangalia maumivu ya leo hii na huja na riwaya ndefu za kuipinga mikakati inayotazama mbali. Wakati wa ujenzi wa barabara ya Ubungo mpaka KIbaha waliolia ni wengi lakini akashikilia mpaka imalizike. Leo imerahisisha sana uwezo wa kuifika Dar kutoka maeneo ya Chalinze.

Wakati daraja la Oysterbay mpaka Aga Khan linataka kuanza kujengwa, wadau walipiga sana kelele mitandaoni, leo hii saa za jioni wanaendesha kwa raha na amani wakiikwepa foleni ya daraja la Salendar, hayo ni maono ya JPM.

Wapo walioelewa maana ya maono ya JPM na wakawa na utayari wa kuipa muda mipango inayotazama mbali lakini wapo ambao wanatazama leo tu, hawakumuelewa kabisa hayati. Rais SSH kwenda kupokea tuzo huko Afrika Magharibi na akajinyenyekeza akisema kwamba watangulizi wake ndio wenye kustahili ni kauli ya sawia kabisa.

Ni ushahidi kuwa JPM aliipenda sana Tanzania na hakuthamini starehe zozote zinazokwenda pamoja na mamlaka ya urais aliyokuwa nayo, Hakuthamini anasa na matanuzi ya kuishi kama wafalme fulani katika dunia ambayo pumzi ni kama kiatu cha kuazima, muda wowote ule kinarudishwa kwa mmiliki. Nadhani hata ule umati uliomsindikiza mpaka uwanja wa Ndege akiwa ndani ya jeneza, uliitambua nafsi yake isiyo na makuu, isiyopenda utajiri wa haraka haraka kwa gharama ya mateso ya wengi.

Alikuwa na upungufu wake wa kushindwa kuweka mipaka ya maamuzi yake, akajikuta anaumiza hata wasio na kosa katika kutekeleza kile alichoamini kinaifaa Tanzania. Alikuwa na udhaifu wa kumtazama huyu ni kijana wa nyumbani anayeongea lugha moja na mimi ngoja nimsaidie kila iwezekanavyo japokuwa jamaa zake hao hakusita kuwafukuza kazi alipoona ufanisi wao hauendani na matarajio.

Tuzo aliyoipokea Rais SSH ughaibuni, nadhani ni ya kwanza kutoka katika mataifa yanayotanguliza mizania ya haki ya kupima ufanisi wa viongozi wa kiafrika. Kama JPM humu hatumuoni wa maana, wapo waafrika wenzetu wanaotambua mantiki ya baadhi ya maamuzi ya kiutendaji serikalini.

Na waafrika hao wala hawajui kuwa wapo wananchi wa nchi yake mwenyewe wasioelewa maana ya kazi zake za kizalendo zinazoongea siku zote kwa niaba yake.

Endelea kupumzika kwa amani JPM.
 
Alikuwa na upungufu wake wa kushindwa kuweka mipaka ya maamuzi yake, akajikuta anaumiza hata wasio na kosa katika kutekeleza kile alichoamini kinaifaa Tanzania. Alikuwa na udhaifu wa kumtazama huyu ni kijana wa nyumbani anayeongea lugha moja na mimi ngoja nimsaidie kila iwezekanavyo japokuwa jamaa zake hao hakusita kuwafukuza kazi alipoona ufanisi wao hauendani na matarajio.

Tuzo aliyoipokea Rais SSH ughaibuni, nadhani ni ya kwanza kutoka katika mataifa yanayotanguliza mizania ya haki ya kupima ufanisi wa viongozi wa kiafrika. Kama JPM humu hatumuoni wa maana, wapo waafrika wenzetu wanaotambua mantiki ya baadhi ya maamuzi ya kiutendaji serikalini.
Wako wanaomsuta kwa mapungufuyake bila kuzingatia yale aliyofanya VEMA.
Na
wako wanaomsifu tu kwa Matendo yake mema bila kuzingatia pale alipo kosea.
Lakini WEWE (Phillipo Bukililo ) umeandika vyema kabisa.
Magu aliuma Mifupa Migumu mno.
Lakini pia Alikanyaga Wengi mno wakati wa kurupushani zake za kuitetea Tanzania kwa Dhana kuwa ilikuwa njia sahihi.
Alijua kuwa Yuko Vitani, Lakini Ni mtu aliyejiwekea ngome ya kuto kupokea Mashauri ya mtu yeyote yule dhidi ya Mafikara yake.
Mimi Sinitamsahau kwa kunivunjia Myumba Zangu mbili Pale Kibamba, na kumfanya Mama Yangu mzazi umri wa miaka 80 kulia kama mtoto mdogo,
Ilinilazimu na mimi kulia kwa kuona sononeko la Mama yangu.
Hakutupa fidia hata kiwanja ili tuweze kupeleka masalia ya kihame na kuanza Maisha mapya.
Hadi leo tunahemea majumbani mwa wandugu na tumeharibikiwa kila kitu..
Sitakaa nimsahau na sitakaa nimuombee dua njema.
NAOMBA MOLA AMLIPE STAHIKI YAKE HUKO ALIKO KWA KUTOJALI DHAMANA YAKE ALIPOKUWA KIONGOZI WA WATU WANYONGE HAPA DUNIANI.
 
Unaweza ukamkejeli kadri unavyojisikia kwamba alikuwa mtesaji, alikuwa mkabila alikuwa mkatili. Unaweza ukamsimanga kadri ya uwezo wa akili yako utakavyokuwezesha, hataweza kukujibu amelala usingizi wa milele na hataweza kuamka.

Amepumzika nyumbani kwake Chato, na siku alipokuwa njiani kuelekea huko, kina Mama walimtandikia kanga njiani na wakalia machozi halisi ya kutoka moyoni na sio yale ya usoni ya kutimiza wajibu. Ameacha ushahidi mwingi wa kazi yake, ambazo kwa kweli zilikuwa ni kazi zenye ugumu wake katika kuzianzisha.

Unaweza ukasema alijfufua shirika la ndege kwa kodi zetu, lakini kuweza kufanya hivyo mpaka shirika likasimama kulihitaji ujasiri mkubwa, siku zote kuwa na mtaji wa kuanzisha shirika la ndege katikati ya majukumu mengine mengi ya kitaifa kunautaka uwezo wa ziada wa kuiongozi ambao hayati JPM alikuwa nao.

Kuweza kusimama mpaka viwanja vya ndege vikaweza kujengwa karibu nchi nzima huku majukumu hayo akiwapa TANROAD badala ya mamlaka ya viwanja vya ndege Tanzania, ni sehemu ya maamuzi magumu yasiyoweza kueleweka miongoni mwa wengi wetu wenye mawazo ya kirasimu ya jumla jumla. Alikuwa na uthubutu na ukampatia umaarufu dunia nzima.

Kuweza kuanzisha ujenzi wa SGR kutoka hapa Dar mpaka mikoa ya kanda ya ziwa, ni zaidi ya maamuzi ya kishujaa, watangulizi wake wengi walipita wakishindwa kufanya maamuzi ambayo ni lazima yaumize sehemu ya uchumi wetu lakini katika kipindi cha muda mredu unaokuja yanakuwa na faida kwa Taifa zima. Mtaji wa kufanya hivyo kuupata haikuwa ni suala jepesi tu.

Kuwakoromea watu wa madini mpaka bosi wa BARRICK akafunga safari kutoka Canada mpaka Ikulu pale Magogoni, yalikuwa ni maamuzi ya kijasiri yaliyompaisha kimataifa, kwamba Tanzania imepata mtetezi wa kweli wa rasilimali zake, watangulizi wake walishindwa au hawakupenda kuonyesha msimamo unaojisimamia katika maswali yanayogusa hatima za mamilioni ya wanaowaongoza na ni hapa ndio JPM anapojitofautisha na kizazi cha viongozi wengi wa kiafrika.

Nimemuelewa Rais Samia kuuheshimu hadharani mchango mpana sana wa mtangulizi wake hayati JPM. Hakukuwa na sababu ya kujikweza na ameonyesha uungwana wa kiuongozi wa kuheshimu kazi nzito iliyofanywa na hayati japokuwa akiwa ni msaidizi wake mkuu walifanya mengi kwa pamoja.

Madaraja anayoyamalizia kuyajenga Rais SSH yalianzwa kujengwa na hayati, miradi inayoisha kwa sasa ni jasho la JPM pamoja na marais waliomtangulia. Ni suala la haki kabisa kwamba jema linalofanyika siku zote huwa na malipo mema hata kama anayelitenda anakuwa keshatangulia mbele za haki. Na hii ni maana ya uongozi kwa mapana yake.

Haufanyi haya yote kwa malengo binafsi, kiongozi mwenye maono na mwenye uthubutu huyafanya mengi yanayokuja kumtetea hata akiwa ndani ya kaburi kwa miaka na miaka. Kiongozi wa kweli hajali sana dhihaka za wanaompinga na maneno mengi ya kebehi na yenye kumkatisha tamaa, husimamia katika utimizaji wa maono yake.

Na siku zote watu huangalia maumivu ya leo hii na huja na riwaya ndefu za kuipinga mikakati inayotazama mbali. Wakati wa ujenzi wa barabara ya Ubungo mpaka KIbaha waliolia ni wengi lakini akashikilia mpaka imalizike. Leo imerahisisha sana uwezo wa kuifika Dar kutoka maeneo ya Chalinze.

Wakati daraja la Oysterbay mpaka Aga Khan linataka kuanza kujengwa, wadau walipiga sana kelele mitandaoni, leo hii saa za jioni wanaendesha kwa raha na amani wakiikwepa foleni ya daraja la Salendar, hayo ni maono ya JPM.

Wapo walioelewa maana ya maono ya JPM na wakawa na utayari wa kuipa muda mipango inayotazama mbali lakini wapo ambao wanatazama leo tu, hawakumuelewa kabisa hayati. Rais SSH kwenda kupokea tuzo huko Afrika Magharibi na akajinyenyekeza akisema kwamba watangulizi wake ndio wenye kustahili ni kauli ya sawia kabisa.

Ni ushahidi kuwa JPM aliipenda sana Tanzania na hakuthamini starehe zozote zinazokwenda pamoja na mamlaka ya urais aliyokuwa nayo, Hakuthamini anasa na matanuzi ya kuishi kama wafalme fulani katika dunia ambayo pumzi ni kama kiatu cha kuazima, muda wowote ule kinarudishwa kwa mmiliki. Nadhani hata ule umati uliomsindikiza mpaka uwanja wa Ndege akiwa ndani ya jeneza, uliitambua nafsi yake isiyo na makuu, isiyopenda utajiri wa haraka haraka kwa gharama ya mateso ya wengi.

Alikuwa na upungufu wake wa kushindwa kuweka mipaka ya maamuzi yake, akajikuta anaumiza hata wasio na kosa katika kutekeleza kile alichoamini kinaifaa Tanzania. Alikuwa na udhaifu wa kumtazama huyu ni kijana wa nyumbani anayeongea lugha moja na mimi ngoja nimsaidie kila iwezekanavyo japokuwa jamaa zake hao hakusita kuwafukuza kazi alipoona ufanisi wao hauendani na matarajio.

Tuzo aliyoipokea Rais SSH ughaibuni, nadhani ni ya kwanza kutoka katika mataifa yanayotanguliza mizania ya haki ya kupima ufanisi wa viongozi wa kiafrika. Kama JPM humu hatumuoni wa maana, wapo waafrika wenzetu wanaotambua mantiki ya baadhi ya maamuzi ya kiutendaji serikalini.

Na waafrika hao wala hawajui kuwa wapo wananchi wa nchi yake mwenyewe wasioelewa maana ya kazi zake za kizalendo zinazoongea siku zote kwa niaba yake.

Endelea kupumzika kwa amani JPM.

Kiatu ukikivaa ndio utajua kinapobana. Hao wa huko nje wametoa sifa kwenye eneo lao na sio katika ubora wake kwa ujumla.
 
Wako wanaomsuta kwa mapungufuyake bila kuzingatia yale aliyofanya VEMA.
Na
wako wanaomsifu tu kwa Matendo yake mema bila kuzingatia pale alipo kosea.
Lakini WEWE (Phillipo Bukililo ) umeandika vyema kabisa.
Magu aliuma Mifupa Migumu mno.
Lakini pia Alikanyaga Wengi mno wakati wa kurupushani zake za kuitetea Tanzania kwa Dhana kuwa ilikuwa njia sahihi.
Alijua kuwa Yuko Vitani, Lakini Ni mtu aliyejiwekea ngome ya kuto kupokea Mashauri ya mtu yeyote yule dhidi ya Mafikara yake.
Mimi Sinitamsahau kwa kunivunjia Myumba Zangu mbili Pale Kibamba, na kumfanya Mama Yangu mzazi umri wa miaka 80 kulia kama mtoto mdogo,
Ilinilazimu na mimi kulia kwa kuona sononeko la Mama yangu.
Hakutupa fidia hata kiwanja ili tuweze kupeleka masalia ya kihame na kuanza Maisha mapya.
Hadi leo tunahemea majumbani mwa wandugu na tumeharibikiwa kila kitu..
Sitakaa nimsahau na sitakaa nimuombee dua njema.
NAOMBA MOLA AMLIPE STAHIKI YAKE HUKO ALIKO KWA KUTOJALI DHAMANA YAKE ALIPOKUWA KIONGOZI WA WATU WANYONGE HAPA DUNIANI.
Pole sana mkuu ni mpaka mtu awe katika nafsi yako wewe ndio aweze kuelewa uzito wa hiki ulichokiandika.
 
Magufuli jembe na atabaki kuwa jembe, bado sanamu yake kama hujengi watajenga waafrika wengine, period
 
Alikuwa na upungufu wake wa kushindwa kuweka mipaka ya maamuzi yake, akajikuta anaumiza hata wasio na kosa katika kutekeleza kile alichoamini kinaifaa Tanzania. Alikuwa na udhaifu wa kumtazama huyu ni kijana wa nyumbani anayeongea lugha moja na mimi ngoja nimsaidie kila iwezekanavyo japokuwa jamaa zake hao hakusita kuwafukuza kazi alipoona ufanisi wao hauendani na matarajio.
Agenda ya kuwa na katiba mpya itakayoweka muundo mzuri wa governance unatokana na mapungufu ya aina hii..ni rahisi sana kuona mtu mmoja ndie anastahili lawama zote sababu alikuwa kwny nafasi hiyo..alilazimika kufanya maamuzi ya aina hiyo kutokana na katiba ilivyo, pili alirithi nchi ikiwa ktk hali iliyomfanya asiwaamini wasaidizi aliowakuta, sabab ni moja watamshauri nini km waliacha mambo yakaharibika kiasi hi cho nchi imejaa wizi kiasi cha kufanya Jamii yote ya watanzania inanufaika na uhalifu uliokuwa unatokea miongoni mwao..mtu yeyote atashawishika kutokubali ushauri kutoka kwa watu wa aina hii, naamini hali ingekuwa tofauti km katiba ingesema wazi kuwa Rais mpya awe pia na timu mpya ya washauri..hilo la kujali watu wa lugha yake yeye si wa kwanza kufanya hivyo wapo waliofanya hivyo kwa kigezo cha dini au elimu nk ukisoma Biblia vzr, Bwana Yesu alikuwa na ndugu zake watatu kati ya wanafunzi wake 12 wakati fulani alilazimika kuwachukua ndugu zake kuongea nao pembeni akiwaacha wale wengine tisa..hakuna ubaya km yanayofanyika ni mazuri kwa nchi..kwa maana hiyo bado JPM anabaki kuwa kiongozi bora kabisa kupata kutokea hapa Tanzania, ndio maana hata AfDB wameona jambo hili na kuamua kutoa tuzo kwa nchi! Ukimtizama JPM kwa jicho binafsi utaona alikuwa katili lkn ukimtizama kwa jicho la utanzania utaona ndie kiongozi nchi na watanzania walikuwa wanamhitaji kwa wakati huo..na sisi binadamu hatupaswi kuwa wabinafsi..mwangalie mwingine kwanza kabla ya kujiangalia mwenyewe.
 
Agenda ya kuwa na katiba mpya itakayoweka muundo mzuri wa governance unatokana na mapungufu ya aina hii..ni rahisi sana kuona mtu mmoja ndie anastahili lawama zote sababu alikuwa kwny nafasi hiyo..alilazimika kufanya maamuzi ya aina hiyo kutokana na katiba ilivyo, pili alirithi nchi ikiwa ktk hali iliyomfanya asiwaamini wasaidizi aliowakuta, sabab ni moja watamshauri nini km waliacha mambo yakaharibika kiasi hi cho nchi imejaa wizi kiasi cha kufanya Jamie yote ya watanzania inanufaika na uhalifu uliokuwa unatokea miongoni mwao..mtu yeyote atashawishika kutokubali ushauri kutoka kwa watu wa aina hii, naamini hali ingekuwa tofauti km katiba ingesema wazi kuwa Rais mpya awe pia na timu mpya ya washauri..hilo la kujali watu wa lugha yake yeye si wa kwanza kufanya hivyo wapo waliofanya hivyo kwa kigezo cha dini au elimu nk ukisoma Biblia vzr, Bwana Yesu alikuwa na ndugu zake watatu kati ya wanafunzi wake 12 wakati fulani alilazimika kuwachukua ndugu zake kuongea nao pembeni akiwaacha wale wengine tisa..hakuna ubaya km yanayofanyika ni mazuri kwa nchi..kwa maana hiyo bado JPM anabaki kuwa kiongozi bora kabisa kupata kutokea hapa Tanzania, ndio maana hata AfDB wameona jambo hili na kuamua kutoa tuzo kwa nchi! Ukimtizama JPM kwa jicho la binafsi utaona alikuwa katili lkn ukimtizama kwa jicho la utanzania utaona ndie kiongozi nchi na watanzania walikuwa wanamhitaji kwa wakati huo.
Alikuwa anafanya kazi na upinzani wa aina mbili. Wa kwanza ni uhalisia wenyewe wa nchi aliyokabidhiwa kuiongoza na wa pili ni ulekutoka ndani ya CCM yenyewe kutoka kwa wale waliojiona wana haki ya kuzaliwa ya kuwaamulia watanzania mustakabali wa maisha yao.

Hivyo hakueleweka sio kwa sababu ya nia yake, la hasha. Ni kwa sababu ya aina ya watu waliokuwa wanafaidika na CCM iliyokuwepo kabla yake, aina ya utawala ambao limetengenezwa tabaka la watu fulani wenye kufanya unyama kama dhuluma na mambo kama hayo.

Kitendo cha maelfu ya watu kukimbia sambamba na msafara wake kuanzia uwanja wa uhuru mpaka katika ile lami ya wanaosafiri sehemu ambako ndege zinapaa ni kielelezo cha kueleweka alikuwa anafanya nini ikulu, miongoni mwa wananchi wa kawaida kabisa.
 
Alikuwa anafanya kazi na upinzani wa aina mbili. Wa kwanza ni uhalisia wenyewe wa nchi aliyokabidhiwa kuiongoza na wa pili ni ulekutoka ndani ya CCM yenyewe kutoka kwa wale waliojiona wana haki ya kuzaliwa ya kuwaamulia watanzania mustakabali wa maisha yao.

Hivyo hakueleweka sio kwa sababu ya nia yake, la hasha. Ni kwa sababu ya aina ya watu waliokuwa wanafaidika na CCM iliyokuwepo kabla yake, aina ya utawala ambao limetengenezwa tabaka la watu fulani wenye kufanya unyama kama dhuluma na mambo kama hayo.

Kitendo cha maelfu ya watu kukimbia sambamba na msafara wake kuanzia uwanja wa uhuru mpaka katika ile lami ya wanaosafiri sehemu ambako ndege zinapaa ni kielelezo cha kueleweka alikuwa anafanya nini ikulu, miongoni mwa wananchi wa kawaida kabisa.
Siku watanzania watajua adui hasa wa hali waliyo nayo ni nani..pengine ndio itakuwa mwanzo wa ukurasa mpya kuelekea hali bora ya maisha, adui wa watanzania ni tabaka dogo ndani ya CCM kudhani wao ndio waamuzi wa watanzania wote juu ya nini kifanyike kwa nchi hii..kulaumu mtu mmoja ni kupoteza muda sababu hutakaa upate jibu la chanzo cha matatizo uliyo nayo.
 
Back
Top Bottom