TV1 Kurusha Live ligi kuu ya Uingereza(EPL)

TV1 Kurusha Live ligi kuu ya Uingereza(EPL)

Bora tu aisee! Nami nifaidi epl bhana kila siku niwe naskiliza kwa radio tu
 
Kituo cha Televisheni nchini, TV1 leo hii kimezindua kampeni yake inayokwenda kwa jina la Toroka Uje ambayo inawaletea watazamaji wake matangazo ya bure ya mechi zote za ligi kuu ya Uingereza maarufu kama English Premier League zitakazoanza kutimua vumbi kuanzia Agosti 13 mwaka huu.

Akizungumzia kampeni hiyo Meneja Mkuu wa TV1, Joseph Sayi alisema kuwa watanzania kwa kipindi kirefu wamekuwa wakitumia pesa nyingi kuangalia ligi hiyo maarufu duniani lakini kupitia TV1 ambayo inapatikana kwenye king’amuzi cha Startimes, watanzania watakuwa wakitazama mechi hizo bure bila gharama yoyote.


Naye Meneja Masoko wa TV1, Gillian Rugumamu aliongeza kuwa mbali na watazamaji wa TV1 kufurahia mechi hizo ambazo zitarushwa kuanzia mechi ya kwanza hadi ya mwisho wa ligi, pia wamejiandaa kukutana na watazamaji wa TV1 kupitia michezo mbalimbali, matamasha na mashindano yatakayokuwa na zawadi mbalimbali zikiwemo vifurushi vya king’amuzi cha Startimes na nyingine kibao.

Akizungumzia kuhusu kampeni hiyo ya Toroka Uje, Mkuu wa Uzalishaji vipindi wa TV1, Mukhsin Mambo, alisema kuwa kipindi hicho kitakachoanza kuruka tarehe 10 mwezi huu kitakuwa katika siku tatu ambapo kutakuwa na mijadala ya kandanda, mpira laivu na uchambuzi kuhusu mechi zijazo ambapo uchambuzi huo utaongozwa na wachambuzi wakubwa akiwemo Dr Leaky Abdallah na Ally Kashushu.

Aidha Meneja Masoko wa Startimes, Damien Li aliwahakikisha Watanzania kuwa Startimes haitaongeza bei ya vifurushi wala kutoza chochote kwa watazamaji wa Ligi hiyo kupitia TV1 kwa kuwa ni bure kabisa.
 
Kituo cha Televisheni nchini, TV1 leo hii kimezindua kampeni yake inayokwenda kwa jina la Toroka Uje ambayo inawaletea watazamaji wake matangazo ya bure ya mechi zote za Ligi Kuu ya Uingereza maarufu kama English Premier League zitakazoanza kutimua vumbi kuanzia Agosti 13 mwaka huu.

Akizungumzia kampeni hiyo Meneja Mkuu wa TV1, Joseph Sayi alisema kuwa Watanzania kwa kipindi kirefu wamekuwa wakitumia pesa nyingi kuangalia ligi hiyo maarufu duniani lakini kupitia TV1 ambayo inapatikana kwenye king’amuzi cha Startimes, Watanzania watakuwa wakitazama mechi hizo bure bila gharama yoyote.


Naye Meneja Masoko wa TV1, Gillian Rugumamu aliongeza kuwa mbali na watazamaji wa TV1 kufurahia mechi hizo ambazo zitarushwa kuanzia mechi ya kwanza hadi ya mwisho wa ligi, pia wamejiandaa kukutana na watazamaji wa TV1 kupitia michezo mbalimbali, matamasha na mashindano yatakayokuwa na zawadi mbalimbali zikiwemo vifurushi vya king’amuzi cha Startimes na nyingine kibao.


Akizungumzia kuhusu kampeni hiyo ya Toroka Uje, Mkuu wa Uzalishaji vipindi wa TV1, Mukhsin Mambo, alisema kuwa kipindi hicho kitakachoanza kuruka tarehe 10 mwezi huu kitakuwa katika siku tatu ambapo kutakuwa na mijadala ya kandanda, mpira laivu na uchambuzi kuhusu mechi zijazo ambapo uchambuzi huo utaongozwa na wachambuzi wakubwa akiwemo Dr Leaky Abdallah na Ally Kashushu.


Aidha Meneja Masoko wa Startimes, Damien Li aliwahakikisha Watanzania kuwa Startimes haitaongeza bei ya vifurushi wala kutoza chochote kwa watazamaji wa Ligi hiyo kupitia TV1 kwa kuwa ni bure kabisa.
Mkuu TV1 inapatikana pia kwenye king'amuzi cha Azam, je tutaona live kupitia huku pia? Au TV1 ya startimes na TV1 ya Azam ni tofauti?

Ufafanuzi tafadhali.
 
Kwenye kunitangaza wanasema watarusha zote labda na marudio sijui, ila ukweli utajulikana ligi ikianza.
 
Hii nchi wanamichezo tunapata shida sana.Heri tungekuwa walevi wa kitu kingine
 
Wengi wanafikiri kuwa sasa TV1 inaenda kurusha mechi zote za epl kama supersports.Haki ya matangazo yakulipia kwa ukanda wa jangwa la sahara bado dstv wana exclusive right.Njia hii ya kununua ili kuuza ndiyo pekee inampa muuzaji haki yakurusha mechi zote kwa wateja wake kupitia chaneli atakazozichagua.Hapa sasa ndo unaona dstv wanarusha kupitia supresports channels.

Njia nyingine ni kununua mechi moja ya jumamosi itakayochezwa kati ya saa nane mchana mpaka saa kumi za uingereza.Mnunuaji wa haki hii yeye analazimika kutouza hizo mechi,anatakiwa kuzirusha kupitia free to air channels(FTA) ambazo atakuwa ameingia nazo makubaliano ya kibiashara.Hapa sasa unawakuta ECOMAT wa Zimbabwe ambao wamepewa haki hizo mpaka msimu wa 2018/19.Wao watarusha hiyo mechi moja ndani ya muda huo tajwa siku ya jumamosi kupitia hizo TVs.Moja ya hizo TV ni TV1 ambao wamekubaliana na ecomat kurusha mechi moja siku ya jumamosi kwa hapa Tanzania na popote inapofika TV1 ndani ya kusini mwa jangwa la sahara.

Kwahiyo sio kama watu wengi walivyoelewa.Ukiangalia ratiba ya epl mechi nyingi kali hazichezwi jumamosi.Na hata zile kali chache zilizopangwa jumamosi hazichezwi muda huo ulioruhusiwa kwa tv za FTA.Hii inafanywa makusudi ili kuto wakosesha wateja watu wa pay TV kama dstv ambao wanalipa pesa nyingi kununua hizo haki.

Kwa hiyo umuhimu wa dstv kwa hapa bongo bado hauwezi kupunguzwa hata kidogo na hili suala la TV1.Kuna jumamosi zitakuwa hazina mechi hata moja kwa watu wa FTA kwakuwa tu mechi siku hiyo zinaanza late,zaidi ya ule uliokuwa stated kwenye mkataba wao na epl board.

Kwa makadirio ya mechi moja kila wiki tv1 wangerusha mechi 33 tu kwa msimu mmoja.Lakini kwa sababu ya limitation ya muda ni dhahiri zitakuwa chini ya 33.Sasa unawezaje kuibana dstv mwenye mechi 330 kwa season za epl huku wewe unapewa mechi chini ya asilimia 10 tena za kuchaguliwa kimkakati?
Umeeleweka
Hakuna jipya km CRTV ya Cameroon tu
 
bora itupunguzie adha ya kwenda vibandaumiza na bukubuku zetu kwa sie tusio na DSTV.
 
Wasidanganye mechi zote kwani nyingine zinachezwa muda mmoja pili chaneli hyo itakuwa ya EPL tu?
 
Back
Top Bottom