TWAWEZA: Asilimia 67 ya watanzania wanakubali kwamba tozo ni njia muhimu ya serikali kupata mapato

TWAWEZA: Asilimia 67 ya watanzania wanakubali kwamba tozo ni njia muhimu ya serikali kupata mapato

The Sunk Cost Fallacy

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2021
Posts
19,582
Reaction score
14,167
Kwa mujibu wa utafiti wa TWAWEZA asilimia 67% ya watanzania wako tayari Kulipa tozo kwa sababu wanatambua ni muhimu kwa maendeleo ya nchi.

Kwa matokeo haya ni wazi Waziri Mwigulu na serikali inazidi kuwaumbua CHADEMA ambao kila siku ni kudandia hoja na kupotosha 😂😂.

CHADEMA kazi mnayo, tafuteni hoja za kwenda nazo kwenye uchaguzi 👇

=============

Maoni ya wananchi kuhusu tozo za miamala ya pesa kwa njia ya simu yanatofautiana. Wananchi walio wengi wanakubali kwamba tozo hizo ni njia muhimu ya serikali kupata mapato (asilimia 67) na kwamba inahakikisha kuwa kila mtu anachangia maendeleo ya taifa (63%). Hata hivyo, wachache wanakubali kwamba tozo hizo zitapunguza utegemezi kwa wafadhili (46%) au kwamba kodi kwenye miamala ya pesa kupitia simu ni jambo zuri (43%).

Wananchi wanaonesha dalili kwamba wangeunga mkono zaidi tozo hizo iwapo wangekuwa na taarifa kamili za namna mapato yanayopatikana yanavyotumika. Wengi (63%) wanasema wangekuwa tayari zaidi kulipa ushuru kama wangefuatilia jinsi fedha zinavyotumika. Wachache wanasema wanajua jinsi fedha hizo zinavyotumika (39%) au wanaweza kujua kwa urahisi kutoka serikalini matumizi ya fedha zilizokusanywa (44%).

Walio wengi pia walikubaliana na pendekezo kwamba tozo yenyewe siyo tatizo bali gharama za miamala zinazotozwa na watoa huduma (66%) na kwamba tozo hiyo inapaswa kutumika tu kwa miamala mikubwa (52%). Miongoni mwa wale wanaokubali kwamba tozo hiyo ni njia muhimu ya kuongeza mapato kwa serikali wanasema viwango vya kodi hiyo ni kubwa (26%) kuliko wale ambao hawakubali (11%).

Twaweza.PNG
 
CCM wenyewe wanalalamika na wabunge wao wanataka maelezo ya kutosha kwenye Bunge lijalo
Sidhani maana tozo ni chanzo rasmi cha mapato ya serikali na wao wanafahamu kwamba tozo ndio inaenda Tarura, RUWASA, kujenga madarasa na vituo vya afya.

Umewasikia siku hizi walisema kwenye majimbo yao barabara ni shida?
 
Sasa twaweza ndio nani? na kwa nini unawaamini?

Kama tuzo zinapendwa,kwanini meneja wa trc aliyepinga tozo amefukuzwa kazi?

Yaani wewe unaamini huo utafiti wa mchongo

Kama wabongo walipinga tozo za simu,sasa tozo zimeongezeka ndio wabongo wazipende!kwa maisha gsni mazuri!

Sasa nimeelewa kwa nini Maghu alimshughurikia eyakuze mpaka akashika adabu,Bora angempoteza tu
 
Serikali na Bunge lenu wenyewe mkiyakoroga lazima muitaje Chadema. Mnaleta tafiti zenu za mchongo mnafikiri ndiyo zitatoa hasira ya wananchi? Chadema wanahusika nini kwenye maujinga yenu? Mtanyooka tu, ili mradi mshaanza kutengeneza tafiti fake tayari maumivu mnayo.
 
Sidhani maana tozo ni chanzo rasmi cha mapato ya serikali na wao wanafahamu kwamba tozo ndio inaenda Tarura, RUWASA,kujenga madarasa na vituo vya afya..

Umewasikia siku hizi walisema kwenye majimbo Yao barabara ni shida?

Yule anaelipa anakosa hata ela ya Kula sasa hizo barabara anajengewa apite Nani?

Au maiti zao
 
Wacheni upumbavu wenu, Serikali na Bunge lenu wenyewe mkiyakoroga lazima muitaje Chadema. Mnaleta tafiti zenu za mchongo mnafikiri ndiyo zitatoa hasira ya wananchi? Chadema wanahusika nini kwenye maujinga yenu? Mtanyooka tu, ili mradi mshaanza kutengeneza tafiti fake tayari maumivu mnayo.
Tupe utafiti wako basi maana naona unaleta mapovu Kisa matokeo yameenda against your favour.
 
Back
Top Bottom