Tweets za January Makamba na Zitto kuhusu Hotuba ya Warioba

Tweets za January Makamba na Zitto kuhusu Hotuba ya Warioba

Status
Not open for further replies.
vijana wenzangu tuwe macho sana na hawa wazee hili swala usiingie kichwakichwa matokeo ya serikali mbili au tatu yatalifaidisha kundi mojawapo ndani ya ccm na sio wewe wala ndugu yako, CCM imegawanyika mara mbili kuna wa serikali 2 na tatu kwa maslahi bnafsi. cha msingi tuconcetrate na na maswala muhimu kwenye katiba yetu kama afya, miundombinu, elimu na malazi. katiba inasema nini juu ya haya, hata wao wakiamua nchi iongozwe na jaji mkuu au spika hayo ni yao wanasiasa.

Hujatulia wewe! Unafikiri hata kama afya,elimu na mengine yakiwekwa kwenye katiba kama ccm wakiendelea kutawala haitakusaidia chochote, hata katiba ya sasa ina mambo mengi tu mazuri lakini hakuna kinachofanyika! Unadhani haki ya kupata huduma ya afya haipo. Kwenye katiba? Lakini nini kinachoendelea sasa? Ccm haitaki mabadiliko yoyote ili iendelee kutawala.
 
Zito huwa namsapoti kwenye zengwe lake na chadema. Lakini hivi karubuni ukiangalia comment zake nyingi ni kama mtuu aliyechanganyikiwa.
Hata hizo coment zake za twutter sio za mtu makini tena wa hoja.nadhani hakujitayarisha kisaikolojia kufukuzwa chadema
 
Ooh well Mungu atunusuru......watanzania tumuombe Mungu atupe hekima na busara juu ya hili..elimu pekee yake Haitoshi..tusibishane na kutukanana January anamaoni yake na yaheshimiwe jibuni kwa hoja....fujo siku zote ni hasara tuu...usinitukane Mimi sababu ninadhani serikali tatu Haifai wakati nahisi moja (mbili) inafaa na vice versa.....Kila binadamu anastahili heshima yake....can't wait kusikia From wakenya watakaokuja kutupa experience Yao...Mungu ibariki Tanzania
 
Hoja ujibiwa Kwa Hoja sio viroja,zito na makamba na wenzao wengine wanaleta viroja
 
Zito huwa namsapoti kwenye zengwe lake na chadema. Lakini hivi karubuni ukiangalia comment zake nyingi ni kama mtuu aliyechanganyikiwa. Hata hizo coment zake za twutter sio za mtu makini tena wa hoja.nadhani hakujitayarisha kisaikolojia kufukuzwa chadema
CHezea CDM wewe..hadi Jusa yupo makini wanabadili mawazo na kupewa mawazi na kichwa ingine isiyopindisha habari Tundu Lissu..Tundu Lissue hata kam unacheka naye muda huu ukimetea habari zisizo wala haoni aibu kukupiga stop ..km alivyomwambia Zitto wazi hawatalea matu CDM anayefanya kazi za CCM..zitto akajidanganya...
 
Mfano haujakaa sawa, hauendani na uzito wa suala lenyewe.
 
Kazi kweli kweli. Huyo ndio aina ya vijana waliopo chama tawala.
 
Makamba Jr, Zitto Kabwe na Wassira wana hoja nzito kuliko hata ya Warioba na tume yake.
 
  1. Ndoa ambayo mke anataka kuishi kwao na mume hana kauli na hilo?
  2. Mke hataki kuachia ubini wa kwao pasi na kuchukua wa mume?
  3. Mke anayetaka mshahara wake ale yeye na wa mumewe wale wote?

(Ongezea na hii) Mke anayetaka kuwa na mme mwingine huku akidai ana ndoa na mme wa kwanza anayemlipia gharama zite
 
Hakuna umuhimu wa muungano wala serikali tatu. bora tufufue Tanganyika yetu. Naandika hivi kwa sababu ipo Serikali ya Mapinduzi Zanzbar iliyokamilika ilhali tunafahamu kuwa Tanzania is a centralised union, its not like USA or Mexico where states or provinces have got powers in making, preserving and amending their decisions. To allow the existence of ZanzIbar as a state which identify itself in several aspect was to allow Tanganyika likewise, logically means to kill the URT.

Tunaogopa nini?, tumeweka nin Zbar kinachofanya tung'ang'anie muungano? au maneno ya J.K Nyerere kuwa "tukijitenga na kujiita watanganyika basi laana hiyo haitaisha, tutajitenga kimajimbo hadi kikabila"
Je Zbar haijui hili? mbona wanasonga tu tena wakiwa na confidence, its about time tuwe na taifa letu Tanganyika na tusijue habari za muungano. Hebu tazama sheria za umiliki wa ardh kule Zbar znavobana mtanganyika wakati bara wao wanamiliki ardhi bila kutengwa, tazama bod ya mikopo high edu Zbar kwa mtanganyika,,. hii ni baadhi tu.
 
January Makamba anamuogopa Nape maana yeye ndo amepewa Rungu la kusimamia serikali mbili na baadhi ya vipengele vinavyoigusa CCM.
 
January Makamba ‏@JMakamba 10m Kilichofanyika Bungeni leo ni kuorodhesha matatizo ya ndoa (ambayo ni ya kweli) halafu kisha kusema kwamba kuongeza mke ndio jawabu lake.

Zitto yeye anadai tujiandae kisaikolojia kuvunjika kwa Muungano!

Very low. Kama muungano ni sawa na ndoa, yupi ni mke na yupi ni mume? Bora hata angesema huu muungano ni sawa na timu mbili za mpira. Wakati mwamuzi ni mchezaji wa mojawapo ya timu.

Mzee Warioba kaliona hilo na kushauri timu zote ziongozwe na manahodha na mwamuzi asiwe sehemu ya wachezaji bali atokane na wapenzi na mashabiki.
 
Chadema wengi wakisikia hoja ya zitto lazima waipotoshe.


Toka jumapili usiku walikua kimya wakaibuka jana kumshambulia bila hata kusoma hoja.

Wanaamini stress za kalenga,zitaisha kwa kumponda zitto.

Na bado!
 
Zitto kachelewa sana kuunga maoni ya wananchi nampongeza.naamini amejipima akaona akienda kwenye mbili atakosa ushawishi zitto mjanja bhana safi sana kijana wangu.
 
Mkuu, zote alizo twit uliziona? Je, what if kama alifuta yale yaliofunguiliwa uzi humu jf? Mwache (ZZK) mwenyewe aje ajibu...au umekuwa mkewe unavyo msemea?

Asante mkuu! Kwaakukiweka sawa hili.

Sent from my GT-I9192 using Tapatalk
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom