Tweets za January Makamba na Zitto kuhusu Hotuba ya Warioba

Tweets za January Makamba na Zitto kuhusu Hotuba ya Warioba

Status
Not open for further replies.
Wewe utakuwa bavicha yani una mtukana mtu kisa katoa mawazo tofuti na ya kwako?

Kilichotokea ni kuwa jamaa ana mmindi zitto wakati Hoja ya Zitto hajaielewa, Sijui kwanini haku-tweet back pale pale kuuuliza ili aeleweshwe ili aelewe zaidi.
 
Huyu bwana mdogo ameshakuwa msukule unaoishi kwa kunywa damu za watu. Haeleweki kabisa. Sasa naiona dhambi ya usaliti ivyojidhihirisha kwa huyu mtu. Sasa hivi hata walio ndani chama tawala wanaungana na Watanzania wengine kuipa uhuru Zanzibar na kutambulika kwa Tanganyika. Umoja wenye mashaka hatuutaki.
 
Sioni haja ya kumshambulia mtu badala ya hoja. Hivyo basi, tujiulize kama muungano kuvunjika ni jambo linalowezekana au la. Kama linawezekana, tunajiandaaje kisaikolojia? Kuna haja ya kujiandaa?

Binafsi, naamini mjadala wa muungano wa Tanganyika na Zanzibar unazidi kuwa kwenye vinywa vya wengi hasa kwa sababu kimantiki umepoteza uhalali wa kikatiba pale wazanzibari walipoweka dhahiri kuwa wao kama "Taifa" wana nchi yao inayohitaji kutambuliwa kwa ukamili wake. Ile katiba yao isiyo na mvuto sana kwa wabara wengi (na hata wachache) imevunja sura ya muungano.

Haimaanishi kuwa muungano ulikuwa katika hali nzuri sana kabla ya kutungwa na kupitishwa kwa katiba mpya ya Wazanzibari, la hasha, bali tunazozitambua kama kero za muungano pamoja na manung'uniko mengine toka pande zote mbili na hasa kwa upande wa Zanzibar, pamoja na mapungufu mengi katika katiba ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania na pia ukichanganya na udhaifu wa serikali katika kusimamia katiba ndio vimechochea kutufikisha tulipo leo katika mijadala ya Kikatiba na uwepo/uhalali wa muungano.

Tukiweka uzalendo mbele badala ya kuwa watumwa wa siasa zetu za kinafiki zilizohodhi mchakato mzima wa kuujadili muungano, na kwa uzalendo wetu tukaitupilia mbali hii saikolojia ya kutafakari na kutafakariwa kama kondoo katika zizi linalolindwa na fisi, naamini yanaweza yakapatikana majibu mazuri zaidi ya maswali mengi muhimu.

Siamini kama sisi wananchi wa Tanzania hatuwezi kufikia hatua na kusema hapana, imetosha, tujitazame upya. Waliopo kwenye vyombo vya maamuzi wanapokiuka matakwa na kushindwa kufikia matarajio yetu, hatuwezi kufanya lolote zaidi ya kuwa watu wa "kujiandaa kisaikolojia"? Tuendelee tu na ukondoo wetu au tujitambue kuwa sisi ndio wenye nchi?

Kwako msomaji, Zitto na mleta mada, naomba tutafakari na sote tuchukue hatua.

Ahsanteni.
 
hivi huyu makamba hajui zanzibar hata tatu hawazitaki ? amewasahau uamsho? amemsahau mansour waliemfukuza? wamemsahau mzee moYo na timu yake?

wanawazania wazanzibar wamelala eeeh ?

hapa cha salama ni serikali tatu kila mamlaka ijue mipaka yake.

iweje watanganyika wavae koti la muungano peke yao? huu muungano ni wetu sote
 
ni mpuunzi tu anayetoa majibu ya kisentesi alichoandika kwa sekunde moja bila kufikiria dhidi ya mawazo ya magwiji waliochambua kwa kina habari za Muungano, nyambafu zake.
 
Kwenye account yake ya twitter, ZZK ameandika; Serikali tatu sasa sio suala la mjadala tena. It is fait accompli. Mjadala ni namna ya kuuboresha muundo huo ili jamhuri ya muungano iwe endelevu.... Akaendelea; " Tuelekeze nguvu na akili zetu kuimarisha muundo ULIOPO KWENYE RASIMU YA KATIBA. Mjadala tuufunge. Mbili na moja hazipo tena. Tuimarishe Tatu.".

Ajabu, kuna mtu ameleta Uzi unaodai eti Zitto anasema Serikali Tatu zitavunja muungano!

Pia, kabla ya hapo, Zitto alitweet akisema, Nchi mbili, Uraia mmoja? Tujiandae kisakolojia kuvunjika kwa Muungano. Na hakusema kwamba eti Serikali Tatu zitavunja Muungano.

Mnyonge mnyongeni...........

Mods, naomba msiuunganishe Uzi huu na ule wa mwanzo unaosema January na Zitto wanapotosha.

Asante
 
Mkuu, zote alizo twit uliziona? Je, what if kama alifuta yale yaliofunguiliwa uzi humu jf? Mwache (ZZK) mwenyewe aje ajibu...au umekuwa mkewe unavyo msemea?
 
NANI atakuwa mmiliki wa serikali ya TATU? Nani yuko tayari kuwa Gorbachev wetu?
Kwa nini Jaji Warioba na Tume yake hawakusema wazi kuwa kulikuwa na UDHAIFU wa wazi katika KUILINDA na KUITETEA Katiba iliyopo?

Hapakua na namna yoyote ya kuilinda hii katiba iliyopo kwa sababu wazanzibar ni wamoja kwenye maslahi ya Zanzibar na wanajali matakwa ya Wazanzibari tofauti na wabara wanaojali vyeo na maslahi ya watawala na kusahau mahitaji ya wengi.Wazanzibari wanaheshimu sharia za M/Mungu zaidi na sio katba kandamizi.Wabara ni wanafiki wanaogopa mzimu wa marehemu Nyerere kuliko Mungu.
Pongezi JK kwa kutupa nafasi ya kutafuta muungano tunaoutaka sisi wananchi japo CCM ni kikwazo.
 
Kilichotokea ni kuwa jamaa ana mmindi zitto wakati Hoja ya Zitto hajaielewa, Sijui kwanini haku-tweet back pale pale kuuuliza ili aeleweshwe ili aelewe zaidi.
Jamaa kwa kichwa chake hawezi kuelewa hata kidogo make milango ya kuelewa kaifunga kabisa kabisa.
 
ni mpuunzi tu anayetoa majibu ya kisentesi alichoandika kwa sekunde moja bila kufikiria dhidi ya mawazo ya magwiji waliochambua kwa kina habari za Muungano, nyambafu zake.
We mwehu kweli huo ugwiji wewe ndiyo umewapa huyo warioba mwenyewe serikali ilimshinda akiwa waziri mkuu leo kawa gwiji kwa kipi unamtetemekea bure tu.
 
Walimuelewa sana ila waliogopa Kumuunga mkono watavuliwa Uanachama, CC ya Chadema ilisema itamvua Uanachama Mwanachama yeyote 'ataeshirikiana' na Zitto kwenye Jambo lolote.
 
Walimuelewa sana ila waliogopa Kumuunga mkono watavuliwa Uanachama, CC ya Chadema ilisema itamvua Uanachama Mwanachama yeyote 'ataeshirikiana' na Zitto kwenye Jambo lolote.

hayo maamuzi labda zitto alikueleza ijumaa kwenye kibaraza cha msikiti
 
hayo maamuzi labda zitto alikueleza ijumaa kwenye kibaraza cha msikiti

Press Conference ya Chadema tena ikatangazwa na Tundu Lissu pembeni akiwepo Benson Kigaila kuwa sasa yeyote akishirikiana nae atakiona cha Mtema kuni. Kama unabisha Muunge Mkono halafu Ben na Yericko wakuripoti then usikilizie Reaction, uliza wale wa Geita.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom