Tyson Ndunguru rafiki yake MC Joel wa (Tyzee SwahiliHood) aliyedaiwa amepotea apatikana

Wapi huko? Was you serious seeking for him?
 
Wapi huko? Was you serious seeking for him?
Sijaelezea Kwa kina my point ni kua tunapo safir au kutoka kwenda sehemu at least tue na kitu kinacho weza kututambulisha Kwa uraisi Ili zikitokea Sinto fahamu.......... Inakua rahisi kujua pa kuanzia......

Niliwai safiri kimya kimya Dar to Mwanza njian tuli nusurika kupata ajali ya kikatili so nani angejua??

Kuna walio zama Mv bukoba sabb ya kusafir kimya kimya..

WE CARRY LIFE & DEATH
 
Dege kubwa kama hilo halipotei hivi hivi!!!

Ni either limepotezwa!?....Ama limefichwa mahala na lishangazi!!!
 
amepotea akiwa mtaa gani,kata gani ,kijiji gani,wilaya gani, mkoa gani anafanya katika shirika,taasisi au
 

Kuna issue hapa inaendelea
 
Hana tatizo la afya ya akili?

Nendeni na ITV wana kipindi cha kutafuta waliopotea.

"Yu wapi" cha Anna Malya
 
Tarehe 26 si,tarehe za mshahara kabisa hizi?usikute Kafungiwa sehemu anakula mema ya nchi,hebu tuvute subira mwamba atarejea na kama yupo kwenye msala Mungu amlinde.
 
Wanasema eti huyu ni rafiki wa yule joel mc aliejirusha gorofani,ni kweli?
 
RIP - John Pombe Joseph Magufuli, ungekuwepo wangesema serikali yako inaua watu, kumbe haya mambo yapo tu. Vipi yule dada wa bank alietekwa akauawa Kibaha??Kesi iliishia wapi??? Na kesi nyingi tu za mauaji zimepigwa kimya, lakini sioni mzigo ukirushwa kwa serikali ila wakati wa mwendazake zote alipelekewa yeye.
Miafrika Ndivyo ilivyo.
 

Picha: Tyson Nduguru

Kijana Tyson Nduguru ambaye ni Rafiki wa karibu wa Joel Misesemeko (MC Joel) aliyejirusha ghorofa ya 7 Makumbusho Dar es salaam na kufariki dunia, ametoweka ghafla siku chache tangu kutokea kwa kifo cha MC Joel.

Maswali yaliyozua mjadala ni inakuwaje Rafiki yake ajirushe ghorofani May 23,2023 nae atoweke May 26, 2023 akiwa ameaga anaenda msibani kwa Rafiki yake?

Pia post zake mbili nzito za mwisho zenye mafumbo alizoandika baada ya kifo cha MC Joel katika ukurasa wake wa Facebook zinaongeza maswali pia ambapo May 23,2023 aliandika “Guys!
for the sake of your, Family, dont give up, nilipewa Familia, ni moja ya Famila bora kwangu, tumekuwa Watu wa karibu na kupendana, kifo chako ni mshale ndani yangu ila sababu ya kifo chako ni kuiharibu kutoa mshale kwa kurudi ulipotoka, maumivu yasioelezeka napitia”

AyoTV imefanya mahojiano na Mkewe, Grace Rashid ambaye anahangaika kumtafuta Mumewe kwenye wodi za Wagonjwa, mochwari na hata Vituo vya Polisi “Aliondoka nyumbani akaaga anaenda msibani baadaye nikawa nampigia simu haikuwa hewani nikampigia Rafiki yake, ndio hadi leo hatujamuona”.

Pia Soma
- TANZIA - Joel Misesemo afariki dunia kwa kujirusha kutoka ghorofani jengo la Derm eneo la Makumbusho, Dar

Source: Millard Ayo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…