TZ Trends & Analysis: Hoja 30 za The Economist Kumhusu President Samia. Kuna za Kweli, za Uongo na Uzushi na Kutaka Kumpangia Watakacho Mabeberu, Jee?

sisi kama wananchi tulishamshindwa kwa ukatili wake,bahati nzuri Mungu akango'a mbuyu
Una uhakika kua Mungu ndio kamtoa?Kwani wanaokufa Mungu kawang'oa?Amekufa kama binadamu wengine tu wanaokufa ni kua kifo kimemkuta tu akiwa ni Rais.
Ila hii nchi ilibidi iendeshwe kibishi mpk watu akili zikae sawa,ujinga na kutaniana kulikua kumezidi sana
 
Pascal

Kama huu ndio unauita uchambuzi napata taabu kidogo. Hao wenye kumsema mama walikua na vigezo vyao wewe unasema hapana huu ni uongo una vigezo vyako.

Sisi wasomaji tumekosa kuona locus stand yako. Unaposema sio kwa Jambo hasa unaposema huuu ni uongo lazima useme ukweli ni upi ukishindwa maana yake wote ni waongo.

Ungechambua hoja tano tu zenye mashiko ukatoa na mifano ungekuwa na Andiko bora kuliko hiyo shopping list
 
Kelele zote hizo kumbe wanataka serikali ikubali chanjo, haya waambie itakubali basi watulie mama afanye kazi
 
Wewe Paskali ni mkorofi sana, wewe unafikiri kuwa kila mtu anawaona ni mabeberu hao wanaotusaidia. Wewe baki na theory zako za kuambiwa na Magufuli. Mambo ya mabeberu yamekwenda, yamekwisha na yameondoka na Magufuli.
Achana na mambo ya Magufuli, huyu ameshakufa siku nyingi, acha tujenge diplomasia na nchi za nje.
You are better than that Paskali.
 
Bado upo kwenye ulimwengu primitive.

Katika Ulimwengu wa watu wenye weledi, waliostaarabika na waliokamilika, katika karne hii, hakuna beberu wala jike.

Any country and any individual is your partner in the development journey of every humankind.

Neno hilo la kijinga, 'beberu', tumelizika pamoja na marehemu. Watu wenye Roho wa Mungu, wanatambua kuwa pamoja na utofauti wetu wa rangi, jinsia, maumbile, dini, n.k. sote ni wanadamu. Hakuja beberu wala jike. Ukiona unaamini kuna binadamu beberu na jike, ujue ndani mwako unatembea na roho ya shetani, yaani yule ibilisi aliye baba wa uovu wote.
 
Jingine ni ule waraka wa TLS kumtaka rais mpya Samia kulivunja Baraza la mawaziri la JK na kuunda lake la Awamu ya Sita. Rais Samia kaamua kuanza Awamu yake ya 6, na wachache wapya, na wengi ni mawaziri viporo wa Awamu ya Tano, kwa hoja kuwa kile kiapo chao kwa utii kwa JPM, kinahuishwiwa kwake, kwa hoja kuwa kiapo ni kwa Taasisi ya Urais wa JMT na sio kwa mtu. Kwa maoni yangu, kwa executive appointees, hata rais akibadilika, wao wanaendelea, lakini kwa political appointees wote ilibidi wale kiapo kimya kwa Rais Samia na sio kiapo cha utii kwa JPM, lakini kumtumikia Samia, ndio maana tukamshauri PM Majaliwa ange step down kumpa mama space to start a fresh, na kama bado anamuhitaji PM Majaliwa, ange m reappoint.

Paskali TLS na wewe mmeanza na mguu mbaya kwa kushindwa kutofautisha rais mteule (anayetokana na uchaguzi) na kaimu rais (anayetokana na sababu zingine isipikuwa uchaguzi)
SSH alikuwa kaimu rais mpaka alipoapa - anarithi urais anapoapa na toka japo anaendeleza pale mwendazake alipoishia.
maneno muhimu ni rais mteule na kaimu rais ukikosea hapo unapotea
 
Si hapo wala hapa panahitaji msaada wa P. au nani. Unajua hata kwenye mfumo wa chama kimoja bado kuna executive na political appointees. Wanajulikana kabisa. Wako tofauti sana. Kwenye mfumo wa vyama vingi ndio kabisa tofauti inakuwa kubwa zaidi. Mapenzi kwa chama kimojawapo inakaribia dhambi! Kama yapo ni kwa kificho sana. Na sio uchama katika kazi za umma wa vyama vingi.
Tumechizika. Kwetu ni fahari kuwa daktari wa ccm, polisi ccm, jaji ccm, jw ccm! Utaachaje wakati umeteuliwa kazi ya umma kwa kigezo cha kuwa mwanachama kindakindaki wa chama tawala? Vikao vya chama vinafanyika Ikulu! Kwa jeuri na kiburi tu. Acha aende tu. Tuache uchizi.
 
Chizi ww, wasukuma msahau nafasi ya urais,katiba inabadilishwa kunawekwa kipengele ni marufuku kwa msukuma kushika madaraka ya juu. . .maaana MNA roho mbaya nyinyi Watani zangu
 
Huu msamiati wa Mabeberu tushaachana nao
Kama ulimsikiliza Mama Samia juzi alisema nimekuteua Waziri wa mambo ya nje ukanyooshe diplomasia Ina maana hakubaliani na sera za mwendazake kuwatukana na hapo hapo unawaomba msaada
 
Kwa kuendesha alivyotaka wewe ulinufaika nini?
 
Tena sana
 
Hilo gazeti lilipigwa marufuku Tanzania wenzetu mnalipata wapi wakati serikali ilishalipiga pini marufuku Tanzania?

Mna quote toka gazeti lililopigwa marufuku?
Kwani kuna ubaya gani mtu kama ana access ya kulipata hilo gazeti?
Wewe karagabaho na uhuru na mzalendo yako.
 
Kwahiyo?
 
Tangu lini Pascall akawa na uandishi ulio bora?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…