neggirl
JF-Expert Member
- Jul 30, 2009
- 4,849
- 2,132
Think before..! Aaarrrrrggggg
mkuu unataka kupiga key board
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Think before..! Aaarrrrrggggg
Unajua ufinyu wa mawazo ndio unafanya watu kama wewe wakisikia neno Mwalimu wanajua ni primary na sekondari tu! Kumbuka hata lecturer na Proffesor ni Walimu na hutasikia malalamiko kutoka kwao.
Mwambie mwenzako akaze buti mafanikio hayaletwi na taarabu kama hizi.
Mimi nilikuwa mwalimu. Na nasema kwa dhati na mnielewe hii ni kazi nzuri sana kama mtu ana malengo hutakiwi kurithika kwa kazi ya aina yeyote ile.
Ukiwa mwalimu waweza kufanya biashara maana walimu wana muda mwingi, ktk mwaka wana miezi 3 ambayo hawaendi kazini yaani wapo likizo pindi shule zinapofungwa. Muda wa kukaa kazini ni mchache ukilinganisha na kazi nyingine hivyo mambo yako mengine yanaendelea kama una malengo.
Mwalimu ana nafasi kubwa ya kujiendeleza kielimu na akaweza badilisha kazi kama atadhani kuna umuhimu wa kufanya hivyo, maisha ya Tanzania kupata kazi ni ngumu sana lkn walimu wanaajili moja kwa moja serikalini hivyo ukishapata ajira yako na kama hupendi nenda kasomee kitu kingine unachokipenda ukiwa tayari mwajiliwa wa serikali na ukimaliza omba kubadilishiwa kada ya utumishi (categorization) kwa course mpya uliyosomea, kisheria unatakiwa kubadilishiwa.
Kuna watu wengi wajanja sasa wanafanya hivyo. Akishapata ualimu wake, kuna wanaoenda kusoma uasibu, social work, procurement, sheria, human resourse na kozi tofauti hadi udaktari na baada ya kuhitimu anaomba kubadilishiwa kada na kiuraini anapata ajira yake safi ya bila jasho ndani ya halmashauri yake tena bila interview. Na hapo sasa anaweza kupata uhamisho na kuhamia popote serikalini mf. Wizarani n.k
Amkeni wabongo acheni kudharau kazi. Kwa maisha ya leo Tz. Hakuna kazi bomba kama ualimu ni kutokujua tu.
Mke mwalimu ndo mke bora ndugu zangu. Anajua saikolojia ya mtoto hivyo atamlea mwanao ktk mazingira mazuri, atakuwa na muda mwingi wa kukaa na mwanao anajua tabia mbalimbali za watoto hivyo itakuwa rahisi kwake kumshape mwanao.
Oooh! Nimechoka kuandika, kwa ufupi kuna faida nyingi za kuwa mwalimu.
Ualimi ulivyoniweke nilivyosasa aise nauheshimu mnoooo. Kikubwa usiridhike, Ualimuuuu juuuuuuu!.
kazi zote za kuajiriwa ni kupoteza muda!!
Kumbe wewe ni GREAT THINKER NAMNA HII?
Aisee,Nawee pia GT ndo mana umeappliciate..
kazi hiyo haina seminas, wala overtime. Huko ndugu yangu utakua umejiunga rasmi na chama cha watu maskini duniani. Mtaani jina lako litafutika na utaitwa ticha kwa kejeli tu. Yaani hutaweza hat
a kutoa michango ya harusi. Achiliambali kua shoe shiner ili kupata fedha za kujikimu zaidi.
Ualimu ni kazi kama kazi nyingine.
Mimi nilianza certificate nikapiga vizuri nikapangwa shule mazoezi, mwaka huu nimepiga paper la form six result imekuja vema niko chuo kikuu mwaka wa kwanza na M/Mungu akinijalia nina matumaini ya kufika mbali zaidi.
Ualimu mtamu na siuachi, ukifundisha watu wote kimya wanakusikiliza wewe tu unatema chakula cha ubongo.Mi naona fahari kuwapa watu maarifa ambayo hawakuwa nayo kabla sijawafundisha.
kazi hiyo haina seminas, wala overtime. Huko ndugu yangu utakua umejiunga rasmi na chama cha watu maskini duniani. Mtaani jina lako litafutika na utaitwa ticha kwa kejeli tu. Yaani hutaweza hata kutoa michango ya harusi. Achiliambali kua shoe shiner ili kupata fedha za kujikimu zaidi.
Nyakageni
kama unafundisha na wote wako kimya, hiyo ni ROTE LEARNING! Darasa lazima lichangamke. Participatory approach is the best
mkuu unataka kupiga key board
Na watu wote wangukuwa na upeo kama wa kwako hata haya maandishi usingeweza kuyalambaza humu.