Uamuzi wa NMB ni dalili ya taasisi za kifedha kukosa ufanisi katika utendaji.

Uamuzi wa NMB ni dalili ya taasisi za kifedha kukosa ufanisi katika utendaji.

init

Senior Member
Joined
Mar 22, 2021
Posts
115
Reaction score
109
Awali ya yote nipende kuwasalimu nyote mtakao pata nafasi ya kupitia uzi huu.

Binafsi nimeshangazwa na uamuzi uliofanya na Benki ya NMB leo, kutoa Kompyuta mapaka yaani laptops kwa wamachinga. Nimepata maswali mengi sana, je wamepewa ili wauze ama ziwasaidie katika biashara zao?. Na kama ni kwaajili ya kazi pia nikajiuliza ikiwa Machinga ana mtaji chini ya laki nne, 400,000/= atawezaje kutumia kifaa chenye thamani ya zaidi ya laki sita kuendesha shughuli zake pasipo kuuza hicho kifaa? , na hata asipokiuza kitaongeza nini katika uchumi wa Wamachinga?.

Binafsi nilitegemea na ningependa kuona taasisi za kifedha kama Benki zikitizama njia bora za kuwafanya Wamachinga waweze kukopesheka kwani wengi kwa sasa wana mitaji midogo na pia hawana collateral securities za kuwawezesha kupata mikopo katika taasisi za kifedha. Matokeo yake wanategemea mikopo kutoka kwenye mashirika ya serikali na NGOs zinazotoa mikopo isiyo weza kukidhi mahitaji ya idadi iliyopo pia huja kwa misimu.

Pia Kwakuwapa mikopo hata NMB isingeli baki kihasara kwani ingenufaika na riba kwa kiasi chake na kuongeza watumiaji tofauti na donation zisizo na msingi.
 
Awali ya yote nipende kuwasalimu nyote mtakao pata nafasi ya kupitia uzi huu.

Binafsi nimeshangazwa na uamuzi uliofanya na Benki ya NMB leo, kutoa Kompyuta mapaka yaani laptops kwa wamachinga. Nimepata maswali mengi sana, je wamepewa ili wauze ama ziwasaidie katika biashara zao?. Na kama ni kwaajili ya kazi pia nikajiuliza ikiwa Machinga ana mtaji chini ya laki nne, 400,000/= atawezaje kutumia kifaa chenye thamani ya zaidi ya laki sita kuendesha shughuli zake pasipo kuuza hicho kifaa? , na hata asipokiuza kitaongeza nini katika uchumi wa Wamachinga?.

Binafsi nilitegemea na ningependa kuona taasisi za kifedha kama Benki zikitizama njia bora za kuwafanya Wamachinga waweze kukopesheka kwani wengi kwa sasa wana mitaji midogo na pia hawana collateral securities za kuwawezesha kupata mikopo katika taasisi za kifedha. Matokeo yake wanategemea mikopo kutoka kwenye mashirika ya serikali na NGOs zinazotoa mikopo isiyo weza kukidhi mahitaji ya idadi iliyopo pia huja kwa misimu.

Pia Kwakuwapa mikopo hata NMB isingeli baki kihasara kwani ingenufaika na riba kwa kiasi chake na kuongeza watumiaji tofauti na donation zisizo na msingi.
Labda computee zenyewe wamepewa bure na taasisi ya nje. Bora wangewapatia wanafunzi wa vyuo wanaojitahidi kielimu na ambao hawana laptop. ingekuwa great investment
 
Ulimwengu wa teknolojia na digitali, ukionganishwa unapata chochote unachokitaka, falsafa rahisi sana.
 
Labda computee zenyewe wamepewa bure na taasisi ya nje. Bora wangewapatia wanafunzi wa vyuo wanaojitahidi kielimu na ambao hawana laptop. ingekuwa great investment

Kabla ya kuwapa lap top computers, hawa NMB walijiridhisha vipi kuwa hawa machinga wana ujuzi wa kutumia vifaa hivyo?
 
Mi nadhani hii habari kuna sehemu umeitoa, kama kuna sehemu umeitoa basi natumai pia kuwa kutakuwa na maelezo ya kwa nini wametoa vifaa hivyo kwa wafanyabiashara wadogo.

Iweje uje kuuliza hayo maswali hapa jamvini Ina maana huko ulipoitoa hii habari hakuna maelezo ya kutosha ya kwa nini wametoa hivyo vifaa...?

Sio mbaya kama utatuwekea picha au link ya habari husika huko ulipoitoa aisee.

NAWASILISHA.
 
Kwa huku sasa hii benki ya NMB inapoelekea sio kuzuri Uongozi wa huyu mwanamama Ruth Zaipuna umegubikwa na umbea na majungu kupita kiasi hata wanayoyafanya yote haya ni ishara moja kuwa wamechanganyikiwa na kukosa focus.
 
Back
Top Bottom