Watanzania wenzangu tufike mahali tufunguke macho yetu na tuchoke na huu upotevu wa matrilioni ya fedha zetu tulizochuma chini ya jua kali na baridi kali.
Kila siku tumekuwa tukisikia habari za ubadhirifu, tangu enzi za Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete, Magufuli na Samia, wimbo ni ule ule, uhujumu uchumi, wizi, ubadhirifu, ufisadi, upigaji na sasa sijui tuite jina gani. Haya yote ni matokeo ya kuwa mfumo ule ule mmoja (mfumo CCM) kwa miaka 60! Nchi zote majirani zetu walishaondokana na vyama vikongwe vya enzi ya akina Nyerere, sisi tunategemea nini kutoka CCM?1
Wazungu wanasema don't expect different results with the same procedures, kwamba USITEGEMEE MATOKEO TOFAUTI WAKATI UNAFUATA UTARATIBU ULE ULE!
Watanzania tusikubali kuwa washabiki wa hawa viongozi wanaojifanya kukasirika na kuishia kupiga kelele majukwaani bila kubadilisha chochote. Tuondokane na mfumo CCM la sivyo wachache wanaofaidi wataendelea kufaidi na kuneemeka huku wengine wakiteseka na kufa kwa kukosa mahitaji ya msingi. Tuamke!
Kila siku tumekuwa tukisikia habari za ubadhirifu, tangu enzi za Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete, Magufuli na Samia, wimbo ni ule ule, uhujumu uchumi, wizi, ubadhirifu, ufisadi, upigaji na sasa sijui tuite jina gani. Haya yote ni matokeo ya kuwa mfumo ule ule mmoja (mfumo CCM) kwa miaka 60! Nchi zote majirani zetu walishaondokana na vyama vikongwe vya enzi ya akina Nyerere, sisi tunategemea nini kutoka CCM?1
Wazungu wanasema don't expect different results with the same procedures, kwamba USITEGEMEE MATOKEO TOFAUTI WAKATI UNAFUATA UTARATIBU ULE ULE!
Watanzania tusikubali kuwa washabiki wa hawa viongozi wanaojifanya kukasirika na kuishia kupiga kelele majukwaani bila kubadilisha chochote. Tuondokane na mfumo CCM la sivyo wachache wanaofaidi wataendelea kufaidi na kuneemeka huku wengine wakiteseka na kufa kwa kukosa mahitaji ya msingi. Tuamke!