Ubaguzi: Machotara Hizbu, Zanzibar ni nchi ya Waafrika

Ubaguzi: Machotara Hizbu, Zanzibar ni nchi ya Waafrika

Kwani uongo jamani, chotara hawezi kupewa hii nchi, atarudisha mabwana zake.
 
Catch 22
Muajemi wa kizazi cha kumi na.mbili na
Mnyamwezi kizazi cha tatu
Fumbo
wanyamwezi wa kizazi cha tatu kivipi ina maana Waajemi walipokuja Znz hawakukuta watu? au ndo mkuki kwa Nguruwe?
 
Last edited:
Hilo bango (UJUMBE) limerudiwa tena leo katika kilele cha maadhimisho ya mapinduzi matukufu. Lakini kuna afisa mmoja wa CCM ameomba msamaha kuwa ni "mwananchi" mmoja pengine kichaa (au adui wa CCM, pengine mwana CUF) ndiye ameliingiza uwanjani ili kuwapaka matope CCM!! Kwa hivyo na Bw (maana kumwita dr ni kujisuta) Shein jana alijigeuza kichaa kwa kukubali kupokea bango hilo!
Niikiri kuwa sio tu nimewadharau ma-CCM, bali pia hili limeongeza chuki yangu dhidi ya haya matarahamwe. Nimemchukia Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete, nimemchukia makamo wa Znz na mgombea wa urais (CCM) huyo Shein, nimewachukia mantarahamwe yote ya bara na visiwani.Hamuwatendei haki wananchi wa Zanzibar (weusi, weupe, wabluu, wamanjano, wekundu, nk). Hamwezi kuleta ubaguzi wa rangi wazi wazi katika karne ya 21. Shame on you! Sasa mkisikia weusi wanabaguliwa huko Marekani au weupe wanabaguliwa huko Afrika ya Kusini mtalaani au mtaunga mkono huo ubaguzi? nyambaf Kikwete na Shein & Co
 
CCM NA UNAFIKI ULIOKUBUHU.

Na Kilawa the Iron.

Chama cha mapinduzi kimedhihirisha unafiki wake kwa vitendo. Chama hiki kimekuwa kikijinasibu kuwa ni chama cha watu maskini, wakulima na Watanzania wote kinyume na matendo ya chama hiki.

Bila aibu wala haya leo katika sherehe zinazosherekewa kila mwaka kukumbuka mapinduzi ya kishujaa yaliyafanyika Tr 12/01/1964
Kijana wa CCM ambaye hadi sasa haijajulikana kama ni mwanachama tu au ni kiongozi wa chama hicho ameonekana akiwa ameshikilia bango kubwa la kibaguzi na linalojenga chuki kwa wananchi wa Zanzibar na ulimwengu mzima.

Kijana huyo alishika bango kubwa liloandikwa kwa ustadi na likionekana limefanyiwa maandalizi ya mda mrefu linasomeka hivi
"MACHOTARA HIZBU ZANZIBAR NI NCHI YA WAAFRIKA" je huu sio unafiki wa watu hawa waliotawala kwa miaka yote hii.

Kwanini nasema CCM ni wanafiki? nasema hivi kwa sababu kuu zifuatazo:-

Bango hili linaonekana limeandaliwa kwa umakini likiwa na lengo mahususi kisiasa ndani ya CCM hivyo linadhihirisha kuwa watu hawa wanapenda ubaguzi, na wametudhihirishia kwamba wao ni watu wasiopenda haki, usawa na utawala bora.

Kama bango hili halikuwa kimkakati ni kwanini waliruhusu kijana huyu aingie na bango hili na hata likatumiwa kwa mda wote? je Greenguard, polisi na viongozi wao waliridhishwa na bango hilo hadi kuacha litumike katika sherehe ya kishujaa?

Lakini kama hawakuridhisha au kulipenda bango hilo kwanini viongozi wa CCM walikaa kimya hadi walipoona matamko ya wapinzani kulaani kitendo hicho? ndipo mtu anayeitwa Daniel Chongolo alipoamua kuomba radhi

Kiujumla ni kwamba CCM inakwenda kinyume na imani ya chama chao ambayo inahubiri kuwa "Binadam wote ni sawa" hivyo kwa mktadha huo hakuna usawa badala yake ni ubaguzi unaopandikisha chuki za kudumu vitendo hivi vilaniwe na wapenda haki wote duniani.

Mwisho nimemsikia Dr Shein katika hotuba yake akisema kuwa serikali yake imefanikiwa kulinda na kudumisha demokrasia nchini Zanzibar, pia kudumisha na kuulinda muungano ilihali yeye hadi sasa yupo madarakani kinyume na katiba na sheria za nchi yake

Haya yote yanadhihirisha unafiki wa chama hicho nchini, Kiujumla sisi tunalaani kwa nguvu zote ubaguzi wowote unaoendelezwa na ccm hali itakayojenga chuki za kudumu miongoni mwetu.

Sote ni wanadamu, sote tumeumbwa na Mungu mmoja tuache kuyafanya mambo kwa maslahi binafsi zaidi tuangalie maslahi mapana ya Taifa.
Ahsante.
Msema kweli mara zote huchukiwa na watenda mabaya
 
DSC_2469.jpg


Vijana wa Chama cha Mapinduzi CCM wakipita mbele ya mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akipokea matembezi ya Vijana hao waliotembea katika Mikoa Minee ya Kichama katika kuadhimisha miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar yaliyomalizia leo katika viwanja vya maisara Suleiman Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.]

Picha hiyo hapo juu ni bango la Kikaburu katika mwaka wa 2016 bango linalotukuza ubaguzi wa rangi.

DSC_2827.jpg


Sitaki kuamini kama Ali Mohamed Sheni na uongozi wa juu wa CCM Zanzibar wamewatuma vijana hawa kufanya haya.

Akili yangu inanikatalia kabisa.

Sitaki kuamini kuwa tumeanza kuwatengeza akina Hendrik Verwoerd na Eugene Terre Blanche weusi katika visiwa vya Zanzibar.

CCM Zanzibar inamuiga nani katika hili?

Hitler na Manazi walikuwa na vijana wao waliojulikana kama Stormtroopers ukipenda waite Brown Shirts?

Zanzibar tumeshawashuhudia Ton Ton Macout mfano wa wale wa Papa Doc wa Haiti visiwani wanajulikana kama Mazombie.

Sasa tumefungua ukurasa mwingine wa Adolf Eichman.

Hilo bango mbona litawagusa wengi katika safu ya uongozi wa siasa katika Zanzibar na wengine walipatapo hata kuiongoza nchi?

Machotara?

Nani huyu chotara?

Tumehama kwa Waarabu sasa tuko kwa Machotara!

Lakini huyo chotara si ana wajomba, babu, bibi na mama wakubwa na wadogo Waafrika?

CCM imefilisika kiasi hiki?

Nini hiki ni kiwewe cha CCM kushindwa uchaguzi au ni kitu gani?

Nini khasa tafsiri ya mambo haya?

Tusubiri In Sha Allah wakati utatupa jibu.



Kasema Mwalimu Nyerere karne ya ishirini na moja kuna watu wanapanda basi la ukabila...

Hawa wanapanda jahazi la ugozi.





Mohamed Said nakupongeza kwa ujumbe wako murwa kabisa. japo naona kuna baadhi ya wajumbe humu ndani wamekuona mnafiki lakini ulichosema ni kweli kuwa vijana hawa hawajafanya jambo la kiungwa na sijui viongozi wao wana waza nini.
Ndani ya ccm wapo makaburu na kama wanafikiri Wapinzani wa ccm ndiyo pekee makaburu kama alivosema baba yetu mwalimu Nyerere, baada ya kuwaondoa hao makaburu walio nje ya ccm wataingia ndani ya ccm na hapo ndipo kutakuwa sherehe kubwa kwao.

Zanzibar ni nchi ya watu wote hakuna cha mweusi au mrangi wote ni wazanzibar. natumai viongozi wa ccm Taifa watatoa kauli kali juu ya kitendo kisicho cha uungwana kilichofanywa na vijana hao wa ccm.
 
DSC_2469.jpg


Vijana wa Chama cha Mapinduzi CCM wakipita mbele ya mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akipokea matembezi ya Vijana hao waliotembea katika Mikoa Minee ya Kichama katika kuadhimisha miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar yaliyomalizia leo katika viwanja vya maisara Suleiman Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.]

Picha hiyo hapo juu ni bango la Kikaburu katika mwaka wa 2016 bango linalotukuza ubaguzi wa rangi.

DSC_2827.jpg


Sitaki kuamini kama Ali Mohamed Sheni na uongozi wa juu wa CCM Zanzibar wamewatuma vijana hawa kufanya haya.

Akili yangu inanikatalia kabisa.

Sitaki kuamini kuwa tumeanza kuwatengeza akina Hendrik Verwoerd na Eugene Terre Blanche weusi katika visiwa vya Zanzibar.

CCM Zanzibar inamuiga nani katika hili?

Hitler na Manazi walikuwa na vijana wao waliojulikana kama Stormtroopers ukipenda waite Brown Shirts?

Zanzibar tumeshawashuhudia Ton Ton Macout mfano wa wale wa Papa Doc wa Haiti visiwani wanajulikana kama Mazombie.

Sasa tumefungua ukurasa mwingine wa Adolf Eichman.

Hilo bango mbona litawagusa wengi katika safu ya uongozi wa siasa katika Zanzibar na wengine walipatapo hata kuiongoza nchi?

Machotara?

Nani huyu chotara?

Tumehama kwa Waarabu sasa tuko kwa Machotara!

Lakini huyo chotara si ana wajomba, babu, bibi na mama wakubwa na wadogo Waafrika?

CCM imefilisika kiasi hiki?

Nini hiki ni kiwewe cha CCM kushindwa uchaguzi au ni kitu gani?

Nini khasa tafsiri ya mambo haya?

Tusubiri In Sha Allah wakati utatupa jibu.



Kasema Mwalimu Nyerere karne ya ishirini na moja kuna watu wanapanda basi la ukabila...

Hawa wanapanda jahazi la ugozi.
Pia alisema 'kaburu ni kaburu tu, hata kama ni mweusi lakini una mawazo kama makaburu wa South Africa wewe ni kaburu tu'
 
Catch 22
Muajemi wa kizazi cha kumi na.mbili na
Mnyamwezi kizazi cha tatu
Fumbo
Naomba kuuliza Hizbu Chotara wanatambulikaje? Sura, rangi, nywele na macho. Hilo bango lingefafanua
 
Shein mwenyewe ni chotara .......................!!!
Shein ni chotara mweusi...wao wanazungumzia chotara weupe na sio chotara weusi wala chotara wa maji ya kunde. Wakati huo huo watahamia kwa wapemba dhidi ya waunguja...kisha watahamia Wazanzibari wenye asili ya Oman na wenye asili yaTabora.

CCM wasipofanya jambo la kusaidia mapema yatakuja tokea mabaya sana.
 
Nakuunga mkono kwa asilimia mia moja, na kuna siku Mungu atatenda maajabu mi ccm ianguke, kwa sasa anaipumbaza akili kwanza hii mi ccm kwa namna ili ijione yenyewe ndio yenyewe.
 
Yaani Wazanzibari wana sifa moja kuubwa
'unafiki'....huwezi kumuamini mzanzibari akiongea hiki anamaanisha au la....

Nimeambiwa watu wa visiwani....kote iwe Zanzibar au Ukerewe hii ni sifa yao kuu...
leo ataongea hiki..kesho ataongea kile....hujui msimamo wake hasa ni upi....
Naungana nawewe kwa kiasi kikubwa kabisa,na sababu ni kwamba umenifanya nikarecall na kurefer mambo mengi sana ambayo yamekuwa yakinenwa na kuandikwa na Viongozi flan wa zanzibar over the years pamoja na wadau wengine waliokuwa wakiitetea zanzibar na sasa wamegeuka Mamluki kwa unafiki. Kwa upande wa visiwa vingine sina uhakika.

Mwenyezi Mungu alisema bora uwe Moto au Baridi. Ukiwa vuguvugu atakutapika.

NIMEKUELEWA SANA MKUU.
 
Nakubaliana nawe kwa asilimia 98 kuhusu vijana hao kuweka bango hilo. Lakini lazima pia tuwe wakweli. wale waarabu waliondoka Zanzibar baada ya mapinduzi au waarabu hao waliopinduliwa bado wanadai (siyo rasmi) kuwa Zanzibar ni yao na kwamba kwa kuwa waliondolewa kwa mtutu wa bunduki watarejea kupitia sanduku la kura. Sasa hapo ndipo tatizo. Kinachoonekana hapa ni kuwa waarabu hao wanatumia baadhi ya viongozi wa CUF kutaka kurejea Zanzibar kwa njia ya kura...
Mkuu wewe hujuwi Asp imeanzaje ni mungano wa waafrica na washirazi hawa washirazi ndio machotara za naona wameshageukana sasa hawa kazi imeanza ukiwa kaburu ni kaburu tu kesho watageukana waafrica kwa waafrika itakuwa mmakonde na msukumal
 
Chotara hizbu zanzibar si nchi ya wazungu. Chotara hizbu zanzibar si nchi ya waarabu. Chotara hizbu zanzibar si nchi ya wachina na nk.

Sasa wameandika Chotara hizbu zanzibar ni nchi ya Waafrika.

Ubaguzi ni wa kulaaniwa lakin katika hili sioni wapi ulipo hasa ukitilia maanani kuwa mtawala wa kabla ya Mapinduzi alikuwa mwarabu na kuna hisia kuwa anataka kurudi tena. Kuna ubaya gani kuwaambia wa zanzibar wenzao wanao shabikia kurudi kwa sultani kuwa zanzibar si nchi ya kiarabu bali ya kiafrika?
Mkuu. Dunia yaleo hakuna muwarabu anaetaka kirudi znz kuitawala.
Na isitoshe waarabu wapo znz na haitatokea waarabu kufutika znz itachukuwa karne nyingi waarabu na silka za kiarabu kufutika znz.
Waarabu wapo ccm waarabu wapo cuf waarabu wapo mitaani znz.
Isitoshe hata tamaduni za znz nyingi ni za kiarabu.
Hao wanao sema chotara waondoke sio tu hawaitakii mema znz wajue pia hawazitakii mema ndoa zawatu.
Maana viongozi wengi wengi wa ccm znz wake zao ni machotara.
 
Kila siku UKAWA mnawaandama wahindi kuhusu kuishi kwao kwenye nyumba za NHC...Leo ndio mnajifanya kuwatetea!?

Kumbukumbu zangu Zinasema aliyegombea ilala Chadema alikuwa muhindi. Sijaelewa wanaandamwa vipi lini na wapi bwana Lizaboni.

😎😎
 
Back
Top Bottom