Kuna taarifa za ubaguzi wa ajira ndani ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa wapinzani na hasa watu kutoka kisiwa cha Pemba. Taarifa hizi zinaendelea kuzagaa na kutolewa katikati ya lawama za wakubwa kufumbia macho taarifa hizo au kukanusha bila uthibitisho wa ziada.
Taarifa zinadokeza kuwa mara baada ya kufanyika uchaguzi wa marudio wa Machi, 2016 , mikakati ilipangwa kuhakikisha wapinzani hawapati nafasi za kuajiriwa na vile vile kuhakikisha watu walidhaniwa kuwa wapinzani wanaondolewa katika vitengo nyeti. Taarifa zinadokeza kuwa zoezi hili limefanyika kwa asilimia zaidi ya 90%
NAMNA UBAGUZI UNAVYOFANYWA.
Taarifa zinaeleza kwamba zoezi la uajiri wa nafasi mpya, linaratibiwa vyema kwa kushirikisha vyombo vya usalama (usalama wa taifa) na UVCCM, Vijana wa UVCCM waliomo serikalkini na mawakala wao kwenye TISS wametengeneza mtandao kuhakikisha kila nafasi inashikiliwa na mwana CCM au wanaoitwa ":watu wetu". Mkakati huu umepangwa na kupata baraka za ofisi moja Kupitia Ofisi ya Makamo wa pili wa Rais wa Zanzibar.
Taarifa zinasema kuwa kumekuwa na hamisha hamisha ya wafanyakazi hasa wa utumishi kwenye vitengo ambao waliokuwepo huondolewa na kuchomekwa watu wa mfumo ili kufanikisha suala hili. Kuna idara nyingi na hata taasisi zenye bodi na mashirika zinaingiliwa majukumu yake na Utumishi mkuu kwa watu kuhamishwa na mamlaka ya bodi hizo kunyanganywa kwa kisingizio cha "Utumishi Mkuu"
Zipo taarifa kuwa hata zile nafasi zinapotangazwa zilizohitajika zijazwe na watu kutoka Pemba kwa mfano, hupelekwa watu kutoka Unguja au Bara ambao wanaaminika kuwa wako upande wa Utawala na kuchukuwa nafasi hizo.
MAJIBU MEPESI.
Kupitia tuhuma hizo, Waziri wa nchi ofisi ya Makamo wa pili wa Rais( Mh Muhamed Aboud) amewahi kutolea ufafanuzi suala hili na kubainisha kwamba hakuna ubaguzi na mchakato unakuwa wa wazi ambapo hutangazwa na wenye sifa ndio wanaajiriwa jee huo ndio ukweli ?
Taarifa zinasema hilo sio tatizo, Sheria ya Utumishi wa ummma imeeleza vyema kuhusu mchakato ambapo nafasi hutangazwa na wenye sifa ndio wanatakiwa kuajiriwa, Hapa tatizo si mchakato, Tatizo ni DHAMIRA, inaelezwa kuwa mkakati ni kuwa hata kama mtu ana sifa ilimradi ni Mpinzani anatafutiwa mazingira ya kuachwa. Zipo taarifa kuwa imefika mahali watu wana sifa na wameshachaguliwa na kuhojiwa halafu wanaachwa baada ya kufanyiwa "veting" na kile kitengo kinachoitwa "GSO" Veting hio inasemwa inaelekezwa kwenye siasa na kupekuliwa asili ya familia ya mtu. Hapa ndipo vijana wa mfumo wa UVCCM wanapohusishwa.
Viongozi ama kwa kutojuwa au kwa makusudi hawataki kujiridhisha kadhia hii. Mfano wa karibuni ni uajiri wa walimu na nafasi zinazotangazwa kupitia mashirika na taasisi za Serikali.
ATHARI
Athari ya kwanza ni kuajiriwa watu ambao hawana uwezo na nyengine ni kuigawa jamii. Katika hili Kule Zanzibar , jamii ya watu wa Pemba imeathiriwa sana. Zipo taarifa kuwa ukiwa Mpemba hata kama ni CCM huaminiwi na wako wengi wamekosa kuajiriwa kwa kudhaniwa kuwa wapemba wote ni wapinzani. (huu sio ukweli)
Tetesi hizi ni nyeti. Imefika wakati maofisa wanaohusika na uajiri huwaeleza watu wazi wazi kuwa "...wewe unazo sifa lakini huwezi kuajiriwa, huwa wanasema tatizo liko kwa watu wenu ambao wametoa taarifa kuwa hufai..." Hii ndio hali ilivyo.
Mwandishi amepataa tetesi hizi kupitia kwa vyanzo muhimu na sasa taarifa hizi zimezagaa kule Zanzibar.
MWISHO.
SMZ inatakiwa kuondowa dhana hii kwa vitendo, Kwenye jamii hizi taarifa zpo na hazipaswi kupuuzwa. Wazanzibari wenyewe wanafahamiana na huwa unaambiwa Zanzibar hakuna siri. Ikiwa Mkakati huu upo basi kwa haraka uondolewe kwa maslahi ya Taifa.
Kishada.
Taarifa zinadokeza kuwa mara baada ya kufanyika uchaguzi wa marudio wa Machi, 2016 , mikakati ilipangwa kuhakikisha wapinzani hawapati nafasi za kuajiriwa na vile vile kuhakikisha watu walidhaniwa kuwa wapinzani wanaondolewa katika vitengo nyeti. Taarifa zinadokeza kuwa zoezi hili limefanyika kwa asilimia zaidi ya 90%
NAMNA UBAGUZI UNAVYOFANYWA.
Taarifa zinaeleza kwamba zoezi la uajiri wa nafasi mpya, linaratibiwa vyema kwa kushirikisha vyombo vya usalama (usalama wa taifa) na UVCCM, Vijana wa UVCCM waliomo serikalkini na mawakala wao kwenye TISS wametengeneza mtandao kuhakikisha kila nafasi inashikiliwa na mwana CCM au wanaoitwa ":watu wetu". Mkakati huu umepangwa na kupata baraka za ofisi moja Kupitia Ofisi ya Makamo wa pili wa Rais wa Zanzibar.
Taarifa zinasema kuwa kumekuwa na hamisha hamisha ya wafanyakazi hasa wa utumishi kwenye vitengo ambao waliokuwepo huondolewa na kuchomekwa watu wa mfumo ili kufanikisha suala hili. Kuna idara nyingi na hata taasisi zenye bodi na mashirika zinaingiliwa majukumu yake na Utumishi mkuu kwa watu kuhamishwa na mamlaka ya bodi hizo kunyanganywa kwa kisingizio cha "Utumishi Mkuu"
Zipo taarifa kuwa hata zile nafasi zinapotangazwa zilizohitajika zijazwe na watu kutoka Pemba kwa mfano, hupelekwa watu kutoka Unguja au Bara ambao wanaaminika kuwa wako upande wa Utawala na kuchukuwa nafasi hizo.
MAJIBU MEPESI.
Kupitia tuhuma hizo, Waziri wa nchi ofisi ya Makamo wa pili wa Rais( Mh Muhamed Aboud) amewahi kutolea ufafanuzi suala hili na kubainisha kwamba hakuna ubaguzi na mchakato unakuwa wa wazi ambapo hutangazwa na wenye sifa ndio wanaajiriwa jee huo ndio ukweli ?
Taarifa zinasema hilo sio tatizo, Sheria ya Utumishi wa ummma imeeleza vyema kuhusu mchakato ambapo nafasi hutangazwa na wenye sifa ndio wanatakiwa kuajiriwa, Hapa tatizo si mchakato, Tatizo ni DHAMIRA, inaelezwa kuwa mkakati ni kuwa hata kama mtu ana sifa ilimradi ni Mpinzani anatafutiwa mazingira ya kuachwa. Zipo taarifa kuwa imefika mahali watu wana sifa na wameshachaguliwa na kuhojiwa halafu wanaachwa baada ya kufanyiwa "veting" na kile kitengo kinachoitwa "GSO" Veting hio inasemwa inaelekezwa kwenye siasa na kupekuliwa asili ya familia ya mtu. Hapa ndipo vijana wa mfumo wa UVCCM wanapohusishwa.
Viongozi ama kwa kutojuwa au kwa makusudi hawataki kujiridhisha kadhia hii. Mfano wa karibuni ni uajiri wa walimu na nafasi zinazotangazwa kupitia mashirika na taasisi za Serikali.
ATHARI
Athari ya kwanza ni kuajiriwa watu ambao hawana uwezo na nyengine ni kuigawa jamii. Katika hili Kule Zanzibar , jamii ya watu wa Pemba imeathiriwa sana. Zipo taarifa kuwa ukiwa Mpemba hata kama ni CCM huaminiwi na wako wengi wamekosa kuajiriwa kwa kudhaniwa kuwa wapemba wote ni wapinzani. (huu sio ukweli)
Tetesi hizi ni nyeti. Imefika wakati maofisa wanaohusika na uajiri huwaeleza watu wazi wazi kuwa "...wewe unazo sifa lakini huwezi kuajiriwa, huwa wanasema tatizo liko kwa watu wenu ambao wametoa taarifa kuwa hufai..." Hii ndio hali ilivyo.
Mwandishi amepataa tetesi hizi kupitia kwa vyanzo muhimu na sasa taarifa hizi zimezagaa kule Zanzibar.
MWISHO.
SMZ inatakiwa kuondowa dhana hii kwa vitendo, Kwenye jamii hizi taarifa zpo na hazipaswi kupuuzwa. Wazanzibari wenyewe wanafahamiana na huwa unaambiwa Zanzibar hakuna siri. Ikiwa Mkakati huu upo basi kwa haraka uondolewe kwa maslahi ya Taifa.
Kishada.