Ubahili, silaha ya siri wanayoitumia matajiri wengi ambao walikuwa masikini

Ubahili, silaha ya siri wanayoitumia matajiri wengi ambao walikuwa masikini

Heshima kwenu wakuu wangu

Kama kawaida leo nakuja tena katika jukwaa muhimu kwangu hapa JF.

Hakika kuna mambo mengi sana yanayochangia mpaka mtu kuwa na mali nyingi ama utajiri. Ukiachilia mbali matajiri waliorithi mali, waliopata utajiri kwa bahati kama michezo ya bahati nasibu na wale waliojikusanyia mali kutokana na vipaji vyao kama Sanaa na soka, matajiri wote waliobaki ambao walikuwa masikini na wakawa matajiri wana sifa kubwa ya UBAHILI.

Lakini bila kujali umepata vipi utajiri wako, kama hutakuwa mbahili, hakika utafilisika, hakika hutadumu na mali zako, hakika ipo siku watu watakucheka na kusema umefulia. Kiufupi, matajiri wote unawaona duniani ambao wamedumu kwa muda mrefu ni mabahili. Ni vyema pia ujue kwamba ubahili wa mtu kama Warren Buffet hauwezi ukafanana na ubahili kama wa yule Mkinga wa Kariakoo, wote ni ubahili ila tofauti ni mmoja anafanya ubahili kulingana na matrilioni alionayo na mwingine anafanya ubahili kulingana na mamilioni alionayo.

Naomba pia ieleweke kwamba, ninaposema tajiri natambua kwamba unatofautiana ngazi. Kuna wanaomiliki duka moja kubwa la jumla wakati anaanza maisha alianza kuuza duka la kaka yake, kisha kiosk baadae akamiliki duka kubwa namuita tajiri. Kuna yule ambaye ana estate labda Chicago naye namuita tajiri. Ana hisa timu ya Barcelona, naye ni tajiri.

Nikiri kwamba hii mada imekuja kichwani baada ya mara kwa mara watu, waume kwa wake kupenda kuniita bahili. Ki ukweli huwa nafarijika sana, sababu kwangu bahili ni kinyume cha mfujaji, kwangu bahili ni mtu anayetumia rasilimali zake kwa uangalifu, kwa akili ama mtu anayetumia mali yake baada ya kushirikisha ubongo kuamua na si moyo. Kwangu ubahili ni hatua moja muhimu kwenda kwenye utajiri. Pia ni hatua muhimu sana, kubaki na utajiri.

Ubahili ni kuishi maisha chini ya kipato chako, na si kuishi maisha sawa na kipato chako, au zaidi ya kipato chako. Ubahili ni ku save. Sijawahi kuona mtu aliyeanzia chini kwa kipato na baadae akawa tajiri halafu akose sifa ya ubahili.

Mark Zuckerberg mmiliki wa Facebook, huvaa t-shirt na jinsi, vazi la bei raisi kazini na katika sehemu kubwa ya maisha yake. Amancio Ortega (ana mali zenye thamani ya $ 66 Billions) huwa anakwenda mgahawani kula na wafanyakazi wake chakula cha kawaida sana. Charlie Ergen (anamiliki $14 bilioni) huwa anabeba chakula kutoka nyumbani kila siku kwenda nacho ofisini kwake (kwenye kampuni yake). Warren Buffet kila siku hutengewa na mke wake kati ya $2 na $3 kwa ajili ya chai.

Hii ni kweli hata kwa Tanzania au Africa, tunawafahamu watu wengi waliofuja mali na sasa hivi wamebaki masikini na kituko kwenye jamii zetu hususani wale waliorithi ama kupata mali kwa ghafla. Nawakubali Wachaga wengi, wapare wengi sababu hii silaha huwafikisha mbali sana kimaisha.

Ubahili sio sifa mbaya. Lakini usiwe mbahili kula, ukawa mfujaji kwa mademu, usiwe mbahili kuitunza familia yako, ukawa mfujaji kwenye mitungi. Ishi maisha ya kawaida, kipato unachopata wekeza.

HATA UWE UNAINGIZA HELA NYINGI KIASI GANI, UKIWA MTU WA KUFUJA MALI UTAKUFA MASIKINI. NA HATA UWE UNAINGIZA PESA NDOGO KIASI GANI, UKIWA BAHILI NA KUWEKEZA UTAKUWA TAJIRI ENDAPO MUNGU ATAKUPA UZIMA.
Haya madini yalikuwa wapi!!!
 
Heshima kwenu wakuu wangu

Kama kawaida leo nakuja tena katika jukwaa muhimu kwangu hapa JF.

Hakika kuna mambo mengi sana yanayochangia mpaka mtu kuwa na mali nyingi ama utajiri. Ukiachilia mbali matajiri waliorithi mali, waliopata utajiri kwa bahati kama michezo ya bahati nasibu na wale waliojikusanyia mali kutokana na vipaji vyao kama Sanaa na soka, matajiri wote waliobaki ambao walikuwa masikini na wakawa matajiri wana sifa kubwa ya UBAHILI.

Lakini bila kujali umepata vipi utajiri wako, kama hutakuwa mbahili, hakika utafilisika, hakika hutadumu na mali zako, hakika ipo siku watu watakucheka na kusema umefulia. Kiufupi, matajiri wote unawaona duniani ambao wamedumu kwa muda mrefu ni mabahili. Ni vyema pia ujue kwamba ubahili wa mtu kama Warren Buffet hauwezi ukafanana na ubahili kama wa yule Mkinga wa Kariakoo, wote ni ubahili ila tofauti ni mmoja anafanya ubahili kulingana na matrilioni alionayo na mwingine anafanya ubahili kulingana na mamilioni alionayo.

Naomba pia ieleweke kwamba, ninaposema tajiri natambua kwamba unatofautiana ngazi. Kuna wanaomiliki duka moja kubwa la jumla wakati anaanza maisha alianza kuuza duka la kaka yake, kisha kiosk baadae akamiliki duka kubwa namuita tajiri. Kuna yule ambaye ana estate labda Chicago naye namuita tajiri. Ana hisa timu ya Barcelona, naye ni tajiri.

Nikiri kwamba hii mada imekuja kichwani baada ya mara kwa mara watu, waume kwa wake kupenda kuniita bahili. Ki ukweli huwa nafarijika sana, sababu kwangu bahili ni kinyume cha mfujaji, kwangu bahili ni mtu anayetumia rasilimali zake kwa uangalifu, kwa akili ama mtu anayetumia mali yake baada ya kushirikisha ubongo kuamua na si moyo. Kwangu ubahili ni hatua moja muhimu kwenda kwenye utajiri. Pia ni hatua muhimu sana, kubaki na utajiri.

Ubahili ni kuishi maisha chini ya kipato chako, na si kuishi maisha sawa na kipato chako, au zaidi ya kipato chako. Ubahili ni ku save. Sijawahi kuona mtu aliyeanzia chini kwa kipato na baadae akawa tajiri halafu akose sifa ya ubahili.

Mark Zuckerberg mmiliki wa Facebook, huvaa t-shirt na jinsi, vazi la bei raisi kazini na katika sehemu kubwa ya maisha yake. Amancio Ortega (ana mali zenye thamani ya $ 66 Billions) huwa anakwenda mgahawani kula na wafanyakazi wake chakula cha kawaida sana. Charlie Ergen (anamiliki $14 bilioni) huwa anabeba chakula kutoka nyumbani kila siku kwenda nacho ofisini kwake (kwenye kampuni yake). Warren Buffet kila siku hutengewa na mke wake kati ya $2 na $3 kwa ajili ya chai.

Hii ni kweli hata kwa Tanzania au Africa, tunawafahamu watu wengi waliofuja mali na sasa hivi wamebaki masikini na kituko kwenye jamii zetu hususani wale waliorithi ama kupata mali kwa ghafla. Nawakubali Wachaga wengi, wapare wengi sababu hii silaha huwafikisha mbali sana kimaisha.

Ubahili sio sifa mbaya. Lakini usiwe mbahili kula, ukawa mfujaji kwa mademu, usiwe mbahili kuitunza familia yako, ukawa mfujaji kwenye mitungi. Ishi maisha ya kawaida, kipato unachopata wekeza.

HATA UWE UNAINGIZA HELA NYINGI KIASI GANI, UKIWA MTU WA KUFUJA MALI UTAKUFA MASIKINI. NA HATA UWE UNAINGIZA PESA NDOGO KIASI GANI, UKIWA BAHILI NA KUWEKEZA UTAKUWA TAJIRI ENDAPO MUNGU ATAKUPA UZIMA.
NI KWELI KUPATA PESA SIO SHIDA JEE UNAWEZA KULINDA PESA ? HAPO MTIHANI
 
sasa mwisho wa kuwa tajiri ni nini kama hu spendi hizo hela utatumia kwa ajili ya nini
Mwisho wa utajiri ni usalama, mtoto wako akipata tatizo la moyo kwa mfano, unampeka moja kati ya hospitali bora kabisa India kupata tiba ya moyo.

Utajiri ni kuweza kufanya unachotaka, je wewe ni mshabiki wa soka, vipi ukiwa na kipato cha kutosha cha kukupeleka Qatar mwaka 2022 world Cup kushuhudia hayo mashindano?

Utajiri ni kuhifadhi mali za kutosha na kufika hatua ukiwa bado na nguvu zako na kuamua kustaafu kazi (siongelei kustaafu ajira). Tunataka utajiri kwa sababu kama hizo.

Ubahili ni utamaduni muhimu katika maisha yako. Mfano ukiwa unaingiza milioni 200 kwa mwaka, unaweza sasa kuamua kutumia hata milioni 50 (ni mfano) kwa mwaka na ukawa unauenzi utamaduni wa ubahili na bado maisha yakawa matamu. Mfano ukiwa unaingiza 50 milioni kwa mwaka na ukazitumia zote milioni 50 utakuwa masikini milele
 
hao matajili wanaoenda na vyakula maofisi mwao wanaogopa kuwekewa sumu hamna chochote
Sababu za kiusalama zinaweza zisababishe, lakini vipi kwa hao matajiri wengine wanaokula cafeteria na wafanyakazi wao. Kamprad tajiri wa pili Ulaya mmiliki wa kampuni ya IKEA anakula na wafanyakazi wake cafeteria.

Warren Buffet tajiri wa tatu duniani anaishi nyumba ya vyumba vitano, nyumba hiyo hiyo aliyonunua mwaka 1958 kwa $ 31,500 ndio anaishi mpaka leo. Kumbuka mwaka 1958 alikuwa hajawa hata millionaire, sasa hivi ni billionaire mwenye $ 70 billions

Nina mifano mingi sana mkuu, lakini tuishie hapa. Hoja ya msingi hapa ni kama unataka kufanikiwa kimaisha kwenye eneo la uchumi, lazima u adopt huu utamaduni wa ubahili.
 
Nimesoma
Hii
Imenigusa between 2015 untill this year i have blown money so bad and now imekuwa ngumu to get that pick point again.. i wish nijifunze zaidi about money.. for me i like the good life i use to tell
Myself if i cant live maisha mazuri sasa hela yakazi gani.. the more money napata ndivyo navyoongeza gharama ya maisha yangu... yani this year ndo najuta hasa because i wish i had done better choices and non of the things i have make me happy anymore anyway.. nilikuwa nahisi kuwa navitu vya gharama ni respect ila wala kawaida tuu kwanza i thought itaniketea wateja wamahana in business kujiweka classy ila ndomkwanza people fear that its just gonna be expensive ‍♀️‍♀️‍♀️.. help jamani i wish nipate mtu anifundishe about money.. msiniambie books im too busy.
 
mifano uliyotumia ina mushkeri kidogo kulingana na ulichokiongea ktk uzi labda kama mimi nimekuelewa vibaya
 
Hii ni dhana tuu. Ubahili unaweza kuwa ni sehemu ndogo sana ya sababu zinazochangia mtu kuwa tajiri.

Huwezi kuwa tajiri kwa kuwa mbahili. Huku ni kuwaponza watu.

Matokeo yake ni kutesa watu tuu. Jamaa yangu mmoja aliumwa akalazwa siku mbili tuu, naenda kumbelea akaanza kunipa wasaa nisiwe mbahili. Jamaa alikuwa anaongea kama vile anajutia kurundika hela. Ulikuwa ni woga tuu, mpaka kesho nikimkbusha tunacheka.

Huwezi ushinda umasikini kwa kuwa mbahili, ni majuto ndio huguata baadae.

Utajiri ni illusion guys. Huwezi fundishwa kuwa tajiri ukubwani. Tutakufa kwa madeni, sio kila mwenye hela ni tajiri. Na Ubahili sio utajiri.

.......................
 
Hii ni dhana tuu. Ubahili unaweza kuwa ni sehemu ndogo sana ya sababu zinazochangia mtu kuwa tajiri.

Huwezi kuwa tajiri kwa kuwa mbahili. Huku ni kuwaponza watu.

Matokeo yake ni kutesa watu tuu. Jamaa yangu mmoja aliumwa akalazwa siku mbili tuu, naenda kumbelea akaanza kunipa wasaa nisiwe mbahili. Jamaa alikuwa anaongea kama vile anajutia kurundika hela. Ulikuwa ni woga tuu, mpaka kesho nikimkbusha tunacheka.

Huwezi ushinda umasikini kwa kuwa mbahili, ni majuto ndio huguata baadae.

Utajiri ni illusion guys. Huwezi fundishwa kuwa tajiri ukubwani. Tutakufa kwa madeni, sio kila mwenye hela ni tajiri. Na Ubahili sio utajiri.

.......................
NI KWELI USIWE BAHIRI , USITUPE PESA WAKAATI SIO MUHIMU
 
Hebu nitofautishie ubahili na uchoyo
Mwenyewe nimedhani hapo kwenye ubahili angeweka ubinafsi ingewa na mantiki manake mbahili ni mtu ambaye hatumii kipato chake na hivo hata kuwekeza sijui manake sinibahili lakini mbinafsi ndo anaweza kuwekeza kwa sababu chake ni chake na chako ni chake pia yaani hata kama ana bilioni lakini buku yako anaitaka pia!
 
Yap sure mkuu. Kuna kitabu kinaielezea hii concept vizuri sana kinaitwa Millionaire Next Door.

Kinaelezea mfano lawyer au Banker atalazimika kuishi maisha ambayo jamii inamtazamia aishi. Mfano kuna mitaa ambayo ina maisha ghali, ataona asipokuwa na gari, tena sio paso hataeleweka mbele ya jamii. Wanataka kuvaa, kula, kuwa na marafiki ambao wanaendana na status yao n.k

Kwa kutaka kuishi kama jamii inavyowatazamia, wanajikuta wanaumia sana.
Nimeshakidownload ngoja nianze kukisoma weekend.
 
Mkuu nashukuru kwa kunigusa,huwa nami naambiwa hivyo hivyo namimi nakubali kwel ni mbahili lakini ubahiri wa maendeleo,nakumbuka nilianza na laki 3 ila kwa sasa namiliki vimilion kadhaa si haba,ubahiri huo ndiyo umenisaidia nifike hapa kwa hiyo ubahiri na mimi ni kama maji na Samaki,na siku zote ukitaka mafanikio kuwa bahiri hiyo ndiyo siri na pili usitunze pesa Benk au ndan itafutie kaz ya kufanya,bora ubaki hauna kitu lakini pesa ipo kwenye kaz au inazunguka,na wote waliopata pesa wakazitunza na kuanza kutoa kidogo kidogo waliishia kufirisika,kuna Mtu kutoa hata laki 5 ifanye kaz anaogopa itapotea na hao ndiyo mabingwa wa mipango kabla ya kupata pesa wakipata pesa wanaitelekeza mipango yao.Ubahili ni silaha maishani ila usipite kipimo,kwa mfano Mtu kwa mwezi anaingiza lak 4 lakini ananunua nguo au viatu elfu 50/laki au Mtu anamilik simu ya laki au laki 3 au mbili,mimi huwa najiuliza swali la kawaida tu Mtu anayemiliki simu ya smartphone ya laki moja na mwingine laki 3 huwa kuna utofaut gani? au zinatofautiana kip? cha maana,zingatia-: simpangii Mtu cha kununua au kumilik bali huo ni mtazamo wangu
 
Mkuu Ahsante sana.Mimi kila ninapokaa wananiita bahili ila yangu yananyoka kwa amani kabisa.
 
mifano uliyotumia ina mushkeri kidogo kulingana na ulichokiongea ktk uzi labda kama mimi nimekuelewa vibaya
Mkuu kwenye jambo gani. Kwa mifano ya ulaya/marekani nimelenga kuonesha kwamba hata matajiri wakubwa wanaishi maisha ya chini tofauti na ukubwa wa kipato wanachopata. Na penginevwangeishi maisha extravagant life wasingekuwa hapo walipo.

Na hiyo ninayoongelea ni culture ya kutumia below your means ndio jambo la msingi. Angalia kina bill Gates wanavyovaa.

Kama huamini angalia watumishi/wafanyakazi wanavyovaa, wanavyokula, magari wanayoendesha, matumizi yao bar n.k halafu fananisha na maisha ya wafanya biashara. Kisha angalia maisha ya watumishi uzeeni walio wengi utakuja kugundua, wanaishi magumu kutokana na utamaduni walijiwekea wakati bado wanafanya kazi.

Ubahili unaleta vitu viwili vikubwa. Kwanza unasaidia kulimbikiza mali, pili unaweza kukufanya uishi maisha ya aina yoyote.
 
Back
Top Bottom