Ubalozi wa Japani watoa dola 140,103 kwa ajili ya kujenga jengo la darasa katika shule ya Wasichana Sakura jijini Arusha

Ubalozi wa Japani watoa dola 140,103 kwa ajili ya kujenga jengo la darasa katika shule ya Wasichana Sakura jijini Arusha

Damaso

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
3,978
Reaction score
6,739
Ubalozi wa Japan ulifanya hafla ya utiaji saini Mradi wa Ujenzi wa Kitalu cha Darasa la Kiwango cha Juu katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Sakura iliyopo Wilaya ya Arusha, Mkoa wa Arusha.
1741965978393.jpg


Serikali ya Japani ilikubali kuongeza msaada wa ruzuku hadi kufikia Dola za Marekani 140,103 kwa mradi wa Msaada wa Miradi ya Usalama wa Binadamu wa Grassroots (GGHSP).
images - 2025-03-14T182753.462.jpeg


Mkataba wa mradi huo ulitiwa saini na H.E. Bw. MIKAMI Yoichi, Balozi Mteule wa Japan na Bw. Thomas Reuben, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Sakura.
images - 2025-03-14T182724.902.jpeg


Tusubirie jengo la darasa hilo likamilike kisha sifa apewe Mama Samia ilihali waliotoa pesa ni wajapani. Zimetoka dola 140,103 za kimarekani sawa na shilingi 372,305,724.87 za kitanzania. Muda sio mrefu jengo likisimama tutasikia viongozi wakisema kuwa Samia ametoa mchango mkubwa sana kwa shule hii.

ASANTENI SANA WAJAPANI! ASANTE SHIGERU ISHIBA NA SERIKALI YAKO TUKUFU YA JAPANI.

ARIGATOU GOZAIMASU
 
Hapo tayari mtu kashanunua harrier anaconda

Chezea ngozi nyeusi wewe
 
Kuna wakati walitoa msaada wa ujenzi wa choo kwa shule moja nikaona aibu. Hadi choo tunasaidiwa kujenga? Basi sawa, siku japan ikipata waziri mkuu mwenye sera kama tramp sijui itakuaje kwa JAICA kama USAID
 
😂😂😂

Mi nakuambia hivi

We fuatilia hadi jengo litakapoisha ndio utaona vituko mkuu
Yaani kiufupi watakula pesa zaidi ya 75% kisha sifa za ujenzi mbovu wa jengo atapewa Mama Samia! This is Africa!
 
Kuna wakati walitoa msaada wa ujenzi wa choo kwa shule moja nikaona aibu. Hadi choo tunasaidiwa kujenga? Basi sawa, siku japan ikipata waziri mkuu mwenye sera kama tramp sijui itakuaje kwa JAICA kama USAID
Tutaanza kulia kama mayatima
 
Nahisi ngozi nyeusi itakuwa imelaaniwa eti! Sasa mpaka darasa tunajengewa kwa msaada wa Japan, na wakati kila siku hela zinatapanywa kwenye mambo ya kipuuzi tu.
 
Nahisi ngozi nyeusi itakuwa imelaaniwa eti! Sasa mpaka darasa tunajengewa kwa msaada wa Japan, na wakati kila siku hela zinatapanywa kwenye mambo ya kipuuzi tu.
Usisahau kuwa pia jana viongozi wamekutana tena na Balozi wa Iran, Mhe. Dkt. Mohammed Nikhal kuzungumza kuhusu ushirikiano 😃 hii nchi inatafunwa na wachache 😔
 
Back
Top Bottom