Ubaya hauna kwao. Ya Loliondo ni zao la watanzania kutokemea ubaya

Ubaya hauna kwao. Ya Loliondo ni zao la watanzania kutokemea ubaya

Kituo kinachofuata ni kuwaondoa wamarangu, warombo na wamachame, wanaharibu mazingira ya mlima kilimanjaro kwa kukata miti ovyo na kuzika wafu wao kila mahali.

Eneo la kuwapeleka limeshapatikana kule mlele na kibaoni, Rukwa huko, wakajifunze jinsi ya kutengeneza radi
Tuendelee na ukondoo huu. Soon kila mtu atahamishwa
 
EeenHeeee. Anarekebisha Loliondo hivyo, au siyo?
Kawahimize wamasai watoe fadhira basi!

Na usidhani ni hilo tu; ila akili yako chovu haiwezi kukuonyesha "marekebisho" mabaya zaidi anayotenda yeye.
Mara kadhaa huwa napuuzia mijadala yako
 
Ni hapa hapa JF unapata kusoma, kujifunza tabia na aina ya watanzania wenzako jinsi walivyo.

Yaani kutokana na yanayotokea nje ya JF na haya tunayoandika mitandaoni especially JF huo ndiyo ukweli wa aina ya Mtanzania wa kweli alivyo, hakuna mwenye uwezo wa kutokomeza au kufanya maamuzi!.

Tuna maneno mazuri na yenye ushawishi kweli kweli but at the end ni sawa na huyu dog hapa [emoji1484]...
View attachment 2271099
Hivi mpaka leo hamuamini kuwa mwendakuzimu amekufa? Poleni sana
 
Ubaya hauna kwao. Ubaya hauna macho. CCM Ina unasaba na ubaya. Kila mtu/kikundi ama chama wataonja ubaya wa CCM kwa wakati wake.

Mifno ya vyama na watu waliyoonja ubaya wa CCM.
-Ndugai, Membe, Sumaye, Lowasa, Lisu, Mbatia, e.t.c
-CUF, NCCR, Chadema,
Hivi sasa akina Halima Mdee wako bungeni kinyume na sheria. Wamevunja katiba lkn watanzania hatuandamani, tunadhani ni suala la chadema tu.

Wamasai wa Loliondo wanaporwa ardhi yao, watanzania hatuandamani tumewaachia wamasai.

Wakifanikiwa Loliondo watawaondoa kwenye maeneo yao wakazi wa Kigamboni, Marangu, Kisiwa cha Saanane, Bagamoyo, Mikumi, Kalenga, n.k.

Injustice somewhere is Injustice everywhere.
Mmh ! Injustice somewhere is injustice everywhere !!
 
Kituo kinachofuata ni kuwaondoa wamarangu, warombo na wamachame, wanaharibu mazingira ya mlima kilimanjaro kwa kukata miti ovyo na kuzika wafu wao kila mahali.

Eneo la kuwapeleka limeshapatikana kule mlele na kibaoni, Rukwa huko, wakajifunze jinsi ya kutengeneza radi
Hahaha sounds like mtoto alie nyimwa pipi. Sasa anataka kulipiza. Kwanza wale hawaishi ndani ya hifadhi.Hawana mifugo mingi, hawaswagi ng'ombe.
Pili serikali ihamishe wilaya tatu ndani ya mkoa mmoja?
Keep dreaming man
 
Ubaya hauna kwao. Ubaya hauna macho. CCM Ina unasaba na ubaya. Kila mtu/kikundi ama chama wataonja ubaya wa CCM kwa wakati wake.

Mifno ya vyama na watu waliyoonja ubaya wa CCM.
-Ndugai, Membe, Sumaye, Lowasa, Lisu, Mbatia, e.t.c
-CUF, NCCR, Chadema,
Hivi sasa akina Halima Mdee wako bungeni kinyume na sheria. Wamevunja katiba lkn watanzania hatuandamani, tunadhani ni suala la chadema tu.

Wamasai wa Loliondo wanaporwa ardhi yao, watanzania hatuandamani tumewaachia wamasai.

Wakifanikiwa Loliondo watawaondoa kwenye maeneo yao wakazi wa Kigamboni, Marangu, Kisiwa cha Saanane, Bagamoyo, Mikumi, Kalenga, n.k.

Injustice somewhere is Injustice everywhere.
Watanzania wengi hatuna ufahamu wa jinsi tulivyobarikiwa. Malalamiko mengi yanatokana na upungufu wa uelewa wa utajiri tulionao, siku zote tunajiona wadogo tu na wanapokuja raia wa mataifa yanayofundisha watoto wao maana ya kuhangaikia mkate wao wa kila siku kwa kutoka jasho huwa wanatudharau na kutumia fursa tulizonazo ambazo hatujui kama ni fursa tukiwa tumemezwa na akili za malalamiko.


Eneo zima la Tanzania lenye kutumiwa na uhfadhi wa wanyama lina kilometa za maraba 362,000 ni kubwa kuliko nchi kama tano za Ulaya ukiziunganisha pamoja, lakini hatuelewi maana ya utajiri huu tuliopewa bure na Mungu tunakuwa ni watu wa kupiga siasa nyepesi kila mara.

Hao wamasai wamepelekwa wakaishi Handeni mahali walipowekewa miundo mbinu ya kisasa na kujengewa na nyumba kabisa na malipo ya kuhamishwa kwa maana ya fidia wamelipwa pia. Na vyombo vyao vimesafirishwa na usafiri uliolipwa na serikali.

Lengo ni hizo kilomita za mraba 1500 zitunzwe ili maliasili isije kupotea kabisa. Kwani ikipotea watakaolaumu miaka kumi au ishirini ijayo wataikosoa serikali hawatamlaumu mwingine yoyote yule.
 
Watanzania wengi hatuna ufahamu wa jinsi tulivyobarikiwa. Malalamiko mengi yanatokana na upungufu wa uelewa wa utajiri tulionao, siku zote tunajiona wadogo tu na wanapokuja raia wa mataifa yanayofundisha watoto wao maana ya kuhangaikia mkate wao wa kila siku kwa kutoka jasho huwa wanatudharau na kutumia fursa tulizonazo ambazo hatujui kama ni fursa tukiwa tumemezwa na akili za malalamiko.


Eneo zima la Tanzania lenye kutumiwa na uhfadhi wa wanyama lina kilometa za maraba 362,000 ni kubwa kuliko nchi kama tano za Ulaya ukiziunganisha pamoja, lakini hatuelewi maana ya utajiri huu tuliopewa bure na Mungu tunakuwa ni watu wa kupiga siasa nyepesi kila mara.

Hao wamasai wamepelekwa wakaishi Handeni mahali walipowekewa miundo mbinu ya kisasa na kujengewa na nyumba kabisa na malipo ya kuhamishwa kwa maana ya fidia wamelipwa pia. Na vyombo vyao vimesafirishwa na usafiri uliolipwa na serikali.

Lengo ni hizo kilomita za mraba 1500 zitunzwe ili maliasili isije kupotea kabisa. Kwani ikipotea watakaolaumu miaka kumi au ishirini ijayo wataikosoa serikali hawatamlaumu mwingine yoyote yule.
Mkuu, umeandika mengi ninayoweza kukubaliana nawe, hasa hayo uliyoeleza katika aya ya kwanza. Tanzania tumebahatika sana, lakini wenyewe, na hasa viongozi wetu hawatambui neema aliyotujaalia Mwenyezi Mungu.

Nisipokubaliana nawe ni katika hilo la matunzo, maendelezo na matumizi ya raslimali hii tuliyojaliwa., siyo katika swala hili la Ngorongoro pekee, lakini hata katika raslimali nyingi nyingine hapa nchini, mfano kama madini, na mazao ya misituni- karibu misitu yetu yote tumeiteketeza, lakini huwezi kuona popote tulipofaidika na miti iliyokuwa ikivunwa.

Swala la Loliondo wa kulaumiwa ni serikali (viongozi). Unaeleza hapa kwamba Masaai wamejengewa nyumba , na mengine kadhaa, na kwa upande wa pili kwa hiyo unawatupia lawama hao ambao wanasita kuhama kwa sababu mbalimbali, zikiwemo za kuchochewa (of course) na wanaofaidika na uwepo wao huko Loliondo.
Serikali ilipashwa kujiandaa vyema na kuwaanda wananchi kwa muda mrefu wa kutosha, kuwapa elimu. Hili haliwezi kufanywa kuwa kama jambo la dharura.

Unataka kumhamisha mwananchi aliyeishi miaka na miaka sehemu aliyoizoea. Kaa naye mweleze kinagaubaga yote na kumjengea uelewa wa hali iliyopo. Huwezi kwenda kumvamia, miezi sita unamwambia unbataka ahame, na wala humpi maelezo ya kutosha.

Serikali inapofanya mambo kuwa kama ya hiana, siri, na kuonekana kusema uongo, hali hiyo haimpi mwananchi utulivu na kuamini inachokisema serikali. Hili linakorezwa zaidi na historia ya kutokuwa wazi kwa serikali katika mambo iliyowahi kufanya katika maeneo ya aina hiyo.

Kwa hiyo, katika jambo hili, serikali ilipashwa kuwa na subira nyingi, na kutumia wakati wa kutosha kushirikiana na wananchi ikiwaeleza na kuwaelimisha kinachotakiwa kufanyika.

Kosa inalofanya serikali yetu, na hasa viongozi hawa, ni kujiona kuwa kwa kuwa wao ni serikali wanaweza kuamru na kutumia nguvu wakati wowote ili kutimiza malengo yao. 'Mentality' ya namna hii ni ya kikoloni.

Jambo la pili ninalotaka kukueleza ni hili. Je, serikali ilishawahi kujiridhisha kwamba hakuna njia bora inayoweza ku'manage' eneo hilo bila ya kuhamisha watu wote walioko huko, na bado sehemu hiyo ikaendelea kuwa katika hali yake nzuri? Hakuna njia kabisa za kufanya hivyo, kukawa na watu kiasi kinachoweza kubebwa na eneo hilo, na bado ustawi wa wanyama na uasili wa eneo ukaendelea kustawi?
Kwa nini serikali hupenda kurukia tu mambo yanayoonekana kuwa rahisi kufanyika huku ikiumiza wananchi wake, badala ya kuangalia uwezekano mbadala kama upo?

Kuna hili suala la mifugo kuwa mingi katika eneo hilo na kusababisha uharibifu. Hili kweli ni gumu kulidhibiti?
Kama kuna mifugo inayotoka nchi jirani inayoletwa eneo hilo kwa ajili ya malisho, hili nalo ni swala la kuwaumiza wananchi wako, badala ya kudhibiti hiyo mifugo isiingie kutoka huko kwingine?

Mwisho, nimalizie kwa hili linalosemwa na linalokera zaidi kama ni jambo la ukweli.
Kama wananchi wa nchi hii wanapewa usumbufu mkubwa, na hata upotevu wa maisha kwa sababu za kutaka kunufaisha wageni kwa kisingizio cha uwekezaji, kama hii ndiyo sababu inayoweka msukumo juu ya swala hili la wananchi kuhamishwa makazi yao, hapa nitasema uhuru wetu hauna maana yoyote. Na kama hivyo ndivyo wanavyoliona jambo hili viongozi wetu, basi wananchi wanayo haki ya kupigania uhuru wao unaopotea.
 
Hivi mpaka leo hamuamini kuwa mwendakuzimu amekufa? Poleni sana
Huwa nasoma humu wadau wakireply kwa watu kama wewe as, 'mumeo bado anakupenda?'.

Nilkuwa nashangaa sana why lugha kama hiyo!.
 
Mkuu, umeandika mengi ninayoweza kukubaliana nawe, hasa hayo uliyoeleza katika aya ya kwanza. Tanzania tumebahatika sana, lakini wenyewe, na hasa viongozi wetu hawatambui neema aliyotujaalia Mwenyezi Mungu.

Nisipokubaliana nawe ni katika hilo la matunzo, maendelezo na matumizi ya raslimali hii tuliyojaliwa., siyo katika swala hili la Ngorongoro pekee, lakini hata katika raslimali nyingi nyingine hapa nchini, mfano kama madini, na mazao ya misituni- karibu misitu yetu yote tumeiteketeza, lakini huwezi kuona popote tulipofaidika na miti iliyokuwa ikivunwa.

Swala la Loliondo wa kulaumiwa ni serikali (viongozi). Unaeleza hapa kwamba Masaai wamejengewa nyumba , na mengine kadhaa, na kwa upande wa pili kwa hiyo unawatupia lawama hao ambao wanasita kuhama kwa sababu mbalimbali, zikiwemo za kuchochewa (of course) na wanaofaidika na uwepo wao huko Loliondo.
Serikali ilipashwa kujiandaa vyema na kuwaanda wananchi kwa muda mrefu wa kutosha, kuwapa elimu. Hili haliwezi kufanywa kuwa kama jambo la dharura.

Unataka kumhamisha mwananchi aliyeishi miaka na miaka sehemu aliyoizoea. Kaa naye mweleze kinagaubaga yote na kumjengea uelewa wa hali iliyopo. Huwezi kwenda kumvamia, miezi sita unamwambia unbataka ahame, na wala humpi maelezo ya kutosha.

Serikali inapofanya mambo kuwa kama ya hiana, siri, na kuonekana kusema uongo, hali hiyo haimpi mwananchi utulivu na kuamini inachokisema serikali. Hili linakorezwa zaidi na historia ya kutokuwa wazi kwa serikali katika mambo iliyowahi kufanya katika maeneo ya aina hiyo.

Kwa hiyo, katika jambo hili, serikali ilipashwa kuwa na subira nyingi, na kutumia wakati wa kutosha kushirikiana na wananchi ikiwaeleza na kuwaelimisha kinachotakiwa kufanyika.

Kosa inalofanya serikali yetu, na hasa viongozi hawa, ni kujiona kuwa kwa kuwa wao ni serikali wanaweza kuamru na kutumia nguvu wakati wowote ili kutimiza malengo yao. 'Mentality' ya namna hii ni ya kikoloni.

Jambo la pili ninalotaka kukueleza ni hili. Je, serikali ilishawahi kujiridhisha kwamba hakuna njia bora inayoweza ku'manage' eneo hilo bila ya kuhamisha watu wote walioko huko, na bado sehemu hiyo ikaendelea kuwa katika hali yake nzuri? Hakuna njia kabisa za kufanya hivyo, kukawa na watu kiasi kinachoweza kubebwa na eneo hilo, na bado ustawi wa wanyama na uasili wa eneo ukaendelea kustawi?
Kwa nini serikali hupenda kurukia tu mambo yanayoonekana kuwa rahisi kufanyika huku ikiumiza wananchi wake, badala ya kuangalia uwezekano mbadala kama upo?

Kuna hili suala la mifugo kuwa mingi katika eneo hilo na kusababisha uharibifu. Hili kweli ni gumu kulidhibiti?
Kama kuna mifugo inayotoka nchi jirani inayoletwa eneo hilo kwa ajili ya malisho, hili nalo ni swala la kuwaumiza wananchi wako, badala ya kudhibiti hiyo mifugo isiingie kutoka huko kwingine?

Mwisho, nimalizie kwa hili linalosemwa na linalokera zaidi kama ni jambo la ukweli.
Kama wananchi wa nchi hii wanapewa usumbufu mkubwa, na hata upotevu wa maisha kwa sababu za kutaka kunufaisha wageni kwa kisingizio cha uwekezaji, kama hii ndiyo sababu inayoweka msukumo juu ya swala hili la wananchi kuhamishwa makazi yao, hapa nitasema uhuru wetu hauna maana yoyote. Na kama hivyo ndivyo wanavyoliona jambo hili viongozi wetu, basi wananchi wanayo haki ya kupigania uhuru wao unaopotea.
Umeandika mengi japo unachanganya mambo
1. Ngorongoro ndipo wafugaji wamehamishwa walioridhia mchakato na wamepewa na fidia. Wale ambao wanapiga kelele ni mapapa ambao wananufaika na malisho hawa wako Tz na Kenya. Na wengi wanatumia maneno wamasai wanaonewa wenyewe hawapo (cite ) .
2. Loliondo kuna pori kama Square km 4500 na ambapo Square km 1500 ndio inayowekewa mipaka. Na kuwa pori Tengefu , shughuli za binadamu hazihitajiki hapo. Eneo liliilo salia Square km 2500 ufugaji unaendelea. Hapa hakuna fidia, kama unahama utatoka kwenye eneo la Square km 1500 na kwenda Eneo la Square km 2500.
 
Ubaya hauna kwao. Ubaya hauna macho. CCM Ina unasaba na ubaya. Kila mtu/kikundi ama chama wataonja ubaya wa CCM kwa wakati wake.

Mifno ya vyama na watu waliyoonja ubaya wa CCM.
-Ndugai, Membe, Sumaye, Lowasa, Lisu, Mbatia, e.t.c
-CUF, NCCR, Chadema,
Hivi sasa akina Halima Mdee wako bungeni kinyume na sheria. Wamevunja katiba lkn watanzania hatuandamani, tunadhani ni suala la chadema tu.

Wamasai wa Loliondo wanaporwa ardhi yao, watanzania hatuandamani tumewaachia wamasai.

Wakifanikiwa Loliondo watawaondoa kwenye maeneo yao wakazi wa Kigamboni, Marangu, Kisiwa cha Saanane, Bagamoyo, Mikumi, Kalenga, n.k.

Injustice somewhere is Injustice everywhere.
Tumeaza lini watz kubebeana maumivu ya wengine mpaka kuandamana?acha matumizi mabaya ya neno mandamano,Kiliwaka gesi kwa wamakonde wanajuwa wenyewe walivyolimaliza kwaiyo la masai achaa wapambane utafika tuu mwisho.
 
Umeandika mengi japo unachanganya mambo
1. Ngorongoro ndipo wafugaji wamehamishwa walioridhia mchakato na wamepewa na fidia. Wale ambao wanapiga kelele ni mapapa ambao wananufaika na malisho hawa wako Tz na Kenya. Na wengi wanatumia maneno wamasai wanaonewa wenyewe hawapo (cite ) .
2. Loliondo kuna pori kama Square km 4500 na ambapo Square km 1500 ndio inayowekewa mipaka. Na kuwa pori Tengefu , shughuli za binadamu hazihitajiki hapo. Eneo liliilo salia Square km 2500 ufugaji unaendelea. Hapa hakuna fidia, kama unahama utatoka kwenye eneo la Square km 1500 na kwenda Eneo la Square km 2500.
Haijalishi mkuu, pamoja na ufafanuzi huo.
1. Tuanze na Huko Ngorongoro, unaposema watu wahame. SAWA.
Kwa nini hii inakuwa kama dharura ya tia maji tia maji jahazi lisizame? Hili jambo halikufahamika toka zamani na wananchi wakapewa taarifa, pamoja na kuelimishwa ili watoe ushirikiano wakati zoezi likianza?
Hilo moja.
Pili, serikali ilikwishajiridhisha kabisa kwamba hakuna njia mbadala nyingine yoyote ya kuhakikisha kuwa eneo hili linabaki katika hadhi inayotakiwa, huku likiendelezwa kihimilivu, bila ya usumbufu mkubwa kwa watu? Imejiridhisha kabisa kuwa njia pekee ni kuwavurumisha wananchi wahame toka eneo hilo kwa nguvu (wao wakisema vinginevyo).

Serikali inaona ni rahisi na vyema zaidi kuwavuruga wananchi wake ili wageni waje kufanya shughuli zao hapo?

2. Hata hili swala la Loliondo, tatizo ni lile lile, msukumo wa kuwapa wageni furaha huku wananchi wakinyanyaswa, kwa nini? Nchi hii ilipata uhuru ili watu waje kunyanyaswa tena karne hii ya ishirini na mbili?

Hawa wananchi wanafaidika kufanya shughuli zao za mifugo katika eneo hilo linalowekewa mipaka ili mwekezaji aliendeshe. Huyu mwekezaji kaleta faida kiasi gani ndani ya nchi hii tokea amepewa hiyo sehemu, mbali ya kuwanyanyasa wananchi wa eneo hilo.

Ni katika pumzi hiyo hiyo ninaweza kukuuliza wewe, kuna ubaya gani kwa serikali kufanya kazi na wananchi wa eneo hilo la Loliondo, kuweka mikakati ya kuliendeleza kwa manufaa ya wananchi wenyewe. Serikali haitaki kufanya kazi kuwanufaisha wananchi wake; ila inaona ni bora zaidi kuleta watu watunyanyase nyumbani kwetu kwa vile tu wanawekeza, huku hela yenyewe haijulikani inaishia wapi, kwa maana wananchi hawanufaiki na lolote juu ya uwekezaji huo. Mbali ya manyanyaso tu wanayoletewa na hawa watu.

Sasa vipi, tuanze pilkapilka za kutafuta uhuru tena?
 
Ubaya hauna kwao. Ubaya hauna macho. CCM Ina unasaba na ubaya. Kila mtu/kikundi ama chama wataonja ubaya wa CCM kwa wakati wake.

Mifno ya vyama na watu waliyoonja ubaya wa CCM.
-Ndugai, Membe, Sumaye, Lowasa, Lisu, Mbatia, e.t.c
-CUF, NCCR, Chadema,
Hivi sasa akina Halima Mdee wako bungeni kinyume na sheria. Wamevunja katiba lkn watanzania hatuandamani, tunadhani ni suala la chadema tu.

Wamasai wa Loliondo wanaporwa ardhi yao, watanzania hatuandamani tumewaachia wamasai.

Wakifanikiwa Loliondo watawaondoa kwenye maeneo yao wakazi wa Kigamboni, Marangu, Kisiwa cha Saanane, Bagamoyo, Mikumi, Kalenga, n.k.

Injustice somewhere is Injustice everywhere.
Ubaya hugeuka aibu aibu kabisa kama mwendazake alipomaliza kupora uchaguzi akakosa amani na mwisho wake akachukuliwa kirahisi na shetani mpenda watu bila kumhurumia.
 
Back
Top Bottom