Uber yasitisha huduma zake Tanzania, yazitaja nauli elekezi Latra kama sababu. Itarejea kanuni zikibadilishwa

Uber yasitisha huduma zake Tanzania, yazitaja nauli elekezi Latra kama sababu. Itarejea kanuni zikibadilishwa

Inaweza kuwa kuna rafiki, ndugu au shemeji yako au mtu wako katika familia amekutana na kadhia hii na kumfanya akose ridhiki yake ya kila siku.

Je ? Umefurahia anguko lake katika hustling zake?
Uber nayo utaita hustling?
 
Madereva wengi wa Uber hawajielew

21294738_949691791862402_2474735176425406464_n.jpg
 
Uber
Tumechukua uamuzi mgumu wa kusitisha kwa muda huduma za UberX, UberXL na UberX Saver nchini Tanzania, bidhaa hizi hazitapatikana kuanzia Alhamis ya tarehe 14 Aprili 2022. Kanuni za sasa za usimamizi wa sekta hii zimejenga mazingira ambayo si rafiki na zimekuwa changamoto kubwa katika uendeshaji wa biashara yetu, hadi pale muafaka utakapopatikana, hatutaendelea kutoa huduma za usafiri wa UberX, UberX Saver na UberXL nchini Tanzania.

Tunapenda kuchukua fursa hii kukushukuru kwa dhati - kwa kuchagua mfumo wetu kufanya safari zako jijini Dar es Salaam ambako tumekuwa tukitoa huduma zetu kwa kipindi cha miaka sita iliyopita.

Huu ni wakati mgumu kwetu sote, lakini hii haina maanai kwamba ndio mwisho wa kila kitu. Tuko tayari kushirikiana na mamlaka husika na kuwa na mazungumzo yatakayoleta tija na kujenga mazingira wezeshi na tutarudi na kuendelea na kukupa usafiri wa kutegemewa na wa uhakika ambao umekuwa ukiitumia, baada ya kujiridhisha kwamba mazingira ya kibiashara ni rafiki.

Tunafahamu kwamba hiki ni kipindi kigumu na usumbufu unaotokana na uamuzi huu na tunapenda kukuhimiza uwasiliane nasi kupitia kwenye app ikiwa una maswali yoyote.

Asante Sana, Tanzania!

Timu ya Uber
Sasa hii barua haina hata Logo au stamp au signature si mtu yoyote anaweza kuandika tu. Hebu tuwe serious kidogo barua sio namna hii tena yenye mambo mazito kama haya.
 
Sasa hii barua haina hata Logo au stamp au signature si mtu yoyote anaweza kuandika tu. Hebu tuwe serious kidogo barua sio namna hii tena yenye mambo mazito kama haya.
Simple tu, wewe fanya kutokuamini hio barua then endelea na mambo yako mengine.
 
Kwa kifupi Uber walikuwa wanatafuta pa kufia, kibiashara wao walikuwa wameshatetereka baada mshindani wao kuwazidi.
Uber wako juu sana kwenye cost, mfano unarequest Uber kwa trip ya Posta-Mwenge unaambiwa 23,000 wakati Bolt ukiitisha same trip unaambiwa 10,000 kwa gari ndogo sedan kwa mawazo ya kawaida mteja aki request mara 2 au 3 na kuona hiyo tofauti ana haja gani tena ya kurequst tena hiyo Uber? Kwa kifupi wamejimaliza wenyewe!!!
bro mimi ni dereva wa bolt hyo bei unayosema hapo ya bolt tujiulize wote 10000 hyo bolt wanakata 23.5%kama comision yao dereva anabaki na shilingi ngapi?? bolt wanaumiza sana madereva kwa kigezo cha kumjali mteja kitu ambacho sio sahihi, Latra wametoa bei elekezi na wamewaambia comision yao isizidi 15% nauli za mchana na usiku zitofautioane. na hapo hii bei elekezi LATRA walitoa kabla hata ya mafuta kupanda kama yalivyo sasa. wao wanataka waendelee na bei za zamani na commisiom za zamani dereva na mwenye chombo atapata faida gani??
 
Haya sasa nanunua Passo,Ist na vitz kwa mafungu,zikianzia gari tano zitahesabika kama fungu moja m5 unapewa utaki unaacha.
 
Uber
Tumechukua uamuzi mgumu wa kusitisha kwa muda huduma za UberX, UberXL na UberX Saver nchini Tanzania, bidhaa hizi hazitapatikana kuanzia Alhamis ya tarehe 14 Aprili 2022. Kanuni za sasa za usimamizi wa sekta hii zimejenga mazingira ambayo si rafiki na zimekuwa changamoto kubwa katika uendeshaji wa biashara yetu, hadi pale muafaka utakapopatikana, hatutaendelea kutoa huduma za usafiri wa UberX, UberX Saver na UberXL nchini Tanzania.

Tunapenda kuchukua fursa hii kukushukuru kwa dhati - kwa kuchagua mfumo wetu kufanya safari zako jijini Dar es Salaam ambako tumekuwa tukitoa huduma zetu kwa kipindi cha miaka sita iliyopita.

Huu ni wakati mgumu kwetu sote, lakini hii haina maanai kwamba ndio mwisho wa kila kitu. Tuko tayari kushirikiana na mamlaka husika na kuwa na mazungumzo yatakayoleta tija na kujenga mazingira wezeshi na tutarudi na kuendelea na kukupa usafiri wa kutegemewa na wa uhakika ambao umekuwa ukiitumia, baada ya kujiridhisha kwamba mazingira ya kibiashara ni rafiki.

Tunafahamu kwamba hiki ni kipindi kigumu na usumbufu unaotokana na uamuzi huu na tunapenda kukuhimiza uwasiliane nasi kupitia kwenye app ikiwa una maswali yoyote.

Asante Sana, Tanzania!

Timu ya Uber
Je wanaopanda ambao wengi ni waajiriwa wamepandishwa mishahara?
 
Kwan wanalazimishwa? Wewe mbona unalipwa mshahara kidogo hatusemi
Unaongea bila kuzingatia usawa. Uber wanakata karibu asilimia 30 ambayo kimsingi ni kubwa sana. Anatumia hizo kauli za kikatili kwamba kwani mnalazimishwa?

Mshahara wangu ni mkubwa sana.
 
Huyu mama alifeli mapema sana. Ile hotuba yake ya kwanza aliposema...."mimi ndiye raisi na mimi ni mwanamke". Nilimuweka pembeni saa ileile.
Hakuwa na haja ya kusema yeye ni mwanamke,ni dalili ya kujitutumua.
 
Kwa kifupi Uber walikuwa wanatafuta pa kufia, kibiashara wao walikuwa wameshatetereka baada mshindani wao kuwazidi.
Uber wako juu sana kwenye cost, mfano unarequest Uber kwa trip ya Posta-Mwenge unaambiwa 23,000 wakati Bolt ukiitisha same trip unaambiwa 10,000 kwa gari ndogo sedan kwa mawazo ya kawaida mteja aki request mara 2 au 3 na kuona hiyo tofauti ana haja gani tena ya kurequst tena hiyo Uber? Kwa kifupi wamejimaliza wenyewe!!!
posta mwenge nauli Tsh 23,000/= hiv unaandika uhalisia au ushawah kua dereva wa uber ukapata nauli posta mwenge Tsh 23,000?
 
Back
Top Bottom