Kamgomoli
JF-Expert Member
- May 3, 2018
- 1,896
- 4,058
Mayele ni mchezaji mzuri hasa kwa jitihada zake za kujituma awapo uwanjani. Ila kwa mtazamo wangu licha ya mazuri yake kwa upande mwingine amekuwa akiighalimu sana timu kutokana na uchoyo uliopitiliza. Mechi ya leo na Simba amepiga mashuti mengi akiwa katikati ya uwanja badala ya kuwapa wenzake waliokuwa wamefungua.
Njoo kwenye mechi zile mbili na Al Hilal (home & away) ubinafsi wake ulichangia Yanga kufunga magoli machache hapa nyumbani na kupelekea kutolewa. Amekuwa akilazimisha kufanya vitu vingi peke ake akisahau kuwa mpira ni mchezo wa timu.
Anacheza kutafta "Personal glory" kuliko "Team success". Mara kadhaa nimekua nikimuona kocha akimkumbusha lakini habadiliki.
Mechi ya Dabi km ya leo ni mechi inayochezwa kimkakati sana. Ukicheza kibinafsi vile unawaraisishia wapinzani kukukaba na ndivyo Simba walivyofanikiwa. Kutokana na sifa anazosifiwa Mayele amekuwa akicheza kifadha sana.
Anapoteza mipira mingi na kwa uzembe kabisa! Siamini kama Nabi ameshindwa kumbadilisha na kama ni hivo basi uongozi uingilie kati kwa manufaa ya timu.
Namkumbusha Mayele, mashabiki wa Simba na Yanga huwa hawana mapenzi ya kudumu. Asione watu wapo kimya siku wakilipuka asishangae akianza kuzomewa, kama haamini amuulize Boko. Licha ya timu nzima kutocheza vizuri leo ila Mayele kazingua sana.
Hongereni Simba though, na poleni Utopolo.
Njoo kwenye mechi zile mbili na Al Hilal (home & away) ubinafsi wake ulichangia Yanga kufunga magoli machache hapa nyumbani na kupelekea kutolewa. Amekuwa akilazimisha kufanya vitu vingi peke ake akisahau kuwa mpira ni mchezo wa timu.
Anacheza kutafta "Personal glory" kuliko "Team success". Mara kadhaa nimekua nikimuona kocha akimkumbusha lakini habadiliki.
Mechi ya Dabi km ya leo ni mechi inayochezwa kimkakati sana. Ukicheza kibinafsi vile unawaraisishia wapinzani kukukaba na ndivyo Simba walivyofanikiwa. Kutokana na sifa anazosifiwa Mayele amekuwa akicheza kifadha sana.
Anapoteza mipira mingi na kwa uzembe kabisa! Siamini kama Nabi ameshindwa kumbadilisha na kama ni hivo basi uongozi uingilie kati kwa manufaa ya timu.
Namkumbusha Mayele, mashabiki wa Simba na Yanga huwa hawana mapenzi ya kudumu. Asione watu wapo kimya siku wakilipuka asishangae akianza kuzomewa, kama haamini amuulize Boko. Licha ya timu nzima kutocheza vizuri leo ila Mayele kazingua sana.
Hongereni Simba though, na poleni Utopolo.