Valencia_UPV
JF-Expert Member
- Mar 31, 2016
- 6,974
- 8,750
Siasa aisee
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Waliokopa pesa kutoa rushwa wajiandae namna nyingine ya kuzirudisha.Siasa aisee
kweli kabisa mkuuKiukweli Kama tunataka viongozi wenye uchungu na Tarime wasiangalie aliyetoa pesa
ni kweli Tarime imekuwa shamba la bibi kwa muda mrefu, bora walete hata wa mwisho ambaye hakutoa rushwa ila ana uwezo wa kushinda.Tarime chagueni wa kuleta maendeleo
Mshindi wa kura kiukweli Hana hojani kweli Tarime imekuwa shamba la bibi kwa muda mrefu, bora walete hata wa mwisho ambaye hakutoa rushwa ila ana uwezo wa kushinda.
Haya Majungu ya kishamba tena kijinga jinga zaidi ya yale ya Kigamboni kawe na sehemu zingine CCM walipotoa Rushwa wote, watia nia wagombea wote wa CCM wametoa Rushwa kila kona ya Tanzania ingawa Rushwa zilitofautiana kulingana na mgombea mwenyewe, cha ajabu wale waliofeli wakishindwa kwenye kura za maoni wamekuwa na wivu mkubwa kwa washindi kama ilivyokuwa Arusha mpaka kurekodi video wakitoa tuhuma za Rushwa zisizo na ushahidi wa Takukuru live, CCM wote wametoa Rushwa lakini CCM wengi hawakukamatwa live na Rushwa, wale wenye wivu na roho mbaya wameamua kuwarubuni Takukuru na vyombo vingine wawaandikie report mbaya washindi wa kura za maoni wapate kuwaengua wakose wote, Mfumo wa kijinga mfumo uliopitwa na wakati, CCM nendeni na style mpya ya kuwapata wagombea ubunge acheni Mbinu za kuja kuchuja majina Dodoma mnalea mnakarisha uongo fitna Majungu makubwa.UBUNGE TARIME MJINI: NGICHO/WAITARA WAHAMISHIA NGUVU ZAO KWA GERALD MARTIN
Kura za maoni Jimbo la Tarime Mjini zilifanyika tarehe 21 Julai 2020 na Jackson Kangoye akafanikiwa kuongoza kwa idadi ya kura. Inafahamika kwamba Jackson Kangoye na Mwita Waitara walitengeneza muungano ili kusaidiana katika kura za maoni za Tarime Mjini na Tarime Vijijini.
Na wote wawili walitegemea msaada wa Kamati ya Siasa Tarime katika kupindisha tararibu ili waweze kupata upendeleo dhidi ya wagombea wengine. Itakumbukwa Kamati hiyo ya siasa inayoongozwa na Mwenyekiti Daudi Marwa Ngicho, mchimbaji mdogo wa madini ambaye pamoja na mengine ana tuhuma mbalimbali katika hizo biashara zake.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya, Daudi Ngicho alihakikisha anaweka wabunge ambao watakuwa watiifu kwake na mara nyingi sana amewatishia waliokuwa wakishindana na Mwita Waitara ili kuhakikisha kuwa anapata nafasi ya kupeperusha bendera ya CCM katika jimbo la Tarime Vijijini.
Kura za maoni zilifanikisha mpango wao kwa wote kushinda kura za maoni, japo iko wazi kilichotumika kuwapa hizo kura ni rushwa ambayo iko wazi. Baada ya kura hizo wananchi wengi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi wameonyesha wazi kutokubali mapendekezo hayo ya wagombea maana hayaendani na matarajio ya wapiga kura wa Jimbo la Tarime Mjini na pia Tarime Vijijini.
Baada ya kujiridhisha kuwa Jackson Kangoye hakubaliki, ameruka na kuangalia jinsi anavyoweza kuitumia kamati ya siasa kumpendekeza mshindi wa tatu, Gerlad Martin, ambaye naye alipata kura 20 baada ya kuwa mtoa rushwa pia na taarifa zake zipo wazi.
Ngicho, Waitara wamekubaliana ni bora katika kikao cha kamati ya siasa kujaribu kushawishi na kumpendekeza Gerald Martin, kwani kwao ni mtu dhaifu ambaye wanaweza kummiliki na akafanya yale wanayotaka wao.
Na ikumbukwe Jumuiya ya Vijana Tarime kwa muda mrefu walijigeuza kuwa kikundi cha kumpigia Kampeni kinyume na kanuni za Uchaguzi. Hivyo ilikuwa rahisi Mwenyekiti wa UVCCM Tarime kumshawishi Waitara na Ngicho kuwa bora waende na Gerald, ambaye naye pia kiufupi sio mtu anayekubalika kwa wananchi maana hana mchango wowote kwenye jamii ukilinganisha na Michael Kembaki aliyekuwa mshindi wa pili na ambaye anakubalika.
Ngicho hamtaki Michael Kembaki kwa sababu haoni kama anaweza kummiliki kwa sababu ni mtu anayejitambua, mwenye biashara zake na asiyetegemea mtu katika maamuzi yake binafsi. Hivyo ameona ni bora ampiganie Gerlad, na kwa kuwa kamati nzima ya siasa iko chini yake na huwa anawalipa wote posho basi bila shaka anajua mapendekezo yake yote yatapita kwa asilimia 100.
Tunaomba viongozi wa kitaifa wa Chama waangalie kwa undani hali ya Tarime kwani maamuzi mabaya yatakayofanyika yatapelekea majimbo yetu kuendelea kuwa chini ya CHADEMA.
Wenu,
Venance Marwa,
Mwana CCM Mkereketwa Tarime.
CCM wote wametoa Rushwa asikutanganye mtu tena wale wa mwisho pesa zao huwauma pindi zikiliwa na wajumbe kisha kuambulia patupu wanakuwa vinara wa Majungu kuwakomoa washindi ni wivu umetawala kura za maoni CCMni kweli Tarime imekuwa shamba la bibi kwa muda mrefu, bora walete hata wa mwisho ambaye hakutoa rushwa ila ana uwezo wa kushinda.
CCM nao wametoa pesa nyalandu awe mgombea wa Urais kwa chadema ili magufuli arejee ikulu bila hata ya kufanya kampeniNi kweli hizo tuhuma zipo, Chadema walipambana kutoa pesa ili mgombea anayepita CCM awe ambaye wataweza kumgaragaza kwa urahisi.
Mleta mada hawezi kuweka namba za simu anajua kuwa amepika Majungu ambayo yakibainika yatamgharimuTabia za fisi kula fisi...inasikitisha!
Mleta mada wenzako huacha namba za simu!
Anyways tuwaache wafu wazikane.
Everyday is Saturday........................... 😎
Msimu wa wajumbe Tanzania nzima wajumbe wamekula Rushwa za watia nia wa CCM wote hakuna CCM asiyetoa Rushwa wote wametoa RushwaWajumbe. ... washafanya yao
Tuhuma za Rushwa ikithibitika pasipo shaka huyo waitara atafyekwa Dodoma, cha muhimu ni ushahidi sahihi na kweli usiwe ushahidi wa kutengeneza kimajungu jungu.Waitara kiukweli hakubaliki na hana sita Kama Mama Kabaka. Huyu Mama Kabaka Ni mtu mzuri na anayependwa na wana Tarime wote na sifa zake zinajulikana. Waitara Ni mbunge mwenye sifa mbaya tangu Ukonga na huku kwetu. Kiufupi Wajumbe walijichanganya na Heche atampiga asubuhi kabla jogoo hajawika
NDOTO ZAKO HIZI HAZITATIMIA.Tuache Basi wamteua aliyepata kura ili Jimbo liende CHADEMA
Usitazame tu ukapige na kuraSisi ni wapenzi watazamaji