Uchaguzi 2020 Ubunge Tarime Mjini: Ngicho ahamishia nguvu zake kwa Gerald Martin

Uchaguzi 2020 Ubunge Tarime Mjini: Ngicho ahamishia nguvu zake kwa Gerald Martin

Kiukweli Kama tunataka viongozi wenye uchungu na Tarime wasiangalie aliyetoa pesa.
 
UBUNGE TARIME MJINI: NGICHO/WAITARA WAHAMISHIA NGUVU ZAO KWA GERALD MARTIN

Kura za maoni Jimbo la Tarime Mjini zilifanyika tarehe 21 Julai 2020 na Jackson Kangoye akafanikiwa kuongoza kwa idadi ya kura. Inafahamika kwamba Jackson Kangoye na Mwita Waitara walitengeneza muungano ili kusaidiana katika kura za maoni za Tarime Mjini na Tarime Vijijini.

Na wote wawili walitegemea msaada wa Kamati ya Siasa Tarime katika kupindisha tararibu ili waweze kupata upendeleo dhidi ya wagombea wengine. Itakumbukwa Kamati hiyo ya siasa inayoongozwa na Mwenyekiti Daudi Marwa Ngicho, mchimbaji mdogo wa madini ambaye pamoja na mengine ana tuhuma mbalimbali katika hizo biashara zake.

Mwenyekiti wa CCM Wilaya, Daudi Ngicho alihakikisha anaweka wabunge ambao watakuwa watiifu kwake na mara nyingi sana amewatishia waliokuwa wakishindana na Mwita Waitara ili kuhakikisha kuwa anapata nafasi ya kupeperusha bendera ya CCM katika jimbo la Tarime Vijijini.

Kura za maoni zilifanikisha mpango wao kwa wote kushinda kura za maoni, japo iko wazi kilichotumika kuwapa hizo kura ni rushwa ambayo iko wazi. Baada ya kura hizo wananchi wengi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi wameonyesha wazi kutokubali mapendekezo hayo ya wagombea maana hayaendani na matarajio ya wapiga kura wa Jimbo la Tarime Mjini na pia Tarime Vijijini.

Baada ya kujiridhisha kuwa Jackson Kangoye hakubaliki, ameruka na kuangalia jinsi anavyoweza kuitumia kamati ya siasa kumpendekeza mshindi wa tatu, Gerlad Martin, ambaye naye alipata kura 20 baada ya kuwa mtoa rushwa pia na taarifa zake zipo wazi.

Ngicho, Waitara wamekubaliana ni bora katika kikao cha kamati ya siasa kujaribu kushawishi na kumpendekeza Gerald Martin, kwani kwao ni mtu dhaifu ambaye wanaweza kummiliki na akafanya yale wanayotaka wao.

Na ikumbukwe Jumuiya ya Vijana Tarime kwa muda mrefu walijigeuza kuwa kikundi cha kumpigia Kampeni kinyume na kanuni za Uchaguzi. Hivyo ilikuwa rahisi Mwenyekiti wa UVCCM Tarime kumshawishi Waitara na Ngicho kuwa bora waende na Gerald, ambaye naye pia kiufupi sio mtu anayekubalika kwa wananchi maana hana mchango wowote kwenye jamii ukilinganisha na Michael Kembaki aliyekuwa mshindi wa pili na ambaye anakubalika.

Ngicho hamtaki Michael Kembaki kwa sababu haoni kama anaweza kummiliki kwa sababu ni mtu anayejitambua, mwenye biashara zake na asiyetegemea mtu katika maamuzi yake binafsi. Hivyo ameona ni bora ampiganie Gerlad, na kwa kuwa kamati nzima ya siasa iko chini yake na huwa anawalipa wote posho basi bila shaka anajua mapendekezo yake yote yatapita kwa asilimia 100.

Tunaomba viongozi wa kitaifa wa Chama waangalie kwa undani hali ya Tarime kwani maamuzi mabaya yatakayofanyika yatapelekea majimbo yetu kuendelea kuwa chini ya CHADEMA.

Wenu,
Venance Marwa,
Mwana CCM Mkereketwa Tarime.
Haya Majungu ya kishamba tena kijinga jinga zaidi ya yale ya Kigamboni kawe na sehemu zingine CCM walipotoa Rushwa wote, watia nia wagombea wote wa CCM wametoa Rushwa kila kona ya Tanzania ingawa Rushwa zilitofautiana kulingana na mgombea mwenyewe, cha ajabu wale waliofeli wakishindwa kwenye kura za maoni wamekuwa na wivu mkubwa kwa washindi kama ilivyokuwa Arusha mpaka kurekodi video wakitoa tuhuma za Rushwa zisizo na ushahidi wa Takukuru live, CCM wote wametoa Rushwa lakini CCM wengi hawakukamatwa live na Rushwa, wale wenye wivu na roho mbaya wameamua kuwarubuni Takukuru na vyombo vingine wawaandikie report mbaya washindi wa kura za maoni wapate kuwaengua wakose wote, Mfumo wa kijinga mfumo uliopitwa na wakati, CCM nendeni na style mpya ya kuwapata wagombea ubunge acheni Mbinu za kuja kuchuja majina Dodoma mnalea mnakarisha uongo fitna Majungu makubwa.
 
ni kweli Tarime imekuwa shamba la bibi kwa muda mrefu, bora walete hata wa mwisho ambaye hakutoa rushwa ila ana uwezo wa kushinda.
CCM wote wametoa Rushwa asikutanganye mtu tena wale wa mwisho pesa zao huwauma pindi zikiliwa na wajumbe kisha kuambulia patupu wanakuwa vinara wa Majungu kuwakomoa washindi ni wivu umetawala kura za maoni CCM
 
Ni kweli hizo tuhuma zipo, Chadema walipambana kutoa pesa ili mgombea anayepita CCM awe ambaye wataweza kumgaragaza kwa urahisi.
CCM nao wametoa pesa nyalandu awe mgombea wa Urais kwa chadema ili magufuli arejee ikulu bila hata ya kufanya kampeni
 
Tabia za fisi kula fisi...inasikitisha!
Mleta mada wenzako huacha namba za simu!

Anyways tuwaache wafu wazikane.

Everyday is Saturday........................... 😎
Mleta mada hawezi kuweka namba za simu anajua kuwa amepika Majungu ambayo yakibainika yatamgharimu
 
Waitara kiukweli hakubaliki na hana sita Kama Mama Kabaka. Huyu Mama Kabaka Ni mtu mzuri na anayependwa na wana Tarime wote na sifa zake zinajulikana. Waitara Ni mbunge mwenye sifa mbaya tangu Ukonga na huku kwetu. Kiufupi Wajumbe walijichanganya na Heche atampiga asubuhi kabla jogoo hajawika
Tuhuma za Rushwa ikithibitika pasipo shaka huyo waitara atafyekwa Dodoma, cha muhimu ni ushahidi sahihi na kweli usiwe ushahidi wa kutengeneza kimajungu jungu.
 
Nashauri Tarime Mjini tuweke Mgombea makini wa kupambana na Mbunge anayemaliza muda wake vinginevyo tunaweza kupoteza Tena Jimbo hili.
 
Kikubwa tujitahidi CCM ishinde maana Upinzani bado una nguvu Sana hapa Tarime na hivi vijana maisha magumu wasije wakapiga kura kutukomoa tu
 
Back
Top Bottom